Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all 3173 articles
Browse latest View live

Transparence: Let’s open every boozer’s closet

$
0
0


Tuwanyonge mafisadi na wahujumu uchumi kama China

$
0
0












Image result for james lugemalira            Kwanza nikiri kuwa pendekezo la kuwanyonga wezi na wahalifu wakubwa wanaohujumu nchi yetu si la kuvuita. Laweza kuhusu wengi hasa wale wanaotetea haki za baadhi ya binadamu huku wakifumbia macho haki za wengine hasa wahanga wa maovu nchini. Hata hivyo, nitalitoa na kulijengea hoja ili wasomaji na wahusika wapambue na kuamua wenyewe. Nchi ya China inasifika sana duniani kwa sasa kuliko hata Marekani kutokana na mambo makubwa inayofanya kwa kipindi kifupi tangu ibadili mfumo wake toka ukomunisti kwenda kwenye ubepari mchanganyiko. China kwa sasa ni taifa linalotetemesha magwiji kama Marekani hata Umoja wa Ulaya kutokana namna inavyoendelea hasa kiuchumi. 
Moja ya mambo yaliyowezesha China kufikia hapa ilipo ni ile hali ya kutokuwa na simile na uovu hasa ufisadi, uuzaji mihadarati na jinai nyingine.
Image result for photos of lugumiTanzania kama China, tulikuwa wajamaa muda si mrefu uliopita. Baada ya kuachana na ujamaa na kuingia kwenye ubepari uchwara, hata hivyo, Tanzania hatukusonga mbele zaidi ya kurudi nyuma. Rejea uhaba na ubovu wa huduma za jamii tulizokuwa tukipata wakati wa utawala wa serikali ya awamu ya kwanza ya kijamaa ambayo sawa na China, ilipiga vita ufisadi kweli kweli. Mpaka tunavyoandika, China haisikilizi kelele za haki za binadamu ambazo mara nyingi zimekuwa zikilenga kuwatetea wahalifu huku wakifumbia masikio haki hizo hizo za wahanga wa wahalifu husika. Kama China ingekuwa Tanzania, kashfa kama EPA, Escrow, Lugumi, Kagoda, Meremeta, Mwananchi Gold, UDA na hii iliyoibuka ya mtu kutengeneza mamilioni kwa dakika zisingekuwa zinasuasua au kushughulikiwa kisiasa.
Tofauti na China, Tanzania ilibariki ufisadi kiasi cha kuonekana kama umehalalishwa kwa mlango wa nyuma. Hivi karibuni vyombo vya habari vilifichua kuwa rais John Pombe Magufuli amemtumbua mfanyabiashara mmoja aliyekuwa akiliibia taifa shilingi milioni saba hadi nane kwa dakika. Hata Bill Gates tajiri mkubwa kuliko wote duniani hatengenezi fedha kiasi hiki na kwa njia hii haramu. Je mtuhumiwa kama huyu ameishasababishia taifa hasara gani? Je mchezo wake huu mchafu umeishasababisha vifo vya watu wangapi wasio na hatia kwa kukosa huduma kama vile madawa ukiacha mbali usumbufu wa kukosa huduma kama vile elimu, na hutuma nyingine za huduma tokana na serikali kutokuwa na uwezo kifedha? Je ni kosa kwa mtu kama huyu–akipatikana na hatia kuhukumiwa kifo–baada ya kufilisiwa? Hiki ndicho wenzetu wa China wanachofanya.
Kukamatwa kwa mtuhumiwa huyu ambaye–hata hivyo jina lake limefichwa sijui ni kwanini–kunafanya tuulize: je ni wangapi wameishacheza mchezo huu na serikali imeishapoteza kiasi gani? Mbona majambazi wengine wa kawaida wanapokamatwa au kuuawa majina yao hayafichwi? Je kuficha huku kuna nini nyuma yake au ni mtu ambaye wakubwa wasingependa ajulikane kutokana na utukufu wake na wao. Je mtuhumiwa amefanya mchezo huu kwa muda gani na kusababisha hasara ya fedha kiasi gani? Haya ni baadhi ya mambo tunayopaswa kuchunguza na kujua ili kuwashughulikia wengine kama yeye. Je washirika zake nao wamekamatwa? Maswali ni mengi kuliko majibu. Nadhani, kukamatwa kwa mtuhumiwa huu kunatoa hitimisho kuwa kweli Tanzania si nchi maskini wa fedha wala mali bali maskini wa viongozi wenye maono na uzalendo kushughulikia jinai kama hii.
Wenzetu wa China hawana ubaguzi katika kutekeleza sheria walizojiwekea. Tanzania ni tofauti. Mtu anaiba kuku na kufungwa miaka thelathini wakati mwenzie anaiba mabilioni na kuhukumia miaka michache na kusafisha sehemu za umma! Tusipobadili sheria na kutunga sheria kali na kuzitekeleza dhidi ya maovu kama haya, tutaendelea kupiga siasa na kuwa shamba la bibi kama si kichwa cha mwendawazimu. Tukiendelea kuwaendekeza wakubwa waliosisi hujuma na maovu kama haya, tutaendelea kujidanganya tu.
Japo tunaweza kumlaumu mtuhumiwa–jambo ambalo ni haki–kuna haja ya kujiuliza: serikali ilikuwa wapi siku zote wakati hujuma hii kwa taifa ikifanyika? Je mtuhumiwa aliwezeshwa na mazingira au alijijengea mazingira ya kufanikisha wizi wake? Hapa ndipo unapopata utata kusikia baadhi ya wakubwa wakisema kuwa wanaotaka wakubwa wenzao washitakiwe kwa kuhujumu nchi ni mambo ya hovyo. Wakati mwingine unashindwa kuelewa hata maana ya hovyo. Je hapa wanaotaka wakubwa washitakiwe kweli wanasema mambo ya hovyo kweli au hawa wanaowakingia kifua watu wenye madhambi–ambayo wengine wamekuwa wakiyalalamikia–ndiyo wa hovyo hovyo na wanaofanya mambo ya hovyo? Inashangaza mambo ya hovyo yanapofanywa ya maana na ya maana kugeuzwa vya hovyo. Sidhani kama kutoa taarifa kuhusiana na maovu fulani ni jambo la hovyo au kutopokea taarifa hizo na kuzifanyia kazi ndilo suala la hovyo. Haiwezekani watu wakawa wanajiibia wakati serikali ipo na wale waliokuwa wakisimamia wizi huu au kuzembea na kuuruhusu bado wakawa watu wa kukingiwa kifua au kupewa kinga kisheria. Huku ni kujipinga, kujichanganya na kuwachanganya watanzania; nalo ni jipu linalopaswa kutumbuliwa ingawa linawahusu hao hao wanaopaswa kutumbua.
Tumalizie kwa kushauri kuwa–kama kweli serikali imedhamiria kupambana na uovu hasa ufisadi na uhujumu wa nchi–basi irejeshe maadili ya utumishi wa umma; na ifanye hivyo bila ubaguzi wala upendeleo. China wanaonekana kufanikiwa kutokana na kutokuwa na mambo ya hovyo kama vile kulindana, kuogopana au kufichiana majina.
Chanzo: Mwanahalisi Jumatatu.

Milioni saba kwa dakika; kijiwe chanena

$
0
0

            Baada ya vyombo vya umbea kuripoti jinai ya jizi moja kutengeneza madafu milioni saba hadi nane kwa sekunde, kijiwe kimekaa kutathimini baadhi ya mambo.
Mgosi Machungi analianzisha, “Jamani mnaona hii picha ya jizi toka umangani sijui ugabachoini inaotiibia kana kwamba hakuna siikai?”
Mijjinga anakula mic, “Unashangaa kuliwa wakati ushaambiwa  hili shamba la bibi lililokuwa likisimamiwa na kichaa kiasi cha kuligeuza kuwa kichwa cha mwendawazimu! Wala mie sishangai hasa nikiona magabacholi wanavyoshindana kuja kayani kusaidiana na wezi wetu kujihomolea.”
Kapenda anampoka mic Mijjinga, “Dokta Mijjinga nakubaliana nawe. Hii kaya kweli shamba la bibi lililokuwa likisimamiwa na chizi. Hujaona hata wachainizi wanavyojaa kuja kumalizia tembo wetu waliosalia baada ya wengine kusafirishwa umangani wakiwa hai? Umesikia amefungwa gendaeka hapa? Kwanini wasialikane kuja kufaidi vya bure?”
“Mwenzenu nilipomsikia Dk Kanywaji akitoboa uhalifu huu nilipandwa na presha. Kwanza, sikujua kuwa kumbe kaya inaliwa hivi. Pili, sikuamini kuwa Dk Kanywaji angegwaya kutaja jina la mheshimiwa mwizi huyu ambaye bila shaka anawakilisha mtandao wa wazito.” Anasema Mipawa huku akisogeza gazeti pembeni na kuendelea, “Mimi, hata hivyo, sishangai hasa nikiangalia miskandali kama Lungumi, Escrew na mingine inavyopigwa dana dana huku walioaiasisi wakiahidiwa ulinzi. Kwa taarifa yenu huyu jamaa atapotea kama alivyopotea Chavda baada ya wazito kuogopa kufichuliwa siri zao. Hii Danganyika ati.”
Mpemba anakula mic, “Yakhe mie nshangaa sasa. Sijui yawaje waloendesha serikali ilobariki ujambazi huu sasa wanaenziwa na hawa hawa wanaotufunga kamba kuwa watapambana na ufisadi wakati wanaonea wadogo na wale wasiokula nao? Huyu ntu angekuwa Uchina ashaoza baada ya kufilisiwa. Laiti kama Uchina wasingekuwa wana mizigo yao ya wasaka tonge wallahi mie ningehamia huko.”
Mzee Maneno anakula mic, “Mie mwenzenu niliposoma habari hii nilitamani kuchukua panga na kwenda kuua magabacholi japo mmoja.” Kabla ya kuendelea anamtazama Kanji ambaye naye anamtazama mzee Maneno. Kabla ya kuendelea, Kanji anamchomekea, “Dugu yangu siyo hindi yote mizi bana. Hii mbona maarabu na si hindi? Dugu yangu nakosea sana. Veve fikiri hii hindi na mizi nyingine naiba pekee yake. Kama vote natoka nje nakuwaje ijue vapi iko juluku ya kuiba? Iko Swahili mingi naleta hii mizi baba yangu. Kwanini nageuza hindi bata. Kuku iko kunya veve sema bata.  Hata kama iko hindi nasirika na Swahili kuiba, naonea hindi bure dugu yangu. Si hindi yote baka dugu yangu.”
Msomi anakula mic, “Nakubaliana nawe Kanji. Wizi mkubwa huu lazima uwe na wakubwa nyuma yake. Leo mnashangaa hivi vimilioni saba had inane. Je waliofunga mita ya mafuta walikuwa wakitengeneza bilioni ngapi kwa siku? Je walioruhusu mibwimbwi ijae na kupitishwa kayani hadi Bondeni wakanasa maguni walikuwa wakiingiza bilioni ngapi? Je watoto wa vigogo pale BoT wanaingiza bilioni ngapi kwa siku? Kama alivyosema Dk Mipawa ni kwamba kaya hii ni ya skandali na mali ya chizi. Mie nadhani hapa tunachopaswa kufanya kama wahanga ni kuingia mitaani kudai zirudishwe sheria za maadali ya utumishi na si utumiaji umma ili kila atakayekuwa anapata anachopata aeleze amekipata wapi.”
Anakunywa kahawa. Inamkwama na kukohoa sana kiasi cha kutoa machozi. Anaendelea baada ya kutulia na kusema, “Nakubaliana wanaosema kuwa hii ni dili ya wakubwa. Sitashangaa kugunduliwa ujambazi mwingine kama huu hasa ikizingatiwa kuwa wakubwa waliouwezesha wameahidiwa ulinzi na mkubwa ambaye amekuwa akitufunga kamba kuwa anapambana na ufisadi ili tupate maisha bora wakati anahangaisha wezi na mafisadi wadogo.”
Sofia Lion aka Kanungaembe anakula mic, “Kaka hapa umemaliza kila kitu. Hizi kama si kamba ni Sanaa kama kawa ndugu yangu. Huwezi ukapambana na vifaranga kwa kunya ndani wakati uko kitanda kimoja na jogoo yaani baba yao aliyewafundisha kunya ndani. Huu ni utani mbaya na jipu la aina yake. Sijui nani alitumbue iwapo mtumbuaji ameamua kulisamehe?”
Mbwamwitu aliyekuwa akisoma gazeti na kunong’ona na Mchunguliaji anakula mic, “ Kuna jamaa yangu wa usalama wa Kaya amenitonya kuwa mafisadi wakubwa watapeta hasa ikizingatiwa kuwa wapingaji wamepigwa pini wasiwaletee wenye maulaji yao kelele wala kuwawazidishia mbu. Hivyo, mjiandae kuliwa sana.”
Kabla ya kumaliza Mgosi anamkata jicho na kusema, “Kama kuiwa waiwe wao. Haiwi mtu hapa vinginevyo tutapigana zongo bue ohooo.”
“Hakuna cha zongo wala nini. Kama zongo kawapige hao mafwisadi wanaoendelea kutufilisi wakisaidiana na wezi wetu wa kuzaa wenyewe. Mbona zongo lako hilo hujawapiga akina Escrew, EPA, mzee wa Vijsengi, Lungumi na majambazi wengi bila kumsahau mwanaharamu Kagoda na washitiri wake wa Richmond waliomtosha zigo lao Eddie?”
Mpemba anakula mic tena, “Yakhe umekumbusha. Haya mambo ya kupigana zongo hayatosaidia kitu. Dua la kuku halinpati mwewe ati. Tuamue tufanye kitu hasa kuisulutisha sirikali itusikize badala ya kutegemea maamuzi ya ntu mmoja eti kwa vile tulimpa madaraka. Yeye awatumbua wenzie tena kwa kunchagua atakaye. Je yeye nani antumbua?”
“Ami sasa inaonekana hujitaki. Unaanza hata kuwashuku watakatifu na wenye vifua wakati weshasema hakuna wa kuwashauri kwa vile wao wanajua kila kitu?” anachomekea da Sofia huku akiweka rinda lake vizuri kichwani.
Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita mkewe na jambazi wa bilioni saba. Acha tumtoe mkuku ili tumfanyie kitu mbaya.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Kwa wanandoa na watarajiwa burudika na wimbo huu wa kikikuyu

$
0
0
 Wewe ni nyama ya nyama zangu
Wewe ni mfupa wa mfupa wangu
Wewe ndiye Mungu amenichagulia
Wewe uwe furaha ya moyo wangu

Tumekuja hapa mbele
Mbele ya wazazi wangu
Mbele ya marafiki zangu
Mbele ya kanisa ya Mungu

changu ni chako
changu ni chako
Nitaishi nawe
Si kwa muda bali milele
Tutatenganishwa na kifo


Mtunzi wa wimbo huu ni Joyce Wanjiru

Kumbe tukiamua kama taifa tunaweza!

$
0
0

            Zoezi la ununuzi wa madawati nchini linatia moyo sana. Zoezi hili pia lina somo kuwa kumbe Afrika ikiamua inaweza kujitegemea na kuachana na uombaomba na kopa kopa. Kama alivyowahi kusema marehemu baba wa taifa, kweli uchumi tunao ila tumeukalia.
Jambo jingine linalojitokeza kwenye zoezi la kujitosheleza kwa madawati ni ukweli kuwa tulichokuwa tunakosa ni muamko na vipaumbele. Nadhani, baada ya kumaliza zoezi la madawati, tuhamie kwenye vitanda kwenye hospitali na zahanati zetu. Kama tutaendelea kubana na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, tunao uwezo wa kujitosheleza kwa kila kitu kama taifa kiasi cha kuwa mfano bora kwa nchi nyingine ambazo hazijachukua hatua kama tulizokwisha kuchukua.
Leo tutaongelea mambo machache ambayo taifa letu limeonyesha kuwa waafrika wana kila sababu ya kujikomboa na kuondokana na udhalilishwaji kimataifa na kitaifa.
Mosi, angalia jinsi fedha nyingi za umma zilivyookolewa baada ya kuopiga marufuku safari za nje ambazo nyingi zilikuwa ni kwenda kufanya shopping na kujilipa per diem kwa wezi wachache wenye madaraka.
Eneo jingine ni utenguaji wa uteuzi wenye kutia shaka. Hili litasaidia kila mteuliwa kujua kuwa yuko kwenye ofisi ya umma kuwatumikia wananchi na si kuwatumia au kuzitumia ofisi kama kijiko cha kuchotea utajiri. Ukiachia safari za nje, kuna hili la kuanzishwa kwa mahakama ya mafisadi. Si haba, hatua hii inatoa tahadhari kuwa sasa mafisadi wajiandae. Tusiridhike na kubweteka na mahakama. Tubadili mifumo na sheria zetu ili kupambana na jinai hii inayotishia mshikamano na mustakabali wa taifa. Sasa mahakama tunayo. Twende mbele na kuwakamata mafisadi bila kuangalia sura wala mafungamano kama ilivyo sasa.
Ukiachia kulega lega kwenye mapambano dhidi ya ufisadi–ambayo, kimsingi, yanamtegemea rais peke yake–kuna eneo jingine ambapo tumepiga hatua ambayo ni kupunguza ukubwa wa serikali. Hatua hii  licha ya kuokoa fedha nyingi na kusambaza ajira kwa watu wengine badala ya kung’ang’aniwa na watu wachache imeleta damu mpya kwenye nafasi za juu. Hakuna kitu kimesaidia kupunguza matumizi ya fedha za umma kwenye ajira zisizo na ulazima kama kuwa na baraza kubwa la mawaziri. Sambamba na kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri, tunaishauri serikali kuhakikisha haiongezi idadi ya mikoa au wilaya. Kama tungeangalia kwa makini, kuna baadhi ya mikoa iliyoanzishwa kisiasa zaidi ya uhitaji.
 Pamoja na kufanya vizuri kwenye mambo yaliyotajwa hapo juu, kuna maanguko. Haya ni pamoja na:
Mosi, kuminya demokrasia kwa kuwazuia na kuwafungia wabunge wa upinzani kuhudhiria bunge jambo ambalo linawanyima fursa ya kufanya kazi waliyotumwa kufanya na wale wanaowawakilisha. Pia kuendelea na uhuni ambao umekuwa ukiendelea bungeni ni ushahidi kuwa licha ya kuvunja katiba na haki za binadamu, tunajenga dhana kuwa serikali inaogopa demokrasia hasa kukosolewa jambo ambalo linapaswa kuchukuliwa kama chachu ya maendeleo. Isitoshe, nchi hii si mali ya chama fulani wala kundi fulani la watu eti kwa vile lilipata kura nyingi. Inashangaza kuona serikali inajiwekea rekodi mbaya kwa kuwapuuzia wananchi wapatao milioni sita na ushei ambao hawakuichagua. Hata wangekuwa wawili au mtu mmoja, bado wana haki ya kusikilizwa mawazo yao hata kama hayawafurahishi wala kupendwa na waliopo madarakani.
Sehemu nyingine tulipoanguka ni kutokuwa na ithibati na kutenda haki sawa katika vita ya ufisadi. Unashangaa kuona watumishi wanaotuhumiwa kusaidia wizi kwa mfano bandarini kufukuzwa kazi au kusimamishwa wakati watuhumiwa wa kashfa kubwa kama vile Lugumi, Escrow na nyingine wakiendelea kutanua. Je kunani nyuma ya pazia au nchi yetu imegawika kwenye matabaka ya sacred and black cows?
Sehemu nyingine tulipoanguka sana ni ile rais kuonekana kama yuko juu ya katiba akiamua nani afanyiwe au asifanyiwe nini hasa kuhusiana na tuhuma za ufisadi na matumizi ya fedha za umma, matumizi mabaya ya madaraka na uzembe. Rejea, kwa mfano, rais kutoa hakikisho kwa watangulizi wake hivi karibuni baada ya baadhi ya watanzania–ambao kimsingi, ndiyo wahanga wa kadhia zilizotajwa hapo juu–kutaka baadhi ya wakubwa wafikishwe mahakamani kwa kadhia tajwa. Hii inajenga dhana kuwa kuna watu wasioguswa hata wakabiliwe na jinai kiasi gani. Hii si sawa na si vizuri kwa taifa linalotaka kujirekebisha tokana na makosa ya nyuma huku likitoa onyo kwa wajao.
Sehemu nyingine ni ile hali ya serikali ya sasa kushindwa kuwakamata watuhumiwa wakubwa wa biashara haramu ya mihadarati. Japo ni mapema kuilamu serikali, kwa namna ilivyokaa kimya bila kuonyesha makucha yake dhidi ya kazia hii, uharibifu unazidi kutendeka kwa taifa na watu wetu.
Tumalizie kwa kuitaka serikali irekebishe kasoro zilizotajwa huku ikiongeza mkazo kwenye maeneo ilikofanikiwa. Kwani, bado watanzania wanakabiliwa na changamoto ambazo nyingi zake zinasababishwa na ukosefu wa nia thabiti, vipaumbele na ushirikiano katika kupambana nazo. Pia tunashauri kuwa baada ya kukamilisha madawati mashuleni twende kwenye taasisi nyingine kama mahospitali, zahanati, vituo vya kulelea watoto yatima na wazee na nyinginezo ambazo zina hali mbaya bila kusahau kuongeza nguvu katika kupambana na jinai ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Hapa Dokta Magufuli akubali ameteleza

$
0
0

Hivi karibuni, rais John Pombe Magufuli aliwashangaza, kuwazodoa, kuwanyamazisha na kuwachanganya mengi ukiachia mbali naye kujichanganya. Akipokea ripoti ya uchaguzi mkuu wa 2015, Magfuli aliwamua–kwa makusudi kabisa–kufyatua kombora lake la kwanza lilioacha mashabiki na wapenzi wake wakigawanyika na wengine kuanza kutia shaka spirit na sincerity ya juhudi zake za kupambana na ufisadi. Hii ilitokana na kutoa hakikisho kwa watangulizi wake dhidi ya kashfa mbali mbali zinazowakabili kiasi cha baadhi ya watanzania kutaka wafikishwe mahakamani kujibu tuhuma hizo.
 Magufuli alikaririwa akiwaambia marais wastaafu hawa akisema, “Wala usisikilize kelele nyingine hizi za ovyoovyo. Wewe uko salama na hilo ndilo jukumu langu kama Rais wa Awamu ya Tano kuhakikisha viongozi wote wastaafu wako salama.”  Sijui hapa tuamini nani kati ya katiba na rais? Maana, wajibu wa kumlinda kila mtanzania bila kujali cheo chake ni wa katiba na watanzania wote bila ubaguzi wala upendeleo. Pia marais wastaafu wana kinga kikatiba na si kwa matakwa wala hakikisho la rais. Rais anapata wapi mamlaka ya kuwalinda marais wastaafu? Je hii haiwezi kutafsiriwa kama rais kujiweka juu ya sheria jambo ambalo linapingana na matakwa na matarajio ya waliomchagua?
 Kuzidi kuwatoa hofu aliowaita wazazi wake hofu–pamoja na mengine mengi–Magufuli aliongeza, “Mjue mimi mtoto wenu nipo. Watachonga lakini nataka kuwahakikishia mtaishi kwa amani. Mengine hata mkiyasikia, tupa pembeni kwa sababu mimi ni kiongozi wenu mwenye jukumu la kuliongoza Taifa hili nipo pamoja nanyi.” Je Magufuli anadhamiria kufanya hivyo–huku akijua ni kinyume cha kiapo chake cha kuwatendea kwa usawa watanzania–au alikuwa anatafuta kuungwa mkono kwenye mchakato wa kukabidhiana uenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kulikokuwa kumeanza kuzua utata ukiachia mbali kukwama hata kutokea shutuma za kukwamishana kwa kuogopa kutumbuana? Je Magufuli alikuwa anatania au ulimi uliteleza? Maana Magufuli aliapa kulinda na kutekeleza katiba ya nchi bila upendeleo, huba wala chuki.  Wapo wanaohoji anakopata uhalali, jeuri na nguvu ya kusema haya aliyosema Magufuli. Je anayepaswa kusamehe mtu makosa yake zaidi ya mahakama ni nani nchini? Kama watanzania wanataka wahusika washitakiwe, yeye ni nani au anataka kuifanya Tanzania mali yake binafsi?  Tundhani ni busara rais awasikilize wananchi wanataka nini na si yeye anataka nini; vinginevyo akiri kuwa yuko madarakani kuwatumia na si kuwatumikia wananchi.
 Wakosoaji wake wanaona kama Magufuli anaufanya urais wake kuwa urithi na si dhamana aliyoaminiwa na wananchi anaoanza kuwapiga teke sasa akikumbatia wale waliowanyonya na kuwaongezea umaskini kwa sera mbovu na kuendelea kulipwa marupurupu makubwa na lukuki wakati wengine hakuna walichofanya zaidi ya kuliangamiza taifa kiuchumi. Tunadhani rais hana haja ya kuwapa silaha wakosoaji na wapinzani wake kwa kujiingiza kwenye siasa za kulindana ambazo ni kinyume cha katiba na ahadi alizotoa kwa watanzania kuwatumikia bila ubaguzi wala upendeleo. Rejea maneno ya Magufuli mwenyewe ambaye amekuwa akiwatuhumu watangulizi wake kuridhia utapeli kama vile wafanyakazi hewa, kutofunga mita ya kupima mafuta yanayoingia nchini, kutwaa mali za umma kama vile Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira, UDA, Escrow na kashfa nyingine nyingi. Ni kama Magufuli anaanza kujichanganya, kuwachanganya wananchi na kujipiga mwenyewe.
Wapo wanaoona kama rais anaanza kuwasha moto ambao hawezi kuuzima hasa wakati huu ambapo taifa lipo msambweni baada ya wabunge wa upinzani kuhujumiwa bungeni. Hapa kinachotakiwa ni busara na si siasa za mitandao ya kulindana. Nadhani hata ndani ya CCM Magufuli alisifika kutokuwa na mitandao. Sasa iweje sasa aanzishe mitandao hata kama ni ya wastaafu? Kama watanzania wanataka wahusika washitakiwe yeye ni nani au anataka kuifanya Tanzania mali yake binafsi? Rais awasikilize wananchi wanataka nini na si yeye anataka nini vinginevyo akiri kuwa yuko madarakani kuwatumia na si kuwatumikia wananchi. Nadhani Magufuli alichaguliwa na kuapa kuilinda na kuitekeleza katiba ya nchi bila upendeleo, huba wala chuki. Yuko ikulu kuwalinda watanzania na si watawala wa zamani wanaokabiliwa na tuhuma za ufisadi, ubabaishaji, kuisababaishaji na kuiingiza nchi kwenye umaskini bila sababu. Nadhani Magufuli anajua tuhuma zinazowakabili wahusika. Wapo wanaotuhumiwa kwa kashfa kama vile k uuza mbuga ya wanayama ya Loliondo, EPA, NBC, Kiwira na uwekezaji wa kijambazi wakati wakati wengine wakikabiliwa na wizi wa EPA, Escrow, UDA, utoroshaji wanyama hai, ujangili, uzembe, uzururaji, matumizi mabaya ya fedha za umma na mengine mengi. Siku zote Magufuli amesikika akisema anakerwa na uovu. Je hayo yaliyoorodheshwa hapo si uovu au anachagua nani awe muovu na nani asiwe?
Ifahamike kuwa Tanzania ni ya watanzania wote na si watawala wao wawe waliopo au waliopita.
Kazi ya Magufuli ni kuhakikisha usalama wa kila mtanzania na si marais wastaafu vinginevyo tubadili katiba inayotamka kuwa Tanzania ni mali ya wananchi na si watawala.
Wapo wanaoona kama maneno yake ni tofauti na kauli zake za kuleta Tanzania mpya isiyo na ufisadi wakati anakumbatia ufisadi wa wakubwa akiwapatiliza wadogo.    
Tumalizie kwa kumkubushia kauli yake aliyotoa hivi karibuni akihutubia kwenye kufungua mradi wa mawasiliano wa polisi kwenye viwanja vya Biafra aliposema, “Watanzania wamechoka na fedha zao kuliwa na watu wachache… wakale mali za bibi zao kule.” Kwa waliomsikiliza vizuri, walishangaa mantiki ya kauli yake. Hivi hawa wachache anaoongelea Magufuli ni wapi wakati anaowakingia kifua ni wachache pia; au ni kwa vile walikuwa na madaraka? Je kunani kwenye ndoa hii baina ya rais na marais wastaafu? Inatoa picha gani kwa viongozi wajao?
Chanzo: Mseto wiki hii.

Mlevi hakuangusha futari mwaka huu

$
0
0

Kumbe tukiamua kama taifa tunaweza!

$
0
0

           Zoezi la ununuzi wa madawati nchini linatia moyo sana. Zoezi hili pia lina somo kuwa kumbe Afrika ikiamua inaweza kujitegemea na kuachana na uombaomba na kopa kopa. Kama alivyowahi kusema marehemu baba wa taifa, kweli uchumi tunao ila tumeukalia.
Jambo jingine linalojitokeza kwenye zoezi la kujitosheleza kwa madawati ni ukweli kuwa tulichokuwa tunakosa ni muamko na vipaumbele. Nadhani, baada ya kumaliza zoezi la madawati, tuhamie kwenye vitanda kwenye hospitali na zahanati zetu. Kama tutaendelea kubana na kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, tunao uwezo wa kujitosheleza kwa kila kitu kama taifa kiasi cha kuwa mfano bora kwa nchi nyingine ambazo hazijachukua hatua kama tulizokwisha kuchukua.
Leo tutaongelea mambo machache ambayo taifa letu limeonyesha kuwa waafrika wana kila sababu ya kujikomboa na kuondokana na udhalilishwaji kimataifa na kitaifa.
Mosi, angalia jinsi fedha nyingi za umma zilivyookolewa baada ya kuopiga marufuku safari za nje ambazo nyingi zilikuwa ni kwenda kufanya shopping na kujilipa per diem kwa wezi wachache wenye madaraka.
Eneo jingine ni utenguaji wa uteuzi wenye kutia shaka. Hili litasaidia kila mteuliwa kujua kuwa yuko kwenye ofisi ya umma kuwatumikia wananchi na si kuwatumia au kuzitumia ofisi kama kijiko cha kuchotea utajiri. Ukiachia safari za nje, kuna hili la kuanzishwa kwa mahakama ya mafisadi. Si haba, hatua hii inatoa tahadhari kuwa sasa mafisadi wajiandae. Tusiridhike na kubweteka na mahakama. Tubadili mifumo na sheria zetu ili kupambana na jinai hii inayotishia mshikamano na mustakabali wa taifa. Sasa mahakama tunayo. Twende mbele na kuwakamata mafisadi bila kuangalia sura wala mafungamano kama ilivyo sasa.
Ukiachia kulega lega kwenye mapambano dhidi ya ufisadi–ambayo, kimsingi, yanamtegemea rais peke yake–kuna eneo jingine ambapo tumepiga hatua ambayo ni kupunguza ukubwa wa serikali. Hatua hii  licha ya kuokoa fedha nyingi na kusambaza ajira kwa watu wengine badala ya kung’ang’aniwa na watu wachache imeleta damu mpya kwenye nafasi za juu. Hakuna kitu kimesaidia kupunguza matumizi ya fedha za umma kwenye ajira zisizo na ulazima kama kuwa na baraza kubwa la mawaziri. Sambamba na kupunguza ukubwa wa baraza la mawaziri, tunaishauri serikali kuhakikisha haiongezi idadi ya mikoa au wilaya. Kama tungeangalia kwa makini, kuna baadhi ya mikoa iliyoanzishwa kisiasa zaidi ya uhitaji.
 Pamoja na kufanya vizuri kwenye mambo yaliyotajwa hapo juu, kuna maanguko. Haya ni pamoja na:
Mosi, kuminya demokrasia kwa kuwazuia na kuwafungia wabunge wa upinzani kuhudhiria bunge jambo ambalo linawanyima fursa ya kufanya kazi waliyotumwa kufanya na wale wanaowawakilisha. Pia kuendelea na uhuni ambao umekuwa ukiendelea bungeni ni ushahidi kuwa licha ya kuvunja katiba na haki za binadamu, tunajenga dhana kuwa serikali inaogopa demokrasia hasa kukosolewa jambo ambalo linapaswa kuchukuliwa kama chachu ya maendeleo. Isitoshe, nchi hii si mali ya chama fulani wala kundi fulani la watu eti kwa vile lilipata kura nyingi. Inashangaza kuona serikali inajiwekea rekodi mbaya kwa kuwapuuzia wananchi wapatao milioni sita na ushei ambao hawakuichagua. Hata wangekuwa wawili au mtu mmoja, bado wana haki ya kusikilizwa mawazo yao hata kama hayawafurahishi wala kupendwa na waliopo madarakani.
Sehemu nyingine tulipoanguka ni kutokuwa na ithibati na kutenda haki sawa katika vita ya ufisadi. Unashangaa kuona watumishi wanaotuhumiwa kusaidia wizi kwa mfano bandarini kufukuzwa kazi au kusimamishwa wakati watuhumiwa wa kashfa kubwa kama vile Lugumi, Escrow na nyingine wakiendelea kutanua. Je kunani nyuma ya pazia au nchi yetu imegawika kwenye matabaka ya sacred and black cows?
Sehemu nyingine tulipoanguka sana ni ile rais kuonekana kama yuko juu ya katiba akiamua nani afanyiwe au asifanyiwe nini hasa kuhusiana na tuhuma za ufisadi na matumizi ya fedha za umma, matumizi mabaya ya madaraka na uzembe. Rejea, kwa mfano, rais kutoa hakikisho kwa watangulizi wake hivi karibuni baada ya baadhi ya watanzania–ambao kimsingi, ndiyo wahanga wa kadhia zilizotajwa hapo juu–kutaka baadhi ya wakubwa wafikishwe mahakamani kwa kadhia tajwa. Hii inajenga dhana kuwa kuna watu wasioguswa hata wakabiliwe na jinai kiasi gani. Hii si sawa na si vizuri kwa taifa linalotaka kujirekebisha tokana na makosa ya nyuma huku likitoa onyo kwa wajao.
Sehemu nyingine ni ile hali ya serikali ya sasa kushindwa kuwakamata watuhumiwa wakubwa wa biashara haramu ya mihadarati. Japo ni mapema kuilamu serikali, kwa namna ilivyokaa kimya bila kuonyesha makucha yake dhidi ya kazia hii, uharibifu unazidi kutendeka kwa taifa na watu wetu.
Tumalizie kwa kuitaka serikali irekebishe kasoro zilizotajwa huku ikiongeza mkazo kwenye maeneo ilikofanikiwa. Kwani, bado watanzania wanakabiliwa na changamoto ambazo nyingi zake zinasababishwa na ukosefu wa nia thabiti, vipaumbele na ushirikiano katika kupambana nazo. Pia tunashauri kuwa baada ya kukamilisha madawati mashuleni twende kwenye taasisi nyingine kama mahospitali, zahanati, vituo vya kulelea watoto yatima na wazee na nyinginezo ambazo zina hali mbaya bila kusahau kuongeza nguvu katika kupambana na jinai ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi.
Chanzo: Tanzania Daima.

Fighting graft: Let’s fry all fish like China

$
0
0

            I must make a clean breast that proposing that some criminals be hanged is not such cool, especially for the biggies who commit graft-related crimes aka Ufwisadi. I know; my pals, human rights activists can be tickled. Sweat it not pals. Whose right’s more vital than that of the other?  Some condemn death penalty even for killers! Where do we put the right of the victims of homicide?
            After getting news that one bugger’s making cool $ 3,500 to 4,000 per sec., my friend in Beijing called me. He’s baffled to learn that begging hunk like ours could coddle such a criminal. He wondered where the powers that be were. He asked if we’d a firing squad or a hangman or something to see how his hunk could help in providing us with one. I warned him that human rights don’t allow such actions. He quoted Jeremy Bentham, a renowned social reformer, saying that human rights are but “Nonsense upon Stilts.” Thus, it isn’t bad to goad for the frying of all fish involved in graft, particularly abundant sharks we’ve. If you’ve forgotten, I can jog your mind. Remember Kagoda aka Roast Tamu l’Aziz, Jimmy Rugemalayer, Singasinga Setiiii, Andy aka Vijisenti, Ni Zero Kadamage, Lungumi, Simmie Kisssssena of UdA and many more? If it were China, such buggers would have been history.
To me, criminals have never been in my good graces. If I’d my way, theirs would only be bullets if not a hangman’s noose. I hate them more than the devil itself. They kill many innocent boozers whose offices they use to rob and vend as it’s been for over 30 years since Mzee Mchonga exited power. That time, I remember; a lost friend of mine, Kim Ndayishimiye Abel’s worried; the hunk’d go to the dogs; which it did.
I used to love the West. When it started double standard behavior, I shifted to China vis-à-vis how it deals with criminals who rob the hunk.  China doesn’t pay any hoot to human rights, especially when those defended are animals. Again, I hate Chinese who poach our animals.
Those who grew up under MzeeNchonga may remember how we used to enjoy free social services now fisadis and their abettors in power enjoy alone. At the time, China and Bongo were all socialistic hunks.  When the going got tough, both hunks shelved socialism.  The difference is however; China became an economic miracle of the world for ruthlessly taking on graft. Bongo became an economic debacle for blessing graft. Guess what, if Bongo were China scams such as EPA, Escrow, Lugumi, Kagoda, Meremeta, Mwananchi Gold, UDA and the one in which one puta was making a seven million killing per minute wouldn’t have been shelved up till the dust settles down so that boozers can–once again–forget.  I’m not making this up. Are you updated?   How if all implicated criminals are in our streets eating kukus as their victims are eating dust.
China beats us at dispensing justice. There are no sacred cows or biggies or sharks. China equally ruthlessly fries criminals. It pays no damn even if the culprit’s a president or the presidente sharing bed with the big man as it is in Africa. Remember what happened to Chairman Mao’s concubine,Jiang Qing or Madame Mao?
Though many boozers are blaming the culprit of seven million dosh, where’s the govt? Did this criminal act alone? The day we’re told he’s apprehended, President Joni Kanywaji Mugful said there were abettors in the TRA.  Since then, nothing’s ever been heard about apprehending his accomplices. What’s up? And who’s fooling whom? Mugful told us; the punk’s in good hands. Is that all? Boozers need updates to gauge if justice’s done or not. Why trusting the same crooks that allowed criminals to rob our hunk while they’re supposed to be behind bars waiting to face the music had Bongo been China. Isn’t his case going to end up just like Escrow, Kagoda, UDA, Lungumi and many more that seem to have already been swept under the carpet? Sometimes, I wonder how sane people could become insane and blind this way. So, too, I wonder to hear some complaining that those baying for the blood of criminals are saying vitu vya ovyo ovyo or nonsense, really? It pains behind imagination when nonsense is treated honourably while wisdom is turned into nonsense as it recently happened when one boozer wanted former biggies crucified.
Let’s wrap up asking Danganyika to not only swig China’s dosh. We need to emulate even its doggedness in fighting grafts so that our hunk could enjoy abundant resources it is endowed with.
Guardian: Sunday.

Kunashangaza kule hakuna mizigo

$
0
0
Huu wimbo ni kutoka Zimbabwe
Unasema huko hakuna mizigo
Malaika wanafanya kazi ya kubebea mizigo yako
Sijui kama ni kweli au

Dikteta anaposhuka kwenye gari kuchimba dawa

$
0
0
  President Museveni makes a roadside call Hivi karibuni imla wa Uganda Yoweri Museveni aliwashaza waganda kwa kuchomoka kwenye gari na kuweka kiti barabarani na kuanza kuchonga bila kujali kuwa kulikuwa na watu  nyuma na mbele ya msafara wake wakipoteza muda kwa sababu ya wendawazimu wa mtu mmoja. Kwa habari zaidiBONYEZA HAPA.

Kijiwe: Makufuli tukumbuke kwa maburungutu

$
0
0

            Baada ya kijiwe kushuhudia ukarimu wa rahis Joni Kanywaji Makufuli, kimeamua kumbipa mzinga lau nacho kifaidi utukufu wake.
Mgosi Machungi analianzisha, “Jamani mmeona jinsi rahis Makufui aivyomwaga njuuku kwa Bakuata? Kwanini nasi tusimtwishe mzinga hata kama hatiendi hijai? Maana, jamaa anaonekana anazo; hacheei kukata mshiko.”
“Kweri tunahitaji njuruku kujikimu hasa ikizingatiwa hatuna miladi wala kuripwa mishahala kama hao, ira napinga hii tabia ya munene kumwanga mabulungutu badara ya kuandika cheki,” anachomekea Mbwamwitu huku akimuigiza munene Kanywaji kwa lafudhi yake ya Kizinza.
Kapende anamchomekea, “Hivi kama rahis–anayepaswa kuwa mfano anafanya hivi–sisi akina yakhe tutafanyaje? Hii maana yake ni kwamba jamaa haweki njuluku benki jambo ambalo ni mfano mbaya kiuchumi. Nadhani hata yeye analijua–na kama halimanyi–washauri wake wanapaswa kulijua na kumuonya mfano anaoonyesha. Kumbuka; jogoo aliwafundisha vifaranga kunonihiii ndani.”
“Unashangaa hilo siyo! Mbona jamaa amekuwa akifanya mambo kama vile yeye muungu pamoja na kuwa na shahada ya uzamizi? Rejea anavyosema ‘silikali yangu na si ya wabongo’; au anavyosema ‘nataka si wanakaya wanataka vile na hivi.’ Hapa maana yake ni kwamba jamaa yuko juu ya kila kitu na kila kitu ni mali yake binafsi. Hukuona alivyowakingia fua wanene wa zamani kana kwamba kaya ni mali yake binafsi?” anazoza Mipawa huku akibusu kombe lake la kawaha.
Mpemba anakatua mic, “Yakhe hata mie nshangaa sana. Jamaa yu afanya mambo kama vile tuko kwenye ile miaka ya utwahuti ya 60 ambapo kila mnene alijiendeshea kaya alivotaka. Wallahi huyu jamaa ankumbusha Karumekenge wa kwanza alivogeuza Zenj mali binafsi.”
“Jamani nyinyi taka yeye fanya nini nyinyi. Veve naweza kata shiko kuba kama ile nakata Kufuli? Kwanini hapana kubali juluku nakosekana sipokuwa kwa ile mizi naiba milioni saba kwa dakika,” analalamika Kanji.
Mheshimiwa Bwege hamkawizi; anaramba mic, “Kanji najua nyinyi huabidia ng’ombe na njuluku bila kujali kama zinatolewa kwa utaratibu au la. Tuwe wakweli. Kama rahis haweki njuluku benki, hao wauza bwimbwi si wataijaza kwenye mashimo kiasi cha kuathiri uchumi? Tusiongee kama hatujui uchumi tena wa karne ya 21.”
Mzee Maneno anakula mic, “Mie simlaumu mtani wangu. Hamjui kuwa jasiri haachi asili? Sitegemei Msukusi aweke njuluku benki,” anamalizie akiwaangalia Mijjinga na Mipawa wanaotabasamu; kwa vile ni mtani wao Mzaramizi.
Msomi anapoka mic, “Mimi sikushangaa hasa ikizingatiwa kuwa huku uswekeni viongozi hufanya kama jamaa yule wa kwenye Biblia aitwaye Paul aliyesema, ‘fuateni niwaambiayo lakini siyo nifanyayo.’ Kwani hamuoni anavyotumbua awatakao na kuwasaza awatakao? Hapa hujagusia kutoa maagizo yanayokinzana na sheria kama kuwaagiza wakubwa wa wilaya watumie ulaji wao watakavyo kuwakomesha wabaya wao. Hujagusia namna alivyowahimizi wazee wa mabao kuiba vipuri vya mikangafu watakayokamata na kuamuru ipelekwe kituoni ikakongorolewe. Ama kweli ukishangaa ya Njaa Kaya utaona ya Kanywaji! Hatuwezi kuendesha kaya kama mali ya mja binafsi. Lazima tufuate sheria tulizojiwekea kwa hiari yetu tena kwa usawa bila huba, ubaguzi wala upendeleo au vipi?”
Anabwia gahawa yake na kuendelea, “Kama jamaa hatabadilika, nadhani huu ni mwanzo tu; mtaona mengi. Maana, kwa hali ilivyo, waliomzunguka jamaa wanamgwaya ili wasipoteze kitumbua chao usawa huu wa kuburuzana.”
Da Sofia Lion aka Kaunungaembe anakula mic, “Kaka Msomi usemayo kweli tupu. Kama watani zake walivosema, jasiri haachi asili. Kwani, kabla ya hili la kumwaga miburungutu, tulishuhudia bi mkubwa wake akimwaga misaada kwa wazee ambayo alivyoipata ajua yeye na Mungu wake. Wengi tulimsifu tukidhani asingeanzisha NGO kama dada zangu kina Ana Tamaa na Si Salama. Kumbe tuliingizwa mkenge. Anayo NGO japo hajaitangaza rasmi. Matendo yake yamekaa Ki-NGO, NGO.”
Mchunguliaji anakula mic, “Naungana na brother Kanji kumuunga mkono Dk Kanywaji japo si katika kila jambo. Ni nani–kati ya watangulizi wake–aliyewahi kufanya hivi pamoja na wengine kuiba sana? Usawa huu ukiona mtu anakupa neema kama alivyowafanyia jamaa wa Bakuata, lazima ushuru; tena bila kuuliza amepataje au ametumia utaratibu gani. Hili la bi nkubwa wake kusaka misaada hata kwa wanigeria halinipi taabu kama hatachukua kikubwa na kutoa kidogo kama walivyofanya akina Ana Tamaa na Si Salama.”
Mheshimiwa Bwege anarejea kwa hasira kidogo, “Ama kweli mkiambiwa mwaliwa msitunishe misuli. Hatuwezi kujigeuza mashimo kumeza kila kiingiacho bila kuhoji hata kugoma japo kidogo. Lazima sheria zifuatwe; vinginevyo tutaendelea kutumiwa na kuliwa tena kwa hiari yetu. Angalia jamaa alivyowaziba midomo wapingaji ili wasimghasi atembeze undavandava kama rafiki yake Ka-Game ambaye anaonekana kumhusudu bila kujua kilichoko nyuma ya pazia. Siku atakapogeukwa kama alivyofanyiwa M7 atakumbuka maneno yangu ya busara ambao–bila shaka–mzee Mpayukaji utayaanidika ili wote wasome na kuwa mashahidi wa unabii huu.”
Mbwamwitu anarejea, “Jamani acheni rongo rongo zenu. Kwanini–kama kijiwe–tusitume ujumbe kwa munene atukatie iwe kwa maburungutu au macheki. Sisi tumepigika; tunahitaji njuluku kwanza. Mengine yatafuata baadaye baada ya kuhomola. Kwanini tusijifunze toka kwa Bakuata ambao sasa wamemmezea ili baadaye wamuwashe akiwachemshia kwenye ajenda zao za siri?
Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita manzi aliyejazia kiasi cha kutufanya tuache kila kitu na kumukodolea huku tukila kwa macho!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.

Tunamsihi rais aongee lugha ya taifa

$
0
0

 
            Kwa watu wanaojua maana na sababu ya kuwa na rais kama kielelezo na mwakilishi wa nchi yeyote, watakubaliana nasi kuwa kila anachofanya lazima kiakisi taifa lake. Moja ya kitu kinachotengeneza taifa ni pamoja na kuwa na lugha yake ya taifa. Tanzania–tangu kupata uhuru–tuliamua, kama taifa, kufanya lugha ya Kiswahili iwe lugha ya taifa. Pia, tuliamua lugha ya mtawala wetu wa zamani Uingereza, yaani kiingereza kuwa lugha ya pili ya taifa ili kutuunganisha na mataifa mengine. Hivyo, Tanzania ina lugha rasmi mbili; Kiswahili na Kiingereza.
Baada ya rais John Pombe Magufuli kuingia madarakani, amejitahidi kuepuka kutumia lugha zetu mbili. Badala yake–kwa sababu anazojua mwenyewe–hutumia lugha isiyo rasmi almaaruf Kiswanglish yaani mchanganyiko wa Kiswahili na maneno machache ya Kiingereza.  Japo wapo waliokwisha kutoa shule juu ya umuhimu wa rais kutumia lugha kwa usahihi, huko hatutaenda. Tutakachozungumzia hapa ni umuhimu wa rais kutumia lugha moja ili kuweza kuwasiliana na watu wake. Mfano, rais anapochanganya Kiingereza na Kiswahili–licha ya wananchi hasa wa kada ya chini kielimu–anawachanganya hata wageni wanaotaka kujifunza Kiswahili. Mfano, hivi karibuni, rais alikaririwa akisema, “Ukitumia tuta hilo hilo, it even becomes more cheaper.”  Sijui kama mkulima wa Kahama au Geita anaambua kitu katika mkanganyo huu unaofanywa na kiongozi wao. Hata ukiandika neno more cheaper–kwa wanaotumia kikokotozi lazima kikuonye kuwa umechamsha. Neno sahihi ni cheaper than au much cheaper…..lakini si more cheaper. Mahali pengine ambapo rais anakosea mara kwa mara ni the East African Community ambayo yeye huiita East Africa Community ambayo kisheria haipo.  Nisingependa kuhariri hotuba yote ya rais aliyoitoa kwa muda mfupi ikajaa makosa mengi. Ninachotaka kuonyesha ni umuhumi wa rais wetu kuchagua lugha rasmi na sahihi ya kutuwakilisha kama taifa lenye utajiri wa lugha. Je rais hana washauri na wataalamu wanaopaswa kumwandikia hotuba kama hawezi au kumshauri kuandaa hotuba ya lugha moja kama anaweza? Najua kinachomsukuma Magufuli kupenda kutumia Kiswahili zaidi ni uzalendo. Hata hivyo, anapaswa akubali; Kiingereza ni lugha kubwa kuliko zote duniani kiasi cha kulazimisha mataifa kama China, Urusi na mengine ya Kiarabu kutumia mabilioni mengi kuwatuma watu wao kujifunza lugha hii ya kibiashara duniani. Hapa Kanada tuna lugha mbili za taifa, Kiingereza na Kifaransa. Hakuna anayeweza kuwa waziri mkuu wa Kanada bila kuzimudu lugha hizi barabara. Hata viongozi wa hapa wanapozitumia, huwa hawazichanganyi. Kwani, huchelea kuwachanganya wananchi wao. Hata pale anapochaguliwa mtu anayeona kuwa hawezi lugha moja au zote, hufanya bidii kuzimudu ili aweze kuwasiliana na wananchi wake barabara.
Wakati akimkaribisha rais wa Rwanda Paulo Kagame kufungua Maonyesho ya 40 ya Kimataifa ya Dar Es Salaam, rais Magufuli alichanganya lugha mbili kwa kupachika neno hapa na pale wakati mgeni wake aliamua kuzipanga kwa kuongea moja baada ya nyingine na siyo kuzichanganya ili kuwapa nafasi wakalimani wafanye kazi yao.
Kwa vile Kiswahili ni lugha taifa–tena inayokua kwa kasi–rais anapaswa ashauriwe umuhimu na ulazima wa kuongea Kiswahili safi bila kuchanganya Kiingereza au kama ataamua basi aongee Kiingereza pekee na Kiswahili pekee. Kama akichanganya basi asichanganye maneno bali kila lugha aipe fursa kwa usahihi wake kama alivyofanya Kagame. Nadhani, Magufuli atakuwa amejifunza hilo toka kwa Kagame ambaye amemsifia kwa kumpa kile alichoita madesa ambacho nacho si Kiswahili sanifu. Rais Magufuli–kama ataamua–anao uwezo na sababu za kuongea ima Kiswahili au Kiingereza safi na sanifu bila kulazimika kuchanganya. Tunaona hili kama tatizo kwa taifa lenye lugha inayojitegemea. Kwanza, rais anawafundisha nini vijana walioko mashuleni na watanzania kwa ujumla? Pili, anatoa picha gani kwa wageni kuhusiana na itifaki ya matumizi ya lugha kwa usahihi wake?
Tatu, kwa kiwango chake cha elimu, anapaswa kuzimudu lugha zote mbili bila kikwazo vinginevyo kuwe na namna. Haiwezekani mtu mwenye shahada ya uzamivu (PhD) asiweze lugha husika iwapo ametumia miaka zaidi ya 15 akitumia Kiingereza kama lugha ya kujifunzia asiweze Kiingereza. Najua rais Magufuli si mtaalamu wa lugha. Ni msomi wa kemia. Bado, kwa kipindi alichotumia Kiingereza kama lugha ya kitaaluma, lazima awe anakimanya vizuri tu. Itakuwaje watu wenye elimu ya chini kulinganisha na yake kama vile Kagame, Jakaya Kikwete na hata Amani Karume wakiweze yeye asiweze? Kama rais atahitaji kupigwa msasa kwenye kimombo asione aibu. Hakuna anayeweza kujua yote duniani. Heri akubali kutojua ili asaidiwe kuliko kuendelea kuruhusu utata uliopo kwa sasa kuhusiana na matumizi ya lugha ya rais Magufuli. Pia, ifahamike; kama walio karibu naye wanashindwa au kuogopa kumwambia ukweli, tutamwambia kama watanzania.
Tumalizie kwa kumshauri rais na washauri wake kuliangalia hili ili kuepuka kuwachanganya wananchi wetu hasa wa vijijini. Rais wetu lazima aeleweke kwa kada zote za wananchi wake na si wasomi au wajuzi wa Kiingereza tu kama ilivyo sasa anapochanganya lugha. Pia, ifahamike, tunatoa ushauri kwa nia ya kujenga na si kubomoa. “We should learn languages because language is the only thing worth knowing even poorly.” –Kató Lomb.
Chanzo: Mwanahalisi Jumatatu.
 
 

Tusinunue ndege kwa 'madesa'

$
0
0
 Image result for photos of bombardier c 400
           
            Neno desa au kuchota ujuzi, taarifa au majibu bila kuyafanyia kazi na kuyatumia kwenye kazi yako au kunakiri bila kufuata sheria au kukwepa sheria–kabla ya kuchaguliwa kwa rais John Pombe Magufuli–lilikuwa limefungiwa kwenye kuta za madarasa na vyumba vya mihadhara ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM). Hata hivyo, baada ya kuchaguliwa Magufuli ambaye ni mhitimu wa shahada tatu zote toka UDSM, neno desa limeingia kwenye msamiati tawala (mainstream).
Hivi karibuni vyombo vya habari vilimkariri Magufuli si zaidi ya mara moja akitumia neno desa kuanzia alipohutubia jumuia ya wana UDSM hadi alipomkaribisha rais wa Rwanda Paul Kagame aliyesema amempa desa au mbinu ya kununua ndege mbili kwa mpigo. Magufuli alisema, “Mwezi wa tisa tutakuwa tumepata ndege mbili mpya, nimepewa namna nzuri ya kupata ndege hizo na Rais Kagame baada ya kuwatuma maofisa wake ambao ni wataalam wa ndege waje na kunipa desa.”
Si vibaya kwa viongozi kupeana mbinu za kufanya mambo ingawa hili linatia shaka kwa namna moja au nyingine. Pia linaacha maswali mengi kuliko majibu. Je Tanzania–pamoja na kupata uhuru zaidi ya miaka hamsini iliyopita–haina wataalamu wake wenye ujuzi na wa kuaminika kufanya kazi hiyo hadi tukope wataalamu toka Rwanda? Kwa mujibu wa matamshi ya Magufuli ni kwamba Tanzania haina wataalamu wa kutafuta na kununua ndege jambo ambalo ni aibu kwake na taifa.  Vyema, kuwa Magufuli amepewa desa; je amepewa na wataalamu wa kuendesha ndege husika? Je wataalamu wetu wanaolipwa kumshauri Magufuli wanalipwa kwa kazi gani kama rais analazimika kukopa washauri na wataalamu toka nje?           Je hilo shirika litaendeswa na hao wataalamu wa Kagame?
             Kisa cha Magufuli kupewa “desa” kinanikumbusha kisa cha jamaa mmoja aliyeomba ng’ombe kwa rafiki yake ili naye akafuge na kupata maziwa, mbolea na nyama. Hata hivyo, jamaa huyu alikuwa na kasoro nyingi; hakuwa na uwezo wala ujuzi wa kumtunza ng’ombe aliyezawadiwa. Hivyo, alipoletewa ng’ombe alisema, “Asante sana rafiki yangu. Hata hivyo, naomba mtu wa kumswaga huyu mnyama.” Mwenyeji wake alimjibu, “Umepata. Je una jingine?” mgeni alijibu, “Je nitapata wapi mtu wa kumkamua, kumlisha na kumtunza?” mwenyeji alisita kidogo na kusema, “Ngoja kidogo” alimwambia yule mtumishi aliyekuwa ameleta ng’ombe, “mrudishe huyo ng’ombe kwa wenzake hadi jamaa atapopata ujuzi na uwezo wa kumtunza atajua jinsi ya kuja kumchukua na kummilki.” Jamaa alibaki kujishangaa na kushangaa namna alivyojiaibisha.  Kwa ufupi ni kwamba; sitashangaa ndege husika zikaishia kuuzwa kwa hao hao manoadesa kwao. Hili liko wazi na wenzetu wanalijua. Kwani wengi wamezaliwa na kukulia na kusomea Tanzania. Mbali na hili, hata ukiangalia tulivyoinga kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki kijinga, kuna uwezekano Tanzania ikaishia kuwa kimbilio la watu wasio na ardhi au kuja kuchuma na kurejea kwao. Mimi huwa siamini katika mashirikisho na jumuia za kimajimbo bali muungano wa haraka na moja kwa moja wa Afrika. Je muungano wa Afrika unawezekana wakati kila rais anang’ang’ania ulaji wake? Hili humu si mwake leo.
Japo Magufuli anasherehekea na kujisifia kupewa desa, anapaswa kufikiri na kuangalia mbali zaidi hasa usawa huu ambapo kila nchi inatafuta kila fursa kuwanufaisha watu wake baada ya nchi za kiafrika–kwa ujinga, uroho, upogo na kongwa za kikoloni zilikataa kuungana na kuwa nchi moja kama Marekani au China.  Watanzania kukiri kuwa hamna ujuzi na kuwaamini hawa watoa madesa, mmewapa kishawishi cha kuanga kujiandalia kurejesha ng’ombe zizini hadi mtakapopata uwezo na kuwa tayari kummlilki na kumtunza ng’ombe husika. kama shida ni wataalamu, kwanini Magufuli hakuwatuma wataalamu wake kwenda Rwanda kujifunza badala ya kuwaamini kazi wanyarwanda ambao hawako chini ya kiapo chochote wala uwajibikaji kisheria wa kuitumikia Tanzania? Kwanini hatutaki kujifunza tokana na wale tuliwatengeneza tukidhani ni watanzania wakaishia kutuacha Solemba?  Kwanini watanzania tunakuwa wepesi kufanya mambo muhimu kuwa ya mzaa kama kuamini uchumi wetu kuwa mikononi mwa wageni kama inavyozidi kubainika ambapo matapeli wa kigeni huja nchini wakijifanya wawekezaji wakiwa mikono mitupu na kuondoka na utajiri wa kutisha wakati watu wetu wakiwa maskini?
Kama tutakuwa wakweli, nchi iliyopata uhuru zaidi ya nusu karne ahitaji msaada hata wa namna ya kununua ndege. Hii maana yake–kama inashindwa kuwa na wataalamu wa kununa ndege–maana yake haina hata wataalam wala mipango madhubuti ya kuendesha shirika la ndege linalokusudiwa kuanzisha? Je tatizo ni wataalamu au uzalendo na mfumo bora? Mbona baadhi ya wataalamu wa Rwanda wamesoma tena bure hapa Tanzania wakijionyesha kama watanzania wakati ni wanyarwanda? Ajabu hatukuwachukulia hatua ikizingatiwa kuwa nchi yetu hairuhusu uraia wa nchi mbili. Je hawa waliotukimbia wataweza kutusaidia kweli? Mjinga ni yule anayeng’atwa na nyoka mara mbili kwenye shimo moja.
Tumalizie kwa kumshauri rais Magufuli kufikiria upya kuhusiana na mpango wake wa kuazima wataalamu toka Rwanda au kwingineko. Kununua ndege hakuna haraka. Anapaswa kutuma wataalamu kujifunza si Rwanda tu bali Kanada zinakotengenezwa ndege husika. Kama tunashindwa na jambo dogo ambalo makampuni ya watu binafsi kama lile la bilionea Richard Bronson yamefanya, nini maana ya kuwa huru akiri bila kufuata sheria au kukwepa sheria–kabla ya kuchaguliwa kwa rais John Pombe Magufuli–lilikuwa limefungiwa kwenye kuta za madarasa na vyumba vya mihadhara ya Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam (UDSM). Hata hivyo, baada ya kuchaguliwa Magufuli ambaye ni mhitimu wa shahada tatu zote toka UDSM, neno desa limeingia kwenye msamiati tawala (mainstream).
Hivi karibuni vyombo vya habari vilimkariri Magufuli si zaidi ya mara moja akitumia neno desa kuanzia alipohutubia jumuia ya wana UDSM hadi alipomkaribisha rais wa Rwanda Paul Kagame aliyesema amempa desa au mbinu ya kununua ndege mbili kwa mpigo. Magufuli alisema, “Mwezi wa tisa tutakuwa tumepata ndege mbili mpya, nimepewa namna nzuri ya kupata ndege hizo na Rais Kagame baada ya kuwatuma maofisa wake ambao ni wataalam wa ndege waje na kunipa desa.”
Si vibaya kwa viongozi kupeana mbinu za kufanya mambo ingawa hili linatia shaka kwa namna moja au nyingine. Pia linaacha maswali mengi kuliko majibu. Je Tanzania–pamoja na kupata uhuru zaidi ya miaka hamsini iliyopita–haina wataalamu wake wenye ujuzi na wa kuaminika kufanya kazi hiyo hadi tukope wataalamu toka Rwanda? Kwa mujibu wa matamshi ya Magufuli ni kwamba Tanzania haina wataalamu wa kutafuta na kununua ndege jambo ambalo ni aibu kwake na taifa.  Vyema, kuwa Magufuli amepewa desa; je amepewa na wataalamu wa kuendesha ndege husika? Je wataalamu wetu wanaolipwa kumshauri Magufuli wanalipwa kwa kazi gani kama rais analazimika kukopa washauri na wataalamu toka nje?           Je hilo shirika litaendeswa na hao wataalamu wa Kagame?
             Kisa cha Magufuli kupewa “desa” kinanikumbusha kisa cha jamaa mmoja aliyeomba ng’ombe kwa rafiki yake ili naye akafuge na kupata maziwa, mbolea na nyama. Hata hivyo, jamaa huyu alikuwa na kasoro nyingi; hakuwa na uwezo wala ujuzi wa kumtunza ng’ombe aliyezawadiwa. Hivyo, alipoletewa ng’ombe alisema, “Asante sana rafiki yangu. Hata hivyo, naomba mtu wa kumswaga huyu mnyama.” Mwenyeji wake alimjibu, “Umepata. Je una jingine?” mgeni alijibu, “Je nitapata wapi mtu wa kumkamua, kumlisha na kumtunza?” mwenyeji alisita kidogo na kusema, “Ngoja kidogo” alimwambia yule mtumishi aliyekuwa ameleta ng’ombe, “mrudishe huyo ng’ombe kwa wenzake hadi jamaa atapopata ujuzi na uwezo wa kumtunza atajua jinsi ya kuja kumchukua na kummilki.” Jamaa alibaki kujishangaa na kushangaa namna alivyojiaibisha.  Kwa ufupi ni kwamba; sitashangaa ndege husika zikaishia kuuzwa kwa hao hao manoadesa kwao. Hili liko wazi na wenzetu wanalijua. Kwani wengi wamezaliwa na kukulia na kusomea Tanzania. Mbali na hili, hata ukiangalia tulivyoinga kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki kijinga, kuna uwezekano Tanzania ikaishia kuwa kimbilio la watu wasio na ardhi au kuja kuchuma na kurejea kwao. Mimi huwa siamini katika mashirikisho na jumuia za kimajimbo bali muungano wa haraka na moja kwa moja wa Afrika. Je muungano wa Afrika unawezekana wakati kila rais anang’ang’ania ulaji wake? Hili humu si mwake leo.
Japo Magufuli anasherehekea na kujisifia kupewa desa, anapaswa kufikiri na kuangalia mbali zaidi hasa usawa huu ambapo kila nchi inatafuta kila fursa kuwanufaisha watu wake baada ya nchi za kiafrika–kwa ujinga, uroho, upogo na kongwa za kikoloni zilikataa kuungana na kuwa nchi moja kama Marekani au China.  Watanzania kukiri kuwa hamna ujuzi na kuwaamini hawa watoa madesa, mmewapa kishawishi cha kuanga kujiandalia kurejesha ng’ombe zizini hadi mtakapopata uwezo na kuwa tayari kummlilki na kumtunza ng’ombe husika. kama shida ni wataalamu, kwanini Magufuli hakuwatuma wataalamu wake kwenda Rwanda kujifunza badala ya kuwaamini kazi wanyarwanda ambao hawako chini ya kiapo chochote wala uwajibikaji kisheria wa kuitumikia Tanzania? Kwanini hatutaki kujifunza tokana na wale tuliwatengeneza tukidhani ni watanzania wakaishia kutuacha Solemba?  Kwanini watanzania tunakuwa wepesi kufanya mambo muhimu kuwa ya mzaa kama kuamini uchumi wetu kuwa mikononi mwa wageni kama inavyozidi kubainika ambapo matapeli wa kigeni huja nchini wakijifanya wawekezaji wakiwa mikono mitupu na kuondoka na utajiri wa kutisha wakati watu wetu wakiwa maskini?
Kama tutakuwa wakweli, nchi iliyopata uhuru zaidi ya nusu karne ahitaji msaada hata wa namna ya kununua ndege. Hii maana yake–kama inashindwa kuwa na wataalamu wa kununa ndege–maana yake haina hata wataalam wala mipango madhubuti ya kuendesha shirika la ndege linalokusudiwa kuanzisha? Je tatizo ni wataalamu au uzalendo na mfumo bora? Mbona baadhi ya wataalamu wa Rwanda wamesoma tena bure hapa Tanzania wakijionyesha kama watanzania wakati ni wanyarwanda? Ajabu hatukuwachukulia hatua ikizingatiwa kuwa nchi yetu hairuhusu uraia wa nchi mbili. Je hawa waliotukimbia wataweza kutusaidia kweli? Mjinga ni yule anayeng’atwa na nyoka mara mbili kwenye shimo moja.
Tumalizie kwa kumshauri rais Magufuli kufikiria upya kuhusiana na mpango wake wa kuazima wataalamu toka Rwanda au kwingineko. Kununua ndege hakuna haraka. Anapaswa kutuma wataalamu kujifunza si Rwanda tu bali Kanada zinakotengenezwa ndege husika. Kama tunashindwa na jambo dogo ambalo makampuni ya watu binafsi kama lile la bilionea Richard Bronson yamefanya, nini maana ya kuwa huru na kupoteza fedha kusomesha wataalamu ambao hawawezi hata kununua ndege?

Wiki hii niliwarusha makamanda wangu

$
0
0
Picha ya familia ya pamoja wakati makamanda na baba yao wakijiandaa kupasua anga 
Baba anaposhika usukani huku makamanda wakiwa nyuma yake wakijifunza namna ya kuendesha ndege
Picha na Makamanda baaada ya kushuka chomboni



Tulitumia ndege aina ya 1966 Piper Cherokee. Ni ndege nzuri japo ya kizamani. Hali ya hewa ilikuwa nzuri sana kiasi cha kutokumbwa na misukosuko kama ilivyo kawaida ya ndege ndogo.  Kama baba yao, makamanda wanapenda sana ndege kiasi cha kuwa usumbufu. Hivyo, kila nikipata fursa, nitakuwa nikiwapa ride  japo nao waanze kufuata nyayo mapema.


Hotuba ya Mlevi kwa waziri mkubwa wa Hindi

$
0
0

Image result for narendra modi and magufuli
            




Baada ya kushuhudia ugeni wa mashaka toka Ugabacholini ulioongozwa na Nyabenda Moody waziri mkubwa ukija Bongo na kuondoka bila kujihangaisha kukutana na uongozi wa walevi, nimeshauriwa kutuma hotuba hii kwenye ubalozi wao ili kuwawasilishia yale ambayo rahis hakuyagusia kwenye kuwakaribisha hawa wageni wake tokana na sababu anazojua mwenyewe. Kwa wasiomjua huyu Moody, ni mnyasa wa Mbamba Bay aliyepotelea ugabacholini pamoja na jamaa waitwao Jarawa wanaobaguliwa kama wanyama kule.
Kuna mambo mengi tulitegemea rahis ayataje tena bila kumung’unya badala ya kumwaga ujiko kwa jamaa hawa wanaosifika kwa kubagua waswahili wakiwaita absii, bander, kalu au manyani na majina mengine mabaya tu wakati sisi tukiwaendekeza hapa kaya kiasi cha kuendelea kutubagua bila hata aibu na adabu.
Japo rahis aliipa ujiko sana Ugabacholini kwa kuwekeza kayani, tunachojua ni kwamba imekuwa ikichukua na si kuwekeza hasa ikizingatiwa kuwa kwa sasa ugabacholini inaongoza kwa kuuza tanzanite na si hindinite jambo ambalo rahis alikiri. Hii maana yake ni kwamba wanatuibia madini yetu jambo ambalo ni jinai ambayo rahis alipaswa ailalamikie badala ya kuisifu. Sijui yeye ananufaika vipi na jinai hii?
Ugabacholini imefanikiwa kutujazia wachovu wake wasio na ajira kuja kuajiriwa hapa kibaguzi kwa kujali rangi na asili badala ya maslahi ya pande zote mbili. Anayebisha aende kwenye viwanda vingi vya magabacholi na mahoteli aone waganga njaa waliojazana kule kutoka ugabacholini wakifanya kazi ambayo wachovu wanaweza kufanya. Aende kwenye makazi yao aone wanavyoishi kwa kujitenga.
 Wachovu tunaojazia hawaishii kuchukua kazi tu bali wajihusisha na kuvusha mali zetu kama tanzanite japo rahis alisema eti kuna maslahi ya pamoja wakati ni ya upande mmoja.
Hakuna sehemu rahis aliwaacha hoi walevi kama kuridhia ubaguzi katika kutoa uraia wa kaya mbili au zaidi kwa mlango wa nyuma. Rahis alisikika akisema kuwa baadhi ya magabacholi waliokwenda pale kumpokea mgeni wake ni wabongo waliompigia kura Moody huko ugabacholini. Hii maana yake ni kwamba wana uraia wa kaya mbili jambo ambalo ni jinai kwa sheria za kaya. Watakuwaje na uraia wa ugabacholini wakati wao ni Wadaganyika wanaopaswa kuwa na uraia wa kaya moja au uraia wa kaya nyingi unawafaa wageni kuliko wazawa?
Rahis alisema kuwa Hindi inasaidia kaya za Kiswahili wakati inazijazia bidhaa feki na wasasi ngawira na kazi bila kusahau kuzijazia bidhaa feki na vya chini ya kiwango (substandard goods).
 Rahis alishindwa kugusia namna magabacholi walivyogeuza wanyama ndugu zetu waitwao Jarawa kwenye visiwa vya Andaman tokana na Hindi kujengwa kwenye apartheid iitwayo caste system ambayo inafanyika hata kwenye kaya zetu ikitendwa na wale walioletwa na wakoloni kutuibia na kutunyonya ukiachia mbali kuendelea kutumiwa na wezi wazawa wenye mamlaka.
Inashangaza kusikia kuwa tuna magabacholi kumi mjengoni wakati mamia ya waswahili waishio kwenye visiwa tajwa waligeuzwa vivutio vya utalii bila huduma yoyote ya afya kiasi cha tofauti yao na wanyama kuwa sura zao tu. Kwa wanaotaka kujua zaidi ubaguzi huu http://www.aljazeera.com/indepth/features/2014/01/time-ticking-india-jarawa-tribes-20141314281424904.html.  Inasikitisha sana kuona wale walioletwa na wakoloni wakila kuzaliana, kunenepeana wakatajirika na kuita wengine wakati ndugu zetu wakiteseka kwa sababu ya rangi ya ngozi yao.
Hapa tunaongelea ubaguzi ambao rahis aliogopa kuugusia. Hatujagusia jinsi magabacholi wanavyoingiza wenzao kayani kufanya kazi ambazo wachovu wanaweza kuzifanya. Ajira zao nyingi ni za kibaguzi. Rejea kukamatwa kwa magabacholi wengi waliokuwa wakiishi kwenye kaya bila vibali. Hapa hatujagusia ubaguzi wa wazi wazi hata kwenye makazi ambapo magabacholi wengi wenye mahekalu, hata viwanda kuendelea kuishi kwenye kaya za bei mchekea za Asajile Mwaijumba katikati ya jiji huku wazawa wakitimkia Pugu Kajiungeni na Kimanzichana. Ukiingia downtown Bongo usiku unaweza kudhani uko Bombay. Sijui huyu Bwana Mdogo Po Makondakonda anashindwa nini kupitisha amri kuwa kila wenye uwezo wa kujenga mahekalu shurti waishi kwenye mahekalu yao badala ya kuwabana walevi kwenye nyumba za Asijile za bei poa.
Mlevi amewahi kuishi ugabacholini kwa miezi michache akifanya utafiti juu ya ubaguzi ambao umekuwa ukitokea ugabacholini ukiachia ule wa kwenye kaya ambao tawala zote zilijifanya kutouona. Hebu nionyesha lau binti mmoja wa kigabacholi aliyeolewa na mswahili nitajinyotoa roho kwa aibu ya kusema uzushi.
Kipindi fulani waziri mmoja aitwaye Idd Lion aliwahi kudai kuwa magabacholi kumi tu walikukwa wakimilki uchumi wote wa kaya ya Danganyika. Hata sasa, ukimuondoa mzee Bhakresa, matajiri wakubwa ni magabacholi; kwanini wakati hakuna waswahili matajiri ugabacholini ambako hata kwenda kusoma ni ubaguzi wa kuua mtu hadi waswahili kuitwa absii, bander na kalu yaani manyani.
Walevi wameshangazwa sana kitendo cha rahis kushindwa kumtaka waziri mkubwa wa ugabacholi kuomba msamaha kwa binti wa kitanzania (jina kapuni) akiwa na mwenzake  aliyedhalilishwa na kupigwa hadharani baada ya msudani ambao hupenda kujiita wamanga wakati wamanga wanawaona kama watumwa kumgonga maza mmoja wa kigabacholi.
Tumalizie kwa kusema kuwa walevi hatukuridhishwa na namna masuala yenye siha yalivyotalekezwa zikamwagwa sifa kwa jamaa ambalo halikufaa kumwaiwa ujiko wote huku wakati linaongoza kaya inayosifika kwa ubaguzi na unyonyaji wa waswahili. Lazima usuhuba huu mpya baina ya Bongo na ugabacholini upigwe darubini tusiendelee kulizwa.
Chanzo: Nipashe Jumamosi.

Tulia Ackson anapaswa kutulia

$
0
0
           Pamoja na kwamba uhuni Bungeni haukuanza jana–hasa kiti cha Spika kinapotumika vibaya kwa sababu binafsi au za kisiasa–Bunge la 11 linaweza kuvunja rekodi katika baadhi ya mambo tena yasiyopendeza wala kukuza demokrasia nchini. Zamani uspika ilikuwa ni taasisi yenye kuheshimika sana nchini; hasa ikizingatiwa kuwa ni moja na mihimili mitatu ya dola. Bunge linapaswa kuwa huru bila kuingiliwa au kuingilia mihimili mingine ya dola. Hata hivyo, baada kuingia ushindani wa vyama vingi, Uspika ulianza kugeuzwa sehemu ya utawala jambo ambalo ni kuupunguzia heshima na kuuingilia mhimili huu kati ya tatu ziundazo dola yaani Bunge, Mahakama na Utawala.  Hili si jambo jema kwa taifa hasa Bunge linapofikia mahali ukawa ni uwanja wa kulipiziana visasi kisiasa na kiutendaji.
            Dhana nzima ya kuwepo Bunge ni kutaka kutoa fursa ya mihimili ya tatu kutekeleza wajibu wake ambao kwa Bunge ni kupokea miswaada ya sharia, kuipitisha, kutunga, kurekebisha na kufuta sheria kunakofanywa na wabunge wanaowawakilisha wananchi moja kwa moja.  Baada ya hivi karibuni baadhi ya Wabunge wa kuteuliwa–tena na wakuu wa dola–ambao Spika wa zamani Samuel Sitta aliwahi kuwaelezea kama mizigo kuweza hata kuruhusiwa kugombea uspika au unaibu Spika japo hawamwakilishi yeyote zaidi ya matumbo yao na aliyewateua, ithibati ya Bunge imeanza kushuka au kupotea kabisa. Hali ya Bunge inakuwa mbaya pale inaposimamiwa na mtu au watu wasiotokana na kura za wananchi na badala yake wakateuliwa kirahisi tu. Kwani–mbali na kutowakilisha umma–wahusika hawajui machungu na mikiki mikiki ya kuupata Ubunge. Hivyo, wanaweza kutumia nyadhifa zao watakavyo ima kujiridhisha au kuwaridhisha waliowateua kama ilivyo sasa ambapo ukada na unazi vinaanza kuzoeleka Bungeni tangu kuchaguliwa kwa naibu Spika, Dk Tulia Ackson.
            Hata hivyo, Uspika si sehemu ya kuonyesha ukomavu, uongozi na uzalendo na si mabavu, ubabe wala upendeleo; bali kutenda haki hasa nafasi hii inaposhikiliwa na mtu anayejinakidi kuwa na shahada ya uzamivu katika masuala ya sheria. Inashangaza mtu mwenye kuitwa daktari wa sheria kushindwa kumaizi jambo rahisi kama hili. Je tatizo hapa ni busara, elimu za kuungaunga au uzoefu?
            Kwa wanaoujua thamani na umuhimu wa elimu, wengi walidhani daktari huyu wa sheria angejua umuhimu wa elimu; hivyo, kuonyesha umahiri wake katika kusimamia na kukuza demokrasia badala ya vurugu na kuiminya demokrasia. Hata hivyo–tokana na kadhia tulizoshuhudia ambapo naibu Spika wa Bunge Dk Ackson akionyesha wazi kulalia upande mmoja wa Utawala na kushindwa kujitofautisha na Spika aliyepita Anna Makinda aliyesifika kwa uburuzaji tokana na alivyopatina na kiwango chake cha elimu, wakati mwingine tunashindwa kuwatofautisha wawili hawa japo wana viwango tofauti vya elimu.
            Wengi waliofuatilia vikao vya Bunge na wingi wa Wabunge wa upinzani walioadhibia kwa kuzuia kuhudhuria vikao wanajiuliza: Je tatizo ni Wabunge au naibu Spika? Pamoja na udhaifu wake, mbona wakati wa kipindi cha Makinda, Wabunge hawakuadhibiwa kwa wingi na mfululizo kama ilivyotokea hivi karibuni? Ukiangalia utendaji wa Bunge kwa vipindi mbali mbali vya karibuni kuanzia uongozi wa mzee wa Viwango Samuel Sitta ambaye alikuwa pia mwamanasheria, watakubaliana nasi kuwa Wabunge wengi hasa wa upinzani wameadhibiwa kipindi Dk Tulia alipoendesha Bunge baada ya Spika kuwa nje kwa matibabu tena ndani ya muda mfupi.
            Makinda aliwasimamisha  Wabunge Tundu Lissu (Singida Magharibi), Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Peter Msigwa (Iringa Mjini), Highness Kiwia (Ilemela), Godbless Lema (Arusha Mjini) na Ezekiah Wenje (Nyamagana) mnamo  tarehe 18, April 2013.
            Ackosn amewasimamisha wabunge Zitto Kabwe (Kigoma Mjini), John Heche (Tarime Vijijini), Halima Mdee (Kawe, Tundu Lissu (Singida Magharibi, Godbless Lema (Arusha Mjini), Pauline Gekul (Babati Mjini) na Esther Bulaya (Bunda Mjini). Mei 2016.
 Suzan Lymo (Viti Maalum) na Anatrophia Theonest (Viti Maalum) Juni 2016
Joseph Mbilinyi (Mbeya Mjini), Saed Kubenea (Ubungo) na James Milya (Simajiro) Julai 2016.
            Ukiangalia mfuatano, ni kwamba, karibuni kila mwezi Ackson alikuwa akifukuza wabungu kwa wastani wa wabunge wanne au mbunge moja kila wiki. Je hapa tatizo ni Wabunge au naibu Spika mwenyewe? Mbona huko nyuma hakuwahi kutokea? Kimsingi, Ackson ataingia kwenye historia ya vitabu vya bunge kama mtu aliyekalia kiti cha Spika na kuvunja rekodi–si ya kufanikisha bunge–bali kuwatimua Wabunge wa upinzani. Je huu si ukada wa wazi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho wakubwa zake nao wana rekodi ya kumteua kwa vyeo tofauti ndani ya muda mfupi? Kama Ackson ana mapenzi na ukereketwa wa chama chake hivi, si aende akafanye kazi za ndani ya chama badala ya kuaminiwa wadhifa wa kitaifa ambao ameonyesha kuutia aibu ukiachia mbali kutumia vibaya kiti cha spika?
Tumalizie kwa kumtaka Dk Tulia kutulia na kuonyesha ubobezi wake  katika sheria na si kufanya vinginevyo jambo ambalo linalishushia heshima Bunge naye binafsi kama msomi na kiongozi wa umma. Unapofukuza wabunge–licha ya kuwanyima wananachi uwakilishi–ni kuwafukuza wananchi kwenye chombo chao.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Twarana na nii (Nenda nami) -Jane Muthoni

$
0
0


Huwa napenda nyimbo za Kikuyu kwa vile nakifahamu japo si sana. Wimbo huu wa Jane Muthoni (Mkwe) huburudisha na kufundisha. Hapa nakudonolea kidogo tu.

Umeniita nikufuate
Kuna shida safarini
Nakuomba usiniache

Nenda nami
Twende nyumbani x2

Moyo wangu unataka kukutumia
Ninashindwa na shida za dunia hii
Hauna kifani upendo wako
Nenda nami mungu wangu
Twende nyumbani

Mambo mengi niyaonayo safarini

Marafiki zangu si sawa nawe

Our Lives in History, Today 18 Years Ago

$
0
0




Today 18 years ago I quit bachelor club. It is the time my sweetheart Nesaa came into my life. Since then, we've been happily married. So, too, we're blessed with six children, four girls and two boys. We've cherished and enjoyed  more  our marriage more than anything we've ever had in our lives. Though years have lapsed, it still feels like yesterday. We're still wholeheartedly and sincerely committed to each other. Since the day we made our vows our love has never dwindled.  Our union has always been spiffy despite being mortals.
Today is a day
Our loves got a seal
It from this day
We're declared wife and husband
and, indeed,
It is from this very day
Two became one
We've since soldiered on
Joyful has always been our union

We stood whatever challenge
Love became our refuge
Just like any  human being
Cooperation has always been our forte
Ever since we've never staggered
We've stood together
We indeed are stronger

Our house became a home
for whoever that comes 
We make her or him feel at home
We are always calm
Whenever we face a storm
Love has been our weapon
Indeed, love has made us soldier on

We always thank God
To bring us together
 Going from strength to strength
Our marriage is always healthy
Patience and love are our hush-hush
Today is our anniversary





Kijiwe chastukia uraia pacha wa Kanji

$
0
0
Image result for photos of narendra modi and magufuli
           Baada ya rais Joni Kanywaji Makufuli kufichua siri kuwa Bongo ina wapiga kura wa India, kijiwe kimembana Kanji aeleze kama naye yumo na yuko wapi kati ya Bongo na India.
Mheshimiwa Bwege ndiye anaanzisha mada. Baada ya kumuamkua Kanji na kumpa ofa ya kahawa anasema, “Kanji dugu yangu, iko sikia kuwa veve iko piga kura ya kula kule Indiani. Je hii iko kweli au ongo na veve iko sema nini dugu yangu?”
Msomi Mkatatamaa anadakia, “Hata mimi hili la mkuu kutoboa ukweli huu–ambao hata hivyo, si mpya–lilinistua na kunishangaza; hasa kugundua alivyoridhika nalo badala ya kutamka wazi kuwa ni kinyume cha sheria. Nadhani mkuu anapaswa kuambiwa kuwa anachofanya si kusifia ujinga na ubaguzi kama huu bali kupambana nao kwa vile nalo ni jipu tena la muda mrefu. Inakuwaje waswahili wazuiwe uraia wa nchi mbili nyinyi akina Kanji mruhusiwe? Hivi Mkuu hajui kuwa hiki ndicho chanzo cha kutorosha njuluku na mali za kaya? Nadhani Kanji anaweza kutupa jibu sahihi wakati tukingoja la mkuu mwenyewe.”
Kanji anajitetea, “Veve onea mimi bure dugu yangu. Veve wahi ona gabacholi nakuja kunywa gahawa hapa na veve? Mimi haiko gabacholi; iko hindi sikini nishi na Swahili sikini. Ile gabacholi tajir nabagua hata mimi hata kama haibagui kama nafanya veve Swahili. Kwanini veve lau hindi. Kwani hindi diyo naunda serikalini yenu?”
Mgosi Machungi anakamua mic, “Hata sisi imetishangaza kusikia kuwa kumbe kuna Wadanganyika wanaopiga kua huko ugabachoini. Sijui kwanini wanatinyima sisi hii haki na kuwapa wageni wasio na uchungu na kaya yetu? Hapa azima mkuu atieeze hadi ti-understand na ku-compuihend.” Anamegeukia Kanji na kusema, “Hata veve Kanji iko gabachoi. Huoni unavyosema seikai yenu na siyo seikai yetu? Hii maana yake ni kwamba veve haiko raia ya kaya hii. Hii nayo baguzi kuba ndugu yangu Kanji.”
Mipawa anampoka Mgosi mic, “Mwenzenu sikushangaa; hasa nikizingatia namna jamaa hawa ambavyo wamekuwa wakishirikiana na mafisadi wazawa kusikinisha kaya. Mara hii mmesahau namna majambazi kama Chavda, Saileth Vithlani na magacholi wengine walivyoibia kaya wakaishia kuondoka kayani kwenda kutanua ulaya?”
Kabla ya kuendelea, Mchunguliaji anamchomekea Mipawa na kusema, “Mbona Chavda alisharudi na anapiga mbonji mitaa ya Upanga au hujui. Hii Bongolalaland aka Danganyika bana. Waliwadanganya kuwa Chavda alikimbia kaya wakati yuko Upanga akihomola na kula kuku kama hana akili nzuri. Jiulize, yale mashamba ya mkonge waliyosema alitumia kuibia mbona hayajawahi twaliwa kama kweli aliondoka kayani?”
Mipawa anaendelea, “Hilo nililisikia na lisirikali halikuwa tayari kukanusha au kutoa maelezo. Hata hivyo, silaumu; kwani, wakati wa utawala wa Njaa Kaya, nani angepoteza muda kutoa maelezo? Nadhani lao moja na wao ni dugu moja kwenye kuibia kaya shamba la bibi au siyo?”
Leo ni kuchomekeana mtindo mmoja mmoja. Mpemba anakwanyua mic, “Yakhe hata mie sikushangaa. Nyie mwaongelea akina Chavda, Kagoda na wale wenginewe wa zamani. Mbona yupo huyu Kamran Ahmed aliyetoroshwa wanyama hai zaidi ya mia jana tu naye alitolewa rumande na kupewa pasipoti na pipa akaondoka zake na kaya ikaishia kula hasara? Hawa ndiyo magabacholi alioonya marehemu Chris Mtikisa. Na sasa ameondolewa, sijui nani atawatia kashkash wabaguzi hawa wa kunuka?”
Mijjinga naye anaamua kukamua mic, “Mkuu hakukosea. Huenda ulimi uliteleza au alitaka kuanzisha mjadala kama huu ili asionekane kalianzisha yeye.  Mimi sikushangaa hili la uraia wa kaya nyingi. Nadhani mnapaswa kuelewa kuwa kaya hii ina sheria moja inayotumika tofauti kwa kuangalia rangi na ukwasi wa mhusika. Ukiwa kigogo kama Jimmy Rugemalayer, Singasinga, Andi Chenga au Ni Zero Kadamage unaengwa wakati wezi wa kuku wakisulubiwa kwa uvivu wao wa kufikiri wakaiba kuku badala ya maburungutu.”
Sofia Lion aka Kanungaembe anakula mic, “Usemayo kaka Mijjinga ni kweli tupu. Huoni wanavyofaidi nyumba za Msajili wa Majumba wakiitana kila uchao wakati waswahili wakiendelea kunyanyaswa kwenye mbavu za mbwa za kupanga au kuangamia mabondeni wakati nyumba zinazoitwa zao zikikaliwa na wapiga kura wa India? Nani anashupalia hili jambo ambalo ni ubaguzi wa wazi?”
Kapende anakula mic, “Nadhani tunapaswa kupigania uhuru upya ili tujenge kaya isiyo ya kibaguzi na kigabacholi.sijui kama waswahili wangekuwa ndiyo wanaishi ugabacholini kama wangepewa upendeleo kama huu. Kama kaya, tunapaswa kuwatoza kodi kubwa–kwa vile ni matajiri–ili kuweza kujenga nyumba nyingine kwa ajili ya walalahoi wetu walionyonywa tangu ukoloni hadi sasa. Hapa hakuna cha nini wala nini bali kutendeana haki na kuuangalia ukweli kama ulivyo hata kama ukweli wenyewe ni mchungu. Mnasemaje wazee?”
Kijiwe kikiwa kinango si akapita manzi wa kigabacholi! Wacha Mbwamwitu ajisemee, “Kusingekuwa na ubaguzi huu wa ki-caste, huenda huyu manzi angekuwa bi mkubwa wangu.”
Kanji anajibu, “Dini yetu haikoruhusu Swahili oa hindi.”
Wanakijiwa tunageuka na kuangaliana kugundua kuwa jasiri haachi asili. Kwa pamoja, tulipanga kwenda kukuu kuamuru lisirikali lianze kushughulikia ubaguzi huu wa kizamani na kijima.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano.
Viewing all 3173 articles
Browse latest View live