Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3187

Hotuba ya Magufuli suto kwa Afrika

$
0
0
           Hivi karibuni rais John Pombe Magufuli alionyesha upekee kama kiongozi wa nchi kwa kuwa kiongozi wa kwanza wa  Tanzania kuhutubia mkutano wa wakuu wa Nchi Huru za Kiafrika kwa Lugha ya Kiswahili jambo ambalo lilipokelewa kwa hisia tofauti. Wapo walioona kama ni kujidhalilisha au kukwepa kutumia Kiingereza Lugha ya mtawala wetu wa kikoloni wa zamani huku wengine–hasa wenye kujitambua na kupenda taifa lao–wakimsifu kwa ujasiri na uthubutu huu wa aina yake. Wale ambao bado mabakia ya ukoloni hayajawatoka vichwani walidiriki kusema kuwa rais hajui Kiswahili bila kujua kuwa andiko lake kwa ajili ya shahada yake ya uzamizi (PhD) aliliandika kwa lugha hiyo. Niliwasoma kwenye mitandao wakikejeli kitendo hiki cha kishujaa bila kujua kuwa walikuwa wakifichua ujinga na kujikana kwao.
            Hata hivyo, ujinga na ulimbukeni na woga wa kutumia lugha ya Kiswahili ambayo ni moja ya lugha kubwa za kimataifa kwa baadhi ya wenzetu havikuanza jana wala havitaisha kesho. Zipo nchi tena jirani ambazo watu wake wanaonea aibu Kiswahili kwa kushabikia Kiingereza ambacho nacho hawakijui zaidi ya kukiongea kwa lafudhi za lugha zao asilia.  Wengi hukwepa kutumia Kiswahili au kikionea aibu kutokana na imani mfu kuwa lugha hii ni ya wale ambao hawajaelimika jambo ambalo si kweli. Hivyo, tunampa moyo rais Magufuli asikate tamaa bali aendelee kukienzi na kukitumia Kiswahili popote aendapo ili kutangaza Kiswahili kama lugha ya taifa na ya Afrika yenye asili yake Tanzania.
             Hata hivyo, Magufuli si wa kwanza kukosolewa na kuonekana wa ajabu kwa kutumia Kiswahili kwenye jukwaa la kimataifa.  Kwa mfano, mwaka 1964 marehemu profesa Ali Mazrui gwiji wa sayansi ya jamii alipendekeza Kiswahili kitumike kuwa lugha ya Umoja wa Nchi Huru za Kiafrika (OAU). Badala ya kuungwa mkono, pamoja na usomi wake wa kupindukia, alizomewa na kuonekana kama hakuwa ameelimika vilivyo. Ajabu ya maajabu ni kwamba wengi waliomzomea walikuwa na viwango vidogo vya elimu ikilinganishwa na Mazrui mwenyewe.  Watu wenye mawazo mgando, ya kikale na kikoloni wanaweza kuona kama rais Magufuli kuhutubia Umoja wa Afrika (AU) ni jambo la ajabu bila kujua kuwa ni njia moja ya kuonyesha kujitambua, kujithamini na kuchangia kwa Umoja wa Afrika na kuondokana na masalia ya ukoloni ukiachia mbali kukuza Kiswahili kama lugha ya  taifa na kimataifa ya kiafrika hata kama ina baadhi ya maneno ya lugha za kigeni.
            Kwanini viongozi wa mataifa makubwa kama China, Japan Urusi na mengine hutumia lugha zao hata kama viongozi hawa wanakimanya kiingereza? Wanafanya hivyo ili kuonyesha wanavyojitambua. Tunapaswa kujivunia hatua hii aliyofikia rais Magufuli kwa kupeperusha bendera ya Tanzania na lugha yetu ya taifa. 
            Wapo wanaokosoa hotuba ya Magufuli kwa kuangalia udhaifu uliojitokeza ambao si kosa la rais yaani kutotoa nafasi kwa mkalimani kutafsiri. Ikizingatiwa kuwa hii ni hotuba ya kwanza kwa rais Magufuli kwenye jukwaa kubwa kama hili, hivyo anaweza kujifunza na kushughulikia mapungufu haya. Hata hivyo, ukisikiliza namna wasikilizaji walivyokuwa wakimshangilia, ni wazi ujumbe ulikuwa ukiifikia hadhira yake barabara. Watanzania na waafrika walio wengi wana kasumba ya kujivunia vya wengine wakati vyao wakividhalilisha. Unaweza kuona udhaifu huu kwenye namna ya watu wetu wanavyotetea dini nyemelezi za kigeni huku wakitukana mila zao na kutukuza za wenzao hata kama zinafanana au ni mbovu kuliko zao.
            Lazima waafrika tufikie mahali tujikomboe kutoka kwenye kongwa za kikoloni kama vile kutumia lugha zao bila ulazima au kuamini kuwa sehemu takatifu duniani ziko ughaibuni ukiachia mbali kupachikwa majina ya kigeni na kuomba kwa baadhi ya lugha za kigeni kana kwamba Mungu hajui wala hakutupa maarifa ya kuunda lugha zetu. Wakati mwingine tunawalaumu wazungu na waarabu waliotuletea ukoloni wao tukaugeuza kuwa wetu wakati sisi wenyewe ndiyo tunauendeleza na kuutukuza tokana na kutojitambua, kutojiamini na ujinga.
            Tumalizie kwa kumpongeza rais kwa kuanza kujikomboa mwenyewe ili liwe somo kwa wengine hasa viongozi wenzake wa Umoja wa Afrika (AU) ambao walionyesha kongwa za ukoloni katika uchaguzi uliopita wa Mwenyekiti wa AU kwa kupiga kura kwa kulalia kwenye mgawanyiko wa kikoloni baina ya makoloni ya zamani ya kifaransa na kiingereza ambapo waziri wa mambo ya kigeni wa Chad Moussa Fakhi Mahamat alimshinda mwenzie wa Kenya Amina Mohamed.
            Tunawasihi watanzania wajenge mazoea ya kuithamini lugha yao kama tunu yao. Kwani si mataifa mengi ya kiafrika yenye lugha zenye hadhi na kusambaa kijiografia kama Tanzania. Rais Magufuli ameanza. Naamini hata majirani zetu wanaoona Kiswahili kama ni lugha ya wasiosoma, watabadilika na kuanza kujiamini na kujithamini na kutumia Kiswahili kama Waafrika. Hakika hotuba ya Magufuli kwa AU ni suto kwa Waafrika walio wengi ukiachia mbali kuwa jambo la kupongezwa na kupigiwa mfano.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3187

Trending Articles


Vimeo 10.7.1 by Vimeo.com, Inc.


UPDATE SC IDOL: TWO BECOME ONE


KASAMBAHAY BILL IN THE HOUSE


Girasoles para colorear


Presence Quotes – Positive Quotes


EASY COME, EASY GO


Love with Heart Breaking Quotes


Re:Mutton Pies (lleechef)


Ka longiing longsem kaba skhem bad kaba khlain ka pynlong kein ia ka...


Vimeo 10.7.0 by Vimeo.com, Inc.


FORECLOSURE OF REAL ESTATE MORTGAGE


FORTUITOUS EVENT


Pokemon para colorear


Sapos para colorear


Smile Quotes


Letting Go Quotes


Love Song lyrics that marks your Heart


RE: Mutton Pies (frankie241)


Hato lada ym dei namar ka jingpyrshah jong U JJM Nichols Roy (Bah Joy) ngin...


Long Distance Relationship Tagalog Love Quotes