Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all 3173 articles
Browse latest View live

Makufuli tumbua wachunaji

$
0
0
Image result for photo of gwajima na helkopta
            Juzi nilisika saka saka ya mchunaji mmoja anayejiita mchungaji akiihangaisha sirikali. Wabongo kwa kukuza mambo, hakuna mfano. Kwani, mchunaji mwenyewe punde si punde si alijitokeza. Wacha ndata wamzukie waishie kumgwaya. Kwani, tumepashwa kuwa alikwenda pale kituoni kama mtu anayekwenda mgahawani kupata chai na kuishia zake kwenye hekalu lake ambalo nalo hatujui alivyolijenga. Kwa kazi gani au ni kwa kutumia sadaka?
Huyu jamaa ambaye alijizolea umaarufu baada ya kumpa tafu Eddie Luwasha kwenye uchakachuaji uliopita ameniacha hoi baada ya kumkana na kujifanya anamzimii dokta Joni Kanywaji Makufuli. Ya kweli haya au ni janja ya kusaka ulaji ukiachia mbali kuogopa asitumbuliwe usawa huu anapomilki chopa bila kueleza wala kuonyesha alivyochanganya njuluku hadi akawa bonge la mkwasi ghafla bi vu? Kwa jeuri aliyoonyesha si haba. Who knows. Huyenda naye ana sirikali yake yenye siri kali kubwa kiasi cha ndata kumgwaya. Au ni kwa vile amejitoa kwenye upingani; hivyo, matamshi na tabia zake havihatarishi amani ya walaji wakubwa kayani? Bahati yake, angekuwa bado kitanda kimoja na Ewassa huenda hata hiyo chopa na hekalu vingekuwa vimeishanyakwa baada ya kutumbuliwa.
Ngoja niulize kibangibangi na kigongongo. Je huyu jamaa huwa anafanya kazi gani zaidi ya uchunaji? Hata hivyo sishangai. Baada ya neno la Bwana kugeuka bidhaa adimu ambayo kila tapeli anaweza kutumia kuukata, who knows hata kama uchunaji ni joho tu la kufichia biashara nyingine kubwa? Huoni wanavyoibuka wachunaji kila uchao hadi wengine kumuingiza nkenge Dokta Kanywaji hadi akawazukia kwenye maduka yao? Juzi nilinusurika kuzimia baada ya kusikia wachunaji wengine eti wakiandaa mkutano mkubwa wa kuombea kaya kana kwamba kaya inahitaji kuombewa badala ya kuambiwa ukweli kuwa ni shamba la bibi na kichwa cha mwendawazimu cha mzee Ruxa tulichokiona wakati wa Njaa Kaya na genge lake la ulaji na uzururaji. Tumekuwa na wanene wabovu kiasi cha kufuga mijizi ambapo kaya ilikuwa kwenye outpilot kila mchovu akijifanyia atakavyo. Hata hivyo, chini ya rahis Kanywaji, nina imani mambo yatabadilika kama hawatambadilisha kabla hajawabadilikia na kuwabadilisha.
Siku hizi si ajabu kuona wachunaji wakipanda mingoma mizito na kuishi kwenye mahekalu wakati yule bwana mkubwa wanayemhubiri alikuwa apeche alolo akiombaomba. Rejea Kaisari alipomtakisha kodi. Si alikuwa amewaka kiasi cha kuikopa njuluku kwa samaki? Sasa hawa wachunaji wanapata wapi hii ya kuwa matajiri wakati Yesu mwenyewe alisema kuwa ni heri ngamia kupita tundu la sindano kuliko wakwasi kuingia kwenye ufalme wa God? Msiseme nazusha. Hamuwaoni walivyo na mimali lukuki isiyo na maelezo?
 Linapokuja suala la watu kuwafisidi na kuwaibia wachovu, kaya yetu inaweza kuwa kinara. Hata hivyo, bwana mkubwa aliwahi kusema, “Macho wanayo. Lakini hawaoni. Masikio wanayo. Lakini hawasikii.Wengi wa wachunaji hata ukiona sura zao ni wababaishaji wa kawaida tu waliojificha nyuma ya majoho na madhabahu wakinajisi na kuibia wachovu wa God. Kwanini wachovu wanashindwa kuelewa kitu simpo kuwa; huwezi kutumikia mabwana wawili yaani bwana God na ukwasi ukauona ufalme wake. Kinachowapa ulaji ni ile hali ya wachovu na walevi kumsahau baba yao Kibwetere aliyewabwetere kondoo kwa kuwatia nari na kuondoka na mali zao. Japo nisemayo ni ya kilevi na bangi, sitashangaa kusikia Kibwetere mwingine akiibukia Bongo muda si mrefu. Chukulieni hili kwa makini. Kwani ni utabiri swaafi wa nabii wa walevi.
Wengi wamefikia hata kujiita mitume na manabii wakati ni mitumba na majangili. Hivi anaweza kupatikana mtume au nabii usawa huu kwenye dunia ya walafi na mafisi na mafisadi ambapo mali imechukua nafasi ya God siyo? Mara hii mmesahau aliyenaswa na nyara za umma akijifanya mchungaji wakati ni jangili. Ni manaigeria mangapi walishanaswa na bwibwi huku wakiwa wamevalia kama wachungaji wakati ni wachunaji na wasafirisha bwibwi? Wengine wanajiita watu wa Mungu wakati ni watu wa unga. Ukiangalia biashara fichi ya wachunaji, mbali na wengine kutumia misamaha ya kodi kuingiza bidhaa za wafanyabiashara wezi, kuna kila sababu ya kuamini wana biashara nyingi haramu nyuma ya pazia. Hapa hujagusia michango wanayowatwisha mbumbumbu wengi wenye matatizo na wizi wa sadaka.
Hata hivyo, hawa wachovu wajinga na wapumbavu wana bahati. Kama si mlevi kuwa mcha God, angeweza kuanzisha dhehebu lake la Ufufuko na Utajirisho ili awaibie mchana kweupe kama wanavyofanyiwa na matapeli tena wengi ambao hawakupiga buku kama mimi. Kwa elimu yangu ya saikolojia–kama ningeamua kuwaibia ningekuwa tajiri–kutokana na kuwachezea kisaikoloji. Jitu linatoa mimba linaishia kushindwa kupata mtoto eti linakwenda kuombewa baada ya kutapeliwa na waganga wa kienyeji wanaoishia kulibaka. Kama haitoshi, jingine linaolewa na kushindwa kutunza ndoa yake. Mambo yakiharibika linakimbilia kwa wachunaji. Kimsingi, kinachoendelea kayan–licha ya kuwa ushirikina na wizi wa mchana–ni zao la kukosa kujiamini na kukabili matatizo kama yalivyo. Kimsingi, wachunaji na waganga wa kienyeji tofauti yao ni majina. Sitashangaa siku moja–baada ya kuzoea kuona wachunaji wakibambwa na bwibwi–kusikia kuna wachunaji wamenaswa na viungo vya watu wenye ulemavu wa ngozi. Anyways guys, msinichukulie seriously kwa vile nimeutwika leo. Muhimu, Makufuli anapaswa kuwatumbua hata wachunaji.
Chanzo: Nipashe Jumamosi.

Makonda upangaji Nyumba za Msajili ni jipu lako

$
0
0

Baada ya kuondoa ombaomba, kutangaza kiama cha mashoga, mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda anakabiliwa na kibarua kingine ambacho kitapima sincerity na ithibati yake kama kiongozi wa umma. Sina shaka na uongozi wa Makonda japo mwanzoni nilikuwa na shaka naye hasa kutokana na siasa za ndani ya chama chake–hasa pale alipodaiwa kutaka kumdhalilisha waziri mkuu wa zamani Joseph Wairoba–jambo ambalo alilikanusha kwa umahiri zaidi ukiachia mbali Warioba kutolalamika binafsi.
Leo tunampa changamoto nyingine kubwa ambay–japo wengi hawapendi kuigusia –ipo na imekuwapo kwa muda mrefu. Sijui kama Makonda alishawahi kujiuliza sababu na mantiki ya jamii moja ya kiasia tena si kiasia tu bali ya kihindi kukalia karibu majengo yote ya Msajili wa Majumba ya katikati ya jiji?
Licha ya kuwa ubaguzi wa wazi wazi, kuna kila harufu ya rushwa kuhusu upatikanaji wa upangaji wa nyumba hizi ambazo–licha kuwa za bei nafuu–hazionyeshi sura ya Tanzania.
Ukiachia hayo hapo juu, kuna uwezekano wa kuwapo kwa jinai zinazoendelea ambazo zinatokana na makazi ya kibaguzi kama vile, kuficha wahamiaji haramu ambao ni wakimbizi wa kiuchumi waliojazana nchini wakiishi kinyume cha sheria ukiachia mbali kuchukua ajira na kufanya shughuli ambazo watanzania wanaweza kuzifanya.
Rejea kuwahi kufichuliwa magenge ya wasafirishaji binadamu ambapo wasichana wa kihindi walikuwa wakiletwa nchini kufanya umalaya kwa kisingizio cha kutoa burdani. Rejea tukio la mwaka jana ambapo wanaodhaniwa kuwa ni vyangudoa 22 toka nchini Nepal waliokuwa wameiingizwa nchini na kampuni ya Dhamaka Entertainment Center Limited walivyokamatwa.
Kama tutakuwa makini na wakweli, wakimbizi wa kiuchumi ni hatari kwa taifa letu kuliko ombaomba na mashoga ambao mara nyingi mambo yao ni suala la mtu binafsi na si mtandao mkubwa unaohusisha mataifa yenye watu wengi maskini na wasio na kazi wanaotumia ngozi yao kuhujumu taifa letu. Pia Makonda anapaswa kupambana na mitandao ya wazawa inayoshirikiana na wageni hawa kuhujumu taifa. Kukaa mahali popote nchini ni haki ya kila mtanzania. Inapokuja kufaidi matunda ya nyumba za umma kama vile za Msajili wa Majumba, lazima lisiwe suala la kuchagua bali kufuata sheria inayoakisi usawa wa watanzania. Bila rushwa wala ubaguzi, haiwezekani watu wa tabaka moja waishi sehemu yao maalumu halafu wawadanganye wanaowabagua kuwa wako sawa. Usawa gani huu wa bata na kuku?
Naamini Makonda amesoma historia ya ujio wa wahindi ambao waliletwa na wakoloni ili kujenga reli na baadaye wakawatumia kama watu kati wa kununua mazao ya waafrika ili kuwanyonya na kuwafanya wawe maskini ili iwe rahisi kuwatawala kwa lengo na kuwanyonya milele. Ni bahati mbaya, baada ya kupata uhuru–tokana na huruma ya baba wa taifa, mwl, Julius Nyerere aliyechukia ubaguzi–aliwaruhusu jamaa hawa waliokuwa wakihujumu uhuru wetu wazi wazi kuwa raia wa taifa jipya la Tanganyika.
Wakati wa viongozi wetu kuangalia mambo kama yalivyo ni sasa ambapo wenye uwezo waamriwe kujenga nyumba zao binafsi ili kuwapisha wasio na uwezo kutumia nyumba husika. nyumba hizi, kwanza, ni za umma; na ni alama ya uhuru wetu. Je watu wetu maskini –hasa wafanyakazi wa serikali –wataendeleaje kunyanyasika kwenye nyumba binafsi za kupanga wakati nyumba zao zinakaliwa na matajiri wenye mahekalu wanayopangisha kwa fedha za kigeni? Kama haitoshi, mfumo wetu, umeruhusu tabaka moja la wachache kutajirika wakati umma ukiendelea kuteseka kwenye umaskini. Makonda anapaswa kuanzia hapa. Na hili haliwezi kuonekana kama ubaguzi. Kwanini wao kukalia nyumba za umma tena kama tabaka moja halionekani kuwa ubaguzi wa wazi wa kiuchumi na kijamii?
Kwa wanaokumbuka huu ubaguzi wa wazi ulivyokuwa umehalalishwa, watakambuka namna marehemu Christopher Mtikila alivyoushughulikia hadi kuupunguza kidogo tena kwa muda. Kwa watu wa kizazi cha kuanzia miaka 50 kwenda juu waliokulia kwenye jiji la Dar Es Salaam, watakumbuka ambavyo wahindi–ambao Mtikila aliwaita magabacholi tokana na neno chori au mwizi ambalo walilitumia kuwaeleza waswahili kama wezi–walikuwa hata hawapandi dala dala wala kuchanganyikana na waswahili ukiachia mbali kuwatumia kama watumishi wa madukani na majumbani na walinzi wao.
Japo tunajua kuwa jamaa hawa wanatokana na mfumo mbovu wa kikaburu wa caste system, waliruhusiwa kuendelea na ubaguzi wa wazi wazi. Kama tulivyosema hapo juu, wakati wa kubomoa mfumo huu kimfumo ni sasa ambapo serikali yetu inapaswa kutangaza wazi wazi isivyoridhishwa wala kukubali jinai hii ya wazi.
Tumalizie kwa kumtaka mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam –ambaye ameonyesha kuwa na nia ya kuwakomboa wanyonge–aanze kubomoa mfumo huu wa kibaguzi mkoani mwake–kwa kuanza na nyumba za Msajili wa Majumba. Lazima nyumba hizi zionyeshe sura ya Tanzania na si ya India wala utajiri. Miaka zaidi ya 50 tabaka moja limefaidi nyumba za Msajili itoshe. Tutunge utaratibu wa kuzuia ubangishanaji wa kifisadi ambao umefanikisha na kuhimiri mfumo huu wa kibaguzi.
Tanzania Daima Jumapili.

Kijiwe champongeza Dk Kanwyaji

$
0
0

          Baada ya Dokta Joni Kanywaji Makomeo kupewa rungu la pili ili atumie kutumbua majipu, Kijiwe kinampongeza na kumtega. Kwani, sasa wachovu wanategemea kuona akifanya vitu vyake bila ya woga wowote hasa ikizingatiwa kuwa ana marungu yote.
Mpemba anaingia akiwa amevalia kofia yake nzuri ya tarabushi na kuamkua na kusema, “Yakhe mlokuwa mkisema sana kuhusiana na rahis Dokta Joni Kanywaji Makomeo sasa jiandaeni kusuka au kunyolewa tena bila maji.”
Mheshimiwa Bwege anamchomekea, “Yakhe wamaanisha nini? Unadhani kuna mabadiliko hapa au yale yale ya CcM?”
Mpemba anajibu, “Unakuwa kama wewe si mtu wa pwani? Kwani mie namaanisha nini? Basi ngoja nrudie. Nasema, mlokuwa mkisema sana sasa ntihani kwenu. Ombeni Subhanna huyu jamaa afanye kweli. Lakini asipofanya kweli mtaumbuka kweli kweli kiasi cha kuonekana kama mwalimwa mwajiona.”
Mgosi Makamba anakula mic, “Sisi tinampongeza dokta Kanywaji; pia tinamuombea afanye  kwei ii asijeonekana kanyabwoya kama siyo sanaa na kamba. Maana, sisi tiiofuatiia nchakato nzima tinaona kama kuna namna hasa tikikumbuka  waiovyosifiana.”
Mipawa anakula mic, “Kumbe nawe umeiona namna alivyowasifia wale anaowatuhumu kuwauza wachovu tokana na uzembe wao? Hata mie hapa nashangaa kiasi cha kuanza kuona kama usanii mwingine.”
Kapende, “Ulitegemea nini? Kwani hujui kuwa kambare wote wana sharubu au unadhani watabadilika usawa huu? Nasema wazi wazi tena kwa kinywa kipana; wanaotegemea mabadiliko basi walie tu. Kama yapo ni yale ya kutumbua vidagaa na kulala kitanda kimoja na nyangumi. Jiulize ni kwanini kushitaki mafisadi imekuwa kama aina fulani ya picha.  Mie kusema ukweli sitegemei lolote jipya zaidi ya kuwekana sawa na kufungana kamba kama kawa. Dk Kanywaji akitaka kunishawishi awakamate waliogeuza kaya yetu shamba la chizi.”
“Kaka hapo umetoboa. Hata mie atanitosheleza kama atakamata mafisadi bila kubagua. Nashangaa madudu kama Escrow, EPA, kuficha njuluku ughaibuni hayaguswi. Huoni hata mafisadi wa sukari wamemalizana naye; na sasa wanapeta? Unacheza na Danganyika nini?” anasema da Sofia Lion aka Kanungaembe.
Mbwamwitu ansema, “Da Sofi acha nikuchomekee. Unasema atakutosheleza kama atafanya nini?”
Sofia anajibu, “Wewe unaonaje kama swali hili angeulizwa mama yako? Wenzako wako seriously wewe unaleta utani hapa!  Acheni kucheza makidamakida kama Lyatongolwa Mlemavu aliyekwenda Idodomya kujikomba na kujivua nguo kwa sababu ya tonge la ugali.”
Mijjinga anatia guu, “Usinikumbushe huyu meku ambaye anaonekana hakuumbwa na aibu hata chembe hasa anapobanwa na njaa. Yote tisa, sikujua kuwa kumbe kile kizee cha kigosi bado kipo. Kijamaa kwa kamba. Eti kiliingia na gea ya uhubiri wakati nacho ni yale yale kutafuta ulaji wa dezo. Hakuna kiliponiudhi kama kuwasifia Njaa Kaya na Denjaman wakati waliuza kaya yetu.”
Mzee Maneno anakwanyua mic, “Unashangaa hiki kizee cha mikamba siyo! Ulitegemea kiseme nini wakati huu ambapo mtandao wao wa wizi uko hatarini chini ya Dokta Kanywaji? Pamoja na uhovyo wake, kilinifurahisha kilipomtolea uvivu mchunaji Jose Gwaijumaa aliyejitiatia kumkana Eddy Ewassa akidhani atawaingiza mkenge magamba asijue nao ni kama yeye ni wapigaji na wasanii wazoefu.”
Msomi aliyekuwa akibukua jarida moja la kimataifa akionyesha wazi kutokuwa na hamu na mjadala anaamua kuchomekea, “Hivi kamandoo wa Zenj yuko wapi;maana sikumtia machoni.”
Mpemba anajibu, “Unaulizia shuka matangani. Alikuwa kamandoo zama zile akiua wapemba. Baada ya Nyazi Mungu kuntia laana untegemeani?”
Kanji naye anachomekea, “Veve Somi iko fanya juri sana dugu yangu. Hata mimi iko wazi iko wapi ile kamandoo natingisa sana zama ile.”
Msomi anaamua kuigia jumla, “Nimesikiliza pwenti zenu nyote. Wapo wanaotegemea kuwa Dokta Kanywaji atatumia marungu yake kuwaponga kila nyani wanao na waliohujumu kaya. Mwenzenu nachelea kuamini hivyo hasa nikizingatia kuwa jamaa ni mwanasiasa. Pili, kwa alivyowamwagia ujiko wahujumu viongozi wa kaya hii, sitegemei lolote wala muujiza. Nashangaa amekuwa akilalamika kuwa kaya yetu ililiwa jambo ambalo ni kweli. Je ililiwa chini ya nani kama si hao anaowasifia kwa kumuumba na kumfundisha mengi? Nadhani–kwanza sitaki nionekana nawanga–tutarajie kipindi cha kushangaza ambapo mambo yatakuwa yakienda kutegemea anayeshughulikiwa ni nani. Sitaki kujipa matumaini yasiyokuwepo hasa nikijua namna wanasiasa wetu walivyo. Nadhani lao laweza kuwa moja hasa usawa huu ambapo siasa ni sehemu ya kutengenezea utajiri wa haraka hata kama ni mchafu.”
Anapiga chafya na kuendelea, “Japo namuaminia Dokta Kanywaji, napata shaka japo bado nakuwa na matumaini kuwa mara nyingine siasa za majukwaani huwa ni za kupakana mafuta kwa mgogo wa chupa; hivyo, lolote lawezekana.”
Mgosi Machungi anadandia, “Hapa timekueewa. Nikikumbua aivyomifukuza Ombeeni Sifuwi, naweza kusema loote laweza kutokea kwa Dokta Kanywaji. Hivyo, timpe moyo asiangalie nyani au tumbii usoni atakapoanza kutumia maungu haya aiyopewa juzi.”
Mchunguliaji naye anaamua kuzoza. “Hapo kaka nimekupata tena vizuri sana.”
Kabla ya kuendelea Mgosi anaamua kutaka kumkwida.
Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita manzi chuma kweli kiasi cha kutufanya wote tumkatie shingo!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Mlevi atamani kufanya biashara na NSSF

$
0
0

           Kwanza, nimpongeze rafiki, kaka yangu na msomaji wangu rahis Joni Kanywaji Makufuli kwa kuwatumbua walaji wa Shirika la Utafunaji wa Hifadhi ya Taifa ya Jamii au Nominal Social Syndicate of Fraudsters (NSSF) baada ya jamaa kula kwa mikono na miguu tena bila kunawa. Nampongeza kwa kupewa rungu na nambari wani kuwatumbua majipu yote hata kama ni yale yaliyomkabidhi rungu lenyewe. Nasema bila kumung’unya “Tumbua Kaka.” Nashauri hata kauli mbiu yako ibadilishwe na kuwa “Hapa Kazi na Kutumbua Tu” au siyo? Ila katika kutumbuatumbua angalia usinitumbue mimi. Ukifanya hivyo utakosa ushauri na inshu. Hivyo, nakupa greenlight utumbue kila jipu isipokuwa mimi ambaye ujipu wangu ni wa kupiga mma na kuchoma jani. Pia naomba unikumbuke kama Lyatongolwa  najikomba kwako ding.
Baada ya kumpongeze mnene kupewa rungu ambalo–sina shaka–atalitumia bila huba, upendeleo wala uonevu kuwashughulikia walogeuza kaya shamba la chizi chini ya Jk, sorry, Njaa Kaya.
Hivi karibuni aliwatumbua vigogo wa NSSF tokana na ujinga na uroho ambao hata fisi–pamoja na uroho wa kupindukia–kusema ukweli, hana.  Mnakula hata nyayo wanahizaya nyie msie na aibu wala adabu! Shame on you! Sasa mtakoma na kukomaa. Hapa lazima Dokta Kanywaji afe na gendaeka. Hivi kweli unaweza kuamini; kiwanja kilichopaswa kununuliwa kwa madafu bilioni moja na nusu kilinunuliwa kwa madafu bilioni 15? Ukisikia kiwanja chenyewe unatamani ukamate gendaeka uwafanyie kitu mbaya. Hebu fikiria. Kiwanja Bongo, tena madongo kuinama, kinapunyua madafu bilioni zaidi ya 15 za walevi wanaonuka umaskini wa kutengenezewa na watawala washenzi na wapuuzi kama tulivyowashuhudia hivi karibuni Dk Kanywaji akiwananga kuwa waliachia kaya ikaliwa kama haina mwenyewe. Wakati mwingine unashindwa kuielewa miswahili.  Mijitu inakula hadi mapembe na kwato? Mbona hata Tokyo–kule Ujep na New York kwa Joji Kichaka na Obamiza–ambako viwanja ni aghali kuliko vyote duniani bei haijafika huko? Unashangaa kusikia eti hawa nao eti ni wasomi kweli? Tokana na sakata hili, Mlevi apanga kuonana na rahis Dk Kanywaji–si kujikomba kama Lyatongolwa–kumtaka abatilishe uteuzi wa aliyekuwa bosi wa wizi huu wa mchana aliyemteua balozi. Huyu alipaswa kuwa Keko lakini si zaidi. Anapewa ubalozi wa nini wakati mchezo wake mchafu ndiyo umefumka? Au Dk Kanywaji alipompa ubalozi alikuwa hajapata hili jipu alilotumbua hivi karibuni? Nalo hili nikipata appointment naye nitalipenyeza ili jamaa aende zake lupango akajiunge na wenzake.
Pia, nitamuomba Makufuli ima aniteue kuwa mnunuzi wa mali za NSSF; au niwe muuzaji kwake ili nichanganye njuluku hasa kutokana na kugundua kuwa kumbe kuna fursa za kutengeneza ukwasi kama sina akili nzuri.  Hapa uhitaji kutumia akili. Kinachotakiwa ni kutembeza hongo.  Kwa vile mimi ni msomi wa kweli na mzalendo tena muaminifu, nitakula kidogo na kubakiza kikubwa tofauti na hawa waliokuwa wakiiba kikubwa na kidogo ukiachia mbali kupokea chochote kile katika ujambazi huu wa mchana.
Kwa vile wizi wa mabilioni na matrilioni umezidi kayani, nitamshauri Dk Kanywaji afanye utaratibu wa kupeleka mswaada bungeni wa kuhakikisha wanaokwapua mabilioni na matrilioni wananyongwa sawa na majambazi wa kawaida.  Pia, nitashauri wahakikishe wahusika wakimatwa wasihukumiwe kifo chapchap. Waachwe; kwanza wasote lupango ili ndugu zao wawaletee habari chafu na chungu za washirika zao wa bedroom kuwa na washikaji wapya wa kuwadoadoa. Kwanini wasipate habari chafu wakati wao wameumiza walevi wengi kwa kuhomola njuluku zao?  Lazima hapa wafanyiwe kama akina Hasi Kitiliya, Sirori na Sinari. Unadhani washirika zao huko nje wako salama?  Bahati yao, niko mbali nao, nami ningetia timu kuwabugulia mali zao kama walivyobungua mali zetu. Tena, nilivyokuwa mnoma, usishangae wengine nengewaachia mbegu za walevi kwenye uzao wao ili wanikumbuke milele. Japo si vizuri kumuombea mja maafa, wahanga wa ushenzi huu wanaomba hawa jamaa wanyotoke roho haraka kama lile jambazi la Banki Kuu lililozikwa hivi karibuni kule Moro. Siku hiyo walevi tulikunywa na kuvuta kama hatuna akili nzuri.
Katika kuhakikisha njuluku za walevi hazipotei, napanga kumshauri Makufuli akamate mali za wahusika haraka kabla hazijatobolewa tobolewa na washirika wao. Pia, ahakikishe yule aliyeuza kiwanja kwa mabilioni haya naye anaunganishwa haraka kabla hajatorokea ughaibuni kama ilivyo fasheni ya baadhi ya washirika wa jinai hii hasa wenye uraia wa kaya nyingi.
Pia nitamshauri Dk Kanywaji kuchunguza gharama za ujenzi wa Daraja la Mzee Mchonga pale Kigamboni. Maana, kama wezi hawa wameweza kupaisha bei ya kiwanja, hilo daraja itakuwaje? Kwanza, mwenzenu nilishaapa kuwa sitakaa nipite kwenye daraja hilo kuelekea Mji Mwema. Kwa vile hii ni kaya ya kitu kikubwa na kidogo, nina wasi wasi limejengwa chini ya kiwango kama mighorofa mingi ya Bongo inayongoja kunyotoa walevi roho kama ule wa Uhindini.
Ama kweli Njaa Kaya alijua kututenda! Ajabu eti bado anakingiwa kifua. Achia rungu la ukiti utumbuliwe na wenzako. We ngojeni. Hawa wa NSSF walie tu. Lazima walipe;maana kula na kulipa ndiyo mwendo wa usawa huu.
Chanzo: Nipashe Jumamosi

Je uraia wa nchi mbili ni kwa wageni tu Tanzania?

$
0
0

Japo watanzania wamekuwa na mawazo na misimamo tofauti kuhusiana na uraia wa nchi mbili, kitu kimoja kiko Dhahiri; sheria ya Tanzania hairuhusu raia yoyote wa Tanzania kuwa na uraia wa nchi mbili. Rais Magufuli–sawa na watanzania wengine analijua au anapaswa kulijua hili–hivyo alichosema si kuteleza kwa ulimi wala utani. Hata hivyo–hivi karibuni katazo hili la kisheria lilionekana kuwa la kibaguzi–tokana na ukweli uliofichuliwa na rais John Pombe Magufuli. Akimkaribisha mgeni wake waziri mkuu wa India Narendra Modi aliyetembelea Tanzania hivi karibuni, rais Magufuli alikaririwa na vyombo vya habari akisema, “Amejisikia [Modi] raha sana; alivyoona anakaribishwa na wananchi wengi wa Tanzania ambao naamini katika wale waliomkaribisha wengine ni miongoni mwao waliompigia kura kwenye jimbo lake.” Maneno haya yanajifafanua hasa ikizingatiwa kuwa kwanza, Modi si mtanzania–ni mhindi tena kiongozi wa nchi–hivyo, kwa sheria ya Tanzania, hawezi kuwa na wapiga kura. Pili, kwa mujibu wa rais, Modi–pamoja na sheria za Tanzania kukataza–anajua kuwa ana wapiga kura nchini hata kama ni kinyume cha sheria. Tokana na ithibati ya rais wetu ambaye mara nyingi amekaririwa akieleza wazi anavyochukia unafiki na uongo, aliyosema ni ya kweli tupu na si unafiki wala kufurahisha genge. Pia, tokana na ukweli huu na uzoefu wa watanzania walio wengi hasa wa mijini, unaweza kujenga mahitimisho na kugundua ni kwanini:
Kwanza, wengi wa mafisadi wakubwa wanaoshirikiana na mafisadi wakubwa wazawa serikalini ni wahindi.
Pili, wahindi wamekuwa wakiwabagua waafrika kwa miaka yote waliyokaa Tanzania bila kushughulikiwa kwa vile wana haki zaidi ya wazawa.  Hatutaki kutoa madai bila kutoa ushahidi. Kwa miaka zaidi ya mia waliyokaa Tanzania, nionyeshe ndoa hata tatu baina ya waswahili na wahindi nitaondoa hoja hii na kuomba msamaha. Najua ukweli huu ni mchungu. Lazima usemwe ili tuweze kusonga mbele kama taifa baada ya kujisuta na kusutana kama watanzania bila kujali rangi ya ngozi zetu. Isitoshe mie si wa kwanza kuliona hili. Marehemu Christopher Mtikila aliliona na kuliongelea sana na kwa undani bila woga wala unafiki. Nanachofanya hapa ni kukumbusha tu ili kuondoa kuendelea jinai ya ubaguzi.
Tatu, waziri mmoja wa uchumi wa zamani aliwahi kusema kuwa uchumi wa Tanzania ulikuwa–kipindi fulani–unashikiliwa na wahindi kumi tu. Hili ni kweli. Kwanza, wahusika hawakukanusha na ukweli unaonyesha hivyo.
Nne, matajiri wengi nchini ni wahindi hasa ukiangalia uwiano wa idadi ya watu. Kama hii haitoshi, wengi wa matajiri hawa wanaishi kwenye nyumba za msajili wa majumba kwa bei nafuu wakati wana mahekalu yao wakiyapangisha kwa dola au wana uwezo wa kujenga majumba yao wenyewe.
Tano, Tanzania imeruhusu jamii hii kuwa na shule, dini, na shughuli nyingine za kibaguzi za jamii moja ukiachia mbali kubariki mfumo wao wa kikaburu wa kitabaka (caste system) ambao licha ya kuwa wa kibaguzi ni kinyume cha sheria na haki za binadamu.
Sita, rais alisema kuwa Bunge la Tanzania lina wabunge kumi wenye asili ya kihindi, jamii ambayo hivi karibuni imesifika kwenye vyombo vya kimataifa kwa kuwabagua waafrika ikiwaita nyani au absii, bander au kalu. Rejea kupigwa na kudhalilishwa vibaya kwa mwanafunzi wa kitanzania nchini aliyekuwa akisoma kwenye Chuo Kikuu cha Acharya, Bangalore, India hivi karibuni baada ya msudani mmoja kusababisha ajali ya barabarani bila kutaja mwanafunzi toka DRC Masunda Kitada Oliver aliyeuawa May kwa kugombea Bajaj.
Kweli usilojua ni usiku wa kiza. Sijui kama waswahili wangekuwa huko ugabacholini wangepewa hata ujumbe wa nyumba kumi chini ya mfumo wa kikaburu wa caste system. Ni bahati mbaya kuwa waswahili walifundishwa kujikana na kuwapapatikia wageni kiasi cha kuwa na methali isemayo mgeni karibu mwenyeji apone kuonyesha utegemezi na kutojiamini kwao. Walevi wana shaka na huu ushuhuba wa ajabu ajabu ambao haulengi kutatua matatizo kama vile utoroshaji raslimali zao, ubaguzi wa moja kwa moja tena wa muda mrefu na madudu mengine mengi ambayo tawala karibia zote zimekuwa zijifanya haziyaoni. Wenzetu husema charity begins at home, au hisani huanzia nyumbani.
Tumalizie hapa kwa kumtaka rais Magufuli na serikali yake ima kuruhusu uraia pacha au kuupiga marufuku kwa watanzania wote badala ya kubagua hata kusifia ubaguzi huu. Sheria ni msumemo kama ambavyo rais Magufuli hupenda kusema; haipaswi kubagua wala kupendelea, kutumika kibaguzi au kuwa utashi wa mtu, kikundi cha watu wala taasisi bali utashi wa sheria. Ni aibu kugundua kuwa taifa huru linaweza kuwanyima raia wake wazalendo na kuwaruhusu raia wa kigeni wautumie kuliibia. Je yote haya yanafanyika hivi kwa faida ya nani? Sijui kama India inaweza kuruhusu ujinga kama huu tena kwa waafrika ambao wanasifika kwa wanavyobaguliwa nchini India hata kwenye bara lao wenyewe kutokana na kuwa na uongozi wa kifisadi na usiojithamin kukosa uzalendo na kujiamini.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Happy Birthday Nkwazi Mhango Jr.

$
0
0


Jana ilikuwa siku ya kuzaliwa kwa kitindamimba wetu Nkwazi Mhango Jr katikati. Alitimiza miaka minne jana akiwa anajiandaa kuanza Kindergarten mwakani inshallah. Junior alijumuika na dada zake na kaka yake pamoja nasi. Zawadi yake kwa siku hiyo ilikuwa kumrusha kwa ndege kwa saa moja jambo ambalo huwa analipenda sana.

Kijiwe chalaani Mrema kudhalilisha wanawake

$
0
0
 
Baada ya Agust Lyatongolwa Mremavu kuwadhalilisha wanawake akiwamo washirika wa bedroom wa wazee wa Kijiwe, tumeamua kulaani uchumia tumbo na udhalilishaji huu kwa herufi kubwa. 
Sofia Lion aka Kanungaembe ndiye anayeangusha mada leo. Akiwa amechukia kweli kweli anakula mic, “Jamani mmemsikia huyu njaa kali Mremavu alivyotudhalilisha wanawake wote tena akianza na bi mkubwa wake? Sijui mnashauri tumfanye nini gendaeka huyu mwenye uchu wa fisi mwenye kuweza kujivua nguo hadharani bila hata chembe ya aibu?” 
Mbwamwitu anamchomekea Sofia, “Twende tukamfanyia kitu mbaya na kuhakikisha uteuzi wake unatenguliwa huku naye akitumbuliwa jipu lake la muda mrefu. Huu si wakati wa kuhongana ulaji kwa vile waramba makalio wanamwaga na kuimba sifa kwa munene.” 
Mipawa naye hataki kuachwa nyuma. Anakula mic, “Jamani njaa nyingine bwana, yaani baba zima linajivua nguo hadharani hata kwa kumtusi mama yake mzazi bila chembe ya aibu wala utu ili lipewe tonge na watu wazima wanalinyamazia ukiachia mbali kulishangilia! Huyu hawezi kuwa mpinzani wala kiongozi wa kweli bali msakatonge wa kawaida tu; anayepaswa kuogopwa kama ukoma.” 
Mpemba naye anaangusha hoja, “Yakhe mie hata sikuamini masikio yangu wallahi. Nilisikia ankata kiasi cha kutaka niende ninsake na kuntia adabu mjalaana huyu wallahi. Ajabu ya maajabu, hata hao wanawake waloshuhudia na kusikia mauzauza haya tena vigogo kama dada yangu Sulhu hawakuchukia wala kukemea. Hii, kwao, ni ajabu na aibu. Jamani twendaapi? Ukisikia kuliwa wajiona asemako siku zote Mbwamwitu ndo huku.” 
Mzee Maneno anakula mic, “We unaongelea kukemea wakati walikuwa wakikenua utadhani walikuwa wamemwagiwa sifa. Hata hivyo, tuwe wakweli. Kama wanaume wenyewe tena marahis walinywea na kushabikia jinai hii, ulitegemea wanawake wafanye nini zaidi ya kujiunga na mkumbo wa udhalilishaji? Hivi hamjagundua kuwa katika kaya yetu siku hizi msemaji ni mmoja tu yaani Dokta Kanywaji ambaye watani zake wanaanza kumwita imla? Kama hamjui, kudhalilishana ni sera ya jamaa hawa ambao ukipingana nao lazima wakudhalilishe kama walivyomtumia huyu Mremavu njaa kali ambaye hana tofauti na Don Trump wa kwa Joji Kichaka.” 
Msomi Mkatatamaa naye anakula mic mapema, “Mie sikushangaa na wala sishangai hasa nikizingatia kuwa Mremavu–kwa tunaomjua–hana sifa hata chembe hata ya kuwa mjumbe wa nyumba kumikumi achilia mbali nafasi aliyozawadiwa kwa kujivua nguo na kujikomba.” 
Anaweka simu yake mezani na kuendelea, “Hakuna kilichoniacha hoi kama jamaa huyu kuhoji urume wa wenzake wakati yeye kishawekwa rumenya na Chama Cha Magamba (CCM). Kusema ukweli, hakuna niliyemshangaa na ambaye nitaendelea kumshangaa si mwingine bali daktari mwenzangu Kanywaji aliyeingizwa mkenge na msakatonge huyu kama alivyomeuelezea vizuri Ami pale. Rahis alipaswa kusema wazi wazi kuwa maneno ya Mremavu si msimamo wake, serikali yake wala chama chake. Hata MC wa mkutano ule anaonekana kuwa kilaza ambaye anapaswa kutumbuliwa. Alishindwa nini kusema kuwa maoni ya Mremavu ni yake binafsi hata kwa kuchomekea au kuchombeza?” 
Kanji anamchomekea Msomi, “Somi vacha mimi chomekee veve leo dugu yangu. Mimi hapana shangaa. Kama Jaa Kaya napeleka yeye Bombei tibiwa zani iko veza sema baya chama ile? Swahili iko sema adui yako veve ombea jaa. Hii Rema ongea kwa tumboni badala ya bongo. Veve sikiliza yeye taona point mimi nasema.” 
Mipawa anakatua mic, “Jamani wala mshingae.  Kwani hamkujua kuwa sera ya jamaa wa nambari wani ni kudhalilisha wanawake na vijana ambao siku hizi Dokta Kanywaji ameanza kuwakumbuka? Angalia hizo jumuia zao zinavyotumiwa kuwafunga kamba kuwa nao wamo wakati wanatumiwa kupitisha warume wahomole kwenye ulaji wa juu. Hivyo, usitegemee wanawake wajitete wakati wameishaona kama udhalilishaji ni sehemu ya maisha kama ilivyo ufisadi.” 
“Pamoja na kwamba hakuwadhalilisha washirika zetu wa bedroom, msimsahau mzee Mapesa wa zamani aliyeishia kufilisika kulhali baada ya CCM kumpeleka Ugabacholini kutibiwa kiasi cha kujitoa mwili na roho kama alivyoonyesha kwa maneno yake mwenyewe. Naye alisarura kweli kweli japo kwa kituo. Tofauti ya wawili hawa ni kwamba mmoja alitetea njaa yake bila kuwatukana wala kuwadhalilisha wengine.” Anachomekea Kapende huku akibwia kahawa yake. 
Mgosi Machungi aliyekuwa kimya muda mrefu anakula mic, “Huyu meku ana laana ya mama yake. Hamkusikia aivyomvua mama yake nguo akisema eti aikuwa akizia hovyo hovyo? Hamkuona aivyojivua nguo kwa kuamba matapishi yake akiisifia magamba kwa vile aipewa ulaji wa dezo hivi karibuni ukiachia mbai kupeekwa ugabachoini kutibiwa? Ashindwe na aendee kunyong’onyea. Anadhani njaa yake itaisha kwa nafasi aiyopewa? Ikiisha sijui atafanya nini wakati ameamua kujiacha uchi bia kujua kuna kesho?” 
Anapiga chafya na kuendelea, “Kwa mia zetu wagosi, mwanaume huwa hawezi kumsifia mwanaume mwenzie isipokuwa mwanamke na mwanamke kadhaika tokana na sababu za kimaumbie. Ajabu huyu Muemavu alihoji uanaume wa wenzie wakati yeye aikua akitoa mipasho na sifa za kike. Ama kwei nyani haoni kundue!” 

Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita Lyatongolwa! Acha tummwagie kahawa!
Chanzo: Tanzania Jumatano.

Mlevi ahudhuria mkutano wa Democrat

$
0
0
Baada ya kuboreka na siasa za maji taka pale Idodomya ambapo Chama Cha Magamba (CCM) kilijivua nguo kwa kuruhusu akina Trump uchwara (yule mgombea wa Republican anayesifika kuwadhalilisha na kuwachukia akina mama), kujichafua, niliamua kupanda pipa kwenda zangu kwa Joji Kichaka nilipoalikwa na chama cha Democrat kuwapa ushauri juu ya kushinda uchaguzi. Pamoja na kuwa nilishatia timu Idodomya, baada ya kugundua zengwe na matusi ya akina Trump Mremavu, niliamua kwenda zangu majuu lau kupoza hasira zangu ukiachilia mbali kuunyaka ujiko.
Nilitia timu jijini Philadelphia baada ya kuwa kwenye pipa yapata kama masaa 23. Washirika zangu Hilarious Hill na Bill Kliton kunikaribisha uwanja wa ndeg. Nilikwenda moja kwa moja mkutanoni kumwaga pwenti. Tofauti na akina Trump wa Bongo aka Agust Lyatongolwa Mremavu, mwenzenu nilimpamba mwana mama Hillary badala ya kumponda kwa woga na ujinga wa kizamani.
Katika kukaa kwangu kwa Joji Kichaka na kula pizza na chicken burger na madude mengine matamu, niligundua kuwa wenzetu wademocrat wanaheshimu haki za binadamu. Wanamthamini binadamu kama alivyo bila kujali jinsia yake kama akina Trump na Trump uchwara wa bongo. Nikiwa kwenye ule mkutano niliwakumbusha wenzetu kuogopa wanasiasa wanaotumia ujinsia kutafuta madaraka na ulaji. Hawa wameshindwa na washindwe na kunyong’onyea kama Mremavu ambaye amegeuka kokoro linaloweza kuzoa chochote kijacho kwake hata kama ni uchafu.
Kitu kingine nilichojifunza ni namna wana mama wa kwa Joji Kichaka walivyo na mwamko. Trump alipowalinganisha na nguruwe walimlinganisha na nyoka mwenye sumu kali. Na ukiangalia hapa kuna mantiki–samahani ndugu zangu msiokamata kitimoto–nguruwe ana nafuu angalau analiwa na hana sumu. Je nyoka ana nini zaidi ya sumu na kutoliwa? Hivyo, Trump yoyote awe mweusi au mweupe mbongo au Mjoji Kichaka ajue thamani yake.
Kwa taarifa yenu, kama siyo kuzuiliwa na Bill, nilitaka niende zangu New York na kumfanyia kitu mbaya mpuuzi huyu mbaguzi wa wanawake, waislam, walatino, waarabu, waswahili na kila yeyote asiyekubali upuuzi wake. Eti siku zote anasema yeye ndiye anaweza kuirekebisha Marikani tena peke yake wakati biashara zake zenyewe ni mazabe matupu.
Tukirejea kwa akina Trump Mremavu, hawa wanapaswa si kukemewa tu bali kunyang’anywa ulaji na kufunguliwa mashtaka ya uhaini ambao unatokana na kuvunja katiba ya walevi.
Hakuna kitu kiliniudhi nusu nimalizie uhai wa mgonjwa Mremavu kama kuwashuku wenzake kuwa si warume kwa vile walimkimbia na kumzilia Mjengo Tulia asiyetulia. Yeye ana urume gani wakati anawasifia warume wenzake wakati kimili wanawake ndiyo wanapaswa kuwasifia wanaume na wanaume kuwasifia wanawake kutokana na sababu zinazojulikana. Mremavu aliwashangaa wenzake kususa kama wanawake bila kujishangaa yeye na uroho wake wa fisi wa kupwakia kila kijacho kwake kama mtondoo au kokoro.
Kwa Mremavu Trump kuwa mwanaume lazima uwashambulie wanawake. Ukisikia woga na kutokuwa mwanaume wa kweli ndiyo huku. Mwanaume wa kweli hawabugui wala kuwadhalilisha wanawake. Badala yake, mrume wa kweli hulinda na kutetea haki za wanawake.
Hata hivyo, sikumshangaa Mremavu tokana na njaa na usaka tonge vilivyokuwa vikimsuka kujivua nguo hadharani. Kama amemtusi mama yake, wengine kweli atawaacha? Ama kweli adui yako muombee njaa! Nani alidhani kuwa baba zima lingesimama hadharani na kusarura kama kichanga ili kuganga njaa?
Nimalizie kwa kuwaonya akina Trump Mremavu na CCM kuwa wasipoomba msamaha kwa washirika zetu wa bedroom na maza zetu tunawafanyia kitu mbaya.
Chanzo: Nipashe Jumamosi.

Hapa Maguli nakupa ushauri wako mwenyewe

$
0
0
  Hivi karibunivyombo vya habari vilimkariri rais John Pombe Magufuli akiwashauri makamanda wa polisi waache tamaa ya kuwakatisha tamaa polisi wa chini yao hasa wanapokamata magari ya wakubwa. Alisema, “Hata akikamata gari la IGP, hata akimata gari la rais asikatishwe tamaa.” Huu ni ushauri mzuri unaolenga kutenda haki kwa watanzania kwa kuzingatia sheria badala ya kujuana, ukubwa na mambo mengine ya kihalifu kama ilivyokuwa huko nyuma. Hapa rais lazima aonyeshe mfano na kufanya mabadiliko ya kiutandaji katika serikali yake. Pia Magufuli anapaswa kutojitoa kwenye ushauri huu; kwani naye ni kiongozi wa umma ambaye baadhi ya matamshi yake yameishaonyesha kuwakatisha tamaa walio chini yake.
Pamoja na uzuri wa ushauri wake kwa makamanda wa polisi, waswahili husema; ukimnyoshea mtu kidogo, vinne vinakuelekea wewe. Magufuli aliliona la wakubwa kuwakatisha tamaa wadogo ili kulinda uovu wa wenzao. Ni bahati mbaya kuwa hakuona upande wake kama kiongozi wa nchi ambaye matamko yake ya hivi karibuni kuwa viongozi wastaafu wanaotuhumiwa kuhujumu nchi watalindwa. Je hakikisho hili linatoa picha na ujumbe gani kwa mamlaka zinazoshughulikia ufisadi kama vile Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU). Je ikitokea TAKUKURU au jeshi la polisi wakagundua ufisadi wa viongozi wastaafu, wake au watoto na marafiki zao wataweza kuwashughulikia wakati bosi wao ameishatoa msimamo wake? Je huku si kuwakatisha tamaa hata polisi hao hao sawa na wale aliokuwa akiwaasa kuaacha kukatisha tamaa wa chini yao? Je baada ya Magufuli kutoa hakikisho husika, ni polisi gani awe mkubwa au mdogo anaweza kuwashughulikia wastaafu ambao wengi wao wanakabiliwa na tuhuma lukuki za kuhujumu taifa? Rejea malalamiko ya Magufuli mwenyewe kuwa nchi ilikuwa inaliwa kiasi cha kugeuka chaka la majambazi. Mifano iko mingi. Angalia wafanyakazi hewa, nchi kuingiza mafuta kwa miaka mitano bila kuwa na mita na mengine mengi ambayo hao anaowahakikisha ulinzi waliyatenda kiasi cha taifa letu kulegalega kisiasa na kiuchumi. Rejea kuumka kwa deni la taifa bila maelezo yanayoingia akilini.
 Ili kumsaidia Magufuli–kama alivyowaasa makamnda wakuu wa polisi–nasi tunamuasa kama mkuu wa nchi; asiangalie huyu ni rafiki yangu, huyu ni rais mstaafu au nini bali awakamate pale wanapotuhumiwa kuvunja sheria. Na rais hana uwezo wa kuwakamata wahusika bila kutumia jeshi la polisi na taasisi nyingine kuwachunguza kuona kama tuhuma zinazowakabili ni za kweli au la. Maana, kutowashughulikia wahusika–licha ya kuwakatisha tamaa wananchi ambao ni wahanga wa jinai waliyotenda hawa na kuwapa kiburi wahusika–ni kuonyesha mfano mbaya kuwa sheria za nchi zinatumika kibaguzi na kiupendeleo kwa kuangalia cheo na hadhi ya mtu. Kama alivyowaambia makamanda wa polisi naye aambiwe “Hata akiwa mke wa rais, tumbua; hata akiwa rais mstaafu tumbua tu.” Huu ndiyo uongozi bora na wa sheria. Kama Magufuli hatabadili msimamo wake kuhusiana na wastaafu waliovurunda basi aache kulalamika kuwa yote anayofanya yametokana na serikali zilizopita. Ajinyamazie na kufanya anapoweza na akishindwa ajinyamazie vile vile badala ya kujichanganya.
Wahenga walisema kuwa hisani huanzi nyumbani. Haiwezekani Magufuli awe na uchunguna askari wadogo wanaokatishwa tamaa na wakubwa zao wakati naye anatenda dhambi hiyo hiyo anayowatuhumu wenzake. Mpaka tunapoandika, kuna dalili kuwa tabia ya kukatisha tamaa bado haijatafutiwa dawa.  Itatafutiwa dawa mujarabu pale maafisa wote wa umma wakubwa na wadogo watawajibika kama tunavyomtaka Magufuli awajibike kwa kutowakatisha tamaa walioko chini yake wala wananchi. Huwezi kusema kwa mfano, rais Mstaafu Benjamin Mkapa anayetuhumiwa kujitwalia Machimbo ya Makaa ya Mawe ya Kiwira yeye na familia na marafiki zake kinyume cha sheria kuwa asiguswe ukawa hujawakatisha tamaa wananchi na walioko chini yako. Huwezi kusema mfano rais mstaafu Jakaya Kikwete aliyeruhusu wizi wa Escrow, kufungwa mita ya mafuta, utwaliwaji wa UDA, matumizi ya fedha za umma, kuzurura ughaibuni na kuridhia uwepo wa wafanyakazi hewa asiguswe ukawa hujawakatisha umma tamaa. Huwezi kusema kuwa kashfa ya Loliondo inayomkabili rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi asiguswe wakati ana kashfa inayomkabili.
Nadhani ingefaa kama rais ataanzisha mchakato wa kushitakiana na kuitana na kuombana msamaha ili viongozi wastaafu wasamehewe kuliko kuahidiwa ulinzi dhidi ya makosa ya kifisadi na uhujumu wa taifa. Inashangaza kusikia kuwa imeanzishwa mahakama ya mafisadi wakati wakubwa wanaotuhumiwa kufanya ufisadi wakikingiwa kifua na rais. Huu unaweza kuleta hisia za ubaguzi katika matumizi ya sheria.
Tumalizie kwa kumpa rais Magufuli ushauri wake mwenyewe kuwa katika kushughulikia makosa ya jinai kusiwepo na kuangalia ukubwa, uwenzetu, uzee wangu na mambo mengine zaidi ya sheria kama sheria.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Kijiwe chakumbushia Escrew, Lingumi na UDA

$
0
0
Image result for lugumi
          










Baada ya kufumka kashfa funga kazi kwenye utwahuti sorry utawala uliopita baadhi zikwa ni Escrew, Lingumi na UDA, na kunyamaziwa, wengi walidhani ujio wa dokta Kanywaji Joni Makufuli kungefanya mambo tofauti na upuuzi uliopita. Kadri siku zinavyozidi kuyoyoma na wachovu kusahaulishwa, kuna kashfa zinaonekana kuanza kuminywa kinamna kama siyo kufichwa ili wachovu wasahau kabisa waendelee na madili.
Mgosi Machungi aliyerejea hivi kaibuni kutoka Ushoto ndiye analianzisha. Anasema huku akiwa ameshikila kichwa kwa huzuni, “Mwenzenu pamoja na kuwaetea saamu toka kwa wagosi, kuna kitu kimoja kiinitia aibu kwei kwei.”
Kabla ya kuendelea, Mbwamwitu anamchomekea, “Ulifumaniwa nini?”
“Wewe Mbwamwitu acha utani. Unazani Ushoto kuna kufumaniana au kupigana zongo? Usidhani kue mambo yanafanyika Kizaramizi kama hapa ndugu yangu. Kiichonitia aibu ni kugundua kuwa watu wa vijijini wanajua mambo mengi ya maana kwa kaya kuiko sisi wa mjini,” anajibu Mgosi
Kabla ya kuendelea, Mipawa anamchomekea tena, “Una maanisha nini mbona hueleweki Mgosi? Eti washamba wa kwenu wanajua mambo mengi kuliko sisi watoto wa mjini siyo? Ya kweli hayo Mgosi?”
“Usiwe na haaka utanieewa tu. Je wajua kuwa niipofika kue kia mmoja aikuwa akiniiuizia uipofikia uchunguzi wa kufunga hata kunyonga majambazi ya kashfa za Eskow, Ingumi na UDA? Kusema ukwei sikuweza kupata jibu hasa ikizingatiwa kuwa wengi tiishasahau kashfa hizi. Sijui hata kama Dokta Kanywaji anazikumbuka,” anajitetea Mgosi.
“Kama hii ndiyo mada yako, Mgosi hapa una mashiko. Kuna ukweli japo si wote kwenye mada yako kuwa watu wa mjini wakati mwingine ni wasahaulifu kuliko wa vijijini kutokana na kuwa na unafuu wa maisha. Tunaumeme wa kumwaga siku hizi baada ya kuingia dokta Kanywaji. Wengine wanafaidi maji yaliyokuwa yameadimika miaka mingi kiasi cha kuwa bize na wengine kuridhika wasijue mapambano ya haki ni suala la kudumu na kufa na kupona,” anasema Msomi Mkatatamaa huku akibwia kahawa yake.
Msomi anaendelea, “Ni jambo la kushangaza na la kweli kuwa majipu uliyotaja yanaonekana kuanza kumshinda daktari wa majipu. Sijui kuna wanene zaidi nyuma ya majipu haya hasa wale aliowaahidi ulinzi kwenye madhambi yao au ni woga tu.”
Kanji anadakia na kusema, “Veve hapana iko saka dugu yangu. Rahis nasema takamata fisadi vote na funga. Patia yeye nafasi tafunga tu. Pia mimi ona rahis hapana veza kamata fisadi vote. Sasa kama fisadi ile kuba nakula na fisadi kubakuba ya siasa, ikotegeme veve funga yeye?”
Kapende anamuunga mkono Kanji, “Kanji nakubaliana nawe hasa ikizingatiwa kuwa ufisadi kayani haufanywi na watu wasio na ushirikiano na wakubwa. Ima ni ndugu, wake, zao au wao wenyewe kama si wateule wao. Tukizingatia kuwa kashfa tajwa hapo juu ziligusa wakubwa wengi tokana na utawala wa wakati ule wa kujihudumia, sidhani kama zitaguswa.”
Mpemba aliyekuwa kimya muda mrefu anakula mic, “Ami usemayo ni ya kweli tupu. Kama wale walobainika kuwekewa mabilioni kwenye akauti zao bado wamo bungeni wategemea huyu Kanywaji awafanye nini? Huoni akina Joni Chenga, Profwedheha Ana Kajuamlo, Ngeleza na wengine wanaendelea kutesa mjengoni?”
Sofia Lion aka Kanungaembe, “Hata nami ami hapa kanishawishi,” kabla ya kuendelea Mbwamwitu anachomekea, “amekushawishi vipi na ili iweje?”
Da Sofia hajibu; anaendelea, “Nikiangalia UDA yenyewe ilivyotolewa kama zawadi kwa wezi wale wale waliobainika kuitwaa kinyume cha sheria eti kwa kisingizio kuwa hakuna mzalendo mwenye uwezo wa kuendesha miradi mikubwa. Kwani kinachotakiwa hapa ni kufanya biashara yenye faida au kupeana ulaji kizawa? Mzawa mgeni na yeyote kama ni fisadi ni fisadi tu.”
Mipawa anakula mic tena, “Kaya hii kwa ufisadi mimi sina hamu. Umesikia juzi waliotumbuliwa baada ya kupenyeza watu wao kwenye msafara wa marubani ulioendea ndege mpya kule Kanada? Yaani watu hawamwogopi dokta Kanywaji! Ndege zenyewe hazijatua mmeishaanza kuzifanyia kitu mbaya kama mlichoifanyia Air Tanzia siyo?”
“Hata hii imenishangaza. Huu ni ushahidi na motisha kwa dokta Kanywaji kuwa kazi iliyoko mbele yake ni pevu kweli kweli. Kwani, wengi waliomzunguka ni wale wale walioifikisha kaya hapa. Hivyo, changamoto kama hizi zinapaswa kumfumbua macho kujua kuwa wengi wa mafisadi anaopaswa kuwatumbua wamo nyumbani mwake,” anaongezea Msomi Mkatatamaa.
“Tena Msomi umenikumbusha. Nilisoma mahali kuwa kuna mpango wa kuwatumbua vilaza na vihiyo. Hata hivyo, nina shaka sawa na ilivyo kwa kashfa kama hizi tajwa. Kwani nikiangalia vilaza kama Bill Lukuuvii bado vimo kwenye sirikali ya dokta Kanywaji. Je ina maana hajui kuwa huyu jamaa ni jipu na kihiyo ambaye alitajwa kwenye kitabu cha mafwisadi wa elimu au ameendekeza urafiki na kujuana kama si kufanya utumbuaji kibaguzi?” analalamika Kapende huku akiweka kamera yake vizuri mezani.
Kijiwe kilipokuwa kinanoga si wakapita majambazi wa Lingumi, UdA na Escrew wakitoka kwenye kikao cha kumzidi kete dokta Kanywaji. Acha tuwatoe mkuku ili kuwakamata na kuwafanyia kitu mbaya hadi wake zao waapige karata baada ya kujua hiyo kitu.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.

Ujaji tusitangaze ajira bali kutumbua hata waliopo

$
0
0

 
            Hivi karibuni mahakama imetangaza kuwa sasa kazi za ujaji zitakuwa zikiombwa kama kazi nyingine ili kuepuka kuendelea na mfumo na utamaduni wa kizamani ambao ulijaza majaji vihiyo na wenye mafungamano kisiasa kiasi cha kuinyima mahakama hadhi inayopaswa kuwa nayo kama taasisi ya umma na mhilimi mmojawapo wa dola.
Kwanza, tunapongeza hatua hii ambayo bila shaka italeta mapinduzi na maendeleo makubwa katika utoaji haki nchini.
Pili, tungeshauri hata upatikanaji wa jaji mkuu utumie utaratibu huu kama ilivyo nchini Kenya na Afrika Kusini. Kwanini rais apatikane kwa uchaguzi lakini jaji mkuu apatikane kwa uteuzi?
Tatu, tunashauri mahakama isianzie hapa; bali irudi nyuma na kuhakikisha majaji vihiyo na wenye kutumiwa kisiasa au kwa namna yoyote wanaondolewa ofisini ili kutenda haki na haki ikaonekana inatendeka. Kwani, wa vihiyo ambao sifa zao hazilingani na kazi na mamlaka waliyopewa.
Nne, wa majaji wanaojulikana kuwa uteuzi wao licha ya kutia shaka na kudhalilisha mahakama na mamlaka zilizofanya uteuzi huu na taifa kwa ujumla, unajulikana ulivyosukumwa na kujuana kwao na mamlaka zilizowateua.
Tano, wapo majaji ambao kuna ushahidi kuwa walishiriki vitendo vya kukiuka maadili, hivyo, kutofaa kuteuliwa kuwa majaji ingawa waliteuliwa kutokana na utawala mbovu uliopita kuangalia maslahi binafsi badala ya taifa.
Kwa wale wanaotaka kubaini majaji vihiyo na mabomu wanaopaswa kutumbuliwa kwa kuachishwa ujaji, warejee malalamiko yaliyowahi kutolewa na mwanasheria maarufu Tundu Lissu tena bungeni akidai kuwa baadhi ya majaji hawakuwa na sifa wala hawakupaswa kuteuliwa kwenye nafasi hizo hasa baada ya kubainika kutenda vitendo vinavyokiuka maadili kama vile rushwa na madhambi mengine. Kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima la Novemba 29, 2012, ulimkariri Lissu akisema, “Nilieleza jinsi rais alivyofanya uteuzi wa baadhi ya majaji pasipo kupata ushauri wa Tume ya Utumishi wa Mahakama. Wamekuwa wakijibu kiujumla, mimi niliwataja kwa majina yao na hata hili nilieleza katika Kamati ya Ngwilizi ambayo taarifa yake haikuwekwa hadharani pasipo sababu za kueleweka.”
 Lissu aliwataja majaji Mbaruku Salumu Mbaruku na Fatuma Masengi kama majaji waliteuliwa bila kuwa na sifa za kitaaluma kufanya kazi ya ujaji.
Wengine aliowataja Lissu ni majaji Latifa Mansoor anayedai alifukuzwa na manispaa ya Ilala kwa ubadhirifu na udanganyifu, Kassim Nyangarika aliyewahi kushinda kesi kutokana na urafiki wake na jaji na Zainab Muruke, Pelagia Khaday, Aloysius Mujulizi ambaye licha ya kutuhumiwa kupokea fedha ya Escrow inadaiwa alishiriki kuanzisha kampuni ya Deep Green Finance Co. Ltd iliyotuhumiwa kwa wizi mkubwa wa fedha za umma.
Je wapo majaji wengine ambao waliteuliwa na mamlaka za hovyo ambazo zilidharau au kutofuata vigezo zaidi ya kujuana au kusaidiana kama anavyodai Lissu kuwa kuna majaji waliteuliwa wakiwa wagonjwa mahututi ili waweze kusafirishwa nje kwa matibabu. Lissu anawataja hawa kuwa ni marehemu Jaji Kulwa Masaba na Jaji Madina Muro na majaji Stephen Ihema, Juxton Mlay, Augustine Shayo na Vincent Lyimo. Wengine ni Mwendwa Malecela ambaye hadi Lissu anatoa madai yake alikuwa hajawahi kutoa hukumu yoyote tokana na ugonjwa.
Madai ya Lissu yanazua maswali mengi kuliko majibu. Je inakuwaje mamlaka zinazopaswa kuheshimu na kutimiza sheria kama zilivyochaguliwa na kuapa kufanya vitu visivyoingia akilini mfano kuteua watu wasio na sifa kitaaluma au kusheria kuwa majaji? Je ni wangapi ambao hawajapigwa kurunzi? Je watu hawa wamelisababisha taifa na mahakama madhara makubwa kiasi gani? Je tuhuma za Lissu ni za uongo? Kama ni za uongo, kwanini hajawahi kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma? Kama tuhuma za Lissu ni za kweli–na kama zinavyoonyesha ni za kweli kutokana na kutokuwapo shauri mahakamani–watuhumiwa ambao hawajastaafu au kufariki wanangoja nini kwenye ofisi za umma wakati hawana sifa na wamepatikana kinyume cha sheria? Je hili nalo linangoja rais Dk John Pombe Magufuli au jaji mkuu–kama anasoma habari kama hizi–anaweza kuomba ushauri kwa rais na mamlaka nyingine husika na kuwawajibisha wahusika? Je watanzania wataendelea kuumizwa na watu wasio na sifa kwa kuwanyima haki hadi lini?
Leo hatutaandika mengi. Badala yake tunaomba tuishie hapa kwa kutaka watuhumiwa wote  wajiwajibishe au wawajibishwe mara moja ili kulinda na kurejesha imani na heshima ya mahakama; na wasipewe nafasi na kurejeshwa kazini kwa vile kazi ya ujaji inahitaji mtu asiyekabiliwa na tuhuma yeyote. Kama watahitaji kuheshimika kama raia na wana taaluma wengine ima waende mahakamani kujisafisha au wajiuzulu kabla ya kuwajbishwa. Kwani madai yanayowakabili–hata kama yalifutikwa chini ya busati kwa muda mrefu–ni mazito sana kwa ofisi ya jaji. Kwa habari zaidi wanaweza kutembelea kiunganishi hiki: http://sheriayako.blogspot.ca/2012/08/tundu-lissu-afichua-mengi-juu-ya-majaji.html
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Mlevi aanza kuhisi anaanza kulewa madaraka

$
0
0
Man And A Half
Baada ya walevi kufanya makosa kwa kunichagua kuwa kiongozi wao, walisahau kitu kimoja muhimu. Walisahau kuwa walevi–hasa wana politiki– huwa hatabiriki wala kuaminika. Sawa na mwana politiki yeyote, baada ya kukaa kwenye kitu cha utukufu–nikiwa nimesheheni utukufu wangu–najihisi kuanza kulewa–si kanywaji bali madaraka. Najihisi kama mimi si gendaeka tena bali muungu-mtu ambaye hakosei wala hapaswi kukosolewa. Katika kujitathmini, nimejikuta nikihisi kuwa mimi ndiye kijogoo pekee kwenye kaya ya walevi. Waliobaki wote ni tetea wanaopaswa kunisikiliza, kuniamini na kupokea amri toka kwangu, tena kwangu pekee. Hivyo, zaidi yangu, hakuna anayeruhusiwa kufikiria kuwika achilia mbali kuwika. Wika nikusikie na kukukata hicho kidole na ushungi vinavyokupa kiburi. Kwa wale ambao hawajapata wala kuelewa somo, tafadhalini, nawajulisha kuwa Danganyika ina jogoo moja tu linalopaswa na kuruhusiwa kuwika yaani mimi munene wa wanene na mkuu wa wakuu. Yeyote anayetaka kuwika angoje nipige miaka yangu kumi ndipo afanye hivyo. Hivyo, kwa usalama wa maisha na ulaji wake anapaswa kufanya kitu kimoja tu–kuramba makalio na viatu vyangu na kutenda nitakavyo vinginevyo atakoma na kukiona cha mtema kuni. Nani hajitaki huyu usawa huu wa kulewa madaraka? Najua wengi wanadhani wataniingiza mkenge kwa kucheza na kuimba nitakavyo wakati kimsingi wanatetea ulevi wao. Mie sijali, uwe  unafanya kweli au kuzuga, ilmradi unakubali kuwa mimi ndiye kijogoo pekee anayepaswa kuwika, sijali huo usanii na usaliti wako kwa roho yako.
Kama haitoshi–baada ya kulewa ulaji sana–najihisi kujua na kuweza kila kitu kwenye kaya ya wadanganyika na walevi. Hivyo, amri zanguhisia na mawazo yangu ni sheria zisizopaswa kupingwa wala kuhojiwa. Kuhakikisha hili linatimia bila kukwama, nimeamuru walevi wengine wanaojitiatia kunipinga–eti kwa kuwatetea walevi wengine ambao hata hivyo, ni wangu tokana na kuwa mkuu wa walevi wote bila kujali nani alinipa au kuninyima–wafunge mabakuli yao vinginevyo nitawatia adabu. Wanapaswa kufahamu kuwa mimi najua kila kitu; na lolote nipangalo, lazima litekelezwe bila kusuasua, kuhoji, kushuku wala kuuliza maswali. Walevi walizoeshwa kudekadeka na kujipayukia hovyo hovyo na watakavyo. Kwangu hili halikubaliki.  Anayepaswa kusikika ni mmoja yaani mimi mlevi mkuu mwenye mamlaka na ulaji wote mikononi mwangu na sirikali yangu. Hata chama changu kilichoingia mkenge kikanidhamini hakifui dafu hata nisingekuwa mkiti wake. Mimi ni Alpha na Omega, mwanzo na mwisho, mbele na nyuma, kulia na kushoto. Ukitaka uwe salama, sikiliza na zishike amri zangu vingenevyo unahatarisha maisha yako.
Kama alivyowahi kusema Dan son of Mwai Kibaka kule kwenye kaya ya Nyayo na nyang’au, “Chini ya mzee Jomo nilikuwa naimba kama kasuku. Sasa nimepata ulaji. Kwanini nanyi msiniimbie kama kasuku?” sasa nasema, “Hapa ni kuimba tu.” Na hii ni amri; siyo ombi. Kama wahenga wa Kirumi walivyosema “Roma Lucuta est, causa finita est” yaani kilichoamriwa Roma ni mwisho na hakina rufani. Kama bi nkubwa wa Ku-Tulia pale mjengoni, langu lazima lisikike na kutekelezwa bila kusuasua wala kuwazawaza. Hivyo, wale wote wanaoota mchana kudhani watapingana na mimi wajiandae. Kwanza, wajue mambo muhimu yafuatayo:
Mosi, mimi nina shahada ya uzamivu ya utawala na ubunifu PhD in Creativity and Leadership.
Pili, wafahamu kuwa kila ninachopanga na kusema ni sahihi na hakina shaka yoyote.
Tatu, waelewe huu si wakati wa siasa bali kutekeleza yale niliyojipangia kwa ajili ya walevi.
Nne, waelewe kuwa kwenye kuwania nafasi hii ya kiongozi wa walevi, niliwashinda hawa wanaojitiatia kunikosoa chini ya kisingizio cha domoghasia. Ninataka mambo muhimu matatu yaani:
Wacheze, wafikiri na kutenda nitakavyo. Lazima kila mmoja acheze ngoma niamuruyo na si ngoma yake. Japo unaweza kuuita huu ulevi uliopindukia, kimsingi, ni utawala uliotukuka na kujitenga na utukutu wa domoghasia na ghasia nyingine. Nataka kaya yetu ya walevi iwe Bongolalaland kweli kweli aka Danganyika ambapo hakuna atakayedanganya tena isipokuwa mimi msemakweli. Ninachopanga, kuamuru na kuwaza mimi ndicho kinachofaa; na huu ulaji nimepewa na Mungu kupitia wapika kura ya kula. Kwani, kuna ubaya gani kula hata ikibidi kuwala wote? Kwani, mimi ni wa kwanza au wa mwisho kwenye zama hizi za kuburuzana?
Kwa vile nafaidi ulevi wangu wa madaraka, natoa fursa kwa wote wanaosoma waraka huu ambao umevuviwa na Muumbaji mwenyewe watafakari na kuwa tayari kutekeleza niwaamuruyo na niwaambiayo. Huu ndiyo uhuru wa kutumia madaraka. Nisisikie mlevi yoyote akisema eti mimi ni imla au dikteta. Dikteta gani wa kuchaguliwa tena kwa kishindo? Kama asemavyo munene fulani, meseji sent and received. Hivyo, namalizia kwa kusema wazi kabisa kuwa huu ni wakati wangu wa kufanya vitu vyangu. Sitaki wapingaji wanijazie mbu. Nitawatumbu…we! Koma na ukomae.
Sitaki niseme mengi leo. Acha niwaage kwa kuwataarifu na kuwaonya kuwa atakayekaidi ujogoo wangu ajue ameumia. Siko tayari kuona walevi wakinikwamisha kwa kuhoji au kupinga maagizo, mawazo, mipango na ndoto zangu hata kama ni za kukurupuka au za mchana.
Inshara tuonane wiki rijaro. Ni mimi lais wenu ambaye nimefulahi kufikisha ujumbe wangu. Jitu Pande Makwelini aka JPM.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.

Kufungiwa Mseto ni vitisho na uonevu

$
0
0

            Kufungiwa kwa gazeti la kila wiki la Mseto tokana na kile kinachodaiwa kuandika habari za uchochezi, kuna kila sababu na ushahidi kuwa hatua hii–licha ya kulihujumu  gazeti na kutishia uhuru wa vyombo vya habari–imelenga kulikomoa na kulinyamazisha gazeti kama onyo kwa magazeti mengine yasiyolalia upande wa watawala.
Kwanza, inashangaza kuona Tanzania bado inatumia sheria ya kikale ya mwaka 1976 iliyotungwa wakati wa mfumo wa utawala wa chama kimoja
Pili, kuna mambo kadhaa yanayothibitisha kuwa uamuzi huu umefikiwa kwa hasira, visa au kutojua na kuheshimu haki za kikatiba. Kinachogomba sana ni suala lenyewe lililosababisha kufungiwa gazeti. Mbona magazeti mengine yameandika makubwa kuliko hili na hayakufungiwa bali kuamriwa yakanushe na kuomba msamaha? Rejea gazeti moja la kila wiki kuandika habari za ufisadi wa waziri mmoja mwanadamizi na kupotea kwa zana muhimu ya kivita kwenye taasisi moja nyeti bila kufungiwa? Je kuna sacred cows na black sheep hapa?
Tatu, tokana na ukandamizaji wa haki hizi za kikatiba za raia, kuna maswali kadhaa yanakosa majibu yaani:
Nne, kwanini kampuni moja kufungiwa magazeti mawili ndani ya kipindi kifupi kama hakuna namna? Kukosea kwenye taaluma yoyote ni jambo la kawaida. Linapotokea hili, mhusika hupewa fursa ya kujitetea au onyo; ndipo hatua zaidi hufuata. Kitendo cha kulifungia gazeti la Mseto tena bila kupewa haki ya kisheria ya kueleza upande wake ni dalili za watawala kutoa vitisho na kufanya udhalilishaji hasa kwa vyombo vya habari visivyolala kitanda kimoja nao.
Tano, kwanini waziri mhusika hakujua kuwa kufungia magazeti mawili tena ya kampuni moja ni kuwanyima fursa ya kufanya kazi waajiriwa wa magazeti husika, ukiachia mbali kuwanyima wananchi haki ya kupata na kutoa habari? wakati rais anahangaika kutengeneza ajira, waziri wake anaua hata zile ambazo zimeishatengenezwa na sekta binafsi! Rais wa kwanza wa Marekani George Washington aliwahi kusema, “Iwapo uhuru wa kujieleza utaondolewa, kwa ububu na kimya, tutapelekwa machinjioni kama kondoo.” Je nani takubali udhalilishaji huu?
Kimsingi, msingi mojawapo wa utawala bora na wa sheria, ni kuruhusu, kuvumilia na kuishi sambamba na uhuru wa kujieleza, kutoa na kupata habari. Sitaki niamini kuwa serikali yetu imefikia hapa. 
Sita, kwanini waziri hakuweka maanani kuwa mwandishi aliyeandika habari husika alipewa tip–hata kama baadaye ilibainika kuwa feki, kama inavyodaiwa–akiwa na lengo safi la kufichua uovu?       Saba, je hapa kosa ni nini iwapo mwandishi alitumia taarifa alizopata akiamini ni sahihi? Kisheria, huwa inaadhibiwa nia na si kitendo. Chini ya dhana ya mistake of fact, mtuhumiwa anapotenda kosa akiamini kuwa alichokuwa akifanya si kosa, hupunguziwa makali ya adhabu. Mfano, kama nikimpiga mtu risasi akiwa shambani mwangu nikiamini kuwa niliyempiga risasi ni nguruwe anayeshambulia mazao yangu, siwezi kushitakiwa na kupatikana na hatia ya kuua kwa kukusudia. Sambamba na nayaraka husika, serikali inajua fika kuwa habari za uchunguzi hutegemea tips na nyaraka. Hivyo, basi, kama mwandishi alijiridhisha kuwa nyaraka husika zilikuwa sahihi, waziri hakupaswa kufungia gazeti kwa miaka mitatu.
Isitoshe, hata serikali yenyewe imekuwa na waajiliwa wengi wenye vyeti feki iliowaajili ikiamini ni sahihi; na serikali yenyewe haijatimliwa madarakani kwa kuanjiri watu ilioamini wana sifa hata kama ikibainika kuwa hawakuwa na sifa. Hapa tunaangalia nia (spirit) ya kutenda kosa husika na si kosa. Kwenye makosa ya jinai kuna vitu viwili muhimu viitwavyo mens rea (nia ovu) na actus reus (tendo lililokatwaza kisheria). Katika kushughulikia kesi vitu hivi huangaliwa sana ili kuamua kama mhusika alitenda kosa analokabiliwa nalo kwa makusudi au bahati mbaya.
Nane, kitu kingine, makosa ya kiuhabarishaji yanapotokea, mhusika–licha ya kupewa fursa ya kujitetea, mara nyingi, huambiwa akanushe habari husika na kumuomba msamaha mhanga.
Tisa, kwanini waziri alikurupuka na kuchukua uamuzi mzito hivi ndani ya muda mfupi? Haiwezekani kosa litendeke tarehe 4 Agosti na hukumu ifuatie tarehe 11 Agosti yaani siku tatu baada ya kosa kutendeka–kama kweli lilitendeka.  Waziri alikuwa na haraka ya nini au alifanya maamuzi yake ima kwa chuki au kushinikizwa? Maana haiingii akilini kwa waziri –ambaye tunaamini amesoma barabara–kuchukua uamuzi kwa pupa na haraka hivi na haki ikatendeka. Hapa–kwa ushahidi wa mazingira (circumstantial evidence) ni kwamba waziri alishaamua kuadhibu gazeti bila kutoa muda wa kutosha kusikiliza upande wa pili. Waziri hakuvaa viatu vya mwandishi ndipo akaamua–angekuwa yeye angefanya nini–katika mazingira kama haya ambapo kupambana na ufisadi ni sehemu mojawapo ya malengo mahsusi ya serikali ya rais John Magufuli.
Kumi, sijui kama waziri alijiuliza maswali yafuatayo na kutoa haki kwa watuhimiwa kabla ya kufikia uamuzi wake:
a)      Je aliuita utawala wa gazeti na kuupa fursa ya kutosha ya kujitetea?
b)      Je aliotoa onyo au karipio kabla ya kufikia uamuzi wake?
c)      Je aliwaamuru wahusika kukanusha taarifa husika na kumwomba mhusika msamaha wakakataa?
d)      Je muda uliotumika kufikia hukumu ulikuwa unawatosha?
e)      Je Kama waziri alitoa haki hizo husika; kama alifanya hivyo, wahusika walitoa utetezi gani  na nini misingi ya waziri kukataa utetezi wenu na kutoa adhabu kali kiasi hicho?
f)       Je amewapa fursa ya kupinga uamuzi wake?
            Kimsingi, kuna maswali mengi hasa ikizingatiwa kuwa kisheria, hakuna anayepaswa kuhukumiwa bila kusikilizwa.
            Baada ya kupata habari za kufungiwa gazeti, niliwasiliana na mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya Halihalisi inayomilki gazeti husika Saed Kubenea aliyesema, “Barua ya Maelezo - Idara ya serikali - ilifika ofisini kwetu Jumatatu saa 10 jioni. Kumbuka hii ni siku ya mapumziko hapa Tanzania - Nane Nane. Ikataka tueleze kwa nini tumeandika hiyo stori inayomtaja ‘rais aliyepo madarakani.’ Basi. Tukajibu. Tuliekelezwa majibu yafike ofisini Maelezo kabla ya saa 3 asubuhi ya kesho yake.”
            Kwa uchache, hivyo ndivyo ilivyokuwa hali. Ni vema msomaji ambaye ni mdau wa habari na haki za kiraia za kikatiba ukasoma na kuamua mwenyewe.
            Mwisho, kwa ukiukwaji huu wa katiba, nashauri gazeti liende mahakamani kuitaka ibatilishe uamuzi huu wa ajabu.
Chanzo: Mwanahalisi leo.

Kijiwe chataka CCM irejeshe mali za umma

$
0
0

          Baada ya mwenyekiti mpya wa Chama Cha Makabaila (CCM) dokta Joni Kanywaji Makufuli kufichua kuwa kumbe CCM inamilki vitega uchumi zaidi ya 500 kayani, kijiwe kimeamua kumkabili kumwambia aitumbue CCM kwa kurejesha mali hizo ambazo nyingi ni viwanja  sirikalini.
Msomi Mkatatamaa ndiye analianzisha, “Jamani mmesikia hii mpya kuwa Chama Cha Makabaila kinamilki viwanja na vitega uchumi kayani kote?”
Kabla ya kuendelea, Mpemba anachomekea, “Japo nilikuwa najua kuwa ufisadi huu wa kunyakua umekuwapo kwa muda nrefu chini ya chama kimoja, sikujua kuwa kumbe walokuwa wakifaidi ni mafisadi na si chama hata kama nacho kina hatia ya kukwapua ardhi.”
Msomi anaendelea, “Nakubaliana nawe. Hili si jipya. Jipya ni kwamba huu ni mtihani kwa dokta Kanywaji anayesema anataka kuwaondolea wachovu kero. Nadhani kero mojawapo ni kutwaliwa kwa viwanja na ardhi yao na kutumiwa na chama kimoja wakati ni mali ya wote bila kujali vyama vyao.”
Kapende anapoka mic, “Kisheria, alichosema mkiti ni ushahidi tosha kukishughulikia chama chake. Hapa nashauri tushupae kuhakikisha vile viwanja vinarejeshwa sirikalini kama alivyofanya kwenye kota za Migomigo baada ya mafisadi kutaka kuwadhulumu wachovu.”
Mipawa anakatua mic, “Nakubaliana na ushauri wako. Ila nitaongeza kidogo. Lazima tumbane jamaa si kurudisha tu viwanja vilivyokuwa vikifisadiwa  na kumilkiwa kinyume cha sheria na CCM bali arejeshe na nyumba za wachovu alizouza Nkapa.”
Mijjinga naye anaamua kutia guu, “Ukisikia ujipu ni huu. Kwanza, ilikuwaje kaya ya kijamaa kuruhusu chama tena twawala kujiingiza kwenye uporaji viwanja na ukabaila? Je chama kinachotawala na kufanya biashara kitaacha kuichuuza kaya?”
Kabla ya kuendelea Mgosi Machungi anamchomekea, “Mgosi unataka kaya iuzwe maa ngapi wakati iishauzwa? Huoni jamaa anavyohangaika na ufisadi uioanzishwa na chama hiki hiki kinachotusanifu kuwa kipo kwa ajii ya wachomu? Hapa azima tiseme ukwei kuwa dokta wa majipu azima aitumbue CCM kwanza ndipo aendee na majipu mengine.”
Msomi anarejea, “Nadhani jamaa alipofichua siri hii hakujua madhara yake. Kwa vile tuna ushahidi wa kukiri kwake, kama atafanya vinginevyo, tunaweza kwenda hata kwenye mahakama za kimataifa kudai ardhi ya wachovu au siyo? Hakuna kilichoniacha hoi kama alivyoshangiliwa na wachovu huku vigogo wakishikwa na bumbuwazi kwa kumpitisha kwa kura zote wasijue atawatumbua.”
            dada Sofia Lion Kanungaembe anakula mic, “Hakuna aliponikuna dokta Kanywaji kama kuzifichua asasi za wizi kama vile umoja wa vijana na akina mama na wazazi ambazo ni taasisi za kiulaji zisizo na faida kwa chama wala umma. Nangoja kuona atakavyotumbua wakubwa wa asasi hizi ambazo zimetumika kwa muda mrefu kama mirija. Halo halo!”
Kanji anakula mic, “Veve sangaa hii jumuiya! Iko witu wingi kama vile SUKITA nakula juluku ya chovu. Mimi ona ajabu sana kweli. Kama chama namilki mali nyingi hiwi, kwanini kila chaguzi nenda kwa gabacholi ombaomba kama sikini?”
Mheshimiwa Bwege anatia buti, “Nyie mnashangaa samaki kufa kiu wakati amezungukwa na maji! Kwa kaya yetu ilivyojaliwa–kama chama twawala kisingekuwa kinafanya kazi ya kuwala wachovu–kina uwezo wa kuifanya kaya hii kuwa Ulaya nayo ikatoa misaada kwa kaya chovu duniani. Hata hivyo, unategemea nini unapokuwa na hamnazo wakisimamia shamba la bibi wakati bibi mwenyewe ni kipofu? Hapa kweli mtakoswa kuliwa hata kama neno lenyewe najua linaudhi? Ukisikia ubwege ndiyo huu na siyo wa jina kama langu.”
Mgosi anarejea, “ tate nane tate nane.Waahi maneno yenu yanamiumiza kwei kwei. Yaani tinatenzwa kama hatina akii jamani? Sasa nasema wazi kuwa azima tiende kwa huyo dokta Kanywaji na timwambie atiudishie mai zetu haaka kabla hatijatia mtu zongo.”
Kabla ya Mgosi kumaliza, Kapende anamchomekea, “Kaka ngoja nikuchomekee hata kama sina tabia hii.”
Kabla ya kuendelea, Mgosi anajibu, “Kapende angai maneno yako. Tiheshimiane. Yaani wewe ni wa kunichomekea mimi?”
Kapende anajibu huku akicheka, “Sina maana mbaya Mgosi. Ninachotaka kusema ni kwamba  habari kuwa chama tena kinachojidai kutetea wanyonge kinamilki viwanja zaidi ya 500 ni kufuru ya kupaswa kuwatia chuki wahanga wakafanya kitu cha maana. Hapa lazima ikiwezekana tuanzie hapa kwenda kumuona dokta Kanywaji kumtaka arejeshe mali zetu na kulipa fidia kwa miaka ambazo mali za umma zimetumiwa kinyume cha sheria.”
Kabla ya kuendelea Mipawa anakula mic, “Kwanini tusiondoke hapa tukaanzia pake SUKITA na kutaka kujua walioifilisi huku tukitaka watupe hati zake ili tumpe dokta Kanywaji kama kianzio?”
Kabla ya Mipawa kuendelea, Msomi anamchomekea, “Sidhani kama kuna haja ya kuamini kuwa dokta Kanywaji anaweza kutatua kila tatizo wakati sisi wahanga tukiangalia kama hayatuhusu. Kwanza, yeye ni mwana chama hicho hicho. Pili, hawezi kufanya kila kitu. Hivyo, nashauri tumsaidie kwa kwenda na kukamata mali zote za umma tunazojua bila kungoja CCM iorodheshe na kuficha baadhi. Ni rahisi kujua viwanja vya umma vinavyomilkiwa na CCM kinyume cha sheria. Si huwa wengi wanapaki mikangafu yao pale?”
Kijiwe kikiwa kinanoga si lakipita shangingi la kigogo wa CCM aliyeua SUKITA. Acha tumtoe mkuku!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.

Magufuli ataibadili CCM au itambadili?

$
0
0
            Rais na mkiti wa CCM, Dk. John Magufuli amekaririwa mara nyingi akilaumu serikali iliyopita kwa kulegalega na kuruhusu uhujumu wa taifa. Amekuwa akisikika mara nyingi akisema; Tanzania ilikuwa imegeuzwa shamba la bibi na genge la watu wachache tokana na ufisadi na uzembe wa wale waliomtangulia. Hata hivyo, jambo moja linawashangaza wachambuzi wengi.  Pamoja na Magufuli kufichua na kulaumu uoza wa watangulizi wake, ameahidi kuwalinda wananchi walipomtaka awafikishe mahakamani. Tokana na hili, Magufuli anawapa taabu walio wengi kuamini kama anasema atakachotenda na kutenda atakachosema bila upendeleo, huba wala ubaguzi wakati ameishaonyesha upendeleo wa wazi kwa watangulizi wake wenye madhambi lukuki.
 Tujiulize; je hiyo serikali iliyolegalega ikaruhusu hujuma kwa taifa iliundwa na chama gani kama siyo Chama Cha Mapinduzi (CCM) alichopewa kuiongoza? Je kuna namna Magufuli anaweza kufanikiwa kuibadili Tanzania bila kuibadili CCM? Je Magufuli ataweza kuibadili CCM au itambidili?
Kwa wanaochunguza mwenendo wa Magufuli na timu aliyo nayo, kuna uwezekano CCM kumbadili.  Kwa mfano, wapo wanaoshangaa mantiki ya kubakisha sekretarieti ya CCM iliyosimamia madudu haya yote. Pia, wapo wanaoshangaa mantiki ya kumuacha mtendaji mkuu wa CCM, yaani Katibu Mkuu, Abdrahaman Kinana ambaye aliwahi kutuhumiwa kuhujumu taifa ukiachia mbali kusimamia chama dhaifu na fisadi hadi kilipokabidhiwa mikononi mwa Magufuli. Kampuni ya Kinana imewahi kutuhumiwa kusafirisha nyara za umma.   Nadhani hii ilitoshe kumwashia Magufuli taa nyekundu na kutombakiza kwenye nafasi nyeti chamani.
 Hata hivyo, wapo wanaotabiri kuwa Magufuli ametafuta fursa ya kukifumua chama kwa kumbakisha Kinana akitafuta fursa ya kupata mtu anayefaa. Wengine wanakwenda mbali na kutabiri kuwa Kinana ataondoka kama aliyekuwa Katibu Kiongozi, Ombeni Sefue baada ya Magufuli kumbakisha na akamtumbua baadaye baada ya kupata mtu wa kufaa kwenye nafasi yake. Tunaweza kusema bila wasi wasi kuwa dirisha la kuibadili CCM kabla ya kumbadilisha Magufuli unaweza kuliona kupitia kuendelea kuwepo kwa Kinana ambaye–pamoja na kusifiwa kukiendesha chama–ukilinganisha matarajio ya watanzania kwa chama tawala, huoni cha mno kwa Kinana kuendelea kuwa mtendaji mkuu wa CCM ile ile aliyoiacha ikatekwa na kutwaliwa na mafisadi na magenge ya wahalifu.
Kadhia nyingine inayoonyesha kuwa hadi sasa CCM imembadili Magufuli kabla hajaibadili inahusisha makada wa CCM wenye tuhuma mbali mbali za kifisadi kama vile uuzaji mihadarati, wizi wa mali za chama na umma, uzembe, kujuana, matumizi mabaya ya fedha za umma, ubinafsi, na kadhia nyingine nyingi tena wanaojulika.
Bado Magufuli hatajatangaza kifo cha mitandao ya kifisadi iliyokidhoofisha chama kiasi cha kugeuka kama club ya matajiri kutumia kuliibia taifa.
Kimsingi, bila kukifumua na kukisuka upya chama–jambo ambalo, hakuna shaka, Magufuli anaonekana kukamia kutenda–ataishia kubadilishwa na CCM na kuwa kama wale ambao sasa anawalaumu kwa kukwamisha taifa letu chini ya siasa chafu na za kichoyo za kujuana na kujihudumia kama ilivyokuwa kwa miongi mingi tangu aondoke baba wa taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere mwaka 1985.
Tuseme wazi; ni mapema mno kupitisha hukumu kwa Magufuli japo si vibaya kuanza kuiandaa kulingana na kutokana na namna anavyopambana na matatizo sugu ndani ya chama na nchi.  Kwanza, ni kutokan ana ufupi wa muda. Magufuli hajatimiza hata mwaka tangu aingie madarakani kama rais wa Tanzania ukiachia mbali kuwa kwenye uenyekiti wa CCM kwa mwezi mmoja tu.
  Pili ni ile staili yake ya kutotabirika kirahisi. Wapo wanaoona kuwa Magufuli amejipa nafasi ya kuisoma mifumo ya ndani ya CCM ili kuweza kujua namna ya kukibadili chama kabla hakijambadili; hasa ikizingatiwa kuwa CCM ni taasisi kubwa ambayo imechafuka kwa muda mrefu. Hivyo, si busara kukurupuka na kuanza kufyeka kila kitu bila kujua undani na mbadala wake. Muhimu ni kumbukumbusha Magufuli–ambaye watanzani wengi bado wana imani naye–kuwa timming na muda katika uongozi ni jambo muhimu sana. Kama Magufuli atachelewa kuchukua hatua za kukibadili chama, uwezekano wa kubadilishwa ni mkubwa kuliko kukibadili chama.
Tatu, kutokana na uoza wa muda mrefu wa kimfumo, uwezekano wa Magufuli kuchukua muda mrefu kutimiza anayotaka kutimiza ni mkubwa hata ikiwezekana kumaliza muda wake bila kukamilisha kazi anayoanza kwa chama na taifa.
Nne, kitakachoamua kama Magufuli ameibadili CCM au imembadili ni matunda ya kazi yake. Hapa lazima tuwe wazi. Magufuli anaweza kufanikiwa kutekeleza anayoamini yatabadili mfumo mfu na fisadi uliojengeka kwa zaidi ya miongo mitatu. Ingawa, anaweza asikidhi matarajio ya watanzania kutokana na kuchoswa na kuumizwa na mfumo huu.
Tano na mwisho, vyovyote itakavyokuwa, Magufuli ataacha CCM mpya kulinganisha na ile aliyokabidhiwa ikichungulia kaburi. Rejea kutetemeshwa na kada wake, waziri mkuu wa zamani Edward Lowassa aliyepambana na Magufuli kwenye uchaguzi mkuu akiibuka mshindi wa pili kwa kura 6,072,848 sawa na aslimia 39.97 ya kura zote dhidi ya kura 8,882,935 ikiwa ni aslimia 58.46 ya kura zote (BBC, Oktoba 30, 2015). Unaweza kuona kuwa hapa hapakuwa na ushindi wa kishindo wala wa ki-Tsunami kama ilivyozoeleka.
Kwani mwaka 1995 Jakaya Kikwete alipata jumla ya kura 5,276,827 ambazo ni sawa na asilimia 61.17 ya kura zote zilizopigwa (BBC, 5 Novemba, 2010).
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.

Kijiwe chastukia ushauri wa kufyatua vitegemezi

$
0
0

Baada ya rahis kutoa amri kuwa wachovu wafyatue vinyemelezi, Kijiwe kimeamua kutoa angalizo juu ya ushauri na ushawishi huu ambao unaweza kukwamisha maendeleo na harakati za kaya za kujikomboa na umaskini na uombaomba.
Leo anayelianzisha ni Mbwamwitu. Baada ya kuamkua anakula mic, “Wazee mmesikia amri ya rais dokta Joni Kanywaji Makufuli kuwa lazima wachovu wafyatue vitegemezi kama hawana akili nzuri? Je nyie mmepanga kulitekeleza vipi?” anamalizia maswali yake huku akimdeku da Sofia Lion aka Kaunungaembe.
Mgosi Machungi hajivungi; anakula mic, “Mwenzenu sihitaji hivyo vitegemezi kwani ninavyo vingi kwei kwei. Laiti munene angejua adha za kuwa na vitegemezi ukuki waa asingetoa tamko hii ambao wengi wataichukuia siiyasii kiasi cha kuzaisha tatizo jingine. Tisiunge mkono ushaui huu hasa usawa huu wa kaya maskini na ombaomba.”
Msomi Mkatatamaa anakula mic, “Nadhani daktari wa tujipu alikuwa anatania watani zake wazaramizi vinginevyo–kama alimaanisha–basi akubali kuwa anatengeneza majipu mengine.  Sioni motisha ya watu wenye kuelewa mambo kuongeza vitegemezi hasa usawa huu wa kutumbuana na kubana matumizi. Kama ni elimu ya bure, hivyo vitegemezi si kabichi kuwa vitakuwa ndani ya miezi mitatu ndiyo vifaidi hiyo elimu ya bure. Vingi vya vitakavyofyatuliwa vitaingia kwenye shule za bure wakati jamaa akimalizia ngwe ya pili kama wachovu watampa. Hivyo, ushauri huu uchukuliwe kama utani na si ukweli.”
Mpemba anapoka mic na kudema, “yake mie siamini kama rahis alikuwa atania. Maana alirudia kauli yake ya kutaka watu wafyatue vitegemezi kwa kuwataka hata akina mama wasitumie madawa ya kuzuia kuzalisha vitegemezi. Nimjuavyo mimi dokta Kanywaji huwa si mtu wa utani. Nadhani alishauriwa vibaya au aliangalia vibaya mambo kiasi cha kutoa amri ya kuunda bomu ambalo wakati likifyatuka atakuwa mstaafu.”
Kapende anamuunga mkono Mgosi kwa kusema, “hata mimi nilishangaa kusikia kauli hii ambayo asipotafuta namna ya kuiweka sawa, inaweza kukamisha mipango yake mizuri. Nadhani hao vitegemezi anaotaka tufyatue hawahitaji elimu ya bure tu. Wanahitaji matunzo na mahitaji mengine muhimu kama vile ajira kwa wazazi wao, malazi na makandokando mengine.”
Mzee Maneno anaamua kumpinga Kapende, “kusema ukweli mimi namuunga mkono mtani wangu. Kama kaya inaweza kupokea wakimbizi na kuwapa uraia kila siku ukiachia mbali kujaa magabacholi na machina kibao, kwanini tusipunguze kutoa uraia wetu kama njugu na kujifyatulia wanakaya wenyewe? Nadhani hasara wanayosababisha wakimbizi wa kiuchumi toka Uhindi na Uchinani hata Unigeriani na Kenya ni makubwa kuliko vitegemezi tutakavyotengeneza wenyewe.”
Mijjinga anamuunga mkono Mzee Maneno, “nyie mnashangaa la kujaza wakimbizi wa kiuchumi! Hamuoni hili la kuunda umoja na vijikaya visivyo na ardhi huku vikitushupalia kuwa turuhu free movement vimuvu na kuchukua ardhi yetu? Hamjaona vijikaya uchwara vilivyotuzunguka vinavyotia kila mchakato wa kutaka kuja kufaidi ardhi yetu au hamuoni?”
Mpemba anakamua mic, “yakhe naamini kuwa hapa wasomi tuna tena wengi kweli kweli. Hata mie naona hili laingia akilini sana. Heri huyu bwana azuie uingiaji wa wakimbizi uchwara wa kiuchumi na miungano na vijikaya vingine wakati ule wa Zenj bado wantoa jasho. Heri angefyatua ajira na viwanda kwanza, haya ya vitegemezi yakaja baadaye baada ya kuona matunda ya majaribio yake wallahi.”
Kanji anakula mic, “veve Pemba sema kitu ya maana sasa. Kana Kufuli nafyatua jobs naveza leta endeleo kuba sana. Sana kama chovu nazaa kama kuku hapana ona kaya takosa riziki ya kulisha yeye? Kwanini hapana soma toka India. Kule hindi nazaa kama kuku na kila siku vatu naongezeka na nateseka sana.”
Da Sofia anampoka Kanji mic, “kwa vile mipango ya Kiswahili–mara nyingi ni ya muda mfupi–huenda mhishimiwa ametumia kigezo hicho bila kuangalia mambo mengine muhimu yanayoyitajika kama vile hospitali na zahanati za kutosha, huduma safi, madaktari na wakunga wa kutosha na mambo mengine nyeti.”
Mipawa ambaye muda wote alikuwa akiangalia huku akitabasamu, anawaacha wana kijiwe hoi. Anakula mic, “beng’we, sasa mie acha nitume fedha ya kununulia ng’ombe tayari kuongeza ngoma ya pili ili nitekeleze agizo la rahis bila kughairi wala kuuliza. Nyinyi mmeambiwaga mfyatuage vitegemezi mnaanza kuumiza vichwa wakati sirikali lipo litabeba mzigo wake. Nawashaurini tutekeleze wito wa rahis wa kufyatua vitegemezi huku tukimtaka naye afyatue huduma kama wajibu wake au vipi?”
Msomi aliyekuwa akinong’ona jambo na Mpemba anaamua kutia guu tena, “japo sina wasi wasi na uchapakazi na mipango ya bwana Kanywaji, hili sitaliunga mkono hasa kama mchumi. Huwezi kuongeza idadi ya wana kaya wakati iliyopo inakuelemea. Huwezi. Kufanya hivyo ni kujipiga mtama. Hivyo, nisiseme mengi, kuna haja ya kupanga kwenda kuonana na rahis kumshauri akanushe kauli hii kabla hajatengeneza balaa jingine. Nadhani kwa sasa kaya aihitaji vitegemezi badala kujitegemea.”
Kijiwe kikiwa kinanoga si Mipawa akaaga anaelekea zake usukumani kutafuta ngoma ya pili ili afyatue vitegemezi! Wote tulibaki hoi tusijue la kumshauri. Ama kweli usilojua sawa na usiku wa kiza!
Chanzo: Tanzania Daima leo.

Mlevi kuwa bilionea kupitia bwimbwi

$
0
0
Baada ya kugundua kuwa nyavu za kupambana na uhalifu haziwagusi wauza bwimbwi na mafwisadi wakubwakubwa hasa waliokuwa marahis Mlevi nimeamua kuingia kwenye biashara ya bwimbwi tena bila kificho. Kwa vile mapapa wa bwimbwi ni untouchable, mlevi niogope nini kutia timu kwenye genge hili ili lau nami nichange njuluku ikiwezekana niwe bilionea kama Mo Jewji ambaye nilisikia akisema kuwa amejiunga na club ya mabilionea watakaogawa utajiri wao? Hakuna kilichonishangaza kusikia kuwa Jewji atagawa utajiri wake dunia nzima wakati aliuchuma kayani. Ama kweli, gabacholi wakati mwingine si wa kuamini. Sitashangaa kusikia kuwa Ugabacholini watapewa dau kubwa huku wadanganyika wakiishia kuusoma ukwasi huu magazetini.
Hakuna kitu kingine kilinkata kama kusikia kuwa na yule jambazi wa Kagoda ni bilionea wakati aliiba njuluku za walevi kupitia EPA na ujambazi mwingine. Kesho sitashangaa majambazi kama Ni Zero Kadamage yule jambazi wa Buzwagi aliyekwenda kuingia mkataba hotelini kule Uingerezani akitajwa kuwa bilionea wa Danganyika aka Bongolalaland.
Kama haitoshi, sitashangaa kusikia jambazi mwingine wa UdA ambaye hivi karibuni alibainika kuuziwa kiwanda cha mabilioni ya madafu kwa madafu milioni thelathini juu ya kugawiwa Dart naye akiingia kwenye club ya mabilionea. Hapa usisahau kuwa na mshitiri wake Riz naye siku moja ataitwa bilionea. Kwa wachumi kama mimi, natabiri kuwa Danganyika itazalisha mabilionea wengi kiasi cha kuchanganya dunia. Hapa rafiki yangu Jose Gwaijimmy, Kartortoise, Rwakatarehe, Gamanyue, Mwakasenge na wengine wanaotumia neno la Bwana kuwaibia wachovu nao bila shaka watatia timu kwenye club hii ya wakwasi.
Kwa vile nami nauzimia na kuukamia ukwasi, lazima niuze bwimbwi bila kujali kuwa vijana wetu wanaumizwa nalo. Mwanzoni nilikamia kuuza mibwimbwi baada ya kugundulika kuwa pale uwanja wa ndege wa mzee Mchonga wa Burito madude yalikuwa yanajipitia baada ya wanahizaya kuua mitambo ili kupitisha mizigo yao na wenzao. Baada ya mambo kuchenji, ilibidi nitulize boli na kusaka fursa nyingine ambayo nimeideku baada ya kuangalia historia ya trejecktori ya mapambano dhidi ya utengenezaji ukwasi wa haraka. Bandarini, kwenye mita za mafuta, mipakani, TRA, Banki kubwa na kwingineko ameziba. Kwa vile ameamua kuachia mibwimbwi iendelee kutawala, kwanini bingwa nisiiuze na kuwa bilionea?
Najua wengi wanaona kama ndoto za mchana na matokeo ya ile kitu ambayo huwa navuta. They are dead wrong. Seriously lazima nifanye biashara ya hii kitu hasa baada ya kuona wengi wakiifanya na kuibuka kwa wakwasi wa kutisha na kuogopewa kayani. Hamuoni watu wanavyoangusha mahekalu na migari ya bei mbaya kama Lungumingumi? Nani hataki kuwa bilionea kama kina Jewji na Roast Tamu?
Nina uhakika; hapa nitasepa na kupeta na kutokezea kuwa bilionea ghafla bin vu. Jiulize; tangu itangazwe vita dhidi ya ufisadi na uovu mwingine, mzungu gani wa bwimbwi ameishanyakwa na kunyea debe? Hakuna. Sasa kama hali ni hivyo, kuna haja gani kudharau mitikasi yangu ya kuuza mibwimbwi na kuukata hadi nikaitwa mtukufu, mheshimiwa, mpendwa, bilionea Mlevi mwana wa Mvuta ile kitu? Kwanini wewe unayekandia na kudharau mipango yangu hutaki kuelewa kuwa nikishazinyaka njuluku nitakuwa mwekezaji kama Kisenena ima kwa kununua makampuni kama UdA au ginneries za kuchambulia pamba tena kwa bei ya mchekea kama jamaa alivyofanya hadi kumuudhi dokta Kanywaji aliyetoa amri hivi karibuni kuwa jamaa arejeshe kiwanda lakini akagoma kumwambia arejeshe UdA na Udart aliyogawiwa hivi karibuni? Kwanini Mlevi nilaze damu wakati najua lisirikali linajichanganyasometimes  kama lilivyofanya kwenye kuigawa Udart kwa walioiba UdA badala ya kuwasweka lupango?
Kitu kingine kinachonipa imani ni ile ya kuwa kayani kwetu, ukilala apeche alolo na ukaamka bilionea, hakuna anayekuuliza ulivyochanganya njuluku haraka hivyo. Kwanini hiki kisiwe kishawishi kizuri cha wanjanja kama mimi kutgengeneza njuluk kwa njia yoyote? Danganyika aka Bongolalaland kaya nzuri sana. Angalia baadhi ya wachunaji wanavyomilki hata michopa huku wakipigapiga mikelele utadhani viongozi wa upingaji na wasifanywe kitu hata kuwauliza waeleze walivyochuma ukwasi. Kwanini mimi nilaze damu wakati milango ya kutengeneza ukwasi na kuwa bilionea chapchap kwa njia yoyote iwa halali au haramu iko wazi? My foot! Hii kitu lazima niifanye bila kujali watakaoumizwa nayo.  Mbona viwanda vya fegi vinanyonga wengi na hakuna anayejali wala kuadhibiwa? Mbona uchafuzi wa mazingira utokanao na utapishaji wa vimiminika vyenye sumu unaua wengi na hakuna anayejali? Nani hakuona mafwisadi wa Nida walivyotengeneza njuluku kwa kulangua vitambulisho ukiachia mbali kuwapa hata wasio raia? Nani anajali usawa huu kama wauza bwimbwi na waovu wengine wanaendelea kuwa mabilionea? Lazima niiuze bwimbwi ili kuwa bilionea au ikiwezekana kuazisha Kagoda namba mbili au siyo? Kwanini nisiiunde kama Kagoda one imezalisha bilionea ambaye alipaswa kuwa lupango akingojea kunyongwa?
Leo sitachonga sana. Badala yake nakwenda kusuka misheni ya kufanikisha dili la kuwa bilionea chapchap na kugeuka mwekezaji wa ndani hata kama ni mchuguaji actually.
Chanzo: Nipashe Jumapili Leo.

Makonda kujengea Bakwata hapana

$
0
0

Image result for makonda na bakwata
            Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alikaririwa hivi karibuni akiahidi kulijengea Baraka Kuu la Waislam Tanzania (BAKWATA) makao makuu yenye hadhi. Makonda alisema makao makuu hayo yatakuwa jengo la ghorofa tatu lenye thamani ya shilingi 5, 080, 155, 600. hii si pesa kichele. Wapo waliotaka kujua fedha hii Makonda inatoka wapi; na ni nani wako nyuma ya hisani hii ya aina yake katika historia ya taifa. Makonda anatoa jibu akisema “Leo nimefika hapa ikiwa ni mwanzo wa safari mpya ya serikali ya mkoa wa Dar kujenga makao makuu mpya ya kisasa ya ndugu zangu.” Hivyo wasiojua nani atajenga jengo hili wajue; ni utawala wa mkoa wa Dar es Salaam. Je kuna wanaomtuma na kumtumia kwa faida yao? Hili swali wanapaswa wajibu wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam. Sijui kama wamempa kibali cha kujenga makao makuu ya taasisi ya kidini wakati shule nyingi za serikali ni hoi kimajengo ukiachia mbali wafanyakazi wengi wa serikali kutokuwa na nyumba za uhakika. Je nini mantiki ya kufikia kipaumbele hiki na mchakato gani wa kidemokrasia umepitisha mradi huu? Je watanzania watanufaikaje na mradi huu?
Makonda aliongeza “viongozi wangu wa BAKWATA, najua watu wote wana viongozi kama baba ni kiongozi wa familia, watu wana vyama vyao vya siasa wana viongozi, watu wana makampuni yao wana viongozi lakini viongozi hawa wanatofautiana na viongozi wa dini kwa jambo moja, viongozi wa dini wanatuongoza kutupeleka kwa mola alietuumba sote.”
Kuna maswali ambayo Makonda na waliomtuma walipaswa kujiuliza.
Mosi, je makao makuu ya Bakwata ni muhimu kuliko watoto wetu wengi wanaosomea kwenye majengo mabovu au walimu wao wasio na maslahi na mishahara ya kutosha ukiachia mbali kutokuwa na vitendea kazi vya kutosha na vya kisasa?
Pili, je kweli Bakwata inastahili kupewa kipaumbele hivi? Pamoja na kuwa mpokea zawadi hachagui zawadi ya kupewa, hivi kweli Bakwata ilihitaji hata msaada mchoro kweli? Wapo waliodhani; Makonda alikuwa amekurupuka kutafuta ima umaarufu au kutaka kuwatumia waislamu aonekane anachapa kazi na mtatuzi wa matatizo ya jamii.
Wapo wanaoona kama Makonda ameshauriwa vibaya kwa kuhangaika na kuwajengea watu makao ya kifahari kwa vile hayakukumfurahisha wakati anawaacha wasio na hata mlo mmoja. Wapo wanaohofia Makonda hatafanikiwa katika kupata hicho unachokitafuta. Hali inakuwa ngumu hasa mtumishi wa umma unapojiingiza kwenye mambo ya dini wakati serikali haina na haipaswi kupendelea dini yoyote.  Wapo wanaodhani kuwa bilioni tano na ushei ni pesa ambayo si rahisi kuipata. Hata hivyo, inavyoonekana, Makonda anazo fedha. Maana alikaririwa akisema; anataka jengo lake likamilike ndani ya miezi 14. Huyu atakuwa na fedha. Kinachogomba ni alivyoipata na namna anavyotaka kuitumia kwenye nchi yenye matatizo mia kidogo.
Wapo wanaoona kama serikali ina fedha ya hata kujenga makao makuu ya asasi za kiraia wakati makao makuu yanaishinda, basi imekosa kipaumbele. Je serikali itapata faida gani kujiingiza kwenye biashara ya dini au kuchanganya siasa na dini? Sijui inatoa somo gani kwa watanzania wenye shida za msingi kama vile ukosefu wa maji, umeme na huduma nyingine? Je huku si kuwatumia waumini kisiasa jambo ambalo ni hatari huko tuendako? Wakati mwingine mtu anaweza kutaka kufanya jambo jema kwa njia mbaya. Hapa ndipo utata unapoanza. Huwezi kutumia fedha au nafasi ya umma kupigania haki ya kundi moja wakati ukiyaacha mengine.
Je Makonda na wanaomtuma walijua kuwa:
Mosi, Bakwata wana mali zao kama vile majengo na mali za wakfu ambazo zimetumiwa vibaya kiasi cha kuwaweka matatani baadhi ya waislam wakereketwa kama Shehe Ponda Juma Ponda. Heri Makonda angewapa Bakwata wakaguzi wa mahesabu na mali.
Pili, popote anapopata hiyo fedha, anaigawa kama nani wakati kuna matatizo kibao ya maana yanayolikabili taifa? Kama ni ya serikali ni kwa sheria gani au ni yale yale kuwa kuna watu sasa wana uwezo wa kujifanyia lolote bila kujali sheria kwa vile wako karibu na wakubwa zaidi? Je huu mradi umeridhiwa na mkoa; kwa faida gani na utajiri gani?
Tatu, kwanini hiyo pesa isielekezwe kwenye ujenzi wa madarasa, nyumba za walimu, maabara au kuboresha maslahi ya walimu badala ya kuwajengea wetu wenye uwezo na wajibu wa kujijengea makao yao makuu?
Nne, je Makonda na wenzake wanafahamu; serikali wanayoiongoza inaombaomba kwa wafadhili kutunisha bajeti ukiachia mbali michango kwenye madawati?
Tano, Kwanini serikali hata iwe ya mkoa tu ipate fedha ya kujenga makao makuu ya Bakwata wakati vijijini fedha inaenda kiduchu?
Sita, je lisingekuwa jambo la busara kwa fedha hiyo kuelekezwa kwa vijana wengi wanaohenyeshwa na mikopo ya elimu ya juu au zahanati nyingi zisizo na madawa au majengo stahiki? Hakika maswali ni mengi kuliko majibu.
Tumalizie kwa kuuliza maswali. Je Makonda na wenzake wanafahamu kuwa wanachotaka kufanya–pamoja na uzuri wake–kinaweza kutafsiriwa kama hongo au kishawishi kwa wahusika kwa malengo ya kisiasa hata kama si hivyo?
Saba, je Makonda na wenzake wamepata mchango wa wapinzani ambao nao wanaunda serikali ya mkoa wa Dar es Salaam hasa kwa kuzingatia mileage Makonda na wenzake wataipata kisiasa? Maana, wangefanya wao wangeambiwa wanachanganya dini na siasa.
Mwisho, je utajengea wangapi?
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.

Kijiwe chalaani Makondakonda na wauaji wa polisi

$
0
0
           Baada ya majambazi kuua ndata wasio na hatia tena wakiwa kibaruani, Kijiwe kimekaa kama kamati kulaani mauaji haya pamoja na matamshi ya kishenzi yanayokiuka haki za binadamu.
            Mpemba ndiye analianzisha, “Yakhe mmesikia hii ya majambazi kuua askari tena kwa kuwavizia kwenye banki? Sijui hii kaya yapelekwa wapi hasa usawa huu ambapo baadhi ya waja wanaanza kusingizia hata upingaji wakati ujambazi unajulikana ulivolelewa na utawala ulopita wa kitwahuti.”
            Mbwamwitu anajibu huku akiendelea kusoma gazeti, “Mie sishangai hasa nikiangalia namna kaya yetu inavyokumbatia ufisadi kiasi cha kila mtu kusaka njuluku.”
            Mgoshi Machuni anakula mic, “Hii timeisikia. Hapa lazima tiseme wazi. Hawa majambazi azima yasakwe na kufikishwa kwa piato ii yakapata stahiki yao. Pia tichukue fuusa hii kuonya poisi nao wasionee wanakaya kama njia ya kuipiza kisasi. Kaya yetu ni kaya ya kidemokaasia na inapaswa kuendeshwa kwa utawaa wa sheia na si jazba ya waduwanzi fulani wanaofanya usanii wa kisiasa.”
            Mijjinga anakwanyua mic, “mgoshi hapa nakubaliana nawe hasa nikirejea maneno mbofu mbofu kama hii ya mkubwa wa nkoa Po Makondakonda aliyewahimiza ndata kutoheshimu haki za binadamu asijue kuwa sheria haitumii jazba au umajinuni na ukihiyo kufanya kazi zake. Najua kila mwanakaya amechanganywa na kuchukizwa na vitendo vya kuua ndata. Ni bahati mbaya kuwa badala ya kumsaka adui wa kweli, tunahangaishwa na matokeo. Lazima tushauri wausika kutafuta chanzo cha jinai hii ili kuishughulikia vilivyo kwa akili na si jazba na ujinga.”
            Kapende anakula mic, “hata mimi huyu dogo mpenda ujiko aliniacha hoi kiasi cha kuhoji usomi wake. Wakati watu wenye akili wanazuia wanakaya kujichukulia sheria mikononi au kuonea watu kwa kulipiza visasi, yeye anahimiza ndata wajichukulie sheria mikono asijue matokeo yake–licha ya kujenga uhasama baina ya ndata na wanakaya–kunaweza kutumbukiza kaya kwenye machafuko. Sijui hao waliompa huo ulaji kwanini hawakufanya homework yao vilivyo?”
Tunaendeshwa na sheria na katiba na si hisia wala usongo
            Kanji anakula mic, “mimi iko sangaa sana hii kuu naotoa amri baya kama hii. Hiwi huyu nateua yeye iko goja nini fukuza yeye ili itie adabu na ishike adabu na adabu ishike yeye? Hii takuja chafua rahis kama naacha iseme bila fikiri kama toto dogo. Vatu yote nasikitiko kubwa na nalia chozi kuba kufa data.”
            Msomi Mkatatamaa anaamua kutia guu, “Kanji naungana nawe. Sijui kwanini huyu dogo hawajibishwi haraka na kufikishwa kwa pilato kwa kutishia amani na haki za binadamu. Hata hivyo, sisi hatushangai kusikia na kuona haya tuliyoshuhudia. Tulionya muda mrefu kuwa jamaa ni bomu. Sasa ameanza kujifichua na kuonyesha uhalisia wake. Hata hii ya kudaiwa kutaka kumfanyia fujo na kumdhalilisha Mzee Jose Waryuba inaanza kuonekana kuwa kweli. Unacheza na laana za wazee nini? Kilichompandisha ndicho kitakachomshusha.”
            Anapiga chafya na kuendelea, “nakubaliana na  maneno ya Mijjinga kuwa tunachopaswa kufanya si kutoa amri za aibu na ajabu zitokanazo na jazba bali kukisaka chanzo cha kadhia hii ambacho ni ukosefu wa maadili. Tangu maadili yalivyogeuzwa madili na kila mchovu akataka kuukata hata kwa kuumiza wenzake, ujambazi na jinai nyingine zitaendelea kuongezeka hata kusababisha madhara makubwa kuliko haya yanayotushangaza leo.”
            Mipawa anakula mic, “mwenzenu anatetea kitumbua kwa kila hali hasa usawa huu ambapo kijogoo katika kaya hii ni mmoja. Kama mlisikia munene wake alivyolalamikia watetezi wa haki za waja pale walipohoji mantiki ya kusimamisha baadhi ya watendaji hadharani bila kufuata utaratibu, mtakubaliana nasi kuwa huyu dogo alikuwa anasema aliyosema si kwa upendo wa waenda zao bali kutaka kumridhisha bosi wake.”
            Sofia Lion aka Kanungaembe anakula mic, “kaka nakubaliana nawe. Hakuna jamaa aliponiacha hoi kama kusema kuwa hakuumbwa kusema maneno mazuri na wala huwa hamfurahishi mtu wakati kila mwanakaya anajua lengo la kutoa upupu huu la huyu dogo licha ya kuwafurahisha ndata, lililenga kumfurahisha waliomfinyanga.”
            Mzee Menano anamchomekea Sofia, “dada ni kweli; jamaa anajichanganya kutokana na uchu na njaa ya madaraka. Hii ndiyo hasara ya madaraka ya kupewa na si kusotea. Mbona mkuu wa ndata, waziri na wenene wengine hawakujivua nguo kama siyo umbumbumbu wa mhusika wa kupayuka bila kufikiri. Anadhani kupayuka pwenti ni kazi rahisi siyo?” anamalizia huku akiniangalia mimi hasa baada ya kusema kupayuka pwenti si kazi ya mchezo. Nami natabasamu tu bila kusema neno.
            Mheshimiwa Bwege aliyekuwa akiangalia na kutikisa kichwa muda wote anaamua kutia guu, “wote mmesema vyema na nimewasikiliza kwa makini. Nataka niwaambie kuwa usawa huu, huyu dogo mnayetaka awajibishwe anaweza kusema na kufanya lolote asifanywe kitu hasa ikizingatiwa kuwa amedekezwa akasahau kuwa mchezo anaocheza hauna muamala. Wangapi wameishafukuzwa kama mbwa baada ya uteuzi wao kutenguliwa? Hamjui anayecheza naye na anayemuigiza. Siku moja mtakuja kukumbuka maneno haya ya utume.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si wakapita ndata. Acha tutoke mkuku kwa kuogopa wasitekelezee amri za Makondakonda kwetu.
Chanzo Tanza nia Daima Jumatano jana. 

Fyatueni ajira si vitegemezi

$
0
0

          Baada ya Mlevi mmoja mkubwa tu kuja na mpya akiwataka walevi wafyatue vitegemezi kama hawana akili nzuri, Mlevi nakuja na angalizo. Nafanya hivyo baada ya kusikia walevi wenzangu wakikamia kuoa wake zaidi ili kufyatua vitegemezi kwa vile ilmu sasa ni ya ubwete.
            Katika kuangalia kadhia nzima hasa kwenye kaya apeche alolo iishiyo kwa kutegemea washitiri, kubomu na kukopakopa, nimegundua yafuatayo:
            Mosi, walevi waliopo wanatosha sana kaya hii kiasi cha kugeuka mzigo kutokana na ukosefu wa huduma muhimu kama majumba, maji, skuli bora,, lishe bora, mishahara fiti kwa maticha, nyumba za maticha, maabara na makandokando mengine. Madawati yenyewe yanawatoa walevi kijasho kiasi cha kuchangishana na kubanana hapa na pale. Bado madarasa ambapo vitegemezi vingi kayani hasa kule mashambani vinasomea ima kwenye madarasa mabovu au chini ya miti. Maticha bado wanabanana kwenye mbavu za mbwa hadi wengine kuishi kwenye vyoo. Hapa kweli kuna mantiki ya kufyatua vitegemezi vingine ili vije kuteseka kama hivi tulivyo navyo kwa sasa vikimaliza skuli bila hata kujua kusoma na kuandika? Tunamkomoa nani hapa?
            Pili, uchumi wa kaya hii bado ni wa kujikongoja hasa kutokana na uzalishaji duni, uzalishaji wa mazao ya kikoloni almaaruf kama cash crops yanayotegemea soko moja la wakoloni ukiachia mbali kuuzwa bila kusindikwa na kuwa na Added Valued na siyo VAT.
            Tatu, uchumi wetu licha ya kuwa wa mauzauza na kilevi, umegugunwa na ufisadi kiasi cha kuparaganyika. Hapa sijagusia njuluku zinazotoroshwa kila uchao na wachukuaji waitwao wawekezaji na hasa machainizi na magabacholi.
            Nne, kaya yetu inaongoza kwa kugawa uraia wake kama njugu ukiachia mbali mipaka yetu kuzalisha walaji wengi waingiao na kutoka kama watakavyo. Nadhani machinga toka Ugabacholini na Uchainizi waliojazana kayani wanatosha kula hicho kinachotutia kiburi hadi tukadhani kuwa tunahitaji vitegemezi zaidi.
            Tano, kama nilivyogusia hapo juu, kaya yetu haina huduma za kutosha kwa wajawazito kama vile lishe, tiba bora, hospitali na zahanati vya kutosha. Kama mke wa Mlevi mkuu angekuwa amewahi kujirudufia kwenye hospitali zetu zinazosifika kwa kuwatesa wajawazito, nina hakika asingetoa ushauri huu wa ajabu ajabu so to speak. Nikikumbuka wajawazito waliowahi kujifungulia kwenye mageti ya mahospitali napata kichefuchefu kusema ule ukweli.
            Sita, ukiangalia kanuni za ukuaji, Vitegemezi ya Bangi, Ulabu na Ahadi (VIBUA) vitachukua miaka zaidi ya kumi kukuka. Hivyo, wakati vikifikia wakati wa kwenda shule, mhusika atakuwa ameishakitoa na kumwachia atayerithi ulaji wake bonge la bomu. Na pia ifahamike kuwa maisha siyo skuli tu bali mambo mengine mengi tu. Hapa hatujaongelea mzigo wa kulisha, kuvisha, kulea na kutunza hivyo vitegemezi.
            Saba, kwa sasa ahitaji kufyatua vitegemezi bali inahitaji kufyatua ajira ili kuwawezesha walevi wetu wawe na kile walichoahidiwa na msanii mmoja mkubwa aitwaye Njaa Kaya ya Maisha Bora kwa Wote (MBOWO). Boresheni skuli zilizopo kwanza badala ya kuongeza vitegemezi wakati maisha yanazidi kubana kiasi cha jana kuonekana kuwa bora kuliko leo. Mnataka kuongeza idadi ya ombaomba na machinga nini?
            Nane, kwa wale waliosoma uchumi, watakubaliana nami hata kama naongea kwa ulevi. Kinachowasumbua wanaowahimiza walevi kufyatua vitegemezi ni ile hali ya kuridhika na mafanikio ya muda. Utafyatuaje vitegemezi wakati kipato cha walevi kinazidi kushuka kila uchao? Utafyatuaje vitegemezi bila kuzingatia kuwa kaya sasa inaumia tokana na kujifyatulia vitegemezi bila mpango?
            Tisa, nawataka walevi wachukulie ushauri huu kama wa kisiasa au utani tu lakini si wa kisayansi hasa ikizingatiwa kuwa aliyeutoa si mtaalamu wa uchumi.
            Kumi, ili kupata vitegemezi vingi, inabidi walevi waoe wake zaidi ya mmoja jambo ambalo litasababisha ugomvi katika ndoa. Nadhani, kama tunataka vitegemezi vya kutosha, basi tuhakikishe vile vinavyotupwa kutokana na mimba za utotoni na zisizotakiwa havitupwi kinyama na kuuawa bila kosa lolote.
            Kumi na moja, badala ya kufyatua vitegemezi kama hatuna akili nzuri, nashauri, tupange uzazi na kupunguza kufyatua vitegemezi hasa ikizingatiwa; siku hizi kaya yetu imeingia usuhuba na vijikaya vyenye mizigo mikubwa ya ongezeko la walevi vinavyotaka turuhusu kila mlevi toka kila kaya kwenye eneo hili aende kuishi atakavyo bila kujali uraia wake. Jambo hili nalo ni bomu kwa kaya yetu hasa ikizingatiwa kuwa ndiyo yenye ardhi kubwa na raslimali nyingi ambazo wahusika wanataka kuzifaidi kwa kisingizio cha ushirikiano wa kikanda.
            Japo nasema kwa nguvu ya kanywaji na yale madude mengine ambayo huwa natwika, nashauri tusifyatue vitegemezi. Pia, nashauri tusiwe tunafanya mzaha na utani kwenye serious issues kama population au idadi ya walevi. Hapa lazima tuache kuwa na vipaumbele vya kisiasa vitonavyo na hisia badala ya tafiti na takwimu. Kufyatua vitegemezi kumenikumbusha mnene mwingine uchwara aliyetoa mpya hivi karibuni akijipiga kifua eti kujenga hedikwota ya baadhi ya shirika la kidini wakati eneo lake linasifika kwa uhaba wa nyumba za watumikaji wa lisirikali pamoja na vyumba vya madarasa. Hii ni akili au matope? Japo nafanya mambo kilevi, nisingependa na wanene wafanye mambo kilevi hasa pale wanapolewa ulaji.
            Kwa leo nadhani hii dozi yatosha kulaleki!
            Mlevi mwana wa Mpigakaya…PhD (Utopian Economics).
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
Viewing all 3173 articles
Browse latest View live