Ni hivi majuzi Tanzania na Kenya zimesherehekea zaidi ya miaka 50 ya uhuru wake. Siku chache baadaye taarifa zinakuja kuwa rais Jakaya Kikwete anakwenda Marekani "kuchekiwa" afya yake. Hii maana yake ni kwamba miaka yote zaidi ya 50 ya uhuru haijatupatia hospitali ya kuweza kuwachunguza watawala wetu. Pia miaka hii yote haijatupatia viongozi wanaoweza kujiamini na kuamini katika huduma zinazotolewa na serikali zao. Hii imenikumbusha kisa cha mama ntilie aliyekuwa akiagiza chakuka hotelini kila ikifika saa ya chakula huku akiwauzia wateja wasiojua uchafu na hatari ya chakula chake. Rais anakwenda nje kuombaomba na kuchekiwa afya yake. Ajabu huyo rais asiyeamini usalama wa huduma zinazotolewa na hospitali zinazosimamiwa na serikali yake anawadanganya wananchi kuwa wako sawa na anaipenda nchi yake. Ni unafiki na uhovyo kiasi gani? Mandela alitawala miaka mitano si hamsini. Alihakikisha kila kitu walichoacha makaburu kinaendelezwa kiasi cha kufia nchini mwake bila kwenda kujiaibisha ughaibuni kama hawa. Marais wetu wataendelea kutibiwa, kuchekiwa afya na kufia nje hadi lini? Je hii ni laana kwao kwa kuendekeza ubinafsi,wizi, ufisi, ufisadi na uzururaji hadi afya zao wanaziweka rehani ughaibuni? Je nini yatakuwa matokeo ya uchunguzi huu? Tutegemee yale ya Jangwani au zaidi?Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.
Ni hivi majuzi Tanzania na Kenya zimesherehekea zaidi ya miaka 50 ya uhuru wake. Siku chache baadaye taarifa zinakuja kuwa rais Jakaya Kikwete anakwenda Marekani "kuchekiwa" afya yake. Hii maana yake ni kwamba miaka yote zaidi ya 50 ya uhuru haijatupatia hospitali ya kuweza kuwachunguza watawala wetu. Pia miaka hii yote haijatupatia viongozi wanaoweza kujiamini na kuamini katika huduma zinazotolewa na serikali zao. Hii imenikumbusha kisa cha mama ntilie aliyekuwa akiagiza chakuka hotelini kila ikifika saa ya chakula huku akiwauzia wateja wasiojua uchafu na hatari ya chakula chake. Rais anakwenda nje kuombaomba na kuchekiwa afya yake. Ajabu huyo rais asiyeamini usalama wa huduma zinazotolewa na hospitali zinazosimamiwa na serikali yake anawadanganya wananchi kuwa wako sawa na anaipenda nchi yake. Ni unafiki na uhovyo kiasi gani? Mandela alitawala miaka mitano si hamsini. Alihakikisha kila kitu walichoacha makaburu kinaendelezwa kiasi cha kufia nchini mwake bila kwenda kujiaibisha ughaibuni kama hawa. Marais wetu wataendelea kutibiwa, kuchekiwa afya na kufia nje hadi lini? Je hii ni laana kwao kwa kuendekeza ubinafsi,wizi, ufisi, ufisadi na uzururaji hadi afya zao wanaziweka rehani ughaibuni? Je nini yatakuwa matokeo ya uchunguzi huu? Tutegemee yale ya Jangwani au zaidi?Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.