
Pamoja na kujua kuwa Bi Samia Suluhu Hassan ndiye makamu wetu wa rais na mwanamke wa kwanza nchini kushika wadhifa huu, wengi hatujamfahamu vizuri. Kwa mfano, katika sherehe za kuapishwa kwake na rais John Magufuli tulionyeshwa wana familia ya Magufuli. Ajabu, tangu ateuliwe kuwa mgombea mwenza hadi kuwa makamu wa rais, habari za familia zake ni kama hazipo. Unapokuwa kiongozi wa umma lazima mambo yako mengi yawekwe wazi. Kwa mfano, tunamjua mke wa rais Magufuli kuwa anaitwa Janet. Sambamba naye hatumjui mume wa bi mkubwa huyu. Je ni single, ameachika au vipi?
