Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173

Angalia watawala wetu wanavyotula

$
0
0

Kuna taarifa kuwa viongozi wastaafu wanatengewa pesa nyingi kuliko baadhi ya wizara. Hii imefichuliwa na vyombo vya habari hivi karibuni. Wengi huwa tunajiuliza, kwanini watumishi wengine wa umma wanaostaafu wanaachwa wajifie huku viongozi na wake zao wakiendelea kutunyonya na kutanua huku sisi tukiteseka? Huu licha ya kuwa uroho na roho mbaya, ni ujambazi wa wazi unaofanywa na wanajiita wenye madaraka. Je ufisadi huu wa kimfumo ambao umegeuka ukoloni mamboleo ukitekelezwa na wakoloni weusi utakomeshwa na nani na lini kama siyo sisi na sasa? Je umma unaridhika na wizi huu wa mchana chini ya dhana ya viongozi wastaafu? Inashangaza na kusikitisha zaidi kukuta kwenye orodha ya viongozi wastaafu kuna watu kama Edward Lowassa ambaye aliachia madaraka bila kufikia muda unaopaswa kisheria ukiachia mbali kuondoka kwa kashfa iliyolisababisha taifa hasara ya mabilioni ya fedha. Inaumiza kukuta mijitu kama Benjamin Mkapa anayejulika wazi kujitwalia Machimbo ya Makaa ya Mawe ya Kiwira na mkewe aliyeliibia taifa kuendelea kuongezewa pesa itokanayo na kodi ya mlipa kodi maskini waliyemwibia. Je tumegeuka taifa la hovyo na kuridhika na hali hii? Tafakarini.
Kwa habari zaidi BOFYA hapa.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173