Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3177

Kijiwe chalaani ndoa ya dini na sias

$
0
0

          Hivi karibuni wanakijiwe walichukia nusu ya kuanza kuandamana hata kabla mkuu sijatoa ruhusa. Baada ya kushuhudia ndoa iliyofungwa baina ya viongozi wa kiroho na mafisadi ya kisiasa yanayokwenda kumwaga pesa eti kuyachangia, kimekaa kujadili aina hii ya ufisadi.
Mgosi Machungi ndiye mwanzilishi wa mada leo. Anakwayua mic na kusema, “Hivi mimeona jinsi mafisadi wanavyoingiia hata dini kiasi cha kutichanganya? Tinaambiwa dini na siasa havichanganyikani wakati wao wanavichanganya.”
“Hebu rudia. Eti wanaiingilia dini? Unamaanisha nini na wanaingiliaje dini na kupitia wapi?” Mbwamwitu anauliza huku akitabasamu.
Mgosi anamrushia gazeti na Mlevi lenye kichwa kisemacho, “Fisadi Afunika AR.”
“Kumbe unaongelea haya mauzauza ya chama twawala ya makamu wa Rahis kumtuma fisadi Eddie Luwasha amwakilishe kwenye kudhalilisha mahekalu ya God na kutoa hongo kwa viongozi waroho wa kiroho! Sasa nimekuelewa endelea.” anachomekea Kapende.
Kabla ya Mgosi kuendelea, Mpemba anakwanyua mic na kulalama ile mbaya, “Hivi kweli nyumba ya Subhanna yawezachangiwa na wenye dhambi hasa wezi, wauza unga na malaya wa kisiasa kama chama twawala? Wallahi kama waja wangefufuka, bila shaka Sayyidina Umar ibn Al-Khattab angechinja ntu hapa tena hadharani.”
 Mipawa anakubaliana na Mpemba, “Nyumba ya namna hii bila shaka itakuwa chafu na yenye wingi wa madhambi kiasi cha kutoweza kutoa msamaha wa dhambi.” Anapiga funda mbili tatu na kuendelea, “Hata dua zinazoombwa mle huwa hazifiki kwa mujibu wa sisi maulamaa. Ukisikia ukafiri ndiyo huu.”
Mzee Maneno anauliza swali, “Je hawa wanaochangia kuelekea uchaguzi walikuwa wapi?”
Msomi Mkatatamaa anaingia kwa usongo na kusiliba kwa sana tu, “Je hiyo fedha ni halali au ni ya unga, ujambazi na ufisadi? Ni jambo la hatari kwa wachovu kutegemea misaada badala ya kujengewa mazingira ya kujitegemea. Wawezesha wajenge makanisa na misikiti kwa fedha yao halali badala ya fedha chafu na ya fedheha. Kaya haiwezi kuendeshwa kichokoraa na ikawa kaya. Rahis anaombaomba, mashehena wanaombaomba, wachunaji nao kadhalika.”
“Msomi tafadhali usinilize mkanicheka. Huoni kila kitu kayani kinategemea michango na misaada ya kipumbavu tena ya wale wanaotuibia tukiona? Hata hao wanaojifanya kumwaga mabilioni wameyapata kwa kununuliwa na jamaa hawa hawa ambao ni maarufu kwa kuchangia kila kitu kuanzia michezo na kila kitu wakati wakikwepa kulipa kodi na kufanya biashara nyingi haramu. Nadhani mnawajua,” Anazoza Mheshimiwa Bwege huku akimkata jicho Kanji.
Kanji naye anakula mic, “Mimi kwisajua yote tasema hindi. Siyo hindi yote natoa ruswa au kwepa kodi au pewa samaha ya kodi dugu yangu. Hindi nyingine sikini ya Mungu kama veve dugu yangu.”
“Hayo wayasema wewe. Mimi sijataja mtu vinginevyo ajitaje mwenyewe. Ukiona anayelalamika jua yule yule.” Anazoza Mheshimiwa Bwege.
Mijjinga ambaye amerejea hivi karibuni kutoka Kisesa anaamua kula mic kwa fosi, “Ukiona viongozi wa duni wanafunga ndoa na wanasiasa ujue hivi vitu vinachanganyikana. Ubaya ni pale wanasiasa watakapopata watakacho wakaanza kuwageuka wenzao wa dini kiasi cha kulete hali tete kayani.”
“Hawa wanatumiana tu hakuna mwenye mapenzi na mwenzake,” Mbwamwitu anarusha kimondo.
Sofia Lion aka Kanungaembe aliyekuwa kimya muda mrefu anaamua kunyaka mic, “Kanji huna haja ya kujitetea. Ni kuwadharau tu. Watasema  mchana usiku watalala huku mkiendelea kufaidi maisha bora kwa wote wenye kujibidisha. Halo halo!”
“Sofi acha kujichamba. Kama maisha ni kwa wote inakuwaje wewe hatuoni huo ubora zaidi ya kujigongagonga?” Mchunguliaji anaamua kumtolea uvivu Sofi.
Kapende anachomekea, “Mpe dozi yake hadi azimie.” Sofi anamkata jicho la hasira na kugeuka upande mwingine akisonya.
Mpemba anaamua kurejea kwa chati, “Mie wallahinaona huu licha ya kuwa wizi na ni ufisadi wa kisiasa unolenga kueneza ugaidi baadaye. Kwanini hawa wachanganya dini na siasa wakati watwamba sie tusifanye hivo?”
Mipawa anabuna mic, “Leo wamo kitanda kimoja wakiangusha vicheko. Baada ya kugeukana utayasikia wakitishia usalama wa kaya. Hawana maana hao wala ndoa ya kudumu nakwambia.”
Mgosi anaamua kukatua mic, “Waahi hawa mashehe na wachungaji wanaojiahisi kwa wanasiasa si mashehe wala wachungaji kitu bai mashehena na wachunaji. Wanachuna mabuzi ya kisiasa na kujaza matumbo yao ambayo ni shehena bila shaka.”
Mbwamwitu anampa tafu Mgosi,“Hii pwenti nimeikubali. Kweli, machangu wa kisiasa wanawahonga machangu wa kidini kwa uroho wao halafu wanajitia watu wa sir God. Mshindwe na mnyong’onyee mnaochangisha fedha chafu kujenga hekalu la baba yangu.”
Kapende anaronga tena, “Hivi kweli Kanisa au Msikiti unaweza kuchangiwa na mafisadi kama Ewassa kweli? Mbona mnatutia midole machoni na kututukana matusi ya nguoni?”
Msomi naye anarejea kwa chati, “Afunike asifunike lazima kwenye urahis afunikwe. Anapoteza muda wake hasa ikizingatiwa kuwa afya yake kimwili na kisiasa ni ugogoro mtupu. Nani anataka recycled rais kwenye ikulu akaibe na kujineemesha zaidi? Nani anataka rais mgonjwa ambaye atatumia muda na fedha nyingi kwenye matibabu? Hapa kuna haja ya kukpia afya za wanaotaka kugombea urahis.Hivi walioshindwa uwaziri mkubwa watauweza urahis kweli?”
Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita fisadi Luwasha mmoja. Wacha tumtoe mkuku!
Chanzo: Tanzania Daima Mei 27, 2015.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3177