Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173

Mkiti wa CCM kizimbani kwa kuuza dawa feki

$
0
0
Mkurugenzi wa mashtaka Jinai (DPP) ameamuru mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa mkoa wa Dar Es Salaam, Ramadhani Madabida (Pichani) wa kwanza kushoto kufunguliwa mashtaka matano mojawapo likiwa ni kusambaza madawa feki yenye thamani ya mamilioni ya kurefusha maisha kwa waathirika wa ukimwi.
Hatutajadili kesi iliyoko mahakamani. Hata hivyo ukiangalia mrorongo mzima wa kesi na visa vya Madabida kujihusisha na uuzaji na usambazaji madawa feki havikuanza jana.Hapa unaweza kuona uovu na roho mbaya vinavyotawala Tanzania. Zamani wakati wa awamu ya kwanza mtu mwenye kutia shaka kama huyu asingeweza kuchaguliwa kiongozi hata wa shina. Ukisikia mfumo wa kifisadi ndiyo huu. Mke wa mtuhumiwa huyu ni mbunge ambaye bila shaka anatumia ubunge wake kutafuta dili kwa ajili ya madawa feki. Na hii si mara ya kwanza kwa Madabida kukumbwa na kashfa ya kuuza madawa feki. Mara ya kwanza alituhumiwa na mambo yakaisha kimya kimya. Huyu ibn muthnaq Madabida simtofautishi na habithi Ditopile Mzuzuri. Bila shaka naye atakufa mapema kama ilivyotokea baada ya Mzuzuri kuua na kulindwa na jamaa yake Kikwete asijue Mungu hana rushwa wala kujuana. Maana ukiangalia umati wa waathirika anaowaibia na kuwaua unashindwa kuelewa hata kilichowapa ujasiri CCM kuendelea kumbakiza kwenye wenyekiti.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173