Quantcast
Channel: Free Thinking
Viewing all articles
Browse latest Browse all 3177

Tuvunje Muungano au tuungane kweli kweli

$
0
0

Zanzibar watataka serikali tatu kwa vile si mzigo kwao. Pesa ya kuendesha serikali ya Tanganyika haitatoka Zanzibar ingawa pesa ya kuendesha serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar siku zote imetoka Bara. hivyo kwa watu kama hawa ambao hawataonja machungu ya kuwa na utitiri wa serikali kuwa na serikali tatu si tatizo. Pia wazanzibar wangependa serikali tatu ili kuendelea kuukana utanzania na kuukumbatia uzanzibari.  Kama na watanganyika watachangamkia utaifa wao wa asili hakuna shaka utanzania utabakia kuwa kwenye shubaka na nyaraka na thamani yake itatoweka. Kitendo cha namna hii ni kuvunja muungano hata kama hatutaki kusema wazi. Kama tumeridhika na hili basi tukubali kuvunja muungano badala ya kuutetea mchana na kuuvunja usiku. Huu ni unafiki na kutojiamini. Tuachane na muungano na kushikilia maslahi binafsi kama ambavyo ilivyo. Tuseme wazi kuwa maslahi yetu kama bara au visiwani ni zaidi ya muungano ili dunia ituelewe na tupumue au vipi?  Je kuna haja gani kuwa na utaifa usio na mwenye kuubeba kama ambayo itakuwa kwa utanzania ambao hata hivyo umebakia kubebwa na watu wa Bara huku wa Visiwani wakiuepa kwa gharama yoyote vinginevyo kuwepo na maslahi kama uwaziri ubunge au fursa za kuchuma?
Bara watataka serikali moja ili kuondoa mzigo unaowakabili hadi sasa wa kugharimia uendeshaji wa serikali mbili hasa ukilinganisha vyanzo vya uchumi baina ya pande mbili. Ni ajabu kuwa waliokusanya maoni kutoliona hili! Ni ajabu kuwa wabara wanazidi kuongezewa mzigo ili kuwaridhisha wavisiwani. Pia itakuwa ni ajabu kama tutakuwa na serikali tatu bila muungano kuvunjika kulaleki!
Kuna ushahidi wa kutosha kuwa waanzilishi wa muungano waliamua kuwa na serikali mbili ili baadaye waelekee serikali moja pamoja na kutofautiana mwanzoni kutokana na hali ya kisiasa ya wakati ule. Kwa mujibu wa Jaji Mark Bomani alikaririwa hivi karibuni akisema, “Hayati Karume yeye alipendekeza nchi mbili kuungana na kuwa nchi moja mara moja. Hayati Nyerere yeye alisita kidogo kwa kuogopa kwamba ingeonekana Zanzibar imemezwa na Tanganyika na hivyo pengine kuelekeza maasi Zanzibar.” Wakati ule ilikuwa inaingia akilini. Je baada ya kukaa pamoja kwa zaidi ya miaka arobaini bado tunahofia kumezwa? Mbona Kilwa iliyokuwa na hadhi sawa na Zanzibar hailalamikii kumezwa wala Lamu Malindi na Mombasa nchini Kenya? ni ajabu kuwa tunaongeza wingi wa serikali na kujipa moyo kuwa ndiyo kudumisha muungano wakati tunauvunja kijanja!
 
Je kwa kuongeza serikali ya tatu badala ya kupunguza ya pili tunaimarisha muungano au tunaendekeza kila upande na maslahi yake? Kama kweli tunaamisha kuhitajiana basi tuungane na kuwa na serikali moja badala ya utitiri wa serikali ambazo kwa nchi ombaomba kama yetu zaweza kuwa chanzo cha kusambaratika. Muungano ni sawa na ndoa. Kinachoendelea ni sawa na ndoa ya maslahi au chuma ulete ambapo wanandoa hutumiana kwa maslahi tofauti. Ndoa halisi ni kuwa mwili mmoja na kitu kimoja badala ya vipande vipande.
Tufanye kama Marekani. Nchi zilizotengeneza Marekani au Kanada zilipoungana zilibakia kuwa majimbo na nchi zimeshikana na hakuna anayedai kumezwa. Hawaii ni sawa na Zanzibar. Lakini bado haidai wala kujihisi imemezwa na California au Texas kwa sababu ni nchi kubwa ndani ya muungano wa Marekani. Prince Edward Island nchini Kanada ni kijisiwa kidogo lakini hakijawahi kulalamika kuwa kimemezwa na Ontorio au Nanavut kwenye shirikisho pana la Kanada.  Kimsingi, hii hofu ya kumezwa ni ya si ya msingi na haina maana kwa vile kama tutaungana kweli kweli wote tutakuwa watanzania badala ya sasa ambapo tuna wazanzibari, watanganyika, watanzania, wapemba, waunguja na kesho tutakuwa na waMnemba. Kama kweli tunahitajiana haya madai ya Uzanzibari kama utaifa ya nini iwapo watanganyika kwa miaka zaidi ya 40 wameridhika kuitwa watanzania bila kulalamikia utanganyika.  Muungano mara nyingi hujengwa kwa kile waingereza huita give and take and good will. Unapata hiki na kupoteza kile. Unatoa kile unapokea hiki na mambo yanakwenda.
Tuhitimishe kwa kusisitiza kuwa bila kuwa na serikali moja muungano wa Tanganyika na Zanzibar utaendelea kuwa mzigo na kitendawili ambacho baadaye kinaweza kudhoofisha Tanzania. Tuamua tuwe na serikali moja au tuvunje muungano ili kuwe na nchi mbili ambazo kila moja itakuwa na serikali moja. Hivyo, kuondoa mzigo kwa walipa kodi wa nchi hizi. Kuwa na serikali tatu hata mbili ni sawa na kuwa hermaphorodite yaani mnyama mwenye jinsia mbili ambaye si jike wala dume bali kituko. Kama sote ni wamoja kihistoria na kijiografia, kwanini tunaogopa kuungana na kutengeneza nchi moja yenye nguvu na ustawi? 
Chanzo: Tanzania Daima Juni 19, 2013.

Viewing all articles
Browse latest Browse all 3177

Trending Articles


FORECLOSURE OF REAL ESTATE MORTGAGE


Tagalog Quotes About Crush – Tagalog Love Quotes


OFW quotes : Pinoy Tagalog Quotes


Long Distance Relationship Tagalog Love Quotes


INUMAN QUOTES


Sapos para colorear


Break up Quotes Tagalog Love Quote – Broken Hearted Quotes Tagalog


Patama Quotes : Tagalog Inspirational Quotes


5 Tagalog Relationship Rules


Re:Mutton Pies (lleechef)