![]() |
Picha kwa hisani ya gazeti la Mtanzania |
Inashangaza kwa mtu mwenye elimu ya juu hivi kushindwa kuelewa hata mambo rahisi kiasi cha elimu yake kutia shaka. Tibaijuka acha uhuni. Kitoe tu umeishaishiwa na kuisha. Kutapatapa hakutakuponya na anguko litokanalo na uchoyo, ufisi, ufisadi, ubinafsi na upofu. Watanzania wamechoka na watawala wezi wenye kujificha nyuma ya visingizio mbali mbali. Iistoshe, ofisi ya umma si mali yako binafsi kiasi cha kuing'ang'ania.
Kama unaona umeonewa nenda mahakamani. Pia ufahamu kuwa unachofanya ni dharau kwa Bunge na kamati yake hasa pale uliposema kuwa kinachodaiwa kuwa makosa ni uvumi. Si uvumi ni ukweli tena ukweli mtupu uliofikiwa baada ya kufanyika uchunguzi. Si uende ukaajiriwe na hao mabwana zako kama walivyomwajiri nshomile mwenzako Patrick Rutabanzibwa? Nenda Tibaijuka nenda. Hufai tena nenda tu. Nenda na mapema utuachie ofisi yetu. Nenda ukafanye biashara na huyo Rugemalayer wako.