Quantcast
  • Login
    • Account
    • Sign Up
  • Home
    • About Us
    • Catalog
  • Search
  • Register RSS
  • Embed RSS
    • FAQ
    • Get Embed Code
    • Example: Default CSS
    • Example: Custom CSS
    • Example: Custom CSS per Embedding
  • Super RSS
    • Usage
    • View Latest
    • Create
  • Contact Us
    • Technical Support
    • Guest Posts/Articles
    • Report Violations
    • Google Warnings
    • Article Removal Requests
    • Channel Removal Requests
    • General Questions
    • DMCA Takedown Notice
  • RSSing>>
    • Collections:
    • RSSing
    • EDA
    • Intel
    • Mesothelioma
    • SAP
    • SEO
  • Latest
    • Articles
    • Channels
    • Super Channels
  • Popular
    • Articles
    • Pages
    • Channels
    • Super Channels
  • Top Rated
    • Articles
    • Pages
    • Channels
    • Super Channels
  • Trending
    • Articles
    • Pages
    • Channels
    • Super Channels
Switch Editions?
Cancel
Sharing:
Title:
URL:
Copy Share URL
English
RSSing>> Latest Popular Top Rated Trending
Channel: Free Thinking
NSFW?
Claim
0


X Mark channel Not-Safe-For-Work? cancel confirm NSFW Votes: (0 votes)
X Are you the publisher? Claim or contact us about this channel.
X 0
Showing article 1401 to 1420 of 3177 in channel 8805252
Channel Details:
  • Title: Free Thinking
  • Channel Number: 8805252
  • Language:
  • Registered On: March 5, 2013, 12:54 am
  • Number of Articles: 3177
  • Latest Snapshot: May 18, 2025, 3:16 pm
  • RSS URL: http://mpayukaji.blogspot.com/feeds/posts/default?alt=rss
  • Publisher: http://mpayukaji.blogspot.com/
  • Description: I Fear Nothing But Fear Itself
  • Catalog: //thinking1343.rssing.com/catalog.php?indx=8805252
Remove ADS
Viewing all 3177 articles
Browse latest View live
↧

Vihiyo na vilaza wakae mkao wa kuliwa

September 4, 2016, 8:01 am
≫ Next: Kilichomkweza Makonda ndicho kitakachomshusha
≪ Previous: Fyatueni ajira si vitegemezi
$
0
0
Jamaa akiangua kilio baada ya kubainika kuwa kumbe ni kihiyo aliyeangukia madaraka makubwa kutokana na nguvu ya vimemo. Laiti wangeshughulikiwa wote na kuishia jela, huenda lingekuwa somo kwa wengine.
↧
Search

Kilichomkweza Makonda ndicho kitakachomshusha

September 4, 2016, 8:08 am
≫ Next: When Junior and Senior Engage
≪ Previous: Vihiyo na vilaza wakae mkao wa kuliwa
$
0
0
Image result for photos of magufuli and makonda
           Kuna kisa maarufu cha jamaa aitwaye Kiburi. Huyu bwana alikuwa na kiburi kama jina lake kiasi cha kudhani yeye ni yote katika yote bila kujua avumaye baharini papa! Tokana na kiburiburi chake, bwana Kiburi hakupenda kukanya ardhini. Kila alipokwenda alipanda farasi wake mweupe. Siku moja si bwana Kiburi akajisahau na kumfanyia kiburi farasi wake. Farasi kwa hasira aliamua kupiga mateke na kuacha kumbeba kiasi cha Kiburi kurejea nyumbani akilia kwa maumivu na uchovu vyote vikiwa matokeo ya kiburi.
            Kwa wanaojua mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alivyoibuka tokana na siasa za majitaka za zama zile, hawana wasi wasi; siku atapotea hivyo hivyo kisiasa. Tuliwaona wengi. Wako wapi akina Augustine Mrema?
            Hivi karibuni akiaga miili ya polisi waliouawa na majambazi, Makonda alikaririwa akisema “nakuagiza Kamanda wangu Sirro mkiwapata watu wenye nia kama hizo msiwaache hata watu wa haki za binadamu waseme.” Kisheria, haiwezekani kujua nia ya mtu hadi upate ushahidi wa kutosha na si wa kusikia bali kutokana na jaribio au attempt lakini si hisia zako au za wengine na wala si kutokana na maagizo ya hasira na sanaa za kisiasa bali taratibu za kiupelelezi kisheria. Pamoja na kuwa agizo lilitolewa na layman, asiyejua sheria. Kufanya hivyo, kunaweza kusababisha uonevu hata uvunjaji mkubwa wa haki za binadamu. Vyombo vya dola havipaswi kufanya kazi kwa maagizo ya wanasiasa au watu wasiojua hata mipaka ya madaraka yao bali sheria na utaalamu vilivyo nao. Makonda alikwenda mbali na kuita haki za binadamu uchizi na wendawazimu bila kuthibitisha madai yake. Hakuna anayefurahia mauaji ya polisi au mtanzania yoyote. Makonda alipoteza fursa ya kuonyesha uongozi na ukomavu.
            Wengi walishangaa kusikia kauli za ajabu kiasi cha kuhoji welewa na usomi wa mhusika. Mbona walikuwapo wengi tena walio karibu zaidi na marehemu? Tumemsikia mkuu wa jeshi la polisi akisema kwa uchungu bila kutoa amri za ajabu. Tumemsikia waziri wa mambo ya ndani; lakini hakutoa maagizo ya kiimla. Kimsingi, Makonda anapaswa kuvuliwa nafasi ya ukuu wa mkoa na kushitakiwa kwa kutishia haki za binadamu. Ajabu ni akina Makonda hawa hawa wanaoimba kulinda amani wakati wakitoa amri za kuivunja. Bila kutenda haki na kufuata sheria huwezi kuwa na amani ya kweli.  Hatuna haja ya kutetea waovu. Pia, hatuna haki ya kuwaonea bali kuwashughulikia kisheria.
            Makonda alipaswa kuhimiza vyombo vya dola kufanya kazi yake kwa weledi bila kumuonea wala kumpendelea mtu. Kuonyesha asivyojua dhana nzima ya utawala bora na wa sheria, aliongeza, “Kama wanataka kulalamikia haki za binadamu, basi waje kwangu.” Waende kwake kufanya nini na kama nani? Sijui kama Makonda anajua; yeye si bosi wa wanaharakati wa haki za binadamu. Bahati nzuri, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imeishamwita. Kama tulivyosema awali, THBUB itoe mapendekezo kwa rais yakiwemo kubatilisha uteuzi wake, kumfikisha mahakamani  ili kutoa onyo kwa maafisa wengine wa serikali kujali na kuheshimu haki za binadamu bila kujali ukubwa wa vyeo vyao.
            Tuchukue fursa hii kuwataka wapenzi na watetezi wa haki za binadamu, kulaani amri za Makonda aliyewataka waandamane kupinga mauaji ya polisi. Hii si kazi ya watetezi wa haki za binadamu. Mbona raia wengi wanauawa na majambazi? Mbona, huko nyuma, polisi waliua wananchi wasio na hatia lakini watetezi wa binadamu hawakuandamana zaidi ya kuishauri serikali kufuata sheria na kulinda na kuheshimu haki za binadamu? Watetezi wa haki za binadamu si vikaragosi vya ktumiwa na wanasiasa kama ambavyo Makonda anataka wawe. Pia watetezi wa haki za binadamu si mashabiki wa vyama bali wao humtetea yoyote awaye hata awe mhalifu ilmradi ni binadamu.
            Mimi ninayeandika, nilichukizwa na ung’ang’anizi wa madaraka wa muda mrefu wa Muamar Gaddafi kule Libya; ingawa sikukubaliana na namna alivyoangushwa na serikali za magharibi kulipiza visasi na kulinda maslahi yao. Wala sikukubaliana na namna Gaddafi alivyokamatwa na kuuawa kinyama. Nilitaka afikishwe mahakamani ili mahakama iamue kama alikuwa na hatia ya makosa aliyotuhumiwa au la.
            Hawa wanaotuhumiwa kuua polisi bado ni watuhumiwa tu. Chini ya dhana ya presumption of innocence bado ni watuhumiwa hadi pale wakapofikishwa mahakamani, kusikilizwa, kujitetea, kutolewa ushahidi na kupatikana na hatia au la. Hata wakikutwa na hatia, hawatapigwa mawe wala nini bali watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria. Taifa la amani na huru kama Tanzania haliwezi kuendeshwa kwa jazba za watawala. Litaendeshwa na kanuni na sheria kama zilivyoainishwa katika katiba na vitabu vingine vya sheria.
            Kwa vile rais John Pombe Magufuli ameonyesha kutovumilia wateule wake wanaovurunda, anangoja nini kumwajibisha Makonda au kuna black sheep na sacred cows kwenye serikali yake? Tulishaonya na si mara moja wala mbili; kuna siku Makonda atamuaibisha bosi wake kiasi cha kuanguka ghafla kama alivyopanda.
            Ukandamizaji wa haki za binadamu na kutofuata utawala wa sheria si jambo jipya kwa Makonda. Rejea alivyowaweka watendaji wa manispaa ya Kinondoni ndani kinyume cha sheria kabla ya kuwalisha wengine viapo bila stahiki.
            Kilichomkweza Makonda ndicho kitakachomshusha.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
↧
↧

When Junior and Senior Engage

September 7, 2016, 4:13 am
≫ Next: Kijiwe chamstua dokta Kanywaji asiambukizwe majipu
≪ Previous: Kilichomkweza Makonda ndicho kitakachomshusha
$
0
0
We decided to take a walk.
We then had a talk
As parent it was my work
Listening was Junior's work
What a walk!
What a talk!
A well done work

↧

Kijiwe chamstua dokta Kanywaji asiambukizwe majipu

September 7, 2016, 4:17 am
≫ Next: Walioghushi wafungwe maisha na kutaifishwa
≪ Previous: When Junior and Senior Engage
$
0
0

 
            Juzi Mgoshi Machungi aliibahatika kuhudhuria mapokezi ya mkiti mpya wa Chama Cha Majipu, sorry Magamba, sorry, Mapandikizi (CCM) ambapo mkuu wake mpya alikuwa akirejea mjini baada ya kuizulu kaya lau kuonyesha makali na makucha yake ukiachia mbali kueleza mipango yake kwa wachovu.  Mgoshi alimfagilia sana munene kwa kuweka mambo hadharani kuwa chama chake ni bonge ya genge la mafisadi ambalo–licha ya kumilki vitega uchumi kibao–bado linaombaomba kila unapokaribia uchakachuaji kama alivyosema.
            Mgoshi analianzisha, “mmesikia mkuu aivosema kuwa chama chake ni genge la mafwisadi? Hakika waiosimamia uchafu na ufisadi huu ni majipu yanayomzunguka dokta Joni Kanywaji Makufui. Hivyo, anapswa kutahadhai yasimuambukize majipu kama siyo kumdhuu tokana na kugusa ulaji wao wa dezo.  Anapaswa kutumia hekima ya Yesu kuwa watakaomuambukiza majipu ni wale anayekula nao meza moja.”
Kapende anakula mic, “munene huyu alifanya kazi nyeti kweli kweli kiasi cha kuwavutia baadhi ya wanakijiwe nikiwamo mimi. Pamoja na dokta Kanywaji kuniridhisha sina shaka na baadhi ya mambo hasa baada ya kuonyesha anachopanga kufanya.”
            Mipawa anamchomekea Kapende, “mie sikushangaa kuona analaumu uoza chamani mwake huku akiwakingia kifua waliousababisha na kuuacha ugeuke kansa na jipu la kunuka yaani wanene wastaafu. Hatuna haja ya kurudia; kila mchovu anajua munene alivyosema tena hadharani na kwa kinywa kipana bila tena kunywa kuwa atawalinda wastaafu kwa gharama yoyote bila kujali uoza na uovu walioutenda. Hapa aliniacha hoi kiasi cha kuanza kuona kama kinachoendelea ni mchezo wa sanaa ambapo wanaoshughulikiwa ni wadogo huku wanene wakiendelea kupeta.”
            Kanji anakula mic, “yeye nakuna veve. Naacha mimi hoi. Iko sangaa kwanini safisha jumbani toka nje badala ya vunguni? Hapana ona kitandani yake jaa hii yote natetea?”
            Msomi Mkatatamaa anachumpa na mic, “tokana na spidi yake ya roketi kwenye kushughulikia dagaa, wapo wanaohofia kuwa kitendo chake che kuendelea kuwa karibu na majipu manene ambayo anaonekana kutoshughulikia, kunaweza kumwambukiza daktari mwenyewe majipu kiasi cha kuwa mgonjwa a majipu au jipu. Hili halihitaji shahada kwenye elimu ya siasa. Ukitaka kujua namna uambukizo huu wa hatari unavyoweza kufanyika–mbali na majipu staafu yalomzunguka daktari–tazama, majipu yaliyomzunguka. Hapa hatujaongelea mikashfa ya kunuka kama UdA, Escrew, SUKITA na mengine mengi ambayo yaliwahusisha baadhi ya makamanda wanaounda timu ya utumbuaji wakati wao ni majibu yanayonuka.”
            Mheimiwa Bwege anapoka mic na kusema, “dawa na usalama kwa dokta kuepuka majipu ni kuhakikisha anavaa glovu wakati wa kuyatumbua na kuhakikisha kuwa hayamkaribii popote alipo. Kwani yeye hafanyi kazi ya utume kama alivyosema Yesu kuwa alikuja kwa ajili ya wenye dhambi; hivyo, alikula nao. Dokta hapaswi kula na wagonjwa bali kuwatumbua majipu.”
            Mgoshi anamchomekea Msomi, “ngoja nikuchomekee ushahidi kidogo; hivi Bii Ukuuuviii aiyetuhumiwa kughushi si jipu kwei? Sijui majipu kama haya yanaweza kusaidia nini katika kutumbua mengine? Hata ukiangaia hicho chama chenyewe unashangaa. Kwani, waiokifinya kuwa jipu ni nani kama siyo hao hao wanaoimba sifa za dokta mtumbua majipu wasijue wao ndiyo majipu yenyewe. Sijui kama Andaaman Kinamna pale chamani si jipu. Maana, madudu yote yaiyokitafuna chama hadi kikafikia hata kutaka kumeguka yaifanyika chini yake na afiki yake aiyemteua baada ya kumpigia debe na kuukwaa ukuu aiotumia kama kijiko kwake na marafiki na famiia yake kujitaiirisha kwa kuwaibia wachovu.  Hivi kwei Kinamna ana jipya gani wakati muda wote likaa kwenye chama amekijenga kifisadi badaa ya kukisafisha? Hata hivyo, angesafishaje wakati naye aikuwa akifanya vitu vyake kama vie kampuni ake kudaiwa kusairisha vipusa nje na asifanywe kitu kutokana na wakati ue kaya kuwa kwenye outpiot? Nadhani huyu hana tofauti na Ombeeni Sifui aiyekuwa pale ikuu akipiga dii hadi dokta Kanywaji aipomtumbua. Kaka tumbua na huyu Kinamna kwani sifa zake zina namna.”
Mijjinga anakula mic, “hakuna aliponiacha hoi dokta kama kugusia namna chama kilivyo na mali nyingi kilichoiba kwa wachovu ila hazina faida kwa yeyote isipokuwa mafisadi wenye vyeo chamani. Hivi chama hiki nacho si jipu kweli? Kwanini kinusurike wakati kilinyakua ardhi ya umma wa walevi na kujilimbikizia kinyume cha sheria?”
            Kabla ya kuendelea Sofia Lion aka Kanungaembe anamchomekea, “ajabu ya maajabu, chama kile kile eti hakikuruhusu watu wajimilkishe maeneo makubwa ya ardhi kwa vile ni ukabaila wakati chenyewe ni chama kabaila?  Kuna haja ya wachovu kuanza kujiandaa kisaikolojia kulikabili hili genge na kutaka lirejeshe ardhi mali zao. Pia watamke wazi kuwa sera zake ni ubwanyenye na ukabaila lakini si vinginevyo. Huwezi ukamwaga nyama na mifupa ukabaki na mchuzi ukasema hujali nyama ya kile ulichomwaga. Ukabaila–tena wa kunyakua viwanja vya umma–ni unyama na jinai hasa kwenye kaya inayojinakidi kutenda haki na usawa kwa wote.”
            Leo wachangiaji wengi wamechonga sana kiasi cha kuwanyima wengine nafasi. Hata hivyo, tunachojali ni mipwenti. Naona yule ndege anacheka huku akitikisa kichwa na kushangaa!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
 
↧

Walioghushi wafungwe maisha na kutaifishwa

September 10, 2016, 6:01 am
≫ Next: Tanzania ni zaidi ya Ukuta na CCM
≪ Previous: Kijiwe chamstua dokta Kanywaji asiambukizwe majipu
$
0
0

                        Baada ya kuinyaka hivi karibuni kuwa baadhi ya vihiyo vilaza na vigushi wanaanza kujiondoa kwenye ofisi za umma, nimestuka na kupaswa kutoa angalizo kama mtaalamu wa masuala yote ya uhusiano wa binadamu, elimu, jinai na madude mengine yenye majina magumu ambayo yanaweza kukutia kichaa kama si kizunguzungu na kihindihindi kama nitayaorodhesha hapa. Naona yule anatikisa kichwa akidhani ni utani. I am serious; if I jolt down all stuff that I know, you’ll lose your head dear. Hayo tuyaache.
            Tokana na kuchukia rushwa, ukihiyo na wizi wa njuluku za umma, natoa mapendekezo yafuatayo kuhusiana na vihiyo waliojazana kwenye ofisi za umma wakihomola wakati hawana sifa wala uhalali.
Mosi, washitakiwe wote bila kujali wameacha au kuachishwa au kuendelea na kazi. Hawa ni wahalifu kama wahalifu wengine wanaopaswa kuwa lupango na si uraiani wakitukoga na njuluku zao za wizi.
            Pili, kwa wale ambao wameng’ang’ania ulaji wakati wanajijua ni vihiyo watimliwe na kuswekwa ndani wakingoja kiama chao.
            Tatu, watakaokuwa wamejiachisha kazi wakidhani yamekwisha nao wafuatwe huko waliko na kusweka rumande wakati wakingojea pilato awahukumu na kunawa mikono yake. Niliwahi kusikia mlevi fulani akisema eti lisirikali limeamuru wanaojijua walighushi wajiachishe kazi kabla ya kufikishwa kwa pilato. Lisirikali linatoa ushauri huu wa kipuuzi kama nani wakati na lenyewe lilizembea kiasi cha kuajiri vihiyo. Hili nalo ni jipu linalopaswa kutumbuliwa. Kwani ndilo hilo hilo lililoruhusu kaya kuwa kaya hewa ambapo karibu kila kitu ni hewa, mishahara hewa, wafanyakazi hewa, wanafunzi hewa, wanasiasa hewa, wasomi hewa, bila shaka kuna ndata na ndutu hewa hapa kayani so to speak. Uzuri ni kwamba hakuna walevi hewa. Walevi ni walevi tu; kwa vile wao ni wapigikaji nani anataka awe hewa wakati maisha hewa ya utawala hewa yalishamkamua hewa kiasi cha kubaki hana hili wala lile?
            Nne, wote watakaobainika kuwa vihiyo na vilaza lazima warejeshe mishahara na marupurupu yote waliyofaidi kwa muda wote waliokuwa kwenye ajira wakati hawakupaswa kuajiriwa kwenye nafasi husika.
            Tano, wanyang’anywe mali walizochuma tokana na kutumia vyeti feki
            Sita, wachapwe bakora hadharani ili liwe somo kwa wengine.
            Saba, kuna haya ya kujua mantiki ya vihiyo kuajiriwa. Kama ni kutokana na vimemo vya wanene, na hao wanene wawajibishwe kwani kisheria wanaitwa accomplices au accessories to committing a crime. Hii kaya si ya mama zao. Nao lazima waonje joto ya jiwe. Utakuta wengine ni vihiyo pia wanaotetea vihiyo wenzao kwa kutumia unene wao.
            Nane, hatuwezi kuzeekea na kupofukia darasani hadi tunavaa miwani ili kupata elimu wakati wengine wanaogopa umande na kutanua. Mimi hadi napata PhD zangu nilisota kwelikweli hasa ughaibuni ambako nililazimika kufanya kila aina ya kibarua halali ili kujikimu.
Pia nashauri twende mbele zaidi na kuhoji utendaji wa maafisa wetu hata kama wana shahada orijino. Maana mijitu mingine huenda vyuoni kukariri kama kasuku lakini vikija kwenye utendaji unakuta ziro kabisa. Hivi, hichi kitegemezi alichoteua mkuu hivi karibuni kilichosema eti haki za binadamu ni wendawazi kweli kimeelimika au kukariri tu? Hivi kile kidogo kilichojipiga kifua kuwa kitajenga makao makuu ya dini fulani kweli kimepiga book au ni kukariri na kubebwa bebwa na kujikomba na kujipendekeza kwa wapenda kuabudiwa?
            Tumalizie kwa kuonya kuwa katika zoezi hili kusiwe na aina yoyote ya kujuana, kulindana, kufadhiliana au kuokoana. Walioghushi ni wahalifu wa kawaida wanaopaswa kuishia magerezani hasa ikizingatiwa kuwa kwa ukihiyo na ukilaza wao wamelitia taifa hasara isiyo mithalika.
Mlevi  wa Mpigakaya Phd (Education dynamics).
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
↧
↧

Tanzania ni zaidi ya Ukuta na CCM

September 12, 2016, 5:07 pm
≫ Next: Ahadi za kunasa wazungu wa bwimbwi vipi?
≪ Previous: Walioghushi wafungwe maisha na kutaifishwa
$
0
0
Image result for katuni za ukuta na ccm
          Hakuna ubishi; taifa letu liko njia panda; hasa baada ya kujitokeza kile kinachoonekana kama uvunjaji wa katiba na upingaji wake. Kuanzishwa kwa Umoja wa Kupinga Udikteta Tanzania (UKUTA) ni matokeo ya serikali kupiga marufuku vyama vya siasa kufanya mikutano na maandamano ambazo ni haki zao kikatiba. Hakuna kumung’unya maneno; kisheria, serikali haina mamlaka ya kuzuia vyama vya siasa kufanya shughuli zake kama zilivyoainishwa kikatiba.
Baada ya katazo hili,  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)–ambacho kilikuwa mwanachama wa Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi (UKAWA) hoja ambayo iliuawa wakati wa uchaguzi–ilikuja na UKUTA. Serikali kwa upande wake, haikutaka kusikia hili wala lile. Hivyo, ilivipiga marufuku. Mgogoro unaoendelea unajulikana kwa kila mmoja mwenye kufuatilia. Hivyo, hatutapoteza muda kuelezea chimbuko lake zaidi. Hata hivyo, kuna haja ya busara kutumika badala ya maguvu na kutunishiana misuli. Tanzania si mali ya wanasiasa bali watanzania. Je kwanini serikali haitaki kuja na maelezo yanayojitosheleza na kufuata sheria kufikia uamuzi wake ambao hadi sasa ni batili kwa vile haina mamlaka ya kufanya hivyo?
          Je kama taifa litaingia kwenye machafuko kutokana na kichwa ngumu ya pande moja au pande zote kama taifa tutapata faida gani? Nadhani misingi ya demokrasia ni pamoja na majadiliano, kukubali kushinda na kushindwa katika kila jambo. Nawapongeza UKUTA kwa kuahirisha maandamano yao. Nadhani hii imefanyika kutoa nafasi kwa serikali ima ifikiri upya au ijadiliane na UKUTA na kufikia muafaka. Katika mgogoro wowote, huwa kuna hatua kadhaa uzopitia. Kuna kipindi cha mihemko (flare-up) kunakofuatia na kipindi cha hasira kuyeyuka (thawing) inayofuatia na  kuanza kuuona na kuukubali ukweli (sobering) ambayo nayo hufuatiwa na kuanza kujitoa kwenye kizingo au kujifungia (getting out of the enclave) na mwisho, kuchukua hatua (addressing the conflict). kwa hatua tuliyopo sasa ni flare up kwa upand wa UKUTA ambalo ni jambo jema. Ili kusonga mbele, upande wa pili yaani serikali inabidi itoke kwenye enclave na kujibu kwa mwitikio chanya ili kumaliza tatizo. Na inapofanya hivyo, isitafute fursa ya kuwazidi kete wapinzani (time buying).
          Kitaalamu, kuna namna tofauti za kuushughulikia m[i]gogoro. Kuna kushindana (competition), kukubali yaishe (compromise), kuacha mambo yajiendee (accommodation), kutunisha misuli (confrontation), kujadiliana (negotiation) na kusuluhisha (mediation). Hapa uhitajika watu mashuhuri hasa kwenye mgogoro kama wa sasa kama vile Kofi Anan na viongozi wengine wa kisiasa wenye ushawishi na uzoefu wa kutatuzi wa migogoro. Wahusika wanaweza kuchagua nini wafuate hapa.
          Sasa nizame kwa ufupi kwenye mgogoro. Je katiba inasemaje kuhusu hiki kinachotaka kulipeleka taifa kwenye maangamizi ya kujitakia; na nani yuko juu ya katiba ukiachia mbali aliye sahihi?
          Majibu anayatoa mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe aliyekaririwa hivi karibuni akisema“sisi tunataka nchi iongozwe kwa kufuata sheria na siyo matakwa ya viongozi ambayo yanakinzana na sheria na Katiba ya nchi.” Hoja hii ina mashiko na ndiyo inapaswa kuwa dira ya kuelekea mgogoro huu uliozaa UKUTA. Mbowe anaongeza “tukiamua sote kujifanya wanafiki kusema hewala, nchi haitakuwa salama; itazaa taifa la watu wenye hofu na ndiyo sababu tumeamua kamati kuu kuanzia sasa kufanya kazi kila siku kuisaidia sekretarieti.”
          Mchango mwingine unatoka sehemu ambayo haikutegemewa, jeshi la polisi ambalo msemaji wake Advera Bulimba alikaririwa hivi karibuni akisema “tutawaita na tutazungumza, naomba tujaribu tu kuvuta subira.” Kinachogomba hapa ni ukweli kuwa jeshi la polisi liko mikononi na chini ya serikali. Hivyo, halina sifa wala uzoefu wa kutatua mgogoro kama huu japo mawazo yake ni mazuri. Polisi wameonyesha ukomavu kama hawatabadilika au kutishwa na kufanya tofauti na wanavyosema kama ambavyo imekuwa ikitokea kwenye kuukandamiza upinzani nchini. Je wananchi wa kawaida wamepewa nafasi gani katika kutafuta suluhu? Wakati polisi wakipendekeza kuzungumza waziri wa Mambo ya Ndani Mwigulu Lameck Nchemba alikaririwa akitoa vitisho kuwa serikali ya sasa si kibiriti cha njiti bali cha gesi. Hii si lugha ya mtu mwenye kutaka kujadiliana. Je jeshi la polisi na bosi wao tumwamini nani?
Waziri alikuwa akirudia maneno ya bosi wake yaani rais John Magufuli aliyekaririwa mwishoni mwa mwezi Julai akisema “wasinijaribu kwa kulazimisha maandamano siku ya tarehe moja Septemba…atakayethubutu kufanya hivyo, kitakachompata mmmh, hatasahau kamwe. Mimi ni tofauti sana, wasije wakanijaribu.”
Magufuli aliongeza “Kama wewe ni Mbunge wa Jimbo la Hai (kwa sasa Freeman Mbowe), zunguka kwenye jimbo lako hadi uchoke, si unaacha kwako unaenda Shinyanga kushawishi watu waandamane. Mimi sijazuia shughuli za waliochaguliwa kwenye maeneo yao, bali nimekataa mtu kuondoka jimboni kwake na kwenda kufanya fujo mahali pengine.” Je hapa rais aliongea kama nani wakati katiba iko wazi kuwa watanzania wana haki ya kutoa na kupokea mawazo yao, kusema watakacho na kwenda watakako bila kuvunja sheria? Kwanini serikali isijibu hoja zinazofanya wapinzani kuandamana badala ya kutunisha misuli? Kama wapinzani wanadai Tanzania inaongozwa kidikteta, wanaotuhumiwa wanapaswa kuonyesha uongo wa madai haya badala ya kutoa vitisho. Nadhani hapa ndipo hitajio la majadiliano lilipo. Kwanini rais asiwaite wapinzani akataka wathibitishe madai yao huku naye akionyesha uongo wa madai yao na mambo yakaisha kistaarabu na kwa amani? Inapaswa rais Magufuli ajue yeye ni mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) sawa na wenyeviti wa vyama vingine vya kisiasa. Anachowazidi ni urais ambao nao ukiulinganisha na hoja na umoja wa wapinzani, inakuwa ngoma sawa. Hivyo, tunashauri wahusika wajadiliane badala ya kutunishiana misuli; haijengi bali kubomoa. Nafasi haitoshi. Ila kwa ufupi ni kwamba wahusika wote wajue kuwa asiyekubali kushindwa si mshindani; na Tanzania ni zaidi ya CCM na UKUTA na UKAWA.
          Mwisho wa yote, lazima katiba yetu iheshimiwe. Tusijiruhusu au kuruhusu ichezewe au kuvunja. Hili haliwezi kukubalika hata kidogo. Bila mazungumzo, damu itamwagika tokana na ukosefu wa busara na utumiaji vibaya madaraka. Nadhani wajibu wa kwanza kabisa wa rais na serikali yake ni kulinda katiba na siyo kuivunja au kuitumia kwa maslahi binafsi kisiasa. Wenye akili wameelewa. Tanzania ni mali yetu sote kwa sawa bila kujali madaraka ya mtu au kundi lake.
Chanzo: Tanzania Daima.
↧

Ahadi za kunasa wazungu wa bwimbwi vipi?

September 14, 2016, 6:59 pm
≫ Next: Naja na UKUTA dhidi ya deni la kaya na marahis wastaafu
≪ Previous: Tanzania ni zaidi ya Ukuta na CCM
$
0
0
Image result for katuni za wauza unga
          Baada ya kushuhudia zinavyozikwa kashfa kama vile Escrow, Lungumi, UDa na nyingine nyingi, kijiwe kimeamua kukumbushia na kuhoji ilikoishia vita ya kuwanyaka wazungu wa bwimbwi. Baada ya zungu la ungu jirani yake na Kapende kununua bonge ya nyumba anayopanga Kapende, anaamua kukilazimisha kijiwe kurejea kadhia hii ambayo wanene wengi wanaiogopa.
            “Mwenzenu sina raha leo,” Kapende analalamika. “Kwanini ndugu yangu na nini kimekusibu? Anauliza Mbwamwitu.
            Kapende anajibu, “mwenzenu sina pa kulala baada ya kupewa notisi ya haraka ya miezi mitatu baada ya zungu la unga jirani kununua nyumba kana nane hivi ili kujenga casino kwa ajili ya kuchezesha kamari.”
            “Wewe una bahati wala hupaswi kulalamika. Hukuwasikia wenzako wa Migomigo Kota walivyokuwa wametapeliwa na site hadi mzee mwenye dokta Kanywaji akaamua kuingilia na kuokoa ngoma? Nenda kwa dokta Kanywaji upeleke malalamiko. Huyo dingi wa bwimbwi atanyakwa kama wale jamaa zetu wa NSSF waliokuwa wakitaka kutuuzia uwanja Kigamboni mabilioni. Sijui nao wameishia wapi?” anajibu Mipawa huku akibwia gahawa yake.
            “Wale miji ya NSSF sasa naoze pango hadi sirika yao ya bedroom napata bwana nyingine. Kama na uza bimbi nasugulikiwa kama hii kuba ya NSSF iko zani sasa kaya kuwa huru kabisa bila bimbi. Mimi dhani ile uza bimbi hapa sikwa. Veve nafanya chezo. Ile honga data na kubakuba nyingine wakati hii ya NSSF kuwa choyo kula peke yake dio maana nasikwa natupa pango rahisi.”
            Msomi Mkatatamaa aliyekuwa akibofya ki-Samsung 7 Galaxy anakiweka pembeni na kula mic, “ushauri wako brother Mipawa ni mzuri ila ufahamu kuwa hapa kwenye kaya–pamoja na vitisho na ukali wa dokta Kanywaji–kuna wadude hawaguswi. Hawa ni wale wa Escrow, Lungumi na UDa. Hebu jiulize. Tangu aingie kwenye ulaji hawa wajambawazi wamefanywa nini zaidi ya yule wa UDa kugawiwa mangwalangwala yaendayo kasi? Niambie ni wauza bwimbwi wangapi wamekamatwa wakati wabwiaji maeneo ya Lumumba, Migomigo na kwingineko wanazidi kuongezeka?”
Mpemba anakula mic, “yakhe nkubaliana nawe. Hii vita ya wauza bwimbwi ni danganya toto wallahi. Mie alipoapishwa huyu waziri wa mambo ya chumbani apendaye kuvaa magwanda na bendera ya kaya nilijua ndo kilikuwa kiama cha wauza bwimbwi nisijue ataja wagwaya na kukimbilia kuvaa magwanda ya ndata.”
            Mijjinga anamchomekea Mpemba na kusema, “hii kitu ogopa sana. Huu mtandao si cha mtoto. Mara hii mmesahau alivyodedishwa Amina Chifwupa alipojitiatia kula huku na kule? Nani awakamate wauza bwimbwi wakati wao ni lisirikali ndani ya lisirikali. Hamuwaoni wanene wa bwimbwi wanaotanua chamani au mpaka tutaje majina?”
            Mgosi Machungi aliyekuwa kimya akivuta tasbihi yake anaamua kula mic, “usemayo ndugu yangi ni kwei tupu. Kia siku wanasema titakamata wauza bwimbwi akini hatuoni hata mmoja akikamatwa. Wakijifaagua wanakamata wabwiaji ambao nao wameishapigika. Kwanini wasiwabane hao wabwiaji wakawaonyesha wanaowauzia nao wakawaonyesha wanaowauzia hadi ndata wanaowalinda kama kwei wamezamiia au ni mapambano hewa hasa ikizingatiwa kuwa kaya yetu ni ya kia kitu hewa?”
            Sofia Lion aka Kanungaembe anaamua kula mic, “nami nakubaliana na Mgoshi hasa ikizingatiwa kuwa kwa sasa wahusika wanasema mengi na kutenda machache. Kunasa wauza bwimbwi ni rahisi kama alivyosema Mgoshi. Kamata wabwiaji wakuonyesha wanaowauzia na wanaowauzia wawataje wanaowauzia hadi mazungu yenyewe. Pia nashauri wahusika waangalie namna ya kuwabana matajiri uchwara wa kuibuka ghafla bin vu wataje walivyochuma utajiri wanaoringia wakati ni jinai tupu. Bila kufanya hivi, tunapoteza muda; na hakuna haja ya kutupigia mikelele na vita dhidi ya bwimbwi wakati biashara yenyewe inazidi kushamiri hasa wakati huu dokta Kanywaji alipoamua kubana kila kitu.”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kula mic, “da Sofi kumradhi sana. Ngoja nikuchomekee kidogo,” kabla ya kuendelea kijiwe hakina mbavu namna mheshimiwa Bwege anavyoomba kumchomekea da Sofi.
            Anaendelea, “kusema ule ukweli, sidhani kama biashara ya bwimbwi itakuja iishe hasa ikizingatiwa kuwa watumiaji wengine ndiyo hao hao wanaopaswa kupiga vita balaa hili. Mara hii mmesahau namna mzee wa Mjengo Jobless alivyosema kuna waishiwa tena waliopo mjengoni wanavyobwia hii kitu nao wasikanushe? Hapa unategemea nini kama siyo kufungana kamba. Kamateni mtutangazie kama mnavyotangaza waliotumbuliwa bila kujali ukubwa wa vyeo vyao. Simple.” Anapiga chafya na kuendelea, “kama walivyonena wanenaji wa awali, bwimbwi, Lungumi, Escrow na UDa ni sirikali ndani ya sirikali tena yenye siri kali sana tu. Heri wajinyamazie kama ishara ya kushindwa.”
            Mzee Maneno anakula mic, “kama tumeshindwa kama kaya kupambana na mibwimbwi basi wanyonge tumekwisha. Kwanini tusitumie ujasiri tunaotumia kuwachoma vibaka tuwachome wazungu wa bwimbwi ambao wengi wanaishi nasi’ na tunawajua kwa majina hata sura kama kweli tunachukia jinai hii? Hata dogo wa wendawazimu wa haki za binadamu simsikii akilaani wauza bwimbwi au kule hakuna ujiko na kama upo ni wa hatari?”
            Kijiwe kikiwa ndiyo kinanoga, si akapita teja moja. Wote tuligeukiana na kuangaliana kwa mshangao hasa ndata alipopita akimfuata nyuma bila kumtia nguvuni! Ama kweli ukishangaa ya Escrow, Lungumi na UDa, utaona ya wazungu wa unga!
Chanzo: Tanzania Daima leo Jumatano.
↧

Naja na UKUTA dhidi ya deni la kaya na marahis wastaafu

September 17, 2016, 10:13 am
≫ Next: Kijiwe chawalilia wahanga wa tetemeko
≪ Previous: Ahadi za kunasa wazungu wa bwimbwi vipi?
$
0
0

            Baada ya lisirikali kuwahi kupendekeza kupunguza mishahara ya wanene ili kubana matumizi yasiyo na tija kwa kaya, nilihisi kama kuna ubaguzi. Rahis–kwa kuonyesha mfano–aliagiza mshahara wake ufyekwe ili wengine wafuatie. Ajabu ya maajabu, rahis alisahau kufyeka marupurupu ya watangulizi wake ambao wengi wao walisababisha kutuna kwa deni la kaya tokana na kupenda kwao kutanua na kuzurura hadi wakapachikwa jina la Vasco da Gama, jambazi aliyezunguka dunia akiteka na kuiba.
            Kuunga mkono hatua hii adhimu, Mlevi naja na Umoja wa Kupambana na Ukata Tanzia. Tafadhali, msichanganye huu UKUTA wangu na ule wa wapingaji wala zile ghilba za vijana wa Chama Cha Maulaji (CCM) wa kujigonga kwa munene kwa kutaka kufanya maadamano ya kumuunga mkono wakati anatimiza wajibu wake ukiachia mbali kujikomba kwake kama mzee wa Kirara baada ya kupewa ulaji wa dezo.
            Natoa maangalizo na mapendekezo yafuatayo:
            Mosi, hakuna mantiki kwa dingi wa kaya kufyeka mshahara wake na wanene wengine huku akiendelea kujipinga kwa kuwapa ulaji wanene waliomtangulia kama vile marahis, makamu na mawaziri wakubwa waliopita wakati wengi wao walichofanya; na wanachofanya ni kula tu tena kwa dezo. Hivi wazururaji na watanuaji waliotunisha deni la kaya wana stahiki gani ya kuendelea kukirimiwa njuluku wakati walipaswa kuwa lupango kwa madhambi yao kwa kaya? Najua hili halipendezi kwa walaji wetu. Hata hivyo, kwa wenye akili na uchungu wa kweli na kaya, hii ni habari njema isiyopaswa kupuuzwa. Huwa nashangaa kuona marahis waliokwishafungasha virago kuendelea kupewa walinzi, wafagizi na makandokando mengine kana kwamba walizaliwa nayo.
            Pili, nasema bila kumung’unya. Huu ni wizi wa njuluku za umma ukiachia mbali kuwa matumizi mabaya yanayopingana na dhamira ya rahis kupunguza matumizi uchwara na ya kijambazi.
            Tatu, kuna haja ya kutenda haki kwa kuonyesha kuwa walevi wote ni sawa sawa na wanavyotwishwa zigo lililosababisha na utawala mbovu na wa kijambazi ukiachia mbali wa kilimbukeni uliowekeza kwenye kusafiri badala ya kusafisha kaya tokana na ufisadi na uovu kila aina.
            Nne, kufyeka maulaji wa wanene wastaafu ni njia mojawapo ya kuwawajibisha kinamna ukiachia mbali kupima uzalendo wao.
            Tano, kufyeka marupurupu ya wanene wastaafu, kutawapa fursa ya kuonja matunda ya kazi chafu waliyofanya ya kushindwa kusimamia uchumi wa kaya na kutumia vibaya njuluku za walevi.
            Sita, kufyeka maulaji ya wanene waliojazana kayani, licha ya kutenda haki, ni kuwakumbusha kuwa hakuna aliyeko juu ya sheria; na ukipanda miiba utavuna miiba na si maua kama wengi ambavyo wamekuwa wakidhani hasa baada ya munene kuwakingia kifua kuwa hatawafikisha kwa pilato baada ya baadhi ya walevi kutaka wafikishwe kule wakatubie madhambi yao au kuwajibishwa kwayo.
            Saba, haiwezekani walevi wachovu wadaiwe kila mmoja dola zaidi ya 1,000,000 huku wazembe na wabangaishaji waliosababisha balaa hili wakiendelea kupiga njuluku. Kitaalamu hii huitwa political mission to town ambayo inapaswa kukomeshwa mara moja once and for all. Hadi sasa sijaelewa namna gani vichanga visivyo na hatia vinavyofyatuliwa kudaiwa njuluku nyingi kama hizi wakati bado ndiyo vinaanza mtihani wa kudai maziwa, nepi, yaya na makandokando mengine toka kwa waliovifyatua.
            Nane, ukiachia mbali maangalizo na ushauri niliotoa hapo juu, naweza kusema bila woga kuwa kufyeka makulaji ya wanene wastaafu licha ya kurejesha nidhamu na uwajibikaji pale mlevi anapoangukia maulaji, kutasababisha yafuatayo:
            Mosi, kutatoa picha kwa wale wanaodhani kuwa dhamira ya kubana matumizi ni maigizo kutia akilini.
            Pili, kutapunguza wahusika wajao kuendelea kugeuza ofisi na maulaji ya umma vijiko vya ulaji kwao, familia na marafiki zao ukiachia mbali waramba makalio yao.
            Tatu, kufyeka maulaji ya wanene wastaafu, kutawafanya waanze kuota joto ya jiwe itokanayo na mauzauza waliyofanya tokana na ujinga, uchoyo na upogo wao.
            Nne, sifanyi hivi tokana na roho mbaya au husda bali usongo wangu wa kutenda haki kwa usawa hasa usawa huu wa kuwajibishana bila kuoneana aibu hata inapobidu kutumbuana.
            Tano, utitiri na ukubwa wa marupurupu ya wanene wastaafu nalo ni jipu ambalo watumbuaji hawapaswi kulionea aibu au kujifanya hawalioni. Sijui kwa mwaka tunapoteza mabilioni mangapi ya madafu kulipa wanene ambao wengi wao waliishajilipa nyuma ya pazia?  Nashauri wahusika wasome kitabu changu cha NYUMA YA PAZIA.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
↧
Search

Kijiwe chawalilia wahanga wa tetemeko

September 20, 2016, 7:04 pm
≫ Next: Mlevi aja na suluhu kwa hasara zitokanazo na majanga
≪ Previous: Naja na UKUTA dhidi ya deni la kaya na marahis wastaafu
$
0
0

           Image result for photos of waathirika wa tetemeko kagera
            Baada ya kupokea kwa mstuko taarifa za kutokea kwa tetemeko huko mkoani Kagera, Kijiwe kilikaa na kutathmini baadhi ya mambo ikiwemo kuomboleza na kutuma salamu za rambirambi ambazo mzee Mzima niliteuliwa kuzifikisha baada ya kukusanya uchache wa mchango.
            Tokana na uzito wa suala lenyewe, Mheshimiwa Bwege ndiye alianzisha mjadala akisema “nadhani kila mmoja amesikia yaliyowasibu wenzetu kule kwa akina Nshomile very Much mulangila Rweyesimamia, Rwabukoba, Rwabuganda na wengine wengi.in fwact it was very very eavy staff.”
            “Hata mimi nilishangaa kusikia kuwa tetemeko limepiga tena Bukoba. Hatukuzoea mitetemeko zaidi ya ili ya kutumbuana majipu na ukiachia mbali yale ya zamani yaliyotokea Kagera zama za kizungumkuti cha ukimwi. Rafiki yangu Rwakatongo alinipiga simu akilalamika kuwa his mansion did not see the right of the day,” anajibu Mijjinga ambaye ndiyo anamkabidhi gazeti Mchunguliaji.
            Kapende anakula mic “hapa lazima nasi tuchangishane lau tuwatumia kidogo cha kuweza kuwasaidia katika kipindi hiki kigumu. Sijui mnaonaje wenzangu? Maana ukiangalia ukubwa wa janga lenyewe, lazima hapa tupigane jeki tena haraka sana. Leo kwao; kesho hujui ni kwa nani au vipi?”
            Mipawa anakula mic “umetoa wazo jema njomba sema usawa huu wa kugufulishana inakuwa vigumu hasa ikizingatiwa kuwa wazee wa kijiwe si waajiriwa wala mission town. Hata hivyo, mimi nitajitahidi kuchangia chochote kile nitakachoweza kujinyima. Tena nikitoka hapa lazima nende kumuona jirani yangu Kajuamlo nijue anapanga nini na kama ndugu zake wameathirika.”
            Mbwamwitu anauliza “nani atakuwa mweka hazina wa uchache utakaochangishwa?” Kabla ya kuendelea, da Sofia Lion Kanungaembe anamchomekea “uchache wenyewe haujachangishwa unaanza kuulizia mtunza mfuko! Unadhani uchache huu utapigwa nini wakati hapa hatuna mafisadi wala majizi?”
            “Dada huna haja ya kushangaa hasa kwenye kaya ya kuibiana. Hukusikia juzi juzi kuwa idadi ya wanafunzi hewa inazidi kutuna huku hata madawati yaliyochangishwa hivi karibuni mengi hayafikii kiwango tokana na wajanja kupiga njuluku. Unacheza na kaya hii ya Danganyika!” anajibu Kapende.
            “Usawa huu si wa kuaminiana hasa ikizingatiwa kuwa sisi hatutumbuani kama wao waliokula kitu wakatuacha apeche alolo. Hivyo, si vibaya kujua nani mshika fuko hasa ikizingatiwa kuwa dokta Kanywaji amebana kila kitu au vipi,” anachomekea Mkurupukaji.
            Mgoshi Machungi anakula mic “Si vibaya kujua atakayetunza njuuku hasa ikizingatiwa kuwa kwa nijuavyo kaya yetu, mnaweza kumpa mtu asiye mkwei akaamua kwenda kuoea hasa usawa huu wa kubaniana.”
            Msomi Mkatatamaa baada ya kuona mjadala unaamia kwenye njuluku anaamua kuokoa jahazi. Anakula mic “japo kuwachangia wenzetu ni wazo jema, sidhani kama wachovu kama sisi tuna haja ya kujibana na kubanana na kushikiana wakati lisirikali linajisifu linavyokusanya kodi na kuwa na njuluku kibao hata kutaka kuwajengea matajiri wengine makao makuu kama alivyosema hivi karibuni dogo Po Makondakonda. Nadhani huu ndiyo wakati wa sirikali kuonyesha mwelekeo na kuwajali wana kaya wake.”
            Kabla ya kuendelea Mpemba anamchomekea, “yakhe hapa unnena kitu mujarabu wallahi. Unkumbusha. Hatuna haja ya kubanana bali tuiambie sirikali iwajibike kuwaauni watu wake ati. Nijuavo mie ni kwamba kazi ya sirikali ni kushughulikia kadhia kubwa kubwa kama hizi ambazo wana kaya haweza kuzifutu binafsi. Sirikali ishakiri kuwa ina njuluku za kutosha kiasi cha kununua hata ndege mpya kwa npigo.”
            “Hiyo njuluku wanayoringa nayo iko wapi wakati nao wanachangisha na kuwaomba wafadhili wawasaidie kujisaidia kana kwamba hawawezi kujisaidia wenyewe? Nakubaliana na Msomi; mhatuna haja ya kuchangishana wakati sirikali ipo na ina minjuluku kibao. Ninachoweza kusema hapa ni kwamba tuhakikishe njuluku zinazochangishwa ziwafikie walengwa na siyo kuishia kuliwa na mafisadi wenye ulaji tayari,” anajibu Mipawa huku akibwia gahawa yake.
            Msomi anarejea “nashauri sirikali itumie fursa hii kuanza kuwatajirisha wachovu wetu ili wajenge nyumba bora imara na za kudumu zinazoweza kuhimili tetemeko lijalo. Pia napendekeza tuishauri sirikali itumie zile njuluku za kujengea Bakuata zielekezwe Kagera na siyo Kinondo au vipi?”
            Kanji anakula mic “hii tetemeko naleta huzuni kubwa hadi nalia chozi kuba sana mimi. Mimi iko panga kwenda ona Konda kuambia yeye ile juluku nakwisatenga jengea Bakata peleke Bukoba haraka sana.”
            Mzee Maneno anachomekea “hapa Makondakonda lazima achanganyikiwe. Maana kila mmoja anataka kusikia atakakuja na ipi. Wengi watampima hapa kujua anachotaka ni nini kati ya kaya na umaarufu. Maana haiwezekani akajengea Bakuata mjengo wa mabilioni wakati wanakaya maskini tena waliokumbwa na balaa la kimaumbile wanaendelea kulala chini tena kwenye msimu huu unaokuja wa mvua na baridi kali.”
            Kabla ya kumaliza Mijjinga anamchomekea “nimesikia wanene na wakwasi wengi wakitoa michango ila sijawasikia mabilionea kama akina Ni Ziro Kadamage, Jimmy Rugemalaya, Anna Kajuamlo Tiba na wengine wengi wenyeji wa kule au wao kazi yao ni kupiga njuluku na kutumia peke yao?”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si akapatia tapeli mmoja aitwaye Mulokozi akijidai kuchangisha njuluku ya kutuma kwa waathirika wakati tunamjua alivyo tapeli la kutupwa. Wafia poleni sana. Wanaochagia maafa, chunga sana.  Nahisi ardhi ikitetemeka! Kumbe ni pancha!
Chanzo: Tanzania Daima Kesho.
↧
↧

Mlevi aja na suluhu kwa hasara zitokanazo na majanga

September 25, 2016, 7:09 am
≫ Next: Umma ujulishwe sifa za wateuliwa
≪ Previous: Kijiwe chawalilia wahanga wa tetemeko
$
0
0

            Baada ya kutokea tetemeko la ardhi kule kwa akina Nshomile waitu, Mlevi nimeona ni vizuri niwamegee utaalamu na uzoefu wangu ili kuepuka hasara na mateso bila ulazima. Kwanza, nawapa pole wote waliokumbwa na mkasa huu hata kama ni kilevilevi. Mie ni bora kuliko wale wanaotaka kutapeli wenzao kwa kutumia msiba huu. Hilo moja. Pili, nataka nitoe baadhi ya maangalizo kwa wahanga hata wasio wahanga.
            Tatu, kama umebomokewa na ubavu wa mbwa wako au hekalu lako, usitegemee lisirikali kukujengea. Hiyo si kazi ya sirikali. Bahati nzuri rahis ameishafafanua hili kwa uwazi kabisa. Kwa hiyo wale waliokuwa wakiota mchana kuwa sirikali itawajengea mahekalu, waanze kushughulikia tatizo bila kulikuza. Nadhani hii imeleweka.
            Nne, najua hili gumu kidogo si kwa wahanga tu bali kaya nzima. Napendekeza sirikali itunge sheria ya kulazimisha kila mchovu kulipia mali zake kama tutakavyoziainisha hapa chini.  Hapa mlengwa ni sirikali na walengwa kuhakikisha hili linafanyika badala ya kuacha wahusika wapige politiki. Nadhani haya ndiyo masuala wapinzani wanapaswa kushupalia.
            Tano, kama kuna utaratibu wa bima ya mali inayohusisha mijengo, basi, hakikisha kila mwezi unalipia bima ya ubavu wako wa mbwa au hekalu. Kwa wenye mikweche, mashangingi na ngwalangwala au mikangafu wasisahau kulipa bima. Maana, hujui nini litakukuta na lini na wapi na kwa namna gani.
            Sita, napendekeza pia iwepo bima ya mke, mume na watoto ili kitokea mmojawapo akanyotoka roho kama ilivyotokea kwenye tetemeko au ajali nyingine lau familia ipate kifuta machozi. Najua wengi wasiozoea wataona ama hizi na bangi, ulabu au nawanga. Nope, siwangi; huu ndiyo ukweli hata kama ni uchungu. Kul nafsi zalikatu maut yaani kwa kiarabu, kila nafsi itaonja mauti. Kwa wale wenye nyumba ndogo wala wasipoteze njuluku kuzilipia bima; kwani, kisheria, hazipo. Hapa itabidi wahakikishe wanawabana wawakilishi wao kutafuta namna ya kuweka nyumba zao ndogo kwenye utaratibu mzima wa kulipa bima ya maisha na kifo.
            Saba, bima isiishie kwenye nyumba, mikangafu, mbavu za mbwa. Mahekalu na mashangingi. Kwa wale wanaomilki bunduki, mapanga hata tunguli lazima wayalipie bima. Naona yule anasonya kusoma tunguli. Kama bunduki yako ni silaha ya kukulinda, ina tofauti gani na tunguli wakati vyote vinafanya kazi ile ile japo kwa staili tofauti? Kwenye kaya za hovyo zinazosemekana zimeendelea wachovu wanalipia hata tattoo we unashangaa tunguli! Hiyo tuiache watu wasije kuanza kulipia hata makovu. Hata mie ile kitu navuta sijalipia bima kwa vile ni haramuni! Pia wanasiasa wasilipiwe bima kwa vile hawaaminiki. Unaweza kumlipia ukidhani yuko upinzani akaishia kuingia kwingine kama Lyatongolwa na Joni Choyo.
            Nane, shamba lako ilmradi lisiwe la bangi lazima ulilipie bima. Hapa lazima uhakikishe linapimwa na kupata hati. Kwani, bila hati ni sawa na halipo hata lingekuwa kubwa kama Bongo yote.
            Tisa, tokana na kashkash za kuzidi kughushi vyeti vya kitaaluma, sharti wenye vyeti kuanzia vya kuzaliwa, shahada, vitambulisho na nyaraka nyingine muhimu shurti zilipiwe bima hasa usawa huu vihiyo na vilaza vinahaha kupata vyeti ili viendelee kutanua badala ya kutanuliwa na kutumbuliwa.
            Kumi na mwisho, sirikali lazima ihakikishe inakuja na mfumo safi wa ulipaji bima ili kuepuka usumbufu, ucheleweshaji na utapeli yanapotokea maafa kama haya ya tetemeko. Pia tetemeko la utumbuaji lisimezwe na la ardhi. Pia epukeni matapeli akina Rweyependekeza, Rwebukanyia na akina Rweyetapelila.
            Tuonane wiki ijayo inshallah.
Chanzo: Nipashe Jumamosi jana.
↧

Umma ujulishwe sifa za wateuliwa

September 25, 2016, 7:13 am
≫ Next: Happy Birthday Nkuzi
≪ Previous: Mlevi aja na suluhu kwa hasara zitokanazo na majanga
$
0
0

            Kwa wanaokumbuka enzi za utawala wa kwanza chini ya marehemu Mwl Julius Nyerere, watakumbuka uwazi uliokuwapo karibu katika masuala mengi. Mfano, tulizoea kusikia rais akifanya uteuzi jambo ambalo hadi sasa linaendelea kutokana na kazi na mamalaka aliyopewa. Hata hivyo, tangu kuondoka kwa Mwalimu, kuna mambo mengi ya kiwajibikaji na muhimu yaliuawa kutokana na kuwa na viongozi wasio makini au wanaofuata mkumbo tu kama si kuficha maovu fulani katika utumishi wa umma. Ilifikia mahali hadi idadi na majina watu wanaokuwa kwenye msafara wa rais vilikuwa vikifichwa kutokana na kupenyezwa watu ambao hawakustahiki. Hawa walifaidi matanuzi na per diem bila sababu kiasi cha kulitia taifa hasara bila sababu ya msingi zaidi ya ufisadi wa kimfumo. Huu wakati umepita; lazima tufanye mabadiliko na kuondokana na uovu na uhovyo huu ambao sasa unaanza kugeuka wa kimfumo. Maana vyeo na fedha wanazofaidi ni mali ya umma na si mali ya kundi fulani wala si hisani wala utashi kufichua historia na sifa za wahusika. Hii husaidia umma si kupata kuwajua wahusika bali kujiridhisha kuwa haki inatendeka.  
            Hata hivyo, leo tutaongelea kero tunayopata pale tunapotaarifiwa kuwa rais au waziri amemteua fulani kufanya kazi fulani. Hivyo, kutokana na mapungufu haya, tunatoa maangalizo yafuatayo:
            Mosi, wakati mwingine huwa najiuliza mantiki ya kuutangizia umma kuwa rais au waziri kafanya uteuzi fulani wakati taarifa zenyewe, licha ya kuwa kiduchu, ni fichi na zenye mashimo kibao.     Pili, ukiachia kutaja jina la mteuliwa, cheo na tarehe, umma haupewi fursa ya kumjua mhusika. Kwa wanaokumbuka wakati wa awamu ya kwanza, uteuzi uliokuwa ukifanywa na ofisi ya rais au mamlaka nyingine zilihakikisha zinatuma nakala ya taarifa husika kwa vyombo vya habari ikiwa inaeleweka na kujitosheleza. Kwa mfano, kila mteuliwa alielezwa sifa zake kiasi cha umma kumjua vilivyo. Hata hivyo, baada ya kuingia utawala wa ruksa, mambo mengi ya msingi yalianza kubadilika na mengine hata kupotea mojawapo yakiwa kueleza historia za wateule.
            Tatu, siku hizi watu wanateuliwa; umma unaishia kujua majina yao na tarehe za kuanza uteuzi basi. Inakuwa kama ni siri ya watu au mamlaka fulani. Je nini kinafichwa na kwanini wakati huu ambapo umma unapaswa kujua watendaji wake vilivyo kama sehemu ya uwajibikaji na upashanaji habari? Nadhani uwajibikaji na uwazi ni sehemu muhimu ya utawala bora na ambavyo vinaweza kutumika kama njia ya kuminya mianya ya uhalifu utokanao na kughushi.
            Nne, kwanini mamlaka hazitaki kueleza historia ya wahusika hasa wakati huu tunapopambana na kadhia ya kughushi vyeti vya kitaaluma kiasi cha kupoteza fedha nyingi kuwalipa watu wasio na sifa kama ilivyobainika hivi karibuni kuwa kuna vihiyo na vilaza kibao kwenye nafasi nyeti katika utumishi wa umma?
             Tano, ukiachia mbali elimu, pia kumejitokeza kadhia ambapo matapeli na wahalifu wa kigeni wanakuja nchini mwetu na kuajiriwa wakati ni kosa kinyume cha sheria? Je ofisi ya rais hata kitengo cha mawasiliano kimeshindwa kuona hata jambo dogo kama hili? Najua utawala uliopita ulikuwa wa kishikaji kiasi cha watu–kwa makusudi mazima–kuficha taarifa muhimu za wateuliwa kutokana na uoza uliokuwako nyuma ya uteuzi wao.
            Sita, kama tulivyosema hapo juu kuwa baada ya kuondoka Mwalimu Nyerere, ima kutokana na uoza au kufuata mkumbo, mambo mengi yalivurugwa na kusahaulika mojawapo likiwa hili tunalojadili leo. Je serikali ya rais John Magufuli inajua kuwa imeingia mkumbo wa kufanya uteuzi huku kitengo chake cha mawasiliano kikitoa taarifa hapa kuhusiana na wateuliwa ambao wanapaswa kujulikana kwa wananchi? Wengi wa wateuliwa hatuambiwi historia zao ziwe za kimaisha au kitaaluma.
            Saba, tunadhani wahusika warekebishe kasoro hii ili kuwawezesha wananchi kuwajua viongozi au maafisa wao.  Kwani imefikia mahali hata hao wakuu wa kitengo cha mawasiliano ikulu hatujui sifa zao wala historia yao pamoja na unyeti wa taasisi husika. Iweje tujue sifa na historia ya rais lakini tusijue historia ya wateule wake? Kunaweza kujengeka imani kuwa kuna kinachofichwa hata kama hakipo.
            Nane, kutangaza sifa za wahusika na historia zao kwa ukamilifu itasaidia si kuwajua tu bali kufichua aina yoyote ya kughushi au sifa mbaya ambazo mamlaka zinazowateua hazijui; lakini baadhi ya wananchi wanazijua.
            Tisa, watakuwa kwenye jicho la umma au limelight jambo ambalo litasaidia kuwakatisha tamaa wenye madoa ambao kwa kuhofia hili wanaweza kukataa uteuzi.
            Kumi, kutangaza sifa za kitaaluma na kimaisha za wahusika ni njia mojawapo ya kuwaonyesha umma ubora au ubovu wa uteuzi husika na ni uwazi unaotakiwa kwenye nafasi za umma.
            Mwisho, tunadhani umma una haki na stahiki ya kujua wateuliwa na maafisa wengine wanaoajiriwa kwenye ofisi zake. Huu ni wakati wa kutoaminiana wala kufichana hasa ikizingatiwa kuwa kuna wahalifu wanatumia udhaifu huu kujipatia ajira na kipato huku wakiwanyima wananchi wetu wenye stahiki ya kupata vitu hivyo.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
↧

Happy Birthday Nkuzi

September 25, 2016, 8:54 pm
≫ Next: Je ni Makufuli au uzembe wetu?
≪ Previous: Umma ujulishwe sifa za wateuliwa
$
0
0
Leo ilikuwa siku ya kuzawaliwa Nkuzi. Ametimiza miaka sita.
Hatukuwa na mtoko kutokana na kuwanyesha ,mvua hivyo, tumeishia kusherehekea indoors.

↧

Je ni Makufuli au uzembe wetu?

September 27, 2016, 6:38 pm
≫ Next: Mlevi kuomba kuwa mkurugenzi wa bandari
≪ Previous: Happy Birthday Nkuzi
$
0
0

          Baada ya kugundua kuwa matapeli na wazembe wameanza kumtumia Dokta Kanywaji kama sababu ya kukwama kwao, kimeamua kutoa angalizo miongoni mwa wanakijiwe na wanakaya wote ili waache visingizio cha kuchapa kazi.
            Mpemba analianzisha “yakhe kuna anayeweza nikopesha njuluku lau nkalipie pango langu baada ya Makufuli kusababisha nikose njuluku? Hata yule Shaame nlokuwankindai naye anizungusha na kusema eti hana njuluku kwa vile Dokta Kanywaji kazibana sana ati. Twateseka wallahi.”
            Mbwamwitu anachomekea “kwani una mdai Dk Kanywaji au ni gea tu ya kupatia njuluku kama ambavyo sasa imeanza kuzoeleka kiasi cha kugeuka fasheni? Jamaa yangu mmoja alikwenda baa akatumbua uchache na vyangu halafu akaenda kumdanganya mshirika wa bedroom wake eti kuna mashushu walimsachi wakihofia anauza bwibwi au anakwapua bidhaa bandarini. Nadhani usawa huu kila mchovu atasema lake.”
            “Yakhe wantania au undhamiria? Hivi huoni njuluku zilivyoadimika tokana na Dokta Kanywaji kubana kila idaraaa?” anajitetea Mpemba.
            “Sasa nimekupata vizuri. Kumbe unaimba huu wimbo mpya wa taifa ambapo kila anayekwama anasingizia Dokta Kanywaji utadhani amemkata mikono!” anajibu Mbwamwitu.
            “Yakhe tuheshimiane ati. Wewe wawezasema eti umenipata wamaaanishani kama siyo matusi ya nguoni?” Mpemba anajibu kwa hasira kidogo.
            Kapende anaamua kutia guu, “kweli Dokta Kanywaji kabana lakini tusimbebeshe kila zigo wakati tunapaswa kujilaumu kwa kuzoea vya dezo. Unadhani kila mmoja analalamika kama wewe wakati akina Makondakonda wanapiga njuluku hadi kutaka kuwazawadia Bakuata mjengo wa bei mbaya tena dezo?”
            Msomi Mkatatamaa anaamua kuingilia kati “wakati mwingine nakubaliana na walalamikaji tokana na mazoea ya njuluku za magutu na mazabe ila sikubaliani na kila lawama hasa ikizingatiwa kuwa ilifikia mahali kwenye kaya hii wachovu wakaua uthubutu, ubunifu na kila aina ya namna ya kujikomboa kwa kupambana. Walevi wengi walizoea njuluku chafu zitokanazo na ufisadi, rushwa, madawa ya kulevya na utapeli. Nadhani hapa lazima tukubaliane; bila kubadilika tutalaumu na kuchukia sana wakati si majibu wala nyenzo ya kutatua matatizo yetu.”
            Mijjinga anakatua mic “usemayo kweli tupu. Wengi walizoea njuluku haramu ya rushwa mihadarati na mazabe mengine. Sasa kimeziba kila mchovu anamlaumu Dokta Kanywaji akidhani itamzuia kuendelea na vimbwanga vyake. Huyu jamaa namkubali sema napingana naye kubana uhuru wa kuandamana, kujieleza na kufanya siasa kwa kisingizio cha kutekeleza mipango yake. Najua ana mipango poa japo lazima afuate sheria. Huwezi kukomboa jamii bubu isiyoruhusiwa kufikiri wala kuhoji. Kwani hii kaya ni ya kifalme? Hata wafalme nao siku hizi wanahojiwa kiasi cha wengine kuanza kufuata demokrasia kama ilivyotokea hivi karibuni kule Jordan.”
            Kapende anakula mic “mie namuunga mkono Dokta Kanywaji hasa nikizingatia kuwa wachovu wengi licha ya kuwa wavivu ni walalamishi. Lazima tubane upatikanaji wa njuluku za kupiga ili tuheshimiane. Siku hizi huoni hata hapa kijiweni wajivuni waliozoea kuja kutupa ofa huku wakituhubiri ujinga wametoweka. Unacheza na jamaa nini?”
            Da Sofia Lion aka Kanungaembe anakatua mic “mwenzenu japo nakubaliana na jamaa, naona ni kama amezidisha hasa pale ukiangalia anavyozidi kuruhusu wazito wastaafu kuendelea kulipwa njuluku kibao huku akiwaminya walaji wengine kwenye asasi za umma jambo ambalo linamtia doa. Vinginevyo, kibano alichotoa kinafaa kuungwa mkono kama ataondoa marufuku ya kuzuia wachovu kumkosoa pale anapofanya ndivyo sivyo.”
            Kanji anakula mic “hii Nywaji nabada juluku hadi maisa nakuwa ngumu kama Bombei. Hata ile namiliki dukani hapana pata teja sana. Ile naishi bila lipa kodi sasa nabanwa na hizi electronic machines naleta. Maisa sasa iko gumu sana na sida nakuwa kuba sana.”
            Mgoshi Machungi aliyekuwa kimya akiangalia anaamua kula mic “tiambiane ukwei jamani. Tangu dokta Kanywaji kubana upatikanaji wa njuuku za dezo kwei timeumia. Juzi niipata msiba Ushoto hadi nikashindwa kwenda kuhami wafiwa kutokana na kutokuwa na naui.”
            Mheshimiwa Bwege anakwanyua mic “pamoja na uzuri wa huyu jamaa, lazima tumbane tujue anachopanga kama ni kile tunachotaka na siyo anachotaka yeye. Hapa lazima mimi niseme wazi. Kuna dalili za kaudikteta ambako sitakaunga mkono. Huwezi kuendesha kaya kama kaya yako. Hii ni kaya ya kidemokrasia ambapo haki na mawazo ya wachovu yanapaswa kuheshimiwa. Maana anapotokea yeyote akataka kufanya haki za wachovu kuwa hisani ndipo tunapoanza kujengeana ukuta na kutiliana mikwara ya hapa na pale kiasi cha kutishia mstakabali wa kaya.”
            Mzee Maneno anaamua kupoka mic “huyu mtani wangu kweli noma. Hata nimeshindwa kumcheza binti yangu tokana na kutokuwa na njuluku. Hata hivyo, silaumu kwa vile kama hali itatengamaa kila mchovu akaanza kula haki yake badala ya kulana kama wadudu, hali itakuwa swali. Hali ilikuwa mbaya sana. Napendekeza arejeshe maadili ya utumishi wa umma ili kuondoa takataka zote ambazo hajasafisha. Hatuwezi kuwa kaya ya majambazi na mafisadi tukawa salama. Lazima ifikie mahali kila mchovu aeleze alivyochuma huo ukwasi ambao wahalifu wengi wanautumia kutukoga wakati ni haramu tupu.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si tukamuona Dokta Kanywaji akija kunywa kahawa nasi!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano kesho.
 
 
↧
↧

Mlevi kuomba kuwa mkurugenzi wa bandari

October 1, 2016, 7:16 am
≫ Next: Ungekuwa ni rais huyu mwizi wa magwanda ungemfanya nini?
≪ Previous: Je ni Makufuli au uzembe wetu?
$
0
0
 
             Baada ya kushuhudia, ubabaishaji, ufisadi, ujinga na kila aina ya madudu bandarini alipotembelea Dokta Kanywaji, Mlevi napanga kuandika barua ya kuomba niwe mkubwa wa eneo hili nyeti ili nimsaidie rahis kunyoosha kaya ya walevi inayoliwa kilevi kama shamba la bibi. Kwa ambao hawakuwa wamelewa walivyoona kitimoto Dokta Kanywaji aliyowapa wababaishaji wetu pale bandarini watakumbuka jamaa walivyokuwa wakitoa majibu ya kitoto. Jamani, hata kudanganya hamjui? Halafu eti mnajiita wasomi wakati hamna hata chembe ya uzalendo! Yaani hawa waduwanzi kweli hawana maana. Yaani wanadanganya waziri mkubwa’ na wanaona kama haitoshi. Wanamdanganya hata dingi mwenyewe. Sijui atawafanya nini kwa walivyomuudhi ukiachia mbali kuibia kaya yetu kiasi hiki wakati walishaonywa? Wana bahati tena ya mtende. Kama ningekuwa mimi, licha ya kuzaba majuha vibao, ningeondoka nao waelekee Ukonga wakati wakingojea hatima yao.
            Napanga kuomba niwe mkubwa wa bandari ili kupunguza makali ya kaya yetu kuwa Kaya inakuwa kama ya mfukoni mwa majizi na walafi fulani.  Mie sitalea gendaeka wala kupokea kitu kidogo hata kikubwa kwa manufaa binafsi kama hawa waliotenda dhambi isiyopaswa kusamehewa ya kumdanganya dingi  mwenyewe. Kama nitateuliwa nitaunda kitengo cha ushushu cha kumulika kila kitengo bandarini. Watakaonidaganya ili nimdanganye dingi lazima nishauri wanyongwe haraka.
            Hakuna kitu kilinitisha kama kushuhudia mikompyuta imefungwa lakini haifanyi kazi yoyote ya kukagua mizigo. Hii maana yake ni kwamba magaidi wakiipata na wakaamua kuingia kayani mbona wataingia tena kwa ulaini? Nani anapenda kaya yetu iwekwe rehani kwa sababu ya upuuzi na uroho wa gendaeka wachache wasiotaka kubadilika?
            Lo! Nimechonga sana kiasi cha kusahau kueleza kwanini nina usongo na sifa za kuwa mkubwa wa bandari. Si juzi tukiwa tunakata ulabu akatokea mlevi mmoja akatutukana kinyumenyume akisema kuwa kaya yetu haina walevi bali majipu matupu kuanzia juu hadi chini. Kusema ule ukweli, kama siyo kunizuia huenda ningekuwa Ukonga nangoja kunyotolewa roho kwa kumnyotoa roho mlevi mwenzangu. Hata hivyo baada ya kutafakari niliona ukweli na kumpa ofa huyu jamaa aliyezibua akili yangu na kuamsha usongo wangu hadi nikaamua kugombea udingi wa bandarini.
            Baada ya kusukuti niliona nuru na ukweli kuwa kaya yetu sasa yaweza kuitwa kaya ya madudu. Hebu angalia trajectory ya dingi alipopita utagundua madudu matupu kama si majibu.
Uwanja wa ndege madudu matupu. Mitambo imeharibiwa ili kupitisha mibwimbwi. Sijui nao bado wanaendelea na mazoea yao hata baada ya kufichuliwa kama bandari? Bandari madudu kama mlivyoshuhudia wenyewe mibaba mizima ikiongea vitu vya kitoto vikidhani wote ni watoto kama yenyewe. Mmeua flow meters mnakuja na upuuzi. Mipakani madudu
Mita za kupima mafutaaka flow meters madudu. Wasimamizi madudu, mikompyuta madudu. Nai madudu madudu matupu kiasi cha kufikiri kuita kaya yetu kaya ya madudu kama siyo ya vidokozi, majambazi na mafwisadi.
            Hata hivyo silaumu sana. Kama ilifikia mahali hata bedroom ya kaya yaliyajaa madudu chini ya Njaa Kaya. Hawa wanaoendelea kuendekeza njaa, tamaa na ujanjaunjanja hawahitaji kutumbuliwa bali kuchomwa moto maana ni kansa tupu. Hata hivyo, tusiwalaumu wao tu. Nimepiga kelele hadi koo limevimba nikimtaka Dokta Kanywaji arejeshe maadili ya utumishi wa umma na taifa ambapo kila mlevi atapaswa kueleza alivyopata ukwasi wake. Hata hivyo, bila kurejesha katiba mpya haya yote yatawezekanaje zaidi ya kaya kuendelea kuwa ya madudu?
Tuonane wiki ijayo,
Mlevi-Uwanja wa Fisi
Tandale.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
↧

Ungekuwa ni rais huyu mwizi wa magwanda ungemfanya nini?

October 2, 2016, 3:15 pm
≫ Next: Barua ya wazi kwa Hamad na Lipumba
≪ Previous: Mlevi kuomba kuwa mkurugenzi wa bandari
$
0
0

↧
Search

Barua ya wazi kwa Hamad na Lipumba

October 3, 2016, 10:45 am
≫ Next: Kijiwe chalaani upumbavu wa Iringa Mvumi
≪ Previous: Ungekuwa ni rais huyu mwizi wa magwanda ungemfanya nini?
$
0
0
 
          Waheshimiwa,
Naamini hamjambo na mnaendelea na shughuli zenu kama kawaida. Naandika barua hii kwa uchungu mkubwa kama mpenda mageuzi. Kilichonisukuma kuandika barua hii ni mambo yafuatayo:
            Mosi, mtafaruko ndani ya chama chenu cha Wananachi (CUF) unaoendesha kukidhoofisha chama na upinzani kwa ujumla. Najua siasa ni mchezo unaoweza kuwa mchafu kama utachezwa vibaya na kwa kutofuata kanuni.  Hivyo, nashauri msijiruhusu au kuruhusu huu mtafaruko kukimega, kukidhoofisha hata kukiua chama ambacho mmekijenga kwa muda mrefu. Kubomoa ni rahisi sana kuliko kujenga.
            Pili, nandika kutokana na kuanza kuona kuwa kuna kila dalili za kukiua chama tokana na ima maslahi binafsi ya wawili nyinyi au kutunisha misuli kila mmoja akiamini atashinda. Katika mchezo huu mnaoshabikia na kucheza hakuna mshindi; na kama yupo, basi si mwingine, bali maadui zenu ambao sasa wanachekelea na kushangilia kwa visu mnavyojidunga.
            Tatu, nikiangalia historia ya CUF nagundua; haijawahi kuwa na viongozi waandamizi zaidi ya nyinyi. Mmeshikilia nafasi za juu kiasi cha kugeuka kile kwa kiingereza huita fixtures au kitu kisichoaminishika. Hii ni kinyuma na demokrasia na matarajio ya umma. Kwa mfano, profesa Ibrahim Lipumba amekuwa mkiti wa CUF tangu mwaka 1995 yaani miaka 21 jambo ambalo linamfanya awe mwenyekiti wa chama kwa miongo zaidi ya minne. Aliingia madarakani na Benjamin Mkapa akahudumu kama mkiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa miaka kumi akaondoka na kuja Jakaya Kikwete ambaye alihudumu miaka kumi akaondoka. Sasa mkiti mpya John Pombe Magufuli ndiyo yuko kwenye usukani.  Kwa upande wa maalimu Seif Sharrif Hamad, kadhalika aliingia kwenye uongozi wa juu wa CUF tangu mwaka 1992 akiwa mgombea pekee wa CUF kwenye nafasi ya urais wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar (BMZ). Alianza kugombea urais akipambana na Salmin Amour, kisha Amani Karume na juzi alipambana na Dk Ali Mohamed Shein. Na inavyoonekana, bado ana hamu ya kugombea na mwingine atakayemfuatia Shein anayemaliza muda wake mwaka 2020. Hii maana yake ni kwamba Hamad atakuwa amegombea mara nne mfululizo jambo ambalo linatia shaka udemokrasia wake.
            Nne, kwa kuangalia trajectory hii, unagundua kuwa kuna haja ya CUF kuanza kufikiria kile ambacho kwa kimombo huitwa post-Lipumba-and-Hamad era yaani kipindi ambacho kitakuwa kwenye mikono ya wengine. Hili ni Dhahiri na laweza kukisaidia chama hasa ikizingatiwa kuwa mliyoshindwa kuyafanya kwa miaka zaidi ya 20 mliyokuwa kwenye uongozi wa juu wa chama hamuwezi kuyafanya na kuyafanikisha hata mkipewa miaka 200 zaidi. Hivyo, si vibaya wala uchochezi kuwataka mfikiri kuachia ngazi ili damu mpya iingie na kujaribu kufanya mambo kwa namna tofauti mlivyofanya. Japo CCM imekuwa madarakani kwa miaka mingi tangia uhuru, inawazidi kitu kimoja. Imeweza kuruhusu watu wengine–tena ambao ni wageni chamani–kushika hatamu za uongozi ili kufanya mambo tofauti na wengine waliotangulia. Huu ndiyo ukomavu kidemokrasia. Kwani hakuna aliyeumbiwa kuongoza wala kuongozwa. Yeyote anaweza kuongoza sawa na kuongozwa.
            Tano, kama wanachama wenu bado wanawahitaji, jambo ambalo hata hivyo nina shaka nalo, basi suluhisheni ugomvi wenu ili mkinusuru chama pia nanyi binafsi. Kwani si jambo jema kuingia kwenye vitabu vya historia kama wawili walioua chama tokana na maslahi au uadui binafsi. Sidhani kama mna haja ya kutojifunza toka kwa wanasiasa kama akina Augustine Mrema na John Cheyo walioamua kuvigeuza vyama vyao mali binafsi kiasi cha kutoona wengine wa kuweza kuviongoza zaidi yao.
            Sita, kitu kingine kilichonisukuma kuandika barua hii ni ile hali ya kuona kuwa wanachama wenu, kwanza, hawana mamlaka tosha ya kuwawajibisha kwa pamoja. Na pili wanaonekana kuangukia kwenye mtego wenu wa kuwashabikia kiasi cha kugawanyika badala ya kuangalia chama kama asasi huru isiyopaswa kukwazwa na watu binafsi kama ilivyo kwa CUF kwa sasa. Sisikii wanaowakumbusha kufanya jambo la maana yaani kuachia ngazi ili chama kiendelee kama kinavyopaswa. Wote wamegawanyika pande mbili jambo ambalo linakinyima chama fursa na siha ya kusonga mbele hasa usawa huu serikali ya CCM inapofanya mambo mengi yanayowavutia watanzania. Sijui kwanini hamuoni tishio hili na badala yake mnakuwa waanzishaji wa mauti ya chama chenu. Ili iweje na kwa faida ya nani?
            Nahitimisha barua hii kwa kuwaomba kwa unyenyekevu mchague kati ya mawili yaani kusuluhusisha ugomvi na kusonga mbele au kuachia ngazi ili akili, damu na nguvu mpya ichukue hatamu na kukwamua chama kinachochungulia kaburi. Wapiganapo mafahari wawili ziumiazo ni nyasi (wanachama).
            Pia niwasihi wanachama kuachana na ushabiki wa kisiasa; na badala yake wapiganie mstakabali wa chama.
Nawatakieni kila la heri katika kujipima, kujisuta na kuchukua maamuzi magumu kwa faida ya demokrasia nchini. CUF ni zaidi ya Hamad na Lipumba.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili jana.
↧

Kijiwe chalaani upumbavu wa Iringa Mvumi

October 5, 2016, 6:09 am
≫ Next: Tunapogeuka kaya ya wapumbavu na wanayama!
≪ Previous: Barua ya wazi kwa Hamad na Lipumba
$
0
0

          Kitendo cha kinyama kilichotendwa na wananchi wa kijiji cha Iringa Mvumi kimeacha kijiwe na simanzi, hasira na hata kutaka kulipiza kisasi. Baada ya kuzinyaka kuwa maafisa waKituo cha Utafiti wa udongo na maendeleo ya ardhi Seliani mkoani Arusha waliteketezwa kwa moto na wauaji waliowadhania ni wanyonya damu, kijiwe kinatoa amri kwa lisirikali kuhakikisha wote waliotenda unyama huu wanashughulikiwa kikamilifu.
            Mpemba anaingia na gazeti la Uvumi Leo. Analitupa mezani huku akisonya na kusema “yakhe twendaapi kama baadhi ya wenzetu wawezajichukulia sharia nkononi na kuua watu wasohatia kama ilivotokea kule kwa akina Agwe jana? Wallahi mie sikujua kuwa hata baada ya kupata uhuru bado kaya yetu ina watu wajinga na wakatili kama hawa.”
            “Kaka unashangaa hawa wauaji uchwara waliosukumwa na ujinga, ujuha na upumbavu siyo! Hiyo ndiyo kaya yetu. Hushangai kuona wachovu wanavyoshabikia kuua vidokozi na vibaka huku wakinyenyekea na kushobokea mibaka kama ile ya Escrow, Epa, UdA, Kagoda, na mingine mingi iliyotamalaki na kutapakaa kayani? Hushangai vibinti vyetu vinavyonyotolewa na ngoma kutokana na ujinga na umaskini?” anajibu Kapende huku akionyesha wazi kuchukia.
            Mgoshi Machungi anakula mic “waahi angekuwamo ndugu yangu ningekwenda Ushoto kumtafuta shemtwashua na vijana wetu tiende kue tiwachome nao moto kama siyo kuchoma wake zao kama wangetokea kukimbia. Hata kama ni wajinga, hawa siyo binadamu kusema ue ukwei.”
            Mijjinga anakula mic “japo hawa wauaji na washenzi siwatetei, siwezi kuwalaumu wao peke yao. Nawalaumu walioteka uhuru wetu huku wakichezea kaya yetu kiasi cha kuacha wachovu wetu wawe wajinga na wakatili wa kutupa kiasi hiki. Wana bahati. Laiti waliokufa wangekuwa ni jamaa zao majambazi. Bila shaka wangekitokea hiki kijiji siku moja na kulipiza kisasi kwa kuua wauaji wenzao kama wadudu.”
            Msomi Mkatatamaa anasalandia mic “siwezi kuficha hasira, mshangao, uchungu na kichefuchefu nilivyopata baada ya kusikia habari hizi za kijima kwenye redio. Kwanza, nilidhani nilikuwa nimesikia vibaya. Pili, nilishani haya mambo yametokea sehemu nyingine duniani lakini si Bongolalaland. Hivi kweli bado kuna watu duniani wanaamini kwenye hekaya za mumiani, vibwengo na majini! Ama kweli, aliyesema kuwa aliyeroga kaya hii aliishafariki hakukosea. Je tunajifunza nini kutokana na kadhia hii? Kwanza, tunajifunza kuwa watu wetu ni wakatili wanaoweza kufanya lolote ima kwa woga au kutafuta mlo. Rejea wanavyoua watu wenye ulemavu wa ngozi. Pili, tunajifunza kuwa watu wetu walio wengi ni wajinga wanaoweza kuamini kila kitu. Rejea kutamalaki kwa dini za kishirikina, waganganjaa wa jadi na matapeli kila aina bila kusahau hata vyama vya siasa.”
            Anapiga chafya na kuendelea “huu ni ushahidi tosha kuwa kaya yetu iko hatarini. Leo tunaua wenzetu kwa imani chafu na haba kama hizi. Kweli kesho tutashindwa kuuzana kama walivyofanyiwa mababu zetu waliouzwa utumwani? Mnadhani wote walikamatwa kwa nguvu? Wapo waliouzwa na ndugu zao sawa na viongozi wengi waliopita waliouza kaya hii kwa wachukuaji waitwao wawekezaji ukiachia mbali maafisa wa serikali wanaoendelea kuuza kaya hii ima iwe ni kwa kupewa kitu kidogo kama vile kuuza uraia na vyeti vya kuzaliwa vya wananchi na mengine mengi.”
            Mipawa anampoka Msomi mic “mie nangoja kuona hatua zitakazochukuliwa katika kuadhibu huu ujinga na jinai ya mauaji ya watu wasio na hatia. Nangojea kusikia nini sirikali itafanya kuhakikisha haki inatendeka na hili linakuwa somo kwa wengine wenye mawazo mgando na ya kinyumenyume kama hawa. Ama kweli, agwe wameamua kututia aibu kama kaya. Napendekeza wote waliohusika na unyama huu wakamatwe na kuchukuliwa hatua mara moja ili haki itendeke na liwe somo kwa wengine.”
            Sofia lion aka Kanungaembe anakwanyua mic “naomba nikuchomekee kidogo. Napendekeza kila kijiji kiwe na kituo kidogo cha polisi ili yanapotokea mazonge kama haya polisi waweze kusaidia kuzuia mauaji ya watu wasio na hatia.:
             “Nami vacha nichomekee veve dada yangu. Naunga kono na guu veve. Ile pesa silingi milioni hamsini kijiji napewa basi kijiji natumia kulipa polisi.”
            Mheshimiwa Bwege aliyekuwa akisikiliza kwa makini anaamua kula mic “wote mmetoa mapendekezo ya msingi. Ila mmesahau jambo moja kubwa; yaani kumuua adui aliyesababisha mauaji haya tunayoongelea yaani ujinga. Nakumbuka zama za mchonga, angalau kulikuwa na elimu ya ngumbaru. Mnategemea nini kaya inapokuwa na wajinga wengi? Bila shaka haya ndiyo matokeo yake. Kama kundi dogo la wezi linateka kaya kama mlivyoshuhudia sehemu mbalimbali kama vile bandari, viwanja vya ndege, mipakani, TRA, uhamiaji na kwingineko huku kila mchovu akitegemea usongo wa dokta Kanywaji mnategemea nini? ili kuondokana na ujinga na ujima huu, tuache kumbebesha mzigo dokta Kanywaji. Tumbane atuletee katiba mpya ambayo itaeleza upya haki za wachovu. Vinginevyo tujinyamazie na kuacha kulalamika. Kwani kwa mwendo huu, watakufa wengine wengi tu.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si daladala likapata panchali. Acha tutimke–kwa ujinga wetu–tukidhani ni bomu la nyuklia!
Chanzo: Tanzania Daima jumatano leo.
↧
↧

Tunapogeuka kaya ya wapumbavu na wanayama!

October 8, 2016, 6:09 am
≫ Next: Hayawi hayawi! Afrika yapata treni ya kwanza ya umeme
≪ Previous: Kijiwe chalaani upumbavu wa Iringa Mvumi
$
0
0
          Wiki hii mlevi sikupata vile vitu vyangu. Nilikuwa kwenye msiba hata kama uliwahusu wachovu ambao sikuwahi kukutana nao. Baada ya kunyaka taarifa kuwa wanakaya kwenye kijiji cha Iringa Mvumi waliamua kuwanyotoa roho wataalamu wa kupima udongo ili kuwawezesha kuzalisha vyakula vya kuwatosha, nilijihisi kupasuka kwa hasira. Nilitamani nichukue cha moto na kwenda kutangaza mauaji ya halaiki. Hata hivyo, niligundua kuwa hili si jibu.
            Kuna mambo muhimu ya kujifunza tokana na kadhia hii hata kama ni ya kilevi na kinyama.
            Mosi, kuna haja ya kuhakikisha wote walioshiriki jinai hii wanakamatwa na kutupwa lupango wakingoja kuwa na date na pilato ili wapewe stahiki yao kisharia.
            Pili, nashauri sirikali ianzishe tena elimu ya ngumbalu ili kuondoa huu ujinga uliokwamia kwenye akili za baadhi ya walevi hasa wa kule mashambani ambao wanaweza kupwakia kila upuuzi hata bila kutumia bongo zao. Unategemea nini unapokuwa na kaya inayotumia masaburi kufikiri badala ya bichwa?
            Tatu, kaya ianze safari ya kupiga vita kila aina ya ushirikina uwe ni wa kidini, kisiasa, hata kijamii. Nadhani hapa tunaweza kuona matokeo ya kuruhusu matapeli fulani kuwajaza walevi woga na kuwaibia ima kwa kuwahubiria dini au kujifanya waganga njaa wa jadi. Ama kweli ujinga ni zigo kubwa tena la manonihino! Nani angeamini kuwa hata mchungaji ambaye amethibitisha kuwa wengi ni wachunaji angeshirika dhambi hii? Je tunao wachunaji wapumbavu na katili kama hawa kiasi gani kayani?Rejea kutamalaki kwa dini za kishirikina, kilaji, waganganjaa wa jadi na matapeli kila aina bila kusahau hata vyama vya siasa vinavyoendesha siasa za kitapeli kama vile vinavyomilkiwa na walevi binafsi wakivigeuza NGO zao za kutengenezea njuluku.
            Nne, tuanze mchakato wa kuondoa kaya yetu kwenye unafiki wa kimfumo ambapo halaiki ya walevi hujisikia raha na kushabikia kuua vidokozi na vibaka huku wakinyenyekea na kushobokea mibaka kama ile ya Escrow, Epa, UdA, Kagoda, na mingine mingi iliyotamalaki na kutapakaa kayani. Angalia vibinti vyetu vinavyonyotolewa na ngoma kutokana na ujinga na umaskini na hakuna anayehoji wala kuwa mkali!
        Tano, kaya inapaswa kuanza safari ya kuusaka ubinadamu na kuuzika unyama na uhayawani kama ulioonyeshwa na walevi wa kule Mvumi Iringa. Tumegeuka kaya ya samaki ambao hulani kulingana na saizi.
            Sita, lazima tuanze kuwashughulikia walioteka uhuru wetu huku wakichezea kaya yetu kiasi cha kuacha walevi wawe wajinga, majuha na wakatili wa kutupa kiasi hiki. Kaya haiwezi kuwa salama wakati imejaa mijitu mipumbavu na mikatili inayoweza kufanya lolote ima tokana na woga au kutafuta rizi.  Nani haoni wanavyonyotoa roho walevi wenye ulemavu wa ngozi? Unategemea nini unapokuwa na kaya walevi walio wengi wajinga wanaoweza kuamini kila kitu? Mijitu imekuwa mikatili hadi inauana. Hata hivyo, tuna bahati, zingekuwa zama za utumwa tungeuzana kwa sana kama walivyofanya baadhi ya mababu zetu wenye roho mbaya.
Saba, nashauri kitaalamu kuwa kila kijiji kiwe na kituo kidogo cha ndata ambao wanaweza kusaidia kuzuia unyama na upuuzi kama huu tunaoogelea.
Nane, wataalamu au walevi wetu wanaoingia kwenye maeneo mageni ima wapewe ulinzi wa askari au waruhusiwe kupeperusha bendera ya taifa kwenye magari yao. Kwani, walevi wetu wamezoeshwa kuogopa bendera kama alama ya sirikali. Pia nashauri sirikali izifidie vilivyo familia za wahanga wa ujinga wa taifa unaotishia kuliteketeza taifa letu.
            Kabla ya kusahau, nadhani yote yaliyopendekezwa hapo juu hayawezi kufanyika wala kufanikiwa bila kuwa na ile kitu iliyouawa na mafwisadi wenye ulaji kuogopa kunyea debe yaani KATIBA MPYA. Chonde chonde wahusika. Turejesheeni katiba yetu mpya ya walevi ili tuitumie kurekebisha na kukomboa kaya yetu inayoendelea kutopea kwenye mikono michafu ya mafwisadi na sasa wauaji! Ni hatari; hasa tunapogeuka kaya ya wapumbavu na wanayama.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
↧

Hayawi hayawi! Afrika yapata treni ya kwanza ya umeme

October 8, 2016, 8:21 am
≫ Next: Kumbe 'usanii' unalipa!
≪ Previous: Tunapogeuka kaya ya wapumbavu na wanayama!
$
0
0
Image result for photos of ethiopian electric train
Nchi ya Ethiopia inaingia kwenye vitabu vya historia kama nchi ya kwanza kuwa na Treni ya umeme ukiondoa Afrika Kusini katika Afrika. Hivi karibuni mradi wa ujenzi wa Treni ya umeme kutoka Addis-Ababa kwenda Jibuti ulitangazwa kutarajia kukamilika na kufunguliwa. Pia nchi ya Senegal iko mbioni kuwa na treni ya umeme lakini fupi itakayohudumia mji mkuu wa Dakar. Tunaipongeza Ethiopia kwa mafanikio haya. Pia wiki hii Ethiopia imefanikiwa kuipiku kenya na kuwa kinara wa uchumi mkubwa katika Afrika Mashariki. Kwa habari zaidi tafadhali BONYEZA HAPA.
↧

Kumbe 'usanii' unalipa!

October 8, 2016, 8:40 am
≫ Next: Je watanzania tunaelewa tunachofanya na tunachotaka?
≪ Previous: Hayawi hayawi! Afrika yapata treni ya kwanza ya umeme
$
0
0
Angalia babu wa Loliondo, Ambilikile Mwasapila anavyoonekana kabla ya kuibuka na baada ya kuzinyaka akiwahadaa wajinga kuwa ana tiba ya ajabu wakati alichokuwa nacho ni uongo wa ajabu. Je namna hii mfumo wetu haujaruhusu jinai ya kuibia maskini na wenye shida kwa manufaa binafsi. Ingekuwa Ulaya wala huyu tapeli asingefanikiwa. Maana angetakiwa athibitishe tiba yake kimaabara. Ama kweli wajinga ndiyo waliwao!
↧
Remove ADS
Viewing all 3177 articles
Browse latest View live

Search

  • RSSing>>
  • Latest
  • Popular
  • Top Rated
  • Trending
© 2025 //www.rssing.com