Quantcast
  • Login
    • Account
    • Sign Up
  • Home
    • About Us
    • Catalog
  • Search
  • Register RSS
  • Embed RSS
    • FAQ
    • Get Embed Code
    • Example: Default CSS
    • Example: Custom CSS
    • Example: Custom CSS per Embedding
  • Super RSS
    • Usage
    • View Latest
    • Create
  • Contact Us
    • Technical Support
    • Guest Posts/Articles
    • Report Violations
    • Google Warnings
    • Article Removal Requests
    • Channel Removal Requests
    • General Questions
    • DMCA Takedown Notice
  • RSSing>>
    • Collections:
    • RSSing
    • EDA
    • Intel
    • Mesothelioma
    • SAP
    • SEO
  • Latest
    • Articles
    • Channels
    • Super Channels
  • Popular
    • Articles
    • Pages
    • Channels
    • Super Channels
  • Top Rated
    • Articles
    • Pages
    • Channels
    • Super Channels
  • Trending
    • Articles
    • Pages
    • Channels
    • Super Channels
Switch Editions?
Cancel
Sharing:
Title:
URL:
Copy Share URL
English
RSSing>> Latest Popular Top Rated Trending
Channel: Free Thinking
NSFW?
Claim
0


X Mark channel Not-Safe-For-Work? cancel confirm NSFW Votes: (0 votes)
X Are you the publisher? Claim or contact us about this channel.
X 0
Showing article 1441 to 1460 of 3177 in channel 8805252
Channel Details:
  • Title: Free Thinking
  • Channel Number: 8805252
  • Language:
  • Registered On: March 5, 2013, 12:54 am
  • Number of Articles: 3177
  • Latest Snapshot: May 18, 2025, 3:16 pm
  • RSS URL: http://mpayukaji.blogspot.com/feeds/posts/default?alt=rss
  • Publisher: http://mpayukaji.blogspot.com/
  • Description: I Fear Nothing But Fear Itself
  • Catalog: //thinking1343.rssing.com/catalog.php?indx=8805252
Remove ADS
Viewing all 3177 articles
Browse latest View live
↧

If Clinton trumps Trump Tomorrow

November 7, 2016, 8:06 pm
≫ Next: If Clinton loses it Michelle Obama Should Warm up to Run for President
≪ Previous: Mihadarati: Kwanini Kikwete hamsaidii Magufuli?
$
0
0
         Arguably, when the superpower of the world does anything, it automatically becomes an international subject. This is why the coming elections in the United States (US) always hit headlines all over the world.
    Strikingly, the US seems to have started divorcing its stinking past sexual and racial xenophobic past. For, Clinton–if she smashes the glass ceiling once again–is taking the reins from the first Afro-American president and a colleague Democrat which is rare in the politics of the US. It is no longer a speculative matter that Hilary Clinton, former first lady and Democratic presidential flagbearer is likely to trump Donald Trump, a billionaire Republic presidential flagbearer. Shall she, and chances are that she will. She’ll smash the double glass ceiling for the second time with a single year. She became the first woman to be nominated by a major party as its presidential candidate. Now, she becomes the first woman and the first lady to become president of the US.
            This time around, the US has two record breakers in the presidential race. Clinton’s archnemesis, Trump, is also a record breaker. A smart guy though in bad way, he’s the first presidential candidate that the US has ever had that’d say lewd things about and against his opponent not to mention trading insults as it recently happen in downtown New York’s Waldorf-Astoria hotel at which venue Trump and Clinton attended the annual fundraiser for Catholic charities known as the Al Smith Dinner. He is the first candidate who refused to disclose his tax returns not to mention not paying tax. So, too, he is the first candidate who didn’t come from the establishment who can say whatever that pops up in his mind. He also, is the outsider who beat bigwigs in his party. Furthermore, Trump is the first openly racist, misogynist who is alleged to have called women dogs, pigs slobs and whatnot without forgetting calling all Latinos rapists and Muslims terrorists. As if it is not enough, Trump is the first US presidential candidate to allege that elections will be rigged even before they were conducted which is something new in the history of the US. He goes further asserting that he’ll never accept results otherwise he’s the winner.
            Apart from being an allegedly stinking misogynist, Trump’s another burden. He loves and hates women at the same time. Up until now, there have already come forth ten women who alleged that Trump sexually assaulted them after the surfacing of what famously became ‘a locker-room banter’ in which Trump’s heard bragging about how he groped women and did whatever he wanted.
            Although the US has changed tremendously–especially after electing a black president, Barack Obama, who proved that even a black man can do bigger things than white if he is compared to George Bush–it still has a long way to go. Thanks to the support Trump got after coming up with his raves and rants against immigrants, Muslims, women, homosexuals and other, it shows that there are  millions of Americans who still live in the dark past subscribing to things such as demonization of others, racism and the likes. Otherwise, Trump wouldn’t have made it up to becoming a presidential candidate for a major party.
            Trump had rubbed many people the wrong way. For instance, he once said that Africa needs to be recolonized so that it can develop. He went further proposing that if he becomes president, he’d erect a wall on US-Mexico border to stop illegal immigrants from entering the US.
            When it comes to policies, apart from having none, Trumps says expressly that he can run a country singlehandedly like his private business. He’s been oft-quoted saying that he’s the only one who can fix the problems that the US have currently. After saying that, Clinton hit back saying that Trump lacks the temperament of being president; and there’s no way a single individual can fix the US Trump said he wanted to make great again as if it were not great. In the beginning of the campaigns Trumps seemed to be the force to be reckoned with. But as they day went by; and a true Trump surfaced, slowly, he started losing mojo and support altogether.  Thanks to the current opinion polls, now Trump is paying the price dearly for his lewd outbursts which seem to have turned voters against him. For the first time, Republican bigwigs such as former presidents George Bush Jr and Sn speaker of the US House of Representatives, Paul Ryan, and many more that openly distanced themselves from scum Trump. If Clinton trumps Trump, the US will temporarily get off the hook. Again, it needs to learn from the mistakes that cloned Trump so as to cause a hell of fear.
↧
Search

If Clinton loses it Michelle Obama Should Warm up to Run for President

November 8, 2016, 9:30 pm
≫ Next: Kijiwe chashangaa Makufuli kuogopa ‘makaburi’
≪ Previous: If Clinton trumps Trump Tomorrow
$
0
0


What a tight race! Shall Clinton lose it Michelle Obama should prepare herself to become the first US;s female president. Again, it is still too early to call.
Nkwazi
↧
↧

Kijiwe chashangaa Makufuli kuogopa ‘makaburi’

November 9, 2016, 8:22 am
≫ Next: Bila kufukua ‘makaburi’ tutakufa kwa uoza
≪ Previous: If Clinton loses it Michelle Obama Should Warm up to Run for President
$
0
0
 
       Baada ya Dokta Joni Kanywaji Makufuli kutoa mpya akisema kuwa anaogopa kufukua makaburi kwa vile hawezi kuyafukia, Kijiwe kimeamua kumpa ushauri tena wa bure. Kijiwe hakikuamini kuwa mtu jasiri na jabari kama yeye angeogopa makaburi.
            Mgosi Machungi analianzisha “wagoshi mmesikia huu nkanda wa makabui aitoa dokta Kanywaji juzi akisema eti anaogopa kufukia akini si kuchimbua makabui? Je mnafahamu haya makabui ni akina nani na waifanya nini kayani kwetu? Je mnafahamu kuwa haya makabui si makabui kama muyajuavyo bai waja waio hai akini waiofanya mambo kama wafu kiasi cha kuitwa makabui?”
            “mgosi hapa sasa nimeamini kuwa wewe ni bonge la mfalasafa jirani na Msomi na mzee Mpayukaji mwenyewe baba wa busara au Abu Hikma kwa lugha ya kinyantuzu.”
            Msomi Mkatatamaa ambaye siku hizi hajivungi anatia guu mapema anakula mic “kama anaogopa makaburi tena si kufukua bali kufukia, atawezaje kuweka kaya kwenye mstari kama anavyotuaminisha? Nadhani hapa tukubaliane tu. Jamaa amepotoka; au tuseme amepitiwa hata kuyataja hayo makaburi. Alipaswa ayaogope; kwa vile yana walio hai tena waliomtangulia katika ukaburi na ufu wao kisiasa na kiutawala. Hata hivyo, nampongeza kwa kuwaita makaburi wakati bado wako hai. Kwa tunaojua ukubwa wa makaburi tajwa, tunaanza kutia shaka dhima na dhamira yake ya kupambana na uovu kwa kuchagua. Huwezi kufukua na kufikia matuta tu ukakingia kifua makaburi. Nadhani makaburi yana uoza zaidi ya matuta hata majipu.”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kula mic mapema “hebu tusiogope kuita kulego kulego. Ameyataja vipi wakati ametumia mafumbo. Je mwafahamu kuwa haya mnayodhani ni makaburi ni waja hai tena wenye majina yao? Tena ni wale ambao hamuwezi kuwategemea japo mnawafahamu. Wengi walijipiga vifua na kujitukuza wasijue ulaji una mwisho. Hata naye anapaswa kulijua na kulikubali hili tena kwa unyenyekevu. Sitaki niseme mengi. Kila kilicho na mwanzo shurti kiwe na mwisho. Hata haya makaburi hai yatakufa hata kama yamemeza mali kibao za wachovu.”
“Yakhe kwa mafumbo sikuwezi. Yaani mwenzio aogopa kuwataja watu kwa majina na hali yao wewe wafumbua kila kitu tena waweka wazi. Hapa unkata kweli kweli. Hata mie nlisituka sana kusikia watukufu wakiitwa makaburi japo kweli kwa walotutenda ni makaburi yaniyotembea hata kuenziwa na kuabudiwa bila chochote cha maana walotenda kwetu sie wachovu ati,” Mpemba anachomeka kwa nahau za kipwani.
            Mipawa anakula mic, “kama huyu jamaa anaogopa makaburi, ataweza mizungu na wazungu wa bwimbwi, majambazi, mafisadi na kila aina ya wahalifu waliotamalaki kayani? Je amesahau ahadi alizotoa kuwa hataogopa wala kupendelea mtu awe hai au mfu? Sasa kwanini anawakingia tena kifua hawa wafuhai aliokwisha kuwaahidi ulinzi? Kwani alilazimishwa kurongo aliyoronga au ndiyo hayo ya kupayuka,” ananigeukia na kuniangalia na kusema “mzee simaanishi kukosea heshima. Ila wanapaswa kujua kuwa kupayuka pwenti kuna mwenyewe na mwenyewe ni wewe.” Sijibu kitu zaidi ya kutabasamu kwa ujiko anaonipa huku akimkandia big mwenyewe.
            Kapende naye hangoji; anakwatua mic “kaka usinchekeshe. Ina maana jamaa ameanza kuishiwa nguvu, kuisha, kutuingiza mkenge au ndiyo hivyo anaanza kubadilishwa na mfumo uliofuma na kufunika haya makaburi ambayo hataki kuyafunika japo anao uwezo wa kuyafukua?
Kama hawezi hata kufunika makaburi basi aseme mapema kuwa mzigo umemshinda.” Anapiga chafya na kuendelea, “kama hali ndiyo hii si awapishe wenye msuli wayafukue kuyapekua na kuyafukia hayo makaburi na hata kuchoma moto uchafu uliomo makaburini hasa ikizingatiwa kuwa hakuna maiti mle zaidi ya uchafu.”
            Da Sofia Lion aka Kaunugaemba anakula mic “mwenzenu nimeshangaa sana. Sikutegemea kusikia niliyosika kwa niliyemsikia tena mwenye jabari asiyeogopa kitu wala ntu. Ameaniachia swali moja kuu: Kama nawezafukua kaburi sasa naogopa nini kyafukia au anataka tumsadie kufanya hivyo kama kweli anaogopa?”
             Kanji anaamua kumchomekea mshirika wake Sofi; anampoka mic na kuronga “mimi ona siyo ogopa kaburi. Iko ogopa maiti. Kaburi iko simo tu. Kule Bombey kaburini iko ishi mitu mingi kweli. Vatu hapana naogopa witu kama makaburi bali iti.”
Mzee maneno naye anaamua kumchomekea Kanji; anachonga “naona mtani wangu anaanza kujua Kiswahili hadi mafumbo. Maana alivyowaumbua wenzake kwa kuwapa sifa ya ukaburi sina hamu. Na kweli hawa jamaa ni makaburi yaliyowahi kukaa ikulu na kugeuza pango la wanyang’anyi kama alivyowahi kuonya mzee Mchonga (Mungu amuweke mahali pema peponi mzee wetu). Nadhani hata wao hawakutegemea kuwa–pamoja na kuwakingia kifua–bado jamaa anawalinganisha na makaburi. Wazaramizi tuna msemo mmoja kuwa aliyekuchoka hakuna anachoweza kukulinganisha nacho bali kaburi.”
                        Kijiwe kikiwa kinanoga si ukapita msafara wa mashumbwengu ya kaburi moja! Wacha tuyatoe mkuku kuona yana nini yananuka vipi! Kama siyo ndata kufunga barabara, tungemnasa kwenye mataa na kumpa vipande vyake huku tukimfukua na kutaka, atumbuliwe na kufukiwa lupango.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
↧

Bila kufukua ‘makaburi’ tutakufa kwa uoza

November 15, 2016, 7:04 am
≫ Next: Kijiwe champongeza Dk Kanywaji na mkewe
≪ Previous: Kijiwe chashangaa Makufuli kuogopa ‘makaburi’
$
0
0

 
            Kwanza, nichukue fursa hii kumpongeza dokta Joni Kanywaji wa Makomeo kwa kutumiza mwaka mmoja kwenye ulaji. Pili nimpe salamu za walevi kuwa tumekubali baadhi ya vitu vyake hasa kuwapiga wapigaji waliozoea kutupiga tukapigika japo tumekataa vingine. Leo nataka nimpe ushauri wa nguvu biggie ili afanye maamuzi magumu. Hii ni kutokana na kauli aliyotoa hivi karibuni akiongea na waandishi wa umbea wakati wa kuadhimisha mwaka wake mmoja kwenye ulaji. Kwanza, tumpe shavu; tunamkubali ingawa hatukubali huu msimamo wake mpya wa kusema kuwa hawezi kufukua makaburi kwa sababu hataweza kuyafunika. Oh boy oh bo! We need to open all closets to see the skeletons in there. Lo! Hivi kazi hapa iko wapi hata nikifikiri kilevi kati ya kufukua na kufukia makaburi? Kama yamemshinda si aniite nimpe tafu kwa kuyafukua na kuyafunika tena bila kuhitaji tingatinga wala ndinga? Sisi kwa ngoa, usongo na uchizani wetu tutayafukua, kuyafukia hata kuyatia nari kama ikitakiwa kufanya hivyo.
            Wakati aliposema anaogopa kufukua makaburi kwa vile hana uwezo wa kuyafukia, nilikuwa kwa mama Beti nikinyaka kanywaji na washirika na washikaji zangu. Kwanza, tulidhani jamaa alikuwa akitania. Lakini baada ya kurudia kuwa hatakuwa tayari kuyashughulikia makaburi yaliyozika uchumi wa kaya yetu, tulijua kweli jamaa hatanii; anaogopa majinamizi, mabufulu na ndogo za ajabu ajabu ambazo kwa walevi ni kitu cha kawaida hasa usawa huu ambapo maisha yamegeuka jinamizi la kutisha katika mpito wa kuweka kaya kwenye mstari. Pili, tuliona hapa kuna fursa kama atatushirikisha tukamsaidia kuyashughulikia hayo makaburi bila kujali ukubwa wake wala harufu yake. Tatu, tunadhani kuwa kufukua makaburi na kuyahakiki na kuyafukia ndiyo njia ya kuweka mambo hadharani ili kila mmoja ajulikana ana nini kwenye closet yake kama wasemavyo kwa kimombo. Nne, tunashauri kama anahofia ujasiri wetu si basi atumie ndata na ndutu wayafukulie na kuyaufikilia mbali haya makaburi yanayomhangaisha jamaa?
            Baada ya kugundua kuwa Kanywaji hatanii, baadhi ya walevi walianza kuguna na kuhoji: ujasiri wa jamaa umeende wapi hadi anapambana na majipu, ugonjwa hatari, lakini anaogopa makaburi tena yaliyojaa mifupa na uchafu? Mbona alisema kuwa hataogopa yeyote linapokuja suala la kusafisha kaya hata kama ikihitaji kufukua makaburi?  Je ni kwa sababu ya waliozikwa humo au ni sababu tu? Je anaogopa mabaki yaliyomo au ukubwa wa makaburi yenyewe? Kama ataogopa makaburi, atawaweza wauza bwimbwi na mafisadi na majambazi ambao wako hai? Je haya makaburi anayogopa ni ya watakatifu au wahalifu tunaowajua waligeuza kaya yetu shamba la chizi?
            Mlevi mmoja alituacha hoi alipodai kuwa hata angekuwa yeye angeogopa kuyafukua makaburi hasa ikizingatiwa kuwa waliozikwa humo wengi wao ni hai. Baada ya kusema hivyo, wengi walimtaka athibitishe. Ndipo akatuacha hoi kwa kuulizwa swali. Je ni wangapi wanatembea lakini wamekufa siku nyingi na ni wangapi walikusa miaka mingi lakini bado wana nguvu kuliko waliohai hawa ambao wamo kwenye makaburi anayoogopa dokta Kanywaji pale ikulu?
            Tokana na bangi, ujinga na ulevi, kila mlevi alianza kutafsiri tamko la kuogopa kufukia makaburi. Wapo waliopendekeza dokta Kanywaji akaribishe walevi wamsaidie kuyafukua na kuyafukia makaburi anayoyagwaya. Kwetu sisi tuliokwishapigika makaburi ni makaburi bila kujali ukubwa wa waliomo wala ukubwa wa makaburi yenyewe. Tukishafyatua ile kitu yetu hata hiyo harufu mbaya itokayo kwenye hayo makaburi wala haitusumbui.
            Hivyo, tunamshauri jamaa aangalie kwenye makaburi husika aone kama kuna mifupa na midude kama EPA, Kiwila, Loliyondo, NssF, NbC na madude mengine yanayojulikana na wale waliozikwa nayo au walioyazika. Kama siyo kutafuta visingizio, hakuna sababu ya kuwashughulikia wagonjwa tena wa vichaa kama wale wa kwenye bandari na kuogopa makaburi vinginevyo hayo makaburi yawe yamejaa mabomu yanayoweza kumlipua yoyote aliyeshiriki kwenye zama zake au wale waliojaa kwenye makaburi yale. Hapa naona kama ile mikangafu ya walevi iliyotwaliwa ikichungulia toka kwenye hayo makaburi ogopwa. Naona  mabulungutu ya noti na mihadarati kwenye makaburi. Naona majina makubwa ya zama zile yakichomoza toka kwenye makaburi ogopwa. Naona wasiotarajiwa wakichomoza mikono yao kuomba makaburi yao yasifukuliwe. Naona tuliodhani ni waja, kumbe vinyamkera, wakianza kupumua baada ya Dokta Kanywaji kusema hatafukua makaburi yao.
            Tumalizie kwa kusema wazi: bila kufukua makaburi, hatuwezi kutatua matatizo yaliyosababishwa na makaburi haya ukiachia mbali kutotenda haki kwa waathirika, waadhirika na hata makaburi yenyewe.
Chanzo: Nipashe Jumamosi juzi.
↧

Kijiwe champongeza Dk Kanywaji na mkewe

November 16, 2016, 5:30 am
≫ Next: Kama Magufuli hataki kuchimbua makaburi anyamaze
≪ Previous: Bila kufukua ‘makaburi’ tutakufa kwa uoza
$
0
0






         
Taarifa zilizozagaa kama moto wa nyika za kuugua na kulazwa kwa mke wa rahis Joni Kanywaji Makufuli kwenye Hospitali chakavu ya Muhimbii, kama apendavyo kuiita Mgoshi Machungi, zilimekikuna kijiwe. Hivyo, katika kikao cha leo kinawatumia salamu wawili hawa kuwamotisha waendelee na uzalendo wao usio kifani.
            Kapende leo ndiye anayeanzisha mada. Anaamkua na kuronga “jamani mmesoma hii stori iliyofurika kwenye magazeti yote ya wiki hii?” kabla ya kuendelea, Mgoshi Machungi anamchomekea “habai gani wakati magazeti yamejaa habai mbai mbai; hemu fafanua tieewe na kumwaga pwenti Mgoshi.”
            Kapende anajibu “Mgoshi umenionea. Sijamaliza kueleza wewe unanchomekea! Habari nimaanishayo ni ya kuugua ghafla na kulazwa kwa mke wa rahis mama Jane pale kwenye mkangafu wa Muhimbii. Nadhani kama nimekupata hili ndilo jibu unalotaka kusikia toka kwenye kichaka cha habari au vipi?”
            Mipawa anakwanyua mic “kusemaga ukweli, hili nami limenistua licha ya kunifurahisha. Nimefurahi kwa sababu rahis na mkewe wamejitahidi kuonyesha wanavyojali kaya yetu kwa vitendo na si kwa tambo na upuuzi wa majukwaani ambao wanasiasa wengi wanafiki hupenda kutumia. Ni faraja nadhani kwa wachovu wote kuona rahis na bi mkubwa wake wanavyoshirika huduma wanazohimiza wachovu kuwa wanajenga kwa ajili yetu sote.”
            Msomi Mkatatamaa hangoji Mipawa amalize utamu was tori. Anaamua kula mic “hata mimi licha ya kunistua, rahis na bi mkubwa wake wameniacha kinywa wazi hasa kwenye kaya hii ya wabinafsi, waroho, wachoyo, wajivuni na malimbukeni wanaopenda kukimbilia Ulaya kwenda kupima mafua ukiachia mbali wengine kupeleka hata wanyama wao kama paka na mbwa kutibiwa kule kwa kodi ya wachovu wa kaya hii.” Anakohoa kidogo na kuendelea “hakika big ameweka historia ya aina yake ya kubana matumizi na kuwa mzalendo wa maneno na matendo. Lazima kijiwe tutafute namna ya kukutana naye na kumpa ushauri kuhusu kuwapiga marufuku wa chini yake waliozoea kutumbua njuluku zetu kwenda kujiangalia afya zao.”
            Mheshimiwa Bwege naye anaweka guu “nakubaliana na wasemaji mliotangulia. Lazima rahis apige marufuku wakubwa uchwara kwenda ughaibuni kuunguza njuluku zetu. Hata hivyo, kwa kitendo cha mkewe kulazwa kwenye hospitali uchwara kama hii, ni katazo la nguvu kwa wenye akili. Najua; wapo watakaojifanya kutoelewa somo na kutaka waendelee na mazoea yao ya kishenzi na kilafi na kibinafsi. Nadhani hili ni suto kwa wote walioshindwa uzalendo wakaishia kuuhubiri majukwaani wakati wakiupiga mtama kwa vitendo nyuma ya pazia.”
            Mpemba naye anaamua kula mic “yupo jamaa yangu alonitonya kuwa huyu jamaa hata wale aniowaongoza bado hawajamwelewa. Huyu rafiki yangu alonitonya asema alisoma na dokta Kanywaji. Asema kuwa jamaa ni mtu wa vitendo zaidi ya maneno na wala si nnafiki wala mpenda sifa. Hamkuona alivoita daraja la Kigamboni mzee Nchoga badala ya kupendekezewa liitwe jinale? Je walo chiniye wanfahamu haya aniyotenda au wangoja watumbuliwe?”
            “Nyie mnaongelea hili tendo la nkewe kulazwa Muhimbii. Mbona kuna jamaa alinitonya hivi karibuni kuwa hata watoto wake wanasoma hapa kayani na si ughaibuni ukiachia mbali kuwatolea nje jamaa zake wanaotaka kutumia nafasi yake kujitajirisha? Angalia hata bi mkubwa aliyelazwa Muhimbii. Hana NGO kama wezi waliopita walivyozoea kutumia afisi ya rahis kujiingizia utajiri wa haraka. Huyu jamaa, kama wabongo watamwelewa, watanufaika,” anazoza mzee Maneno.
            Sofia Lion aka Kanungaembe anakwanyua mic  “nakuunga mkono kaka Maneno. Huyu dada yetu si mpenda utajiri kama wenzake waliomtangulia. Nawajua wakina mama. Angeweza kumlazimisha mumewe aunde NGO; hata kwenda kutibiwa nje ikizingatiwa kuwa kisheria ana haki ya kufanya hivyo. Nadhani dada yangu anaelewa anachofanya mumewe na kukiunga mkono kwa moyo wote na kwa vitendo kama alivyoonyesha kwa kukubali kulazwa Muhimbi. Si mchezo; ni somo la kutosha kwa wenye akili kusema ule ukweli.”
            Kanji hangoji Sofia amalize. Anamchomekea “Mimi iko sangaa san asana. Iko ona vatu kuba mingi nakwenda Bombei. Hii mama Kufuli natoa somo kuba sana kama ile iko chini ya zee najua nini anawofanya witu yake. Hii mana iko nakuna mimi kweli kweli; na nahesimu na kupenda yeye sana. Kesho takwenda jamatini na kuambia venzangu tuombee yeye afya jema sana.”
            Mchunguliaji ambaye huwa hana tabia ya kuchangia anakula mic “Kanji umenikumbusha. Sasa utasikia matapeli wa majoho wa ndani na nje ya kaya wakiandaa mikesha ya kumuombea wakati ukweli watataka kumtumia kujipatia ujiko na kujenga ukaribu naye ili wafanikishe utapeli wao. Mimi nawapongeza madaktari wa Muhimbii ambao hawakumwangusha kiongozi wetu. Pia nitumie fursa hii kutaka kijiwe kipange mkutano na dk Kanywaji ili kumtaka apige marufuku utumiaji wa mashangingi kayani. ”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si ukapita msafara wa magari wa Mama Kanywaji akitokea hospitali. Acha tuukimbize lau tumpe mkono wa pole. Kama si mataa kutukatili, huenda tungempa salamu zetu kwenda kwa mumewe kuhusu kupiga marufuku kwa malimbukeni kwenda kutibiwa ughaibuni utadhani walizaliwa na kulelewa kule wakati wengi wao walibebwa kwenye ngozi na mbuzi na kunywa kukuzwa na maji ya madimbwi waliyozoea kushea na ngiri na nguruwe huko madongo poromoka walikozaliwa.
Chanzo:  Tanzania Daima Jumatano leo.
↧
↧

Kama Magufuli hataki kuchimbua makaburi anyamaze

November 16, 2016, 5:33 am
≫ Next: How the West Depends on Africa but not vice versa
≪ Previous: Kijiwe champongeza Dk Kanywaji na mkewe
$
0
0

 Image result for photos of mafisadi tanzania
          Hivi karibuni, rais John Pombe Magufuli alikutana na waandishi wa habari katika siku ya kuadhimisha mwaka mmoja wa kuwepo kwake madarakani. Baada ya kuongea na waandishi wa habari, rais aliulizwa swali kuhusiana na mategemeo yake alipoingia madarakani.Akijibu swali aliloulizwa na mwandishi wa habari aitwaye Anna Kwambaza kuhusu mambo aliyoyakuta ikulu kama yalikuwa sawa na mategemeo yake, rais Magufuli, pamoja na majibu marefu, alikaririwa na akisema “nimeshughulikia changamoto mbalimbali lakini siwezi kuyafukuwa makaburi yote; kwa sababu kuna mengine nitashindwa kuyafunika, sikuja kufukua makaburi nataka kuanza na yale niliyoyakuta ili tujenge Tanzania yetu.” Hapa alimaanisha madudu aliyoyakuta Ikulu kama yalivyotendwa ima na watangulizi wake au yalivyovumiliwa kama kashfa mbali mbali ambazo zimelitikisa taifa kwa muda mrefu. Aliendelea mbele kutoa mfano kuwa ilifikia mahali ambapo meli zipatazo 60 zilitia nanga bandarini na kutoweka bila kulipa ushuru wala kuingizwa kwenye kumbukumbu yoyote. Hii ina maana kuwa nchi ilikuwa ikichezewa hakuna mfano. Je kama anachukizwa na uhujumu huu wa taifa, anashindwa nini kuunda tume ya kuchunguza kashfa hii na kuwabaini walioutenda na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria hata kukamata mali zao? Je waliotenda uovu huu hawajulikani? Je hili nalo ni kaburi analoweza kulifukua akashindwa kulifukia?
            Kwa wanaojua namna Magufuli anavyojitahidi kuelezea uovu alioukuta kwenye serikali,  wapo wanaosema kuwa makaburi anayomaanisha Magufuli, ima unaweza kuwa uchafu wa watangulizi wake au hata wao wenyewe hasa ikizingatiwa kuwa ikulu kunaishi watu . Pia wapo wanaodhani kuwa rais anamaanisha kuwa mtangulizi wake alifuja madaraka kiasi cha nchi kufikia kujiendea kama vile hapakuwa na serikali wala kiongozi wa serikali. Hii inaweza kuwa kweli au vinginevyo. Yote inategemea namna unavyoliangalia suala hili na namna unavyotafsiri na kutathmini utendaji wa tawala zilizotangulia.  Maana, kama utaangalia ukweli wa mambo kwa kuzingatia ukweli na hali halisi vitokanavyo na utawala uliopita, utapata jibu kuwa hapa kuna tatizo tena kubwa. Kinachogomba hapa ni ukweli kuwa ni kwanini Magufuli alikuwa wa kwanza kumtetea mtangulizi wake na wenzake hata wale wanaojulikana kubariki uhujumu wa taifa kwa muda mrefu ukiachia mbali ufujaji wa fedha na mali za umma kama kweli anaamisha kuweka nchi kwenye mstari kama ambavyo amekaririwa mara nyingi akisema? Je kama rais mwenye vyombo vyote vya dola analalamika na kuishia kukiri kushindwa, amechaguliwa kufanya nini? Je hao wananchi wa kawaida ambao ndiyo waathirika wakubwa wasemeje au kufanya nini? wapo wanaodhani kuwa ima rais ayafukue makaburi na wananchi watamsaidia kuyafukia au ajinyamazie na kuchapa kazi pale anapoweza badala ya kutumikia mabwana wawili; yaani wananchi na hao wakubwa wa hovyo anaowalinda kwa kugopa kufukua makaburi wakati yanajulikana yamejaa uoza unaonuka?
            Bila kupambana na ufisadi bila kuwa na simile, Magufuli atajipiga mtama mwenyewe. Kwa vile amekiri kuwa amekuwa serikalini kwa zaidi ya miaka 20, anajua kila kitu na vipi kila kitu kiliharibika. Mfano, kuna kashfa zinazojulikana kama Escrow, UDA, TICTS, na nyingine nyingi tu zinazojulikana.
            Japo hataki kuchimbua makaburi kwa kushindwa kuyafukia, inakuwaje anaruhusu makaburi yaendelee kuwatesa wasio na hatia? Tuna makaburi ambayo yanachimbuka na kufikika hasa kama atawashirikisha wananchi na taasisi zake. Kwanini, kwa mfano, tusichimbue makaburi kama NBC, Richmond, SUKITA, Meremeta, Kagoda, UDA, DART, EPA, Escrow na mengine mengi ili kuepusha vifo vya watanzania wasio na hatia ukiachia mbali waliokwishafishwa na hayo makaburi? Je kama rais mwenye kila taasisi anaogopa makaburi, ataweza kuwakabili mafisadi wenyewe wachimba makaburi ya kufichia mali zetu? Kama Magufuli ameshindwa kuchimbua makaburi, basi ajitoe na kuwaachia wenye ujasiri wa kuweza kuyachimbua makaburi na kuyafunika. Je kwanini anaogopa makaburi? Atawezaje walio hai kama vile wauza unga, majangili, mafisadi kila aina wenye kuendelea kushikilia mitandao yao ya kihalifu?
            Alipoulizwa kuhusiana na kurejea mchakato wa Katiba Mpya, Magufuli aliogopa tena kugusa kaburi kwa kusema “tutengeneze nchi kwanza, nimezunguka nchi nzima wakati wa kampeni sikuzungumzia Katiba Mpya; kwa hiyo katiba zinaweza kuwa nyingi tu lakini kwa sasa mniachwe ninyooshe nchi kwanza.” Hapa nilishindwa kumwelewa Magufuli hasa ikizingatiwa kuwa Katiba Mpya iliyofishwa na mafisadi ililenga kupambana na ufisadi na kujenga taifa la uwajibikaji. Magufuli anapaswa kufahamu kuwa nchi si mali yake binafsi. Hawezi kuinyoosha kwa mapenzi yake bila kuwa na sheria inayomsaidia kufanya hivyo. Kama kweli anamaanisha anayosema, hana budi kurejesha mchakato wa Katiba Mpya kama watanzania walio wengi wanavyotaka badala ya kutoa visingizio. Lazima tujenge nchi kikatiba na si kwa kutegemea usongo wa mtu mmoja yaani rais badala ya Katiba Mpya ambayo ililenga kujenga taasisi zenye nguvu badala ya watu wenye nguvu katika kuendesha nchi. rais wa Marekani Barack Obama aliwahi kusema kuwa Afrika ahitaji mabwana au strong men bali taasisi imara yaani strong institutions. Na Tanzania kadhalika, inahitaji Katiba Mpya yenye nguvu badala ya rais mwenye nguvu na utashi wa kufanya atakavyo. Kama rais anaogopa kuchimbua makaburi kwa vile hawezi kuyafunika, awaachie wananchi wamasaidi kayafunika au ajinyamazie tu.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
↧

How the West Depends on Africa but not vice versa

November 16, 2016, 5:12 pm
≫ Next: Exiting the ICC: This is Lovely
≪ Previous: Kama Magufuli hataki kuchimbua makaburi anyamaze
$
0
0

↧

Exiting the ICC: This is Lovely

November 17, 2016, 4:59 am
≫ Next: Mlevi afuta safari kwenda kutibiwa Ughaibuni
≪ Previous: How the West Depends on Africa but not vice versa
$
0
0
source: Daily Nation (17 November 2016).
↧
Search

Mlevi afuta safari kwenda kutibiwa Ughaibuni

November 19, 2016, 2:33 am
≫ Next: Je Tanzania inao wageni wanaohodhi ardhi wangapi?
≪ Previous: Exiting the ICC: This is Lovely
$
0
0

 
            Baada ya rais Joni Kanywaji Makufuli kuonekana kwenye hospitali ya kaya ya Muhimbiza akimjulia hali mshirika wake wa bedroom, Bi mkubwa Jane, mlevi ambaye bi mkubwa wangu alikuwa akitarajiwa kuondoka kayani kwenda kutibiwa ughaibuni nilijihisi kushushuka na kuona aibu. Nilipiga moyo kondo na kujisuta; ndipo nilipoamua kumkabili Bi Mkubwa wangu Mama Domokubwa kumpasha kuwa hatakwenda kutibiwa ughaibuni.  Kama kawaida yake, aliamka na kunikaba shati kuuliza kulikoni naongea kama hamnazo. Alidhani wazo hili lilisababishwa na mma na yale majani ninayovuta. Baada ya kuninusa na kukuta sina harufu ya zali lolote ilibidi aniachie. Alijifunga kibwebwe na kushika kiuno. Aliuliza tena “we baba Shikaadabu, unayosema ni kweli au umeanza kunitania siku hizi?” nilimjibu kwa kumpa gazeti la Sema Nao la siku ile lililobeba picha ya Bi Nkubwa Jane akiwa kwenye lango la kutokea la  wodi ya Sewa al Haji. Stori ni ndefu  na ina mivutano na misutano kibao.
            Kwa ufupi, tokana na somo nililopata tokana na kitendo cha Bi Nkubwa Jane kupiga mbonji kwenye Hospitali uchwara, rasmi na wazi wazi, natangaza rasmi kwa walevi wote. Mshirika wangu wa bedroom hatakwenda ughaibuni kutibiwa wala kuchekiwa afya yake baadaye. Badala yake atakwenda kutibiwa Muhimbiza; na siku zote zijazo, atakuwa akichekiwa afya yake pale. Nadhani hii licha ya kuwa kuunga mkono spirit ya rahis, ni kutaka kuwaaminisha walevi ninaowaongoza kuwa ninasema ninayotenda na kutenda ninayosema kuhusiana na uzalendo na kuacha ulimbukeni na kujitukuza kana kwamba hakuna atakayenyotoka roho. Wangapi tumeshuhudia wakienda kutibiwa ughaibuni na kurejea kwenye jeneza? Hakuna kusiko na kifo.
            Kitendo hiki ninachopanga kufanya kitashangaza wengi wapenzi na wabaya wangu. Ukiachia bi mkubwa kwenda kutibiwa Muhimbiza, kuanzia sasa nitaagiza walevi wote wawe wakubwa au wadogo kuchekiwa afya zao kayani na si ughaibuni. Nadhani hii itawasaidia wanaohujumu huduma za jamii kuacha kufanya hivyo; kwa vile watakuwa wakijiumiza wenyewe baada ya kuziba uchochoro wa kuzihujumu na kukimbilia ughaibuni kuunguza kodi za walevi. Mbali na hilo, nitaamuru walevi wote kuacha kupwakia vitu vya nje; na badala yake nitawaamuru watumie vya kayani ili kukuza uchumi wetu.
            Pili, msishangae kusikia nikitoa amri kuwa hata vitegemezi vya walevi wote visomee kayani badala ya kupelekwa ughaibuni na kurejea na kufanya kazi kayani. Kama kuna wazazi wanaoogopa vigegemezi vyao kusomea kayani, kwanini waviamini kufanya kazi kayani? Nadhani na hii itasaidia kuwapa somo wale wanaohujumu elimu kwa kutegemea kutumia njuluku wanazopiga kupeleka vitegemezi vyao ughaibuni. Mbona biggie wetu wote waliosomea hapa kayani na wameweza kuukata wakati wengi wa waliosomea ughaibuni wengine tunawaona wakisuasua kisiasa?
            Tatu, tokana na mfano wa rahis ambao bila shaka alidesa toka kwa walevi kama sisi ambao hujinywea mataputapu ya hapa kaya badala ya kunywa wine, whisk na vinywaji vya kigeni, nina imani kuwa hata mahoteli yetu yanayoitwa ya kitalii yatajifunza hili toka kwetu. Kwa walevi ulevi ni ulevi. Unywe mimaa ya kigeni au ya kienyeji mwisho wa siku wote mtalewa na kuangusha magari, simple and clear au vipi?
            Nne, lazima tukubaliane hata kama hatutaki. Wakati wa wanene kwenda kuchekiwa mafua ughaibuni lazima ugeuke historia. Kuna mlevi mmoja alituacha hoi; alipodai kuwa kuna wakubwa walifikia makufuru hata ya kupeleka mbwa na paka wao ughaibuni kuchekiwa afya kwa kufuja kodi za walevi waliopigika ile mbaya. Hawa wangekuwa chini ya utawala wangu wangekula shaba kama siyo kutimuliwa kibarua ili wakarejee huko madongo poromoka walikotokea.
            Tano, naona hata wakati wa kupunguza mashangingi ya wanene umefika. Kwani, haiigii akilini kwa kaya ya wachovu kuendelea kununua mishangingi hata ya kupelekea mbwa kliniki na vitegemezi vya wanene shuleni. Tunamkomoa nani zaidi ya sisi wenyewe?
            Naona mhariri anaanza kusonya na kupiga kipenga cha kuniondoa dimbani. Acha niwaageni kwa kuwaomba mzingatie aya hizi nilizotoa mimi mtume wa walevi wa kaya hii. Achene ulimbukeni, ubinafsi na roho mbaya ya kufuja mali na njuluku za walevi kwenda kuchekiwa ughaibuni. 
Chanzo: Nipahe Jumamosi leo.
↧
↧

Je Tanzania inao wageni wanaohodhi ardhi wangapi?

November 19, 2016, 4:17 pm
≫ Next: Magufuli unangoja nini kumtumbua Makonda?
≪ Previous: Mlevi afuta safari kwenda kutibiwa Ughaibuni
$
0
0

 
            Hakuna ubishi. Chini ya utawala rais mstaafu Benjamin Mkapa, Tanzania ilipwakia uwekezaji bila maandalizi wala ujuzi wa kile ulichokuwa ukiingia. Mkapa atabaki kwenye vitabu vya historia ya Tanzania kama rais aliyeuza nchi kwa wawekezaji. Hili unaweza kuliona kwenye kashfa zilizohusisha uwekezaji zilizofumka wakati wa utawala wake. Jikumbushe iliyokuwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) iliyouzwa kwa ABSA Group ya Afrika Kusini kwa bei ya kutupwa na kifisadi. Rejea mdororo wa Shirika la Umeme la Taifa (TANESCO) lililowekwa chini ya uendeshaji wa kampuni ya Afrika Kusini. Rejea kuuzwa kwa viwanda vingi vilivyoishia kuwa mabohari na vingine kunyofolowa vifaa hadi juzi tu rais John Magufuli alipoamuru wenye kuvifuja kuviendeleza kabla hajavitwaa.
            Kwa ufupi, uwekezaji chini ya Mkapa ulikuwa ni wa kijambazi na kifisadi uliotokana na rushwa ambao uliliingiza taifa kwenye mdororo wa kiuchumi jambo ambalo baadaye Mkapa alijutia. Alilwahi kukaririwa akisema “kwenye uongozi wangu kitu ambacho mpaka sasa ninajuitia ni kuanzisha sera ya ubinafsishaji na kushindwa kuweka mfumo au chombo cha kuudhibiti.”  Kwa kushindwa kuudhibiti uwekezaji, Mkapa alijenga tabia chafu ya kuabudia wageni ambao kwao wanasifika kuwabagua watu weusi.
            Mbali na Mkapa, utawala wa Jakaya Kikwete ndiyo ulivuruga kila kitu. Kwani, Kikwete alipokuwa akifanya kampeni, aliahidi kurekebisha mikataba ya uwekezaji. Hata hivyo, baada ya kuingia madarakani wala hakufanya hivyo. Badala yake alianzisha utawala wa hovyo ambao wengi waliuona kama uholela ambao uliiweka nchi kwenye autopilot kwa miaka yote kumi aliyokuwa madarakani akisifika kwa kuizunguka dunia akiandamana na marafiki na wapambe wasio na umuhimu kiasi cha kutunisha deni la taifa.
            Tukiacha na tawala zilizopita ambazo hazina lolote la maana kwa sasa, tuangalia hali ilivyo kwa sasa.
            Mosi, chini ya kivuli cha uwekezaji, kumekuwapo na tabia ya kuendekeza njaa kiasi cha maafisa wa serikali kugeuka makuwadi na vijakazi wa wawekezaji. Wamekuwa wakiwasaidia kukwepa kodi na kuingia mikataba ya kipumbavu kama mkataba wa TICTS ambao rais Magufuli alitaka ubadilishwe hivi karibuni badala ya kuubatilisha na kuwachukulia sheria walioingia mkataba huu wa hovyo.
            Pili, tumeendelea kuwa na mfumo mbovu wa udhibiti wa mali za umma. Mfano wa hivi karibuni ni kufutwa hati za umilki ardhi kwa Hamant Patel ambaye alighushi vyeti vya kuzaliwa na kujitwalia ardhi kinyume cha sheria. Je huyu Patel, hata kama angekuwa mtanzania wa kuzaliwa, aliruhusiwaje kuhodhi ardhi kila mahali? Je tunao patel wangapi walioodhi ardhi yetu na kuifanyia biashara huku wakiishi nje wakati hakuna mswahili anaweza kupata hata inchi moja huko watokako?
            Kumekuwapo na ukurupukaji katika kushughulia kadhia zinazotokana na uwekezaji na wizi mwingine wa mali na raslimali za umma. Mfano, tunaambiwa Patel amefutia hati. Je alikamatwa na kujibu tuhuma? Je waliomwezesha wamebainiwa, kukamatwa na kushughulikiwa?
            Nne, je nini kifanyike? Fanyeni ukaguzi mpya wa ardhi na raslimali zote ambazo majambazi wa kigeni wamezoea kuzitumia kukopea na kuishi ughaibuni kwa starehe. Ni bahati mbaya kuwa taifa letu lina tatizo la kusahau na kutojifunza kutokana na historia na makosa yake. Uozefu unaonyesha; hatukujifunza tokana na kashfa na hujuma ya Chavda aliyemilkishwa mashamba ya mkonge akaishia kuyatumia kujipatia mikopo na kutoroka nchi.
            Tano, tujibu maswali makuuu yafuatayo:
            Mosi, ilikuwaje huyu Patel hakuitwa na kukamatwa kwa makosa ya kujipatia ardhi na nyaraka kinyume cha sheria ili lau aonje joto ya jiwe na liwe somo kwa wahalifu wengine?  Bila kuwa na kuwaadhibu wahalifu waliokwishathibitika, tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu.
            Pili, je tunao majambazi kama hawa kiasi gani nchini wakichezea mali zetu wakati watu wetu wanaendelea kuangamia kwa ujinga na umaskini?
            Tatu, je ni nani hao waliompatia nyaraka na kumpa umilki wa ardhi? Haya ni maswali ambayo yalipaswa kujibiwa kabla ya kumstua mhalifu huyu. Je waliochukua hatua hii ya pupa na hasara kwa taifa hawakujua vitu rahisi kama hivi; au kuna namna kama siyo watu wasio na sifa na ujuzi kupewa nyadhifa nyeti kama hizi?
            Nne, je tutaendelea kuwa shamba la bibi hadi lini? Inashangaza kuona taifa lililojaliwa raslimali lukuki kuzidiwa hata na viinchi vidogo na visivyo na raslimali hata nusu yetu.
            Tano, je nini kifanyike? Kagueni hati zote za kuzaliwa za watanzania. Mchezo wa wageni hasa wahindi kuja kununua vyeti vya kuzaliwa nchini ukiachia mbali paspoti ni biashara inayojulikana kuwapo muda mrefu tena wakisaidiwa na watanzania wenzetu waroho umezidi kuzoeleka kiasi cha kuwa janga la kitaifa. Nadhani tunapaswa kupambana na genge hili na kulitokomeza kwa kuwafunga walioko nyuma yake vifungo vya maisha ili liwe somo kwa wengine.
            Sita, tungeni sheria kali ya kuhakikisha wanaokamatwa na mawakala wao wanafia gerezani. Bila kuwa na sheria kali za kupambana na jinai hii, hata hii amani tunayojivunia itatokea. Wananchi watakapojua kinachoendelea, watajichukulia sheria mkononi. Tumeishasikia wengi wakivamia mashamba na kujitwalia baada ya kugundua yalichukuliwa kifisadi.
Je namna hii twaweza kusonga mbele kiuchumi wakati ardhi na mali zetu zinatwaliwa na mahalifu wa kigeni na kuacha watu wetu wakiendelea kuteketea kwa umaskini? Je tunao akina Patel wangapi?
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
↧

Magufuli unangoja nini kumtumbua Makonda?

November 19, 2016, 4:19 pm
≫ Next: Kijiwe chashangaa wanaoshupalia njuluku ya tetemeko
≪ Previous: Je Tanzania inao wageni wanaohodhi ardhi wangapi?
$
0
0
         Mheshimiwa rais John Pombe Magufuli,
                 Najua unajua kuwa hivi karibuni Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makond alitoa mpya ya kufungia mwaka.Makonda alikaririwa na vyombo vya habari akidai kuna wafanyabiashara wa shisha (kumradhi sijui maana yake) wapatao 10 waliomwendea na kutaka kumhonga shilingi 5,000,000 kila mwezi kila mmoja akakataa.  Madai haya, licha ya kushangaza, yamezua maswali mengi kuliko majibu. Je ni kweli kuwa Makonda alikataa rushwa hii au inaweza kujenga dhana kuwa alisema haya ili aonekane safi na kupata sifa kirahisi?  Mosi, tokana na uzito wa shutuma hizi, basi wengi wangetaka Makonda awataje hadharani wahusika ili sheria ichukue mkondo wake. Pia ingekuwa vyema Makonda aeleze ni kwanini hakuwawekea mtego wakakamatwa?
Pili, Makonda, awaombe radhi aliowatuhumu bila ushahidi wala sababu za msingi zaidi ya kile kinachoweza kutafsiriwa kama kutaka kujijengea umaarufu kwa kuwachafua wengine. Maana kufanya hivyo kunawaonyesha kama wala rushwa na mawakala wa shisha bila sababu na ushahidi vya kutosha. Nitashangaa kama wahanga hawatamchukulia hatua za kisheria Makonda. Wasipofanya hivyo, watakuwa wanathibitisha ukweli wa madai ya Makonda.
Tatu, je kwanini Makonda, kama hakuwa na maslahi na biashara hiyo aliamua kuwaficha wahusika wakati akijua kuwa ni wajibu wa kila mtanzania kulipoti kosa la jinai anaposhuhudia ima likitendeka au likiwa katika harakati za kutendeka?
Nne, je kama mkuu wa mkoa kama Makonda analalamika lalamika, hao wa chini–ambao wengi wao ni waathirika wa jinai hii–wafanye nini?
Tano, je Makonda huwa anajitahidi kuruhusu kinywa na ubongo viwasiliane kabla ya kunena; au ndiyo hayo hayo ya kujisemea kila kinachotoka ima kujijenga, kujifurahisha na kuifurahisha hadhira yake?
Sita, kama Makonda atashindwa kuwataja wahusika, basi awajibishwe mara moja ima kwa kuwaficha wahalifu au kutaka kuuongopea umma kwa faida binafsi. Hatuwezi kuendelea na kuuzoea mchezo huu ambao madhara yake yanaweza kuwa makubwa huko tuendako. Kwa kauli kama hizi, umma unaweza kuishiwa imani na serikali, jambo ambalo si jema kwa nchi.
Saba, hata hivyo, Makonda ana bahati kuwa aliyemweleza, yaani waziri mkuu Kassim Majaliwa alichukulia tuhuma zake kimzahamzaha kama si kumuonea huruma na kumuepusha na aibu. Vinginevyo, Waziri Mkuu–kama naye angeamua kuwajibika kwa wadhifa wake–bila shaka alipaswa kumtaka awataje wahusika au kutoa kueleza ni kwanini hakuvitaarifu vyombo husika ili viwashughulikie.  Hapa napo Waziri Mkuu alionyesha udhaifu mkubwa kiutendaji.  Nadhani aliyosema Makonda, kama angeyasema mbele yako, ungemtaka awataje pale pale vinginevyo atumbuliwe; vinginevyo angetumbuliwa yeye. Rejea ulivyokataa taarifa, tena kwenye msiba, kuwa meya wa zamani wa jiji la Dar es Salaam, Didas Masaburi alikuwa na mke mmoja wakati alikuwa nao wengi tu.
Nane, je fungate ya Makonda inaanza kuisha kiasi cha kuanza kufichua kilichoko nyuma ya pazia ya Makonda waliyezoea kumuona watanzania? Maana madai ya Makonda; na namna alivyoshughulikia hii rushwa ni ya ajabu na ushahidi kuwa kuna tatizo tena kubwa tu.
Tisa, ikumbukwe. Hii si mara ya kwanza Makonda kulalamika bila kufuata hata utaratibu. Nani amesahau namna alivyomchomea utambi Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam wa zamani marehemu Wilson Kabwe badala ya kufuata utaratibu? Nani amesahau Makonda alivyowahi kuwaweka ndani watumishi wa Manispaa ya Kinondoni?
Kumi, mchezo wa kujisemea na kutoa madai ya ajabu si jambo jipya kwa baadhi ya watendaji wa juu wa serikali ya awamu ya tano. Rejea hapo mnamo mwezi Machi mwaka huu waziri wa Ardhi, William Lukuvi, kama Makonda, alikuja na madai kuwa kuna wafanyabiashara wawili walanguzi wa ardhi walitaka kumhonga shilingi bilioni tano akazikataa bila kuwawekea mtego wakamatwe wala kuwa tayari kuwataja majina.
Hivi kweli Makonda hajui kuwa kumshawishi mtu tena kiongozi wa juu kama yeye kupokea rushwa ni kosa la jinai?  Je hapa Makonda haoni kuwa alitenda kosa la jinai kwa njia ya kutochukua hatua (omission) kama raia na kiongozi? Usomi wake sasa ni wa nini kama hajui vitu rahisi kama hivi? Tokana na ukali na kutenda haki vilivyoonyeshwa na serikali ya awamu ya tano, nakushauari umtumbue Makonda mara moja ili liwe somo kwa wengine wanaodhani vyeo ni sehemu ya kuchezea na kujifanyia mambo watakavyo hata kwa kukiuka wazi sheria. 
Nimalizie kwa kumtaka Makonda auambie umma ukweli na kwanini hakuchukua hatua kama si mnufaika wa jinai aliyoieleza. Hakuna haja ya kuwang’ang’ania viongozi wa aina hii hasa ikizingatiwa kuwa kuna watanzania wengi wenye sifa tosha. Huu hakika ni mtihani kwako hasa ikizingatiwa kuwa ulimtumbua Mkuu wa zamani wa Mkoa wa Shinyanga Anna Kilango Malecela kwa kueleza umma uongo. Itashangaza kama utamvumilia Makonda. Maana, hii itaonyesha kuwa kuna wasioguswa katika serikali ya awamu ya tano jambo ambalo si zuri na linaloweza kuchafua sifa nzuri ya seriakali husika katika kuwatumikia na kuwakomboa watanzania toka kwenye uovu na uoza uliokuwa umeanza kuzoeleka.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
↧

Kijiwe chashangaa wanaoshupalia njuluku ya tetemeko

November 23, 2016, 8:17 am
≫ Next: Miaka mitatu bila Dk Sengondo Mvungi
≪ Previous: Magufuli unangoja nini kumtumbua Makonda?
$
0
0

         
            Wiki jana baada ya vyombo vya umbea kusheheni malalamiko ya wahanga wa tetemeko kule kwa akina Nshomile, Kijiwe kimeamua kuingilia kati lau kutoa elimu na ushauri vya bure.
            Leo anayeanzisha mada ni Mipawa tokana na baadhi ya marafiki zake aliokwenda nao shule kukumbwa na tetemeko ikiwemo shule alikosomea kidato cha tano na sita kabla ya kwenda Ng’ambo kunyaka shahada zake nyingine. Anaonyesha gazeti la Rongorongo lenye kichwa cha habari “Wahanga wa Tetemeko waijia juu Lisirikali.”
            Anatongoa “mmeona hii kasheshe kati ya wahanga na akina Nshomile baada ya lisirikali kusema kuwa njuluku iliyokusanywa itaelekezwa kwenye ujenzi wa miundombinu badala ya mbavu za mbwa binafsi? Jamaa wanapokoma kama hawana akili nzuri.”
            “Kwa lisirikali la sasa watalia sana na wamechemsha. Si rahis keshasema kuwa si kazi ya lisirikali kunjengea mchovu; sasa wanadhani malalamiko yatasaidia,” anachomekea Mbwamwitu.
            Msomi Mkatatamaa anakula mic “hapa nakubaliana na lisirikali. Kwani miundombinu ni muhimu kuliko wachovu binafsi. Nadhani wanaolalamika–pamoja na kuwa ni haki yao kufanya hivyo–wanapaswa kujiuliza baadhi ya maswali hata kama si ya kufurahisha. Mfano, mbona mbavu zao za mbwa zilipopukutishwa na tetemeko, wengi licha ya kulilalamikia na kupata misaada toka kwa lisirikali hilo hilo wanaloliaani sasa walitegemea miundombinu hiyo hiyo hiyo kama vile mashule, barabara, kliniki na mahospitali kupata huduma za kwanza, kujihifadhi na hata baada ya hapo? Mnyonge mnyongeni; lakini haki yake mpeni jamani.”
             Kabla ya kuendelea Mgoshi Machungi anamchomekea na kusema “Kwei Mgoshi, shue ni bora kuiko ubavu wa mbwa wa mchovu binafsi.  Nadhani badaa ya kulaamika, waathiika wanapaswa kukaa na seikai na kuangalia namna ya kusaidiana akini siyo kuazimishana na kutoa laana bue.”
            Kapende aliyekuwa ndiyo anamaliza kusoma gazeti la Rongorongo anakatua mic, “nasikia lisirikali lilikusanya madafu kama bilioni 15 na ushei. Kwa wachovu maskini wanadhani hii njuluku ni kubwa na lukuki wasijue gharama ya miundombinu usipite. Hebu fikiria mfano kujenga barabara moja yenye urefu wa kilometa kumi toka njini Bukoba kwenda huko kwa waathirika ni bei gani?”
            Kabla ya kuendelea, Da Sofia Lion aka Kanungaembe anadakia “hapa hujaongelea shule, hospitali, zahanati, na miundombinu mingine. Hapa wajanja hawajapiga chao hasa ikizingatiwa kuwa kaya yetu ina ugonjwa wa kuwa na vitu hewa.”
            Leo inaonekana ni kuchomekea mtindo mmoja. Kwani kabla ya da Sofi kumaliza si Mchunguliaji anamchomekea akisema “sitashangaa kusikia kuna wahanga hewa, na madai hewa bila kusahau, misaada hewa. Mara hii wahanga wamesahau wapigaji waliokuwa wameishafungua akaunti kujipatia njuluku za dezo! Ama kweli kufa kufaana. Lazima na serikali iboreshe miundombiu yake hata kama ilikuwa imeishabomoka hata kabla ya tetemeko kuimalizia au vipi?”
            Kanji anaamua kula mic “Sahili iko penda sana lalamika sana. Sasa dugu yangu tetemeko naangusa jumbani yako veve lau sirkali diyo naangusa? Je kama sirkali haikotangaza tetemeko, hiyo saada veve iko weza pata bila sirkali tangaza na kusimamia ili janja chache isiibe saada?”
            Mpemba aliyekuwa kimya akisikiliza anaamua kula mic “mie ndhani watu wafanye tathmini kwanza. Pia waangalie kipi cha kupata kipaumbele kwanza yakhe. Huwezi jenga nyumba ya Shaame au Makame kabla ya kujenga shule wala hospitali ati. Hivi kama tetemeko likirejea, hawa wanaolalamika watanlalamikia nani kutaka nsaada kama siyo hiyo hiyo sirikali waniyoilaumu sasa? Hapa zahitajika busara na subra vinginevyo twaweza shikana uchawi na hilo siyo jibu ati.”
            Mheshimiwa Bwege anaamua kula mic “mie silaumu wahanga wala lisirikali. Naweza kusema tu kwa ufupi kuwa usawa huu wa kuadimika njuluku, kila mmoja analalamika hata wale waliozoea za kupiga na wavivu. Je kama hawa wanaolalamika hawajakumbwa na janga lolote zaidi ya kukatwa mirija yao, hawa wahanga wa tetemeko usawa huu unategemea wafanye nini? Nadhani lisirikali lingeacha ung’ang’anizi. Kama wahanga wataona kuwa mbavu zao za mbwa kwao ni muhimu kuliko miundombinu, basi ikae nao na kuwaelimisha juu ya nini kinahitajika kwanza badala ya kuwaacha Solemba wakilalamika. Nadhani hapa hakuna kilichoharibika zaidi ya mawasiliano haba. Kama wakubwa wa lisirikali watakutana na wahanga na kuwapa sababu za kutoa kipaumbele kwa miundombinu wataelewa na kukubali yaishe huku wakijipa matumaini na kungoja zamu yao au vipi?”
            Mgoshi Machungi anarejea na kukatua mic “hapa azima isiikai iseme ukwei vinginevyo wahanga watazani imekula ushwa kama yue bwana mdogo Makondakonda aiyewahifadhi wahaifu akijidai kakataa ushwa bila kueeza namda aivotaka kuhongwa njuuku iii aluhushu shisha.”
            Msomi aliyekuwa akibofya kisimu chake anamchomekea Mgoshi “sasa Mgoshi hili la dogo Makondakonda kuchemsha na kuramba mlungula linaingiaje au umechanganya madawa au vipi?”
            Mgosi anagundua alivyochemsha na kuamua kujitetea “kwei kaka nimechemsha. Unajua wakati mkizoza niikuwa namtumia meseji bi mkubwa Nesaa ujumbe kuwa aniandaie ie mboga ya kishambaa iitwayo kinyeto. Shamahani ndugu zangu kwa kuchemsha. Hizi simu nazo!”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si ikapiga radi! Acha tutoke mkuku tukidhani ni tetemeko jingine!
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
↧

Miaka mitatu bila Dk Sengondo Mvungi

November 26, 2016, 9:20 am
≫ Next: Nchi ya viwanda Escrow, UDA, NSSF nk wapi na wapi?
≪ Previous: Kijiwe chashangaa wanaoshupalia njuluku ya tetemeko
$
0
0
 
           Leo ni miaka mitatu na siku chache tangu Dk Sengodo Mvungi afariki dunia.  Kwanza, niwatahadharishe wasomaji wa safu hii. Makala hii nimeiandika nikiwa soba kabisa bila kupata kitu chochote. Hivyo, msishangae mkidhani nimedesa kwa mtu. Hii inaonyesha sura yangu ya pili ambayo wengi hawaijui. Hayo tuyaache.
            Japo Mvungi alizikwa, kuombolezwa hata kupendwa na wengi, sijui kama bado wengi hao wanamkumbuka. Sijui kama wanakumbuka yale mema yote aliyosimamia na kutenda.  Sijui kama wanamkumbuka kama moja wa watu waliosukuma taifa mbele taifa. Sijui kama kama ndani ya kipindi kifupi tu cha miaka mitatu aliyotoweka angesahaulika kirahisi hivi hasa kwa wale walioangusha kazi pevu aliyofanya. Kusema ukweli; kitendo kilichofanywa cha kuzika Katiba Mpya ni dharau ya aina yake kwa marehemu Dk Mvungi. Kwa utamaduni wa kiafrika, mja anapoaga dunia, waliosalia hupenda kuyaenzi yale aliyoyatenda hasa katika mwisho wa uhai wake.  Hata hivyo, tokana na dhuluma na dharau hii, sijui kama hao watukufu bado wana hamu naye kwa namna wanadamu tulivyo wasahaulifu kana kwamba kuna watakaoishi milele.  Dk Mvungi aliyefia nchini Afrika Kusini mnamo 21 Novemba, 2013 wakati akifanyiwa matibabu baada ya kushambuliwa na majambazi nyumbani kwake. Heri wangemwimbia wakamwachia uhai wake ili aendelee kulitumikia taifa lake na watu wake bila kinyongo wala kuchoka katika nafasi zote alizotumika nchini. 
            Kwa tunaomfahamu na kumkumbuka, Mvungi alikuwa msomi mbobezi wa sheria, mchangamfu, asiye na makuu ambaye angeweza kujichanganya na makapuku bila kujali hadhi yao kimaisha, mwanasiasa na mtetezi wa haki za binadamu wa kupigiwa mfano. Kituo cha Haki za Binadamu (LHRC) wanalifahamu hili na ni mashahidi tosha wa umahiri wa Mvungi katika kutetea haki za wanyongo. Mbali na hiyo, mchango wake katika kuandika Katiba Mpya iliyouawa na mafisadi haumithiliki ingawa umesahaulika kutokana na kuzikwa kwa katiba husika na majahiri wasiojua kuwa siku yao nao ipo. Wale waliofanya kazi naye kwenye tume hii wanajua umahiri na kujitoa mhanga kwake kwa niaba ya wenzake. Wale waliobahatika kukutana naye iwe ni kikazi au nje ya kazi, ni mashahidi tosha wanaoweza kumweleza marehemu Mvungi alivyokuwa mtu wa watu. Kwa maana hiyo, wengi walidhani; wenye mamlaka walilomteua kuwa mjumbe wa kamati ya kukusanya maoni ya wananchi ya Katiba Mpya wangeipitisha tena bila kuichafua na kuichakachua kama njia mojawapo ya kumuenzi mzalendo huyu mtoto wa taifa hili aliyelipenda bila shaka yoyote. Hata hivyo, hii haikuwa. Ni kiburi na kujilisha pepo kiasi gani? Kwani, wao wataishi au kudhulumu milele? Binadamu ni nini zaidi ya kuwa mavumbi yanayongoja kutawanyishwa na upepo na wadudu?
            Dhumuni ya kuandika waraka huu–licha ya kumkumbuka Mvungi angalau iwe faraja kwake, familia yake, marafiki zake na wapendwa wake–nalenda kumrejesha kwenye hadhira lau kutafakari urathi alioacha kama mwadamu muadilifu na mpenda na mtetea haki. Najua hawezi kujibu waraka wangu; lakini anaona. Kwani walichoua ni mwili si roho ya marehemu. Katika kumbukumbu yangu ya Dk Mvungi, licha ya kuongea na wasomaji, naongea na wenye madaraka watende haki kama sehemu ya kumuenzi Dk Mvungi aliyekuwa mpigania haki mahiri na asiyechoka.
            Pili, tupambane na ujambazi na kila aina ya jinai vilivyotamalaki nchini mwetu. Kwani, kilichomuua Mvungi si kingine bali ujambazi huu huu ambao utawala uliopita ulionekana kuridhika nao kiasi cha kuulea kutokana na serikali kuwa goigoi na iliyokuwa ikijiendesha bila uongozi imara na wenye visheni. Sasa mambo yamebadilika. Tuna serikali mpya yenye makali angalau. Tunawaomba wenye mamlaka waliopo kulifanyia kazi hili ili tusipoteze Dk Mvungi wengine ambao taifa linawahitaji. Hatutaongelea waliomuua Dk Mvungi kwa vile kesi iko mahakamani.
            Tatu, tupambane na ufisadi na ulafi wa kimfumo unaohamasisha wahalifu kutafuta utajiri wa haraka hata kwa kuwaua wenzao. Ningependa siku moja kila mtanzania aeleze alivyochuma mali zake ili wanaopata utajiri kwa njia haramu wataifishwe na kuwajibishwa kisheria jambo ambalo bila shaka litaondoa motisha wa baadhi ya wenzetu kutenda maovu kama, kuwadhuru, kuwaua na kuwaibia wenzao.
            Nne, katika kutenda haki kwa watanzania wote, tunapaswa kurejesha kanuni na maadili ya utumishi wa umma. Maana bila kanuni hizi tutapoteza muda kwa kutegemea ukereketwa wa viongozi wachache.
            Mwisho, napenda kuiomba jamii ya watanzania popote ilipo, imuenzi marehemu Mvungi kwa kupigania na kutenda haki; vitu ambavyo vilimtambulisha ulimwenguni. Pia tunaipa mkono wa rambirambi familia ya marehemu katika kuadhimisha miaka mitatu ya kifo cha Mvungi. Najua wao huadhimisha maisha ya marehemu kila sekunde, kila dakika, kila siku, kila wiki, kila mwezi na kila mwaka. Nawaombea faraja katika safari hii ngumu yenye kila majaribu na kukatisha tamaa. Faraja kubwa ni moja kuwa yeye alitangulia, sie tuko nyuma yake. Kwa wale waliozoea ulevi naomba wanisamehe. Huu ni msiba. Auhitaji utani hasa ikizingatiwa kuwakila nafsi itaonja mauti.
Chanzo: Nipashe Jumamosi leo.
↧
↧

Nchi ya viwanda Escrow, UDA, NSSF nk wapi na wapi?

November 27, 2016, 6:35 am
≫ Next: Kijiwe chamuunga mkono askofu Mokiwa
≪ Previous: Miaka mitatu bila Dk Sengondo Mvungi
$
0
0
         Baada ya rais John Pombe Magufuli kuingia madarakani na kukuta madudu na mdororor wa uchumi, alikuja na mipango ya kuifanya Tanzania nchi ya viwanda. Magufuli, pamoja na mengini, alilenga kutengeneza ajira, kufufua uchumi, kuwezesha watanzania kupata huduma safi na kufaidi raslimali za nchi yao na kuboroesha maisha ya watanzania.
            Pamoja na mipango na nia nzuri vya rais, kuna mambo yanapaswa kuwekwa wazi kabla ya kuendelea kujiaminisha kuwa tunaweza kujenga Tanzania ya Viwanda bila kuyakabili bila simile. Yafuatayo ni mambo yanayopaswa kuzingatiwa katika safari yetu ya kwenda nchi ya viwanda:
            Mosi, kwanza tuunde sera ya kitaifa ya viwanda bila kutegemea sera ya chama kinachotawala. Hapa lazima tubadili katiba na kutamka wapi Tanzania inapokwenda na itafanya hivyo vipi. Kwani, kwa sasa, sera ya viwanda ni ya kisiasa na si ya kiuchumi. Mpaka sasa si rahisi kuelezea Tanzania inatumia mfumo na sera zipi zaidi ya ujamaa unaoendelea kubakia kwenye katiba wakati haupo tena.
            Pili, lazima tuliandae taifa kwenda kwenye nchi ya viwanda. Mfano, tueleze tutakavyovuna nguvu kazi iliyopo na kutengeneza wataalamu wa kutufikisha kule. Hata nchi ya Ulaya zilipoamua kufanya mapinduzi ya viwanda (industrial revolution), pamoja na kutumia nguvu kazi ya bure ya watumwa, zilijiandaa kupata na kuvuna nguvu kazi hiyo. Kwa sasa utumwa haupo tena. Tuna watu wetu; tuwaandae na kuwatumia vilivyo. Kwani mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe. Je tumewaandaa wananchi wetu kwa kuijenga nchi ya viwanda au tutategemea wawekezaji wasioaminika na ambao wanaweza kuondoka wakati wowote maslahi yao yanapoguswa?
 Tatu, lazima tupambane na ufisadi kwa maana ya kupambana bila kubagua, kubangaiza, kuonea wala kupendelea.
            Nne, tuangalie kama sheria zetu zinapambana na ufisadi na wizi wa mali za umma na makosa yatokanayo na hayo. Kama hazifai tuzibadili au kutunga mpya na kufuta nyingine.
            Tano, tumifunze toka kwa nchi zilizotoka kwenye mazingira kama yetu. Kwani, nchi ya viwanda kama China haijengwi kwa woga na matamanio bali mipango madhubuti na ya makusudi.  Huwezi kujenga nchi ya viwanda wakati huandai maisha ya kuzalisha na kukusanya kodi vilivyo. Tunapaswa kuwashughulikia wote wanaotukwamisha na waliotukwamisha bila huruma. Hapa lazima wahusika wafilisiwe na watanzania wawe na mfumo wa kila mmoja kutoa taarifa za kodi na mapato kila mwaka ili kubaini wanaotuibia na kutukwamisha. Huwezi ukajenga nchi ya viwanda katikati ya kashfa kama EPA, Escrow, NSSF, UDA na nyingine nyingi ambazo karibu tawala zote zimeonyesha kuzigwaya au kuzivumilia kwa sababu wajuazo wahusika.    
            Sita, nchi ya viwanda inahitaji mtaji ambao nao unaibiwa na tunaangalia au kusuasua kushughulikia majizi yanayojulikana kwa sura na majina. Hivi kashfa tajwa hapo juu zilisababisha taifa hsara ya mabilioni mangapi? Je fedha hiyo ingejenga viwanda vingapi au kusaidia kuweka msingi wa viwanda nchini kama ingesimamiwa vizuri au kuwakamata wahusika wakairejesha?
             Saba, je tunahofia nini na tunamdanganya nani kwa kutaka kujenga nchi ya viwanda bila sera ya kitaifa iliyowekwa kwenye katiba ya nchi? Haiwezekani tukashughulikia kashfa ya NSSF kwa kuchagua. Inakuwaje, kwa mfano, aliyekuwa mkurugenzi mkuu wa NSSF ateuliwe balozi badala ya kuchunguzwa kusikia ana ushahidi na utetezi upi kuhusiana na kashfa iliyotendeka chini ya uangalizi wake?
            Nane, kama ilivyodokezwa hapo juu, China imepiga hatua kwa kasi ya ajabu kiuchumi kutokana na kasi ya ajabu katika kushughulikia ufisadi na wizi wa mali ya umma. Imeishafunga vigogo zaidi ya milioni moja tangu idhamirie kubadili mwelekeo wa maendeleo yake. Zamani nchini China ukiwa kwenye chama tawala basi umeula na huguswi sawa na ambavyo ilivyo nchini ambapo baadhi ya wazito wanatuhumiwa hata kusafirisha nyara za taifa ughaibuni na bado wako ofisini ukiachia wale waliotuhumiwa wazi wazi kujihusisha na mihadarati.
             Kwa mujibu  wa Kamati kuu ya Ukaguzi wa Nidhani ya China (CCDI), serikali ya China  imeanzisha kampeni tangu rais Xi Jinping  achukue usukani wa  Chama  Kikomunisti cha China (CCP) mwishoni mwa mwaka 2012, maafisa wa ngazi za juu 414,000 wameishawajibishwa na chama kwa ufisadi; na maafisa wapatao 201,600 walishashitakiwa. Mfano kwenye mkoa wa Shanxi, mmoja wa mikoa fisadimaaafisa wapatao 15,450 walipatikana na hatia mwaka jana ambalo ni ongezeko la aslimia 30 ikilinganishwa na mwaka 2013.  Kauli mbiu ya inaelezea hatua hii kama kuua chui na kupunga inzi.
            Tisa, ukiangalia maendeleo ya kupiga vita ufisadi iliyofikia China, kwetu ni kinyume. Tunaua inzi na kupunga mapapa. Vinginevyo walioko nyuma ya kashfa tajwa hapo juu wangekuwa wameishauwa na si kupungwa.
            Kumi, na mwisho, tunasisitiza kuwa lazima tubadili katiba na kuja na katiba mpya ya uwajibikaji na uchapa kazi badala ya kutegemea nguvu ya kisiasa chama au mtu mmoja. Nchi ya viwanja inajengwa na wananchi wote wanapotambua na kujua wanachotaka na wanachotaka kufanya.
Nashauri tuanzie kwa haya machache, pamoja na mengine, kuiandaa Tanzania kwenda kwenye nchi ya viwanda.
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili leo.
↧

Kijiwe chamuunga mkono askofu Mokiwa

November 30, 2016, 6:07 am
≫ Next: Makonda na Sirro wachunguzwe wote
≪ Previous: Nchi ya viwanda Escrow, UDA, NSSF nk wapi na wapi?
$
0
0
 
             Baada ya kuzidi kuongezeka kwa matapeli na wapigaji wanaotumia majoho, askofu Zaky Mokiwa ameamua kuwatolea uvivu. Ameripotiwa akitaka mamlaka kuwachunguza hasa aina ya mahubiri wanayotoa. Uzuri hili limetoka kwenye kinywa cha mwenzao ambaye hata hivyo siyo wa kujipachika wala kanjanja kama wale alishauri washughulikiwe.
            Mipawa ndiye anaanzisha mada baada ya kutua gazeti la Rongaronga mezani ambalo Mchunguliaji analidaka na kuanza kulibukua. Anauliza “wazee mnalisemeaje hili la kutaka wachungaji, wachunaji na wapigaji wanaotumia neno la Mungu kutuvuruga, kutunyonya, kutudanganya, kutuibia hata kutudhalilisha ambalo limetolewa na askofu wa kweli Zaky Mokiwa?”
            Kapende anakula mic “hili halina njadala. Lazima wajanja hawa wanaowarubuni na kuwaibia wajinga wetu wachunguzwe ndani na nje bila ya cha nsalie Ntume. Haiwezekeni kama kaya tukaendelea na aina hii ya ufisadi wa kiroho ulioshamiri uroho.”
            Mpemba anampoka mic Kapende na kuronga “hata mimi nakubaliana na pendekezo hili hasa wakati huu wa “Hapa Kazi Tu”. Kwani, waliachiwa na kujitajirisha huku wakiwasikinisha wajinga wengi walioharibikiwa maisha kutokana na elimu haba. Wanachofanya baadhi ya wachunaji waliojivisha majoho ni ufisadi, ujambazi na wizi wa wazi wazi. Lazima mahubiri yao yachunguzwe na wanaokiuka maadili, sheria na taratibu washughulikiwe mojawapo ikiwa ni kuwapiga marufuku hata kuwatupa lupango.”
            Msomi Mkatatamaa anakula mic “ushauri huu umekuja kwa wakati wake. Kwanini tuwawajibishe watumishi wa umma kama vile vihiyo, watumishi na wanafunzi hewa wakati tuna wachungaji wanaohubiri mahubiri hewa na hasi? Napendekeza wachunguze mapato kama ni ya kweli na kama sadaka zinatumika vizuri na si kupigia ulabu kama ilivyotokea  kwa mzee wa mipako  hadi akapayuka na kupakwa kinomi.’
            Anakohoa na kuendelea “wachunguze tabia binafsi maana wapo walevi, mafisadi, wazinzi na kila aina ya matapeli. Wachunguzwe elimu zao kubaini vilaza na vihiyo. Wachunguzwe biashara zao wapo wauza bwimbwi na utumiaji misamaha ya kodi kujineemesha kwa kupitisha bidhaa za wafanyabiashara wezi wanaowatumia. Wachunguzwe historia zao maana wengine hata si wana kaya bali wakimbizi wa kiuchumi toka kaya jirani. Hapa ni kuchunguzana ili kuepuka kuchuuzana kama ilivyokuwa chini ya tawala zandiki zillizopita ambazo nazo zinapaswa kuchunguzwa na kutumbuliwa bila huruma wala kulindana.”
            Mgoshi Machungi anakatua mic “ningependa nimchomekee askofu Mokiwa kwa kupanua wigo wa uchunguzi. Hapa lazima tiwachunguze hata maisha yao binafsi ikiwezekana tiwatoze kodi na kukagua shuhui zao. Napendekeza wakaguzi wa fedha za umma wawe wanawakagua hawa jamaa ii kuepuka kuendeea kuwabia wachovu watu na kutajiika wakati sisi tikipigika kwa ukapa. Niseme wazi. Nakubaiana na wae wanaoita huu kuwa aina mpya ya ufisadi na ujambazi wa kumtumia Mungu.”
            Kanji hajivungi. Anakwanyua mic “mimi iko sangaa sana. Naona chungaji hubiri lakini hapana nafanya kazi. At the end nakuwa tajir sana. Nazidi hata ile nafanya biasara. Sana napata wapi juluku? Iko uuza neno na kupata juluku au iko biasara nafanya sirini?”
            Mpemba anakamua “yakhe hapa unkuna kweli kweli. Hata mie nshangaa kuona watu wasiofanya kazi yoyote isipokuwa kupiga kelele kuishi kwenye mahekalu, kununua hata madege na kuishi maisha ya kikwasi. Hapa lazimu iwepo biashara waniyofanya nyuma ya pazia wallahi.”
            Da Sofia Lion aka Kanungaembe anampoka Mpemba mic na kudema “kumbe hamjui! Baada ya dokta Kanywaji kuwabana wapigaji, sasa dili limebakia kuwa kuanzisha madhehebu ya dini. Hapa ndipo hitajio la kuchunguza maisha yao binafsi linakuwa muhimu. Lazima wataje vyanzo vya mapato na matumizi yao hasa wakieleza zinapokwenda sadaka. Hamkuona mmoja alivyofikishwa kwa pilato akidaiwa kuiba bilioni 15 za waumini? Kimsingi, hawa hawana tofauti na waganga wa kienyeji. Hawahubiri kuchapa kazi, uadilifu wala ukweli bali uponyaji utadhani kaya nzima ni ya wagonjwa. Wapo matapeli wanaojifanya kuombea ndoa, biashara hata elimu bila kujua kuwa ufanisi wa mambo haya hutegemea juhudi na si maombi.”
            Kabla ya kuendelea Mbwamwitu anamchomekea da Sofi na kusema “wao wenyewe wanapaswa kuombewa kwa ushirikina na uganga wa kienyeji na uganga njaa wanavyofanya. Na niseme hapa.  Kama kweli kuna pepo, hawa hawataingia. Wataingiaje wakati wametengeneza pepo zao hapa duniani? Kama pepo hii ipo sitaingia kama nitwakuta hawa wezi wa majoho kusema ule ukweli.”
            Mheshimwa Bwege anapoka mic “msemayo ni kweli. Nakubaliana nawe Mbwamwitu. Hawa wezi walishajitengenezea pepo zao hapa hapa duniani kwa kuwaibia wachovu. Angalia migari, mijumba na wengine midege wanayoangusha wakati Yesu wanayemhubiri alikuwa kapuku wa kutupwa. Je wanamhubiri Yesu yupi zaidi ya farao tajiri mwenzao? Biashara ya kuchuna inalipa. Unajenga duka na kuliita nyumba ya ibada. Unaweka mabenchi na wajinga wanafurika kulipa kodi wakidhani ni sadaka. Miaka nenda rudi wanamchangia Mungu. Mungu gani maskini asiyejajirika pamoja na kupewa sadaka miaka yote hii. Je yeye atatoa lini? Haiwezekani Mungu akageuzwa pakacha lisiloshiba wakati ukweli Mungu mwenyewe ni hao hao wanaowanyonya wachovu wa kaya hii. Ama kweli wachovu hawa wanahitaji ulinzi wa lisirikali hata kama wanaibiwa kwa ujinga wao na kutojiamini.”
            Kijiwe kikiwa kinanoga si akapita mzee wa Upayuko akiwa amelewa chakari akitukana na kumwaga radhi! Acha tumtokee na kudai arejeshe chetu!
Chanzo: Tanzania Jumatano leo.
↧
Search

Makonda na Sirro wachunguzwe wote

November 30, 2016, 6:29 am
≫ Next: Bye bye Yahaya Jammeh
≪ Previous: Kijiwe chamuunga mkono askofu Mokiwa
$
0
0
            Kwanza niombe msamaha kwa kutowataarifu wasomaji kuwa nilikuwa na mpango wa kuendeleza makala ya wiki jana juu ya tuhuma za ulaji rushwa wa wazito wa mkoa wa Dar Es Salaam. Vyombo vya habari viliripoti kuwa Kamishina wa kipolisi, Simon Sirro, wa Jiji la Dar Es Salaam na RPC wa  Kinondoni, Susan Kaganda wanachunguzwa tokana na tuhuma zilizotolewa dhidi yao na Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Paul Makonda. Hili ni jambo ambalo ni jema–japo kuchunguzwa watuhumiwa bila kumchunguza Makonda itakuwa si kuwatendea haki makamanda hawa–ukiachia mbaliku kujenga mazingira kuwa kuna watu wasiogusika (untouchables) nchini. Tunasema; Makonda naye achunguzwe. Kwani, alionyesha uzembe na, unaweza kusema, ubabaishaji na kukwepa wajibu wake kama kiongozi wa ngazi ya juu na raia kwa kutoripoti makosa ya jinai yaliyokuwa yakitaka kutendeka kwa kumhushisha. Makonda, kama mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa, kwanini–kama hakuwa na maslahi kwenye kadhia hii–hakuchukua hatua kama vile kuripoti kwa waziri mkuu hata rais na badala yake akaishia kulalamika kama hapakuwa na namna au mvutano? Hili swali linajirudia kuliko mengine ili  kumpa picha msomaji afanye tathmini hata hitimisho lake.
            Pili, Makonda anapaswa abanwe awataje wahusika ili washughulikiwe na kueleza kwanini hakuwataja awali. Na hapa lazima tuwe wazi. Tusizugwe na watuhumiwa walioripotiwa na vyombo vya habari kukamatwa siku moja tu baada ya vyombo vya habari kuja juu. Kwanini wakamatwe siku moja baada ya tuhuma hizi kufichuliwa kama hakuna namna? Je mamlaka zilikuwa wapi siku zote hizi? Je hapa nani anatuchezea mahepe kati ya Makonda, Sirro na Kaganda? Hii maana yake ni kwamba watatu hawa, kwa sababu wajuazo wenyewe, walikuwa wanawaachia wauza shisha. Je, kama hakuna namna, ilikuwaje wawajibike sasa na si kabla? Maana, vyombo vya habari vimeripoti hivi karibuni kuwa watu watatu wamekamatwa kwa makosa yahusianayo na uuzaji shisha.
            Ukiachia maswali hayo mama, kuna mengine:
            Mosi, je tutaendelea kufanya kazi kwa namna ya kuzamia na kuchomeana hadi lini?
            Pili, je hawa watatu tu waliokamatwa wanatosha; au wahusika wanatafuta kutuliza hasira na shuku za wananchi ili waendelee na business as usual kama ilivyokuwa kabla ya kuchomeana utambi?
            Tatu, baada ya Makonda kumshutumu Sirro na mwenzake, je wao wanajitetea vipi lau wananchi wapime na kujua mbivu na mbichi ni ipi?
            Nne, je wawili hawa watakwenda mbele ya vyombo vya sheria ili kupata stahiki yao au watanyamaza na kuacha yapite ilhali kunyamaza kunaweza kutafsiriwa kama ukweli wa madai?
            Tano, je watatumia njia mbadala za ndani ya serikali na kuutangazia umma kilichofikiwa?
            Sita, kwa upande wa mamlaka zilizowateua, zitafanya kama ilivyokuwa kwa marehemu Wilson Kabwe? Yaani kuwawajibisha wahusika bila kusikiliza upande wa pili jambo ambalo litamfanya Makonda aonekane bora kuliko wenzake (better than thou) jambo ambalo si jema kwenye utumishi wa umma ambapo kila mtu ni sawa. Kama wawili hawa watatoa utetezi au maelezo yao, itakuwa vigumu kwa umma na hata wakubwa wao kubaini nani mkweli na nani muongo, nani mtafuta sifa na nani mchapakazi.
            Saba, je kuna mengine mengi yaliyofichwa nyuma ya utata huu unaoonekana kukiuka kanuni za utawala hata uongozi kwa kufanya mambo hovyo hovyo bila kufuata taratibu zilizowekwa na zinazojulikana? Hivi karibuni, mwandishi mmoja alishuku mbinu ya Makonda ya kumchafua Sirro kama njama ya kumzuia asiteuliwa IGP. Lisemwalo lipo; kama halipo laja. Hili nalo lapaswa kuchunguzwa.
             Nane, je kitendo cha Makonda kumuumbua Sirro na Kaganda hadharani si ushahidi kuwa baadhi ya watendaji wa serikali ya awamu ya tano, ima hawajui mipaka ya madaraka yao au hawajui hata wanachofanya kiasi cha kulimana hadharani tokana na wengine kupewa madaraka makubwa kuliko uwezo wao?
            Tisa, je huu si ushahidi kuwa serikali ya awamu ya tano haikushikamana (incohesive) sifa ambayo si nzuri kwa serikali ilijionyesha kuwa makini? Sijui kama akina Makonda wanalijua na kuliona hili hasa wakati huu ambapo wafanyakazi wanalalamikia kunyanyaswa na wateule wa rais.
            Kumi, tokana na tabia ya Makonda kuwa kujifanyia mambo atakavyo hata kwa kukiuka kanuni, wapo wanaodhani amepewa madaraka makubwa kuliko uwezo wake. Mfano, hivi karibuni, alionekana akiwadhalilisha baadhi ya watendaji kwa kudai wanaamini ushirikina badala ya kufanya kazi bila ushahidi. Kama haitoshi, alimkalisha kiti moto DMO wa Kigamboni mbele ya umma kana kwamba hakuna mechanisms za kushughulikia tatizo kama hili.
            Tuhitimishe kwa kuvitaka vyombo vya dola visimuongope yeyote tokana na cheo au ushawishi wake. Chunguzeni wote; ili ukweli na mengine ambayo yanaweza kuwa yamefichwa vijulikane. Kwani wahusika, licha ya kuwa viongozi wa ngazi ya juu, bado ni wanadamu wenye kila aina ya udhaifu ukiwemo uwezekano wa kushawishika kupokea rushwa hata kukomoana.
Chanzo: Tanzania Daima Jumatano leo.
↧

Bye bye Yahaya Jammeh

December 2, 2016, 6:04 am
≫ Next: Mlevi atathmini mwaka mmoja wa Makufuli
≪ Previous: Makonda na Sirro wachunguzwe wote
$
0
0

Gambian despot, Yahya Jammeh has lost an election he conducted himself It is now official that a tiny West African country of Gambia is now free from Jammeh's iron fist that misruled the country for over 22 years. The fall of Jammeh is a victory for Africa. It is a lesson to other despots such as Museveni and others that there is an end to everything. Nobody would think that Jammeh would fall in a peaceful way. Again, if you live by sword you will die by sword. Jammeh carried out a bloodless 22years ago. So, too, he has been sent packing peacefully. However, his human rights records are  apprehensible.


Bye bye bye bye bye Yahaya Jammeh.

Go Jammeh go ye Yahaya
Go without turning thy head back ever
The game is up and over sir
Go son of hell, a coward in your own right
Go Jammeh go down standing like a dolt
In flames go down like that
In a shame go even faster
Go go Jammeh go go and others will go

Museveni will go
Obiang will also go
Sassou-Nguesso will go
Kabila will follow
Derby too will pack and go
Kagame will go
Bashir soon will go
I am sure many will go
Mugabe is on the go
Afwerki will go
I am saying many will go
Big trees will fall
And Africa will glow

Go Jammeh go
Go the way Compaore went
Go please don't lament
Go for this is your feat
Go leave the mark back
Go like a goon and a stooge
Go the ignoble way go.
Go the world will remember you
Just as a symbol of megalomania

Go son of man
Go Jammeh go
It is time to go
Never look back go
Go Jammeh go
It is time to go.
Go from thy man-made no-go
Go go it’s time to go
go go go go

Don’t turn back go!
Those that you treated like rats
They have used their votes
Who’s between you and em a rat?
Cornered is you tyrant
You are yourself indeed a rat
You treated Gambians like braggarts
Little knowing you are but a rat
Now that they have spoken
Everybody needs to listen
There a big lesson to be taken
Wait your future in the prison
You wrongly thought you’re smart
Cornered is you braggart
Go Jammeh go.

Go your friends will follow
Welcome Adama Barrow
As for Jammeh
Where will you go
To the jail or to exile
Whatever you chose just do
Go Jammeh go
It is only to Zimbabwe you can go
Go Jammeh go
Go Jammeh go
Go go go!

I congratulate Gambians
Yes, you have spoken
The rest of Africa needs to learn
Youths need to stand
The precedent you have set
Indeed, will liberate our continent
Go join the Burkinabe
Let there peace be
Go rebuild your country
You have it back
Stand together as one


↧
↧

Mlevi atathmini mwaka mmoja wa Makufuli

December 3, 2016, 6:32 am
≫ Next: Tunahitaji mfumo wa utawala si makondis
≪ Previous: Bye bye Yahaya Jammeh
$
0
0

            Japo wengi wameishatoa tathmini yao ya utawala wa awamu ya tano, haitakuwa vyema kwa walevi kutofanya hivyo. Hata kama ni mlevi, nina haki ya kutoa tathmini yangu ya kilevi hasa ikizingatiwa kuwa na walevi ni watu kama wengine tena wana kaya orijinali. Isitoshe mabadiliko  yote  yanayotokea kayani yanawakumba. Nilingoja wengi waronge na kumaliza ili nimalizie; na kuwashinda pwenti.
Hivyo, ifuatayo ni tathmini yangu ya utawala wa rahis Joni Kanywaji Makufuli.  Baada ya kufanya mahojiano yasiyo rasmi na walevi na marafiki zangu wa karibu nimegundua yafuatayo:
Mosi, walevi–japo wanalalamika kupigika–wameanza kunyooka. Yapo mambo wanayojivunia yaliyosababishwa na utawala huu. Kwa mfano, ndoa zao nyingi zimeimarika. Hii ni baada ya warume kukosa njuluku za kunywea na hata kuhongea. Hivyo, wengi hurejea majumambani mwao mapema na kuwasaidia washirika zao wa bedroom ukiachia mbali vitegemezi vyao kuwaona kwa mara ya kwanza wakiwa sober.
Pili, matajiri uchwara na wajivuni siku hizi wana adabu.  Wengi wa matajiri tuliokuwa tukiwagwaya kumbe walikuwa wamekopa njuluku toka kwenye mabenki bila kulipa! Huwezi kuamini namna kiama kilivvyowakumba huku wengi wakipoteza mali walizodhani ni zao wasijue za mabenki. Taratibu, tunaanza kuheshimiana na kuthaminiana tofauti na ilivyokuwa chini ya utawala wa mauzauza na holelahola. Migogoro ya ndoa, kama vile ugomvi, nyumba ndogo na unyanyasaji vinaanza kupungua.
Tatu, kazi na uwajibikaji vimeanza kuthaminiwa baada ya mirija yote na misheni town kufyekwa. Bila kuchapa kazi huli. Hata wale waliozoea kuchapa kazi kwa kutumia vyeti vya kughushi au kugeuza ofisi kuwa maduka na vijiwe kwa sasa wanalia na kusaga meno huku walevi tukiwazomea. Huwa nawambia kuwa wameishaisoma namba; na mikogo na maringo yao kwishenei. Walie tu. Lazima tunyooshe kaya hata kama ni ya walevi walioiruhusu ikageuzwa shamba la chizi.
Nne, katika mahojiano nimegundua kuwa matapeli kama vile waganga wa kienyeji na wachunaji wanasherehekea biashara zao kuchanua tokana na kihoro na ujinga vya walevi. Hebu fikiria kwa mfano, eti jitu zima lenye kuitwa msomi linakwenda kwa mganga njaa tapeli au mchunaji kutafuta eti namna ya kuzuia benki isikamate mjengo au biashara zake. Inasikitisha kiasi cha kuhoji maana ya elimu pale unapoona baba au mama zima likilala kwa waganga eti kulinda cheo chake. Yupo mlevi mmoja kigagula aitwaye Wajingandiyowaliwao alinitonya kuwa huwa haamini macho yake kuona walevi wanaofurika kwake eti kutafuta dawa ya bahati wakati mwenyewe maisha yake ni bahati mbaya tupu. Kama haitoshi, utasikia jitu linakwambia kuwa kigagula fulani ni bingwa wa kuzindika kesi. Hivi kweli unaweza kuizindika kesi au ni ujinga wa kutojua namna zinavyofanya kazi?
Naona yule anasonya wakati waraka huu umelenga kumsaidia asiendelee kuliwa na kugeuzwa bwege kwa ujinga na kutojiamini kwake. Unakuta jitu zima ambalo lilijenga uadui na kanisa au nsikiti likikimbilia kwa wachunaji eti liombewe utadhani limeishanyatuka roho. Unaombewa kwani wewe maiti? Si ujiombee tena kwa lugha na namna unavyoyaona matatizo yako. Hata hivyo, kuomba ni suluhu au kujirekebisha na kukubali kufanya hivyo tokana na kubadili kwa mambo?
Tano, siku hizi hata kelele za mabaa ya kukesha zimepungua. Walevi wanatononoa usingizi kama hawana akili nzuri. Hata hivyo, kuna tatizo moja. Kuna uwezekano wa kutengeneza vitegemezi vingi kiasi cha kaya kushindwa kuvihudumia tokana na mkwamo huu.  Maana jamaa wengine walikuwa wakilewa hadi kushindwa kazi ya chumbani. Unadhani nazusha? We ngoja uone vitegemezi vitakavyoongezeka hasa usawa huu ambapo huduma za afya zinaanza kuimarika.
Mwisho, inapotokea mlevi akakupiga ofa ya kanywaji au mapupu unamshukuru na kufakamia kana kwamba ni mara yako ya kwanza na mwisho kupata zana hizi.
Tuonane wiki ijayo jamani.
Chanzo: Nipashe Jumamaosi leo.
↧

Tunahitaji mfumo wa utawala si makondis

December 4, 2016, 7:06 am
≫ Next: When Doctors Strike where does the buck stop?
≪ Previous: Mlevi atathmini mwaka mmoja wa Makufuli
$
0
0

             Baada ya rais John Pombe Magufuli kuingia madarakani, staili yake ya uongozi imeanza kuleta hisia mchanganyiko. Wapo wanaopenda staili yake. Na wapo wanaoiponda kutokana namna baadhi ya mambo yanavyofanywa na baadhi ya watendaji wake. Mmoja wa watendaji wake aliyevutia wengi kwa sababu tofauti si mwingine bali mkuu wa mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda anayesifika kwa ufundi wake wa kuchongea wenzake kwa bosi wake. Pia Makonda amevutia wengi kutokana na kusifiwa sana na rais Magufuli zaidi ya mara moja jambo ambalo wengi wanaona kama ni kumpa kichwa kiasi cha msifiwa naye kukoleza mambo.
            Hivi karibuni, vyombo vya habari viliripoti kuwa rais alimpigia simu kumpongeza na kumueleza kuwa yuko nyuma yake katika kutatua matatizo ya wananchi. Kupiga simu si jambo baya ingawa rais. Ila kwa nafasi yake, angeweza kuwasiliana na Makondakupitia njia za kiofisi bila umma kujua. Wakosoaji wanaona; Magufuli alifanya hivyo kutaka sifa rahisi, cheap popularity ambayo inaweza kuchukuliwa kama mpango wa wawili kufikia malengo yao. Hatusemi hivi kwa kubuni. Ushahidi ni kwamba maongezi ya Magufuli na Makonda umerekodiwa na kuwekwa kwenye mitandao; ukiachia mbali kurushwa moja kwa moja kwa wananchi aliokuwa akiwahutubia Makonda.
            Tunaweza kusema kuwa Magufuli alipiga simu ili kuwaonyesha wananchi anavyokerwa na namna wanavyozungushwa na kukwamishwa. Kwani lazima rais ahangaike kumpigia simu mkuu wa mkoa wakati wana uwezo wa kuwasiliana au ni kutaka umma ujue kuwa anayosema Makonda anatumwa na bosi wake? Nadhani wananchi wanachotaka si kusikia namna Magufuli anavyomkubali Makonda bali wanataka utatuzi wa matatizo yao. Na hili likifanyika rais na wasaidizi wake wanatimiza wajibu wao. Hivyo, hawahitaji sifa wala kuwajulisha wananchi kuwa wanaunga mkono vitu kama hivyo. Tunajua kuwa kwa kumteua Makonda, rais anamuunga mkono sawa na wakuu wa wateule wengine. Rais ana mambo mengi ya kufanya.
            Magufuli hakuishia kupiga simu. Aliwataka wakuu wengine wa mikoa kumuiga Makonda. Je hii ni sahihi wakati kila mkuu amepewa madaraka kamili na kujiwekea malengo na namna ya kuyafikia? Waige nini? Mkuu wa mkoa kwenda kukamata machangudoa wakati mgambo wa jiji wangeweza kuamriwa kulifanya hili? Hiki ndicho naweza kuita cheap populism au tuiite makondism. Hii maana yake ni kwamba, wakuu wa mikoa wengine watapaswa kufanya mambo kwa hofu ya rais; na si kwa namna walivyojipangia. Wakuu wa mikoa hawawezi kutimiza majukumu yao kwa kumuiga mtu bali kufuata sheria na kanuni kulingana na mipango kwa madaraka yao.  Na hili si kwa wakuu wa mikoa tu. Hata mawaziri wetu wengi wanafanya kazi si kwa ujuzi na mipango yao bali kutaka kumridhisha bwana mkubwa. Hapa kunaonyesha ombwe la kukosa mfumo wa kuendeshea nchi; ambao, hata hivyo, Magufuli anaonekana kutopenda na kuwa tayari kuuanzisha tokana kuuhofia unaweza kumbana. Mfano rahisi ni kitendo cha Magufuli kukwepa mjadala wa kurejesha mchakato wa Katiba Mpya iliyouawa na mafisadi walioogopa kuwaumbua na kuwashuhgulikia.
            Tokana na Magufuli kuonekana kumshabikia Makonda, saa nyingine kuliko hata wasaidizi wake wengine kama vile Makamu wa rais na Waziri Mkuu, unaweza kujenga hisia kuwa anamuandalia mambo makubwa huko tuendako. Je atafanikiwa?  Uzoefu unaonyesha kuwa ivumayo haidumu. Kwa wanaokumbuka Augustine Mrema chini ya utawala wa mzee Ali Hassan Mwinyi na alivyojionyesha bora kuliko wenzake, ni rahisi kutabiri nini mwisho wa hali hii. Hakuna ndoa ya maisha kwenye siasa.
            Na Makonda naye kutaka kumfurahisha bosi wake, amelikoleza kweli kweli. Maana, anaamini kuwa asemacho lazima kitakubaliwa na bosi wake. Rejea alivyomchomea aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji marehemu Wilson Kabwe, Kamishina wa kipolisi wa mkoa wa Dar Es Salaam Simon Sirro na RPC wa Kinondoni, Susan Kaganda hivi karibuni. Je tokana na makondism, Magufuli atawatumbua wahusika kama ilivyotokea kwa Kabwe? Kama haitoshi, hivi karibuni, Makonda alikaririwa na vyombo vya habari akiwaita wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa mizigo isipokuwa watatu tu ambao hakuwataja bila kusahau alivyodai wafanyakazi wengi wa mkoa wake ni wapiga majungu na washirikina. Wengi waliona tabia hii kama udhalilishaji wa wafanyakazi wasio wateule wa rais ambao wengi wameishaanza kuulalamikia sehemu mbali mbali nchini.
            Makonda amepata umaarufu ghafla tokana na kujua kucheza ngoma ya Magufuli ukiachia mbali kumsifia kupita kiasi. Kwa mfano, Makonda anaonekana kama kiongozi anayetaka kuleta maendeleo jambo ambalo ni kweli japo kwa kutumia njia za shaka. Huwezi kuleta maendeleo kwa kuwakashfu wenzako. Sijui kama Makonda anajua kuwa akiendelea na tabia hii, wa chini yake ima wanaweza kumtenga au kumkomoa akaishia ambako hakutarajia. Hueanda ni kutokana na kutokuwa na uzoefu au ukomavu kisiasa ukiachia mbali kusifiwa sana.
            Magufuli kweli amedhamiria kuleta maendeleo. Hili halina shaka.  Shaka ni ile hali ya kutumia kisingizio cha kuleta maendeleo kwa kupiga marufuku vyama vya upinzani kufanya siasa.Tunataka maendeleo; lakini si kwa sababu Magufuli anayataka bali tunayataka kama watanzania; na lazima yasitumike kuua demokrasia na kusimika uimla kwa mlango wa nyuma. 
            Je staili ya Makonda ya kufanya mambo ya kiofisi kienyeji itamsaidia Magufuli kupata anachotaka au kuzidi kuwastua wananchi?
            Tumalizie kwa kusema kuwa, kama taifa tunahitaji mfumo unaoleweka wa utawala badala ya kutegemea jazba za watu binafsi kiasi cha kushauriana kuigana na kuigizana.
Chanzo : Tanzania Daima Jumapili leo.
↧

When Doctors Strike where does the buck stop?

December 5, 2016, 8:57 am
≫ Next: Kijiwe toka Gambia kwenye sherehe ya mweleka wa Jammeh
≪ Previous: Tunahitaji mfumo wa utawala si makondis
$
0
0
Cartoon for the courtesy of the Daily Nation Kenya.
↧
Remove ADS
Viewing all 3177 articles
Browse latest View live

Search

  • RSSing>>
  • Latest
  • Popular
  • Top Rated
  • Trending
© 2025 //www.rssing.com