Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173

Wakuu "wapya" wa mikoa, Magufuli achemsha

$
0
0
Ukiangalia orodha ya walioteuliwa kuwa wakuu wapya wa mikoa unashangaa kama imeandaliwa na Jakaya Kikwete au John Magufuli. Maana, hakuna jipya zaidi ya muendelezo wa usanii ule ule. Hapa ndipo alichokificha Magufuli kitafichuka kirahisi. Amerejesha ujeshi, u-CCM, ukale, kujuana na kila aina ya kufadhiliana na kulindana kwenye uteuzi wake mpya usio na upya wowote. Hivi watu kama Makala, Killango-Malecela wamerejeshwa na nini pamoja na kushindwa kwenye kura za maoni zaidi ya kufadhiliana na kulindana kichama? Uhovyo wa Magufuli hauishii hapo. Rejea anavyofanya mambo kibabe na kizamani bila kufuata sheria. Mfano, hadi sasa watanzania wengi wameishaanza kustukia udaktari wake na kiingereza chake broken ukiachia mbali kutoa maelekezo kana kwamba Tanzania ni mali yake binafsi. Rejea Magufuli alivyowaambia Bank of Tanzania (BoT) wafute majina ya wafanyakazi hewa badala ya kutaka wafikishwe mahakamani. Hata hiyo expose yake inatia shaka kama ni kweli au kanyabwoya.
Kwa habari zaidi BONYEZA HAPA.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3173