Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173

Je uraia wa nchi mbili ni kwa wageni tu Tanzania?

$
0
0

Japo watanzania wamekuwa na mawazo na misimamo tofauti kuhusiana na uraia wa nchi mbili, kitu kimoja kiko Dhahiri; sheria ya Tanzania hairuhusu raia yoyote wa Tanzania kuwa na uraia wa nchi mbili. Rais Magufuli–sawa na watanzania wengine analijua au anapaswa kulijua hili–hivyo alichosema si kuteleza kwa ulimi wala utani. Hata hivyo–hivi karibuni katazo hili la kisheria lilionekana kuwa la kibaguzi–tokana na ukweli uliofichuliwa na rais John Pombe Magufuli. Akimkaribisha mgeni wake waziri mkuu wa India Narendra Modi aliyetembelea Tanzania hivi karibuni, rais Magufuli alikaririwa na vyombo vya habari akisema, “Amejisikia [Modi] raha sana; alivyoona anakaribishwa na wananchi wengi wa Tanzania ambao naamini katika wale waliomkaribisha wengine ni miongoni mwao waliompigia kura kwenye jimbo lake.” Maneno haya yanajifafanua hasa ikizingatiwa kuwa kwanza, Modi si mtanzania–ni mhindi tena kiongozi wa nchi–hivyo, kwa sheria ya Tanzania, hawezi kuwa na wapiga kura. Pili, kwa mujibu wa rais, Modi–pamoja na sheria za Tanzania kukataza–anajua kuwa ana wapiga kura nchini hata kama ni kinyume cha sheria. Tokana na ithibati ya rais wetu ambaye mara nyingi amekaririwa akieleza wazi anavyochukia unafiki na uongo, aliyosema ni ya kweli tupu na si unafiki wala kufurahisha genge. Pia, tokana na ukweli huu na uzoefu wa watanzania walio wengi hasa wa mijini, unaweza kujenga mahitimisho na kugundua ni kwanini:
Kwanza, wengi wa mafisadi wakubwa wanaoshirikiana na mafisadi wakubwa wazawa serikalini ni wahindi.
Pili, wahindi wamekuwa wakiwabagua waafrika kwa miaka yote waliyokaa Tanzania bila kushughulikiwa kwa vile wana haki zaidi ya wazawa.  Hatutaki kutoa madai bila kutoa ushahidi. Kwa miaka zaidi ya mia waliyokaa Tanzania, nionyeshe ndoa hata tatu baina ya waswahili na wahindi nitaondoa hoja hii na kuomba msamaha. Najua ukweli huu ni mchungu. Lazima usemwe ili tuweze kusonga mbele kama taifa baada ya kujisuta na kusutana kama watanzania bila kujali rangi ya ngozi zetu. Isitoshe mie si wa kwanza kuliona hili. Marehemu Christopher Mtikila aliliona na kuliongelea sana na kwa undani bila woga wala unafiki. Nanachofanya hapa ni kukumbusha tu ili kuondoa kuendelea jinai ya ubaguzi.
Tatu, waziri mmoja wa uchumi wa zamani aliwahi kusema kuwa uchumi wa Tanzania ulikuwa–kipindi fulani–unashikiliwa na wahindi kumi tu. Hili ni kweli. Kwanza, wahusika hawakukanusha na ukweli unaonyesha hivyo.
Nne, matajiri wengi nchini ni wahindi hasa ukiangalia uwiano wa idadi ya watu. Kama hii haitoshi, wengi wa matajiri hawa wanaishi kwenye nyumba za msajili wa majumba kwa bei nafuu wakati wana mahekalu yao wakiyapangisha kwa dola au wana uwezo wa kujenga majumba yao wenyewe.
Tano, Tanzania imeruhusu jamii hii kuwa na shule, dini, na shughuli nyingine za kibaguzi za jamii moja ukiachia mbali kubariki mfumo wao wa kikaburu wa kitabaka (caste system) ambao licha ya kuwa wa kibaguzi ni kinyume cha sheria na haki za binadamu.
Sita, rais alisema kuwa Bunge la Tanzania lina wabunge kumi wenye asili ya kihindi, jamii ambayo hivi karibuni imesifika kwenye vyombo vya kimataifa kwa kuwabagua waafrika ikiwaita nyani au absii, bander au kalu. Rejea kupigwa na kudhalilishwa vibaya kwa mwanafunzi wa kitanzania nchini aliyekuwa akisoma kwenye Chuo Kikuu cha Acharya, Bangalore, India hivi karibuni baada ya msudani mmoja kusababisha ajali ya barabarani bila kutaja mwanafunzi toka DRC Masunda Kitada Oliver aliyeuawa May kwa kugombea Bajaj.
Kweli usilojua ni usiku wa kiza. Sijui kama waswahili wangekuwa huko ugabacholini wangepewa hata ujumbe wa nyumba kumi chini ya mfumo wa kikaburu wa caste system. Ni bahati mbaya kuwa waswahili walifundishwa kujikana na kuwapapatikia wageni kiasi cha kuwa na methali isemayo mgeni karibu mwenyeji apone kuonyesha utegemezi na kutojiamini kwao. Walevi wana shaka na huu ushuhuba wa ajabu ajabu ambao haulengi kutatua matatizo kama vile utoroshaji raslimali zao, ubaguzi wa moja kwa moja tena wa muda mrefu na madudu mengine mengi ambayo tawala karibia zote zimekuwa zijifanya haziyaoni. Wenzetu husema charity begins at home, au hisani huanzia nyumbani.
Tumalizie hapa kwa kumtaka rais Magufuli na serikali yake ima kuruhusu uraia pacha au kuupiga marufuku kwa watanzania wote badala ya kubagua hata kusifia ubaguzi huu. Sheria ni msumemo kama ambavyo rais Magufuli hupenda kusema; haipaswi kubagua wala kupendelea, kutumika kibaguzi au kuwa utashi wa mtu, kikundi cha watu wala taasisi bali utashi wa sheria. Ni aibu kugundua kuwa taifa huru linaweza kuwanyima raia wake wazalendo na kuwaruhusu raia wa kigeni wautumie kuliibia. Je yote haya yanafanyika hivi kwa faida ya nani? Sijui kama India inaweza kuruhusu ujinga kama huu tena kwa waafrika ambao wanasifika kwa wanavyobaguliwa nchini India hata kwenye bara lao wenyewe kutokana na kuwa na uongozi wa kifisadi na usiojithamin kukosa uzalendo na kujiamini.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173