Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173

Tunaadhimisha siku ya kuzaliwa Muungano au Mgongano?

$
0
0

Imetimu miaka 49 tangu mataifa ya Tanganyika na Zanzibar kuungana na kuzaa Tanzania. Hakika miaka 49 si haba. Je tunasherehekea Muungano au Mgongano? Je watanzania bado wana hamu na hamasa na Muungano? Je nani anafaidi Muungano ukiondoa watawala wa pande zote mbili? Maana ukisikia manung'uniko toka pande zote unashangaa mantiki ya kuendelea na kuwa na Muungano wenye kila aina ya migongano miongoni mwa wananchi wa pande mbili. Ilifikia mahali watu wa visiwani wakahisi kama watu wa bara wanawanyonya ingawa hawana cha kunyonya. Ilifikia mahali tukaanza kuitana majina ya machogo na upuuzi mwingine hata kusingiziana jinai.Kwa vile watanzania wanaanza kujitambua, kuna haja ya kuwasihi wauangalie upya Muungano ambao umegeuka kero. Blog hii ni shabiki wa umoja wa Afrika. Tofauti ni kwamba Umoja huu ujengwe na waafrika wenyewe badala ya watawala. Huwa nashangaa kuona Tanzania inavyopoteza muda na raslimali kujiingiza kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki wakati huo huo ikishindwa kutatua kero za Muungano wake. Je watanzania tutaendelea kufanyiwa majaribio hadi lini? Wakati tukitafakari hali ya Muungano wetu, majibu tutakayopata yatusaidie kupinga kuingia kichwa kichwa kwenye Jumuia hasara ya Afrika Mashariki ambayo inatumiwa na nchi wanachama kutaka kutuibia ardhi na raslimali zetu. Haiingii akilini kwa nchi yenye ardhi nzuri na kubwa na raslimali kuungana na vijiinchi visivyo na lolote bali mzigo wa ongozeko la watu na watu wasio na ardhi.
KILA LA HERI NA TAFAKARINI.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173