
Kwa hali ilivyo ni kwamba CCM watatufanyia unyani na kutuletea "Katiba Mpya" kwa maana tofauti. Badala ya kutegemea Katiba Mpya nadhani tutegemee kitabu kipya chenye kubeba mambo yale yale ya zamani. Kwa hotuba ya juzi ya mwenyekiti wa CCM rais Jakaya Kikwete ni kwamba hakuna kitu kinachoitwa Katiba Mpya. Kama ipo basi ni ya zamani kupitia njia mpya ya kuunda tume ambayo hata hivyo Kikwete aliizodoa na kuidhalilisha huku akijitia mtalaam aliyeishiwa kuumbuka hasa alipojaribu mambo kama takwimu. With this monkey business Tanzanians need to fast and weep.