Quantcast
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3175

Kwa hili nampongeza Kikwete

 Image may be NSFW.
Clik here to view.

Baada ya watanzania kuhuzunishwa na shambulizi la bomu huko Arusha kwenye kanisa la kikatoliki huku wakilalamikia tukio la rais Jakaya Kikwete kufanya ziara nchini Kuwait bila taarifa, angalau watafarijika baada ya rais kukatiza ziara hiyo. Hii itapunguza hasira ya watanzania waliokuwa kwenye mstuko mwingine wa kujua kuwa kumbe rais wao alikuwa amefanya ziara nchini Kuwait tena kinyemela bila kuwataarifu.
Kwa wenye kujua nafasi na umuhimu wa urais, tulitarajia kuwa rais Kikwete angekatiza safari yake na kuwahi Arusha ili kuwafariji wahanga pamoja na kulipa matumaini taifa. Inafurahisha kuwa amefanya hivyo na kutimiza matarajio yetu. Kwa uamuzi wa kukatiza ziara tena yenye utata, tunampongeza rais kwani huu ndiyo wakati watanzania wanamhitaji ili atoe mwelekeo wa kuenenda na tishio hili. Laiti Kikwete angeendeleza uzi huu wa kujifunza kutokana na makosa yake, watanzania wangeweza kumsamehe na kuanza kumuangalia kwa uoni mpya. Kwani yapo maeneo mengi ambayo rais amepwaya na kuendelea kufanya madudu kama vile kubadili mikataba ya uwekezaji wa kijambazi aliyorithi,  kuwatimua kazi mawaziri walioghushi na wale waliosababisha kufeli kwa vijana wetu kati ya mengi. Tunaamini rais atatia maanani hisia zetu na kuzifanyia kazi.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3175