↧
Pinda afute kauli yake, aombe msamaha
↧
Brewing Feuds: Will the EAC Survive?

Those who bother to go back to history books will agree with us that bad blood between former Tanzania President Julius Nyerere and Idi Amin, former Uganda President in 1977 stalled the then EA community that aimed at unifying east African countries.
Of late, the bad blood between Presidents Jakaya Kikwete and Paul Kagame is likely to make history repeat itself. It all started when Kikwete urged Rwanda to negotiate with Forces Democratiques de Liberation du Rwanda (FDLR) rebels so as to move forward. Such proposition received all types of insults and salvos from Kigali. Kikwete, for the first time, dubiously and unfairly, was linked to genocide and called a genocider. Soon after, Kikwete urged Rwanda to negotiate with the rebels, Kigali embarked on media campaigns painting Kikwete as an emissary for rebels who essentially are genociders in the eyes of Rwanda.
One wonders how humans are hard when it comes to learn from history! It goes with the saying, “We learn from history that we don't learn from history!” Desmond Tutu. Interestingly, it is the same Tanzania that tried to negotiate dialogue between Juvenal Habyarimana (former president of Rwanda) and Kagame (then leader of the Rwandese Patriotic Front (RPF) rebels).
I am trying to imagine if Habyarimana would have taken the same stance as Kagame has taken. Would Kagame been in power today after being defeated by Habyarimana for long? Who’s fooling who hither? Maybe, Tanzania is paying for its sins of creating Museveni and Kagame.
While Rwanda is demonizing Kikwete, other SADC countries have supported his move. Sadly though, Rwanda seems to have forgotten the role Tanzania played in ending the Rwanda conflict. Again, I read one article in the New Times of Rwanda which was quoted as thus, "And so he was because, as Tanzanian foreign affairs minister, he was watching as the Genocide was being planned." If my mind serves me well, Kikwete was not minister for Foreign Affairs during and after the genocide. Why are people telling lies to justify their lies?
Since the installment of a new regime in Kigali under Paul Kagame in 1994, Rwanda has nary tolerated any advice pertaining to dialoguing with rebels or introducing true democracy. Whoever tries to tell Rwanda to think about talking to rebels is painted with the same brush.
What irked Rwanda the most is the fact that Kikwete is seen as preempting and executing a bigger plan backed by other countries. Coincidentally, Kikwete’s advice to Rwanda to negotiate with rebels comes at the same time the US president Barack Obama is expected to tour the country. One of the Rwandan daily was quoted as saying, "If President Kikwete’s advice was meant to distract, it has done the opposite. It has put people on their guard and made them more determined not to be derailed but to deliver more imihigo." It is sad to note that Rwanda could openly say that Tanzania wants to derail their efforts to build their country.
Those who know Kikwete do not wonder. In his own country, on many occasions, Kikwete has spoken generously. In 2011, he signed a doctored bill that he later annulled. He once told Tanzanians that he did not know why they are poor. He added that when Tanzanians experience traffic jams, they should take them as economic growth.
Regarding reviving the Eat African Community, only Kenya is left with the sanity to mediate this eminent danger given that Tanzania has now become a part to conflict while Uganda is known also to be in vicariously. Burundi has more on its plate.
Source: The African Executive Magazine June 26, 2013.
↧
↧
Tamaa, upofu, uroho na roho mbaya vitaliangamiza taifa
MATUKIO ya kushambuliwa kwa mkutano wa CHADEMA kule Soweto Arusha na kupigwa na kuumizwa vibaya kwa wananchi wakiwamo viongozi wa chama hicho hayawezi kupita bila kulaaniwa kwa sauti kali.
Tanzania ilisifika kuwa kisiwa cha amani. Kwa sasa bila shaka inaanza kusifika kama kisiwa cha vurugu, ubabaishaji, ufisadi, kujuana, kulindana, kukomoana na hata kudhulumiana. Hivi ni dhuluma kiasi gani kwa kikundi fulani chenye kuamini kuwa madaraka ni staili yake kuwaumiza na kuwahujumu wananchi wasio na hatia?
Ni upuuzi na ukosefu wa akili kiasi gani kwa kikundi kidogo cha watu kujiona kama ndicho chenye kujua na kumiliki kila kitu hata ikiwamo akili?
Je kwanini sisi kama taifa hatutaki kujifunza toka tawala ovu na zandiki zilizofanya haya lakini bado zikaangushwa kwa aibu na kejeli? Walikuwapo akina Muamar Gaddafi (Libya), Hosni Mubarak (Misri) na Saddam Hussein (Iraki).
Waliogopewa sana na kuamini kuwa wao na waramba viatu wao waliumbika kuwatawala na kuwanyonya wengine wasijue arobaini yao ilikuwa imewadia. Kwanini hatupendi kusoma alama za nyakati kuwa wakati tulio nao si ule wa mwaka 47 ambapo kikundi kidogo cha watu kingeweza kuteka taifa na kulitenda litakavyo? Ni vizuri kutambua kuwa vijana wa sasa si wa kuburuzwa kutishwa wala kuchezewa mahepe.
Ni ajabu kuwa tumegeuka taifa la wakandamizaji na wababaishaji kirahisi hivi. Nani hajui kuwa kwa sasa tumo msambweni tukielekea kuzimu ambapo ulaji umechukua nafasi ya huduma?
Leo tunaambiwa kwa mfano deni la taifa linazidi kuumka huku wahusika wakitumia kwa hisrafu na kuiba kama vile hakuna kesho.
Nani hajui, kwa mfano, kuwa hoja ya kurejesha fedha zilizofichwa Uswizi imeuawa kwa vile wahusika ni wakubwa au marafiki zao.
Je ni kosa kuyashupalia haya? Je ni kosa kudai ukombozi? Je kupiga mabomu mikutano au kukata watu mapanga kwa vile wanapinga dhuluma ni jibu?
Hata wenzetu wanaolia na kukumbuka maafa kama Rwanda walianzia huku. Hakika hawa walipaswa kuwa somo kwetu.
Inashangaza kuona kuwa Tanzania imegeuka nchi ya kulipuliwa na mabomu ya kigaidi na hakuna anayekamatwa kwa vile wahusika wana watetezi wao wenye mamlaka. Tunasema hivi si kwa chuki wala uchochezi bali kujibu kilio kilichotolewa na wahanga kule Arusha kuwa walimuona aliyerusha bomu na kutaka kumkamata lakini polisi wakamkingia kifua na kumtorosha.
Je kama polisi na huyu gaidi lao si moja walimtorosha ili iweje kama siyo kuficha ushahidi?
Laiti wangemtorosha kunusuru uhai wake ili ahojiwe na kuwataja wenzake ingeingia akilini. Ajabu badala ya kushughulikia kuwasaka waliolipua bomu, polisi inawashughulikia CHADEMA.
Hali ni mbaya na yenye kutia kinyaa hadi kufikia baadhi ya walevi wa madaraka kusema eti waliolipua bomu ni CHADEMA ili kupata huruma ya wananchi. Hoja dhaifu na ya aina yake kwa uhovyo.
Yaani CHADEMA wawaue viongozi wao ili iweje na hiyo ‘huruma’ iwasaidieje kama siyo utaahira wa aina yake? Waingereza wana msemo : Go tell it to the birds.
Tunadhani badala ya kuingiza siasa kwenye mambo nyeti na mazito kama mashambulizi haya ya kigaidi, serikali iwajibishwe kutuletea wale waliotenda uovu huu. Inashangaza kuona Watanzania wanageuka mateka kwenye nchi yao huku wakiuawa na kuteswa kutokana na kukataa kwako kulala kitanda kimoja na uovu.
Wako wapi waliomteka na kumtesa Dk Steven Ulimboka na Absalom Kibanda?
Wako wapi waliomuua Daud Mwangosi? Kwani hawajulikani?
Je nani anahangaika kuwakamata iwapo walitumwa kutekeleza amri za wakubwa zao walioishiwa?
Je hili ni jibu na hali itaendelea hivi hadi lini?
Tumegeuka taifa la kulalamika lalamika. Ni jukumu la wananchi kujiletea ukombozi na kuhakikisha hatima zao zimo mikononi mwao. Tuwawajibishe watawala wetu waache kutuchezea.
Hakuna kitu kilitushangaza kama matamshi ya kizembe kama yale yaliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) aliyekaririwa hivi karibuni akirusha lawama kwa wahanga akidai kuwa kumekuwapo na tabia ya wananchi kuchukia jeshi la polisi. Lukuvi anayetuhumiwa kughushi vyeti na sifa za kitaaluma ameonyesha ukweli kwa mada hii.
Hivi Lukuvi hajui kuwa wananchi wanachukia jeshi la polisi kutokana na kushindwa kuwahudumia?
Ameshindwa kutambua kuwa wananchi wanaona kila uchao mauaji na manyanyaso yanayotekelezwa na polisi huku wakilipwa kwa kodi za hao hao wanaowaua kama Swala mbugani?
Imefikia mahali hata wanyama pori wana amani kuliko Watanzania. Je Lukuvi alitaka wananchi wawapende polisi kwa kuendelea kuwaua na kuwadhulumu?
Je huku ni kufilisika kimawazo kiasi gani? Wengi walidhani kuwa wasemaji ambao ni makada wa chama tawala angalau wangekuwa wastaarabu wakatoa hata salamu za rambirambi badala ya kutonesha donda.
Kwanini hawajifunzi toka nchi ambapo vyama tawala vilipigwa teke na kutokomea kwenye kaburi la sahau?
Tuhitimishe kwa kulaani kitendo cha wanasiasa uchwara kutetea ugaidi kwa vile unawanufaisha wao baada ya kuishiwa kisiasa.
Hata hivyo wafahamu kuwa Watanzania si mataahira wala mawe yasiyobadilika. Kuna siku yaja watalia na kusaga meno.
Kama taifa na jamii tusipoangalia tamaa, upofu, uroho na roho mbaya vitaliangamiza taifa. Tafakarini.
Chanzo Dira Juni27, 2013.
↧
Walevi kukata kanywaji na Obama

We’ve a dream. Yes we’ve a big dream of changing the kaya. We’ve a dream to meet with Black Obama and talk business and not politics. We will taaalk and taaaalk and taaaalk. Walevi have a dream. Lazima kuongea kimombo kuonyesha usomi wetu usio wa kughushi kama akina Lukuwi na Nchimvi.
Baada ya kuzinyaka kuwa rais Black Obama anakuja kutembelea kaya, walevi hatutaki kuachwa nyuma. Tunajua jamaa ni mwenzetu anapenda sana kanywaji na tufegi ingawa tuliambiwa siku hizi ameacha. Kwa vile mkiti nilsomea kwao Hawaii na dingi wake, najua akitoka ku-surf lazima apate kanywaji kwanza. Tumemuandalia Boha, Rubisi, Gwagwa, Nkojo, Mnazi, Ulanzi, mapuya, kangara, chibuku, common na madude mengine mengi. Tumeadaa party ya kufa mtu ila msigara mkubwa hatutapiga. Maana FBY walisema kuwa hawapatani na kitu hii. Yes we can. We indeed can realize Bongo dream of maisha bora kwa wote.
Hivyo, nasi kama walevi wa siasa, tumepanga kumpa kampani bwana ndogo Obama ili akiondoka akumbuke siku moja aje kutupa tafu akiwa nje ya White House. Ila kwenye party yetu Joji Kichaka hatakanyaga. Tutamsusa kama tulivyomsusa rais wa Uchina kutokana na kutujazia machinga. Hata huyu wa Bangla anayekuja hatutakutana naye maana ni apeche alolo anayetafuta pa kubwaga wazamiaji wake.
Tuna mipango kamambe ya kuhakikisha huyu Jadwong anakumbuka kuwa walevi ni mali kuliko walevi wa siasa. Onyo: Hatutatumia pesa ya walevi kujilisha upepo kumuandalia partya bei mbaya. Tumepanga tumpeleke Uwanja wa Fisi ambayo tutaibadili jina iwe White House ili apate mapupu kidogo na utumbo lau ajue asili yake. Pia, hatutamtumia Obama kuibia walevi kwa kisingizio kuwa pesa yote imetumika kumkirimia. Wala hatutajikanyaga kwake bali tutampa kampani na maongezi ya kikubwa yenye kuonyesha usawa kama walevi na wapenda haki. Yes we can and indeed we should and we will.
Baada ya kukutana na Jadwong Madwong Obama lazima tumwambie kuwa we have a dream awambie ombaomba wavaa masuti waache kunyanyasa ombaomba wavaa manyang’umyang’u kama walevi. Kwa wasiokinyaka kidhuluo Jadwong maana yake ni mtu mkubwa na Madwong ni mkubwa zaidi na mwenye hadhi kama mimi na Obama na Diba Mandela. Jadwong kwa sasa tuko wachache. Kwenye kaya yetu ni mimi pekee nimebakia baada ya Mzee Mchonga bin Musa wa Burito kurejesha namba. Hayo tuyaache. Acha niwape yale tutakayompa Jadwong Madwong mwenzangu:
Mosi, tutampongeza kushinda uchaguzi bila kuchakachua wala kutoa ahadi za kijinga na kitapeli.
Pili, tutawambia fika kuwa Bongo dream imehujumiwa na wahuni na mafisadi fulani kwa kuiba njuluku na kuzipeleka Uswazi aka Uswisi huku wengine wakifunja kwenye kuzurura badala ya kukaa ofisini kutumikia walevi.
Tatu, tutamwambia Obama mambo ambayo baadhi ya wahuni wanaficha na hawataki ayajue. Kwa mfano, tutamwambia kuwa walevi wamesikinishwa kiasi cha kuishi kwa kutegemea ofa na misaada uchwara wakati wana mikono na akili. Hivyo, sisi hatutampiga bomu la njuluku bali kumshauri tufanye biashara kwa usawa na haki.
Nne, tutampa laivu kuwa lazima tufute mikataba yote ya kijambazi ya uwekezaji katika madini ya walevi.
Tano, tutawachomea wahuni wanaotishia maisha na haki za walevi kama wale waliowamuru ndata kutupiga, kututeka hata kutuua kwa vile tunachukia uovu na ujambazi wao.
Sita, tutamshauri next time awe makini. Kabla ya kuja huku Uswekeni ashauriane nasi tumpe picha halisi ya kinachoendelea ili asijikute siku moja anakula sahani moja na wezi, majambazi, wauaji, watesaji wababaishaji hata wahuni wa kawaida kama ilivyomtokea Tommy Blair wa kwa Mother alipopiga picha na akina Mwamali Kadhaffi wa Kashafi aliyenyotolewa roho kule Libya.
Saba, tutamshauri kuwa next time asije kwa mikwara na mibunduki na mimeli. Maana huku watu wanalipua wapingaji kama ilivyotokea kule Arusha. Pia asiwe na hofu kwa vile sisi tutampa ulinzi wa mwagwiji wa karate wanaoweza kumeza bomu na lisilipuke.
Nane, tutashauri akija kutupa tafu asitangaze ili kuepuka kuvuruga shughuli za uzalishaji mali kama vile kufunga anga, barabara, mitaa, hata kusumbua watu bila sababu ya msingi. Maana, nilipokuwa Washington sikuona mikwara kama niliyoiona huku Uswazi ambapo kujipendekeza na kujikomba hata kwenye mambo yasiyomhusu kumezidi. Juzi wakati nikikata kanywaji alitokea ndata aliyetaka kunisachi akidhani eti nilikuwa na bomu la kumdhuru Obama asijue ni mshikaji wangu damu. Baada ya kumkunjia kama kata sita hivi za karate ndata alitoka nduki kama kibaka. Nilimkimbiza na kumkamata na kumuonya asirudie kudhani kila mtu ni fala mwenzie. Hayo tuyaache.
Pia wake zetu wamepanga kum-surprise Mchele bint Wali wa Obama kwa kumuandalia bonge la party ambapo watamshukuru kwa kutowaibia wenzao wa Umarekanini kwa kuunda NGO ya ulaji. Juzi niliwafuma wakipanga mikakati kwenye kikao chao cha maandalizi. Nilimsikia mke wangu akisema lazima wampongeze Mchele kwa kupiga kitabu na kuacha ubabaishaji wa kutumia ulaji wa mumewe. Alisema kuwa amewapa motisha wa kupiga shule na kuwafichua waume zao watakaojaribu kughushi shahada kama wale mawaziri walioghushi Ma PhD. Nimekumbuka. Pia tutamwambia apige marufuku vyuo vya uchochoroni huko Umarekanini vinavyotoa shahada feki kwa vihiyo na waharifu wetu mabingwa wa kughushi wakitumia madaraka ya walevi. Hapa lazima watu kama Bill Lukuvi, Makorongo Mahanga, Marry Nagu, Deodorant Kamala, Emmy Nchimbi na wengine watetemeke. Soma taratibu wasiinyake wakahujumu mpango wetu wa kuwachoma kwa Obama.
Turejee kwenye shinikizo letu kwa Obama, walevi tumepanga kushitaki lile genge liitwalo Coalsced Criminal Mob (CCM- usichanganye na Chama Cha Mapinduzi maana CCM zipo nyingi). Lazima tulishitaki kutokana na ujambazi na undavandava linaofanya kwa walevi hata matumizi mabaya ya ndata kutunyanyasa wakati wakiwalinda waharifu kama vile wauza unga, majambazi, mafisadi. Hili genge la kimafia limekuwa na nguvu kuliko hata serikali ingawa inaonekana kutojua lilipo na linavyofanya kazi.
Tisa, tutambana Obama azuie wazururaji kwenda kutanua majuu kwa njuluku za walevi kama walivyomfanyia yeye asiende kutanua kwenye mbuga za wanyama. Uchumi muhimu yawe! Tutasema wazi wakiomba kwenda Umarekanini awanyime viza na kuwauliza wanakwenda kufanya nini wakati wana matatizo kibao ya kutatua.
Kumi, nimenusa harufu ya Air Force One. Acha niwahi uwanja wa ndege kumpokea Obama.
Welcome to the nether world of wonders such as corruption, nihilism, bootlicking, nepotism, hooliganism especially committed by Pindaboys and whatnot.
Chanzo: Nipashe Jumamosi Juni 29,2013.
↧
Mzee Pinder, hold your shibboleths
When Big Minister Mizengwe Pinder ‘courageously’ encouraged cops to keep on brutalized boozers, many were saddened, sickened and shocked beyond explanation. They said that he did so pointlessly and unreasonably. Again, this is not our take on mzee Pinder. We’re reporting what boozers thought of him. Some interrogated his way of doing things. Others were baffled by his snap judgment.
Those of us who studied heuristics, the science of experience-based techniques for problem solving; we’d an answer already. In what we call anchoring or getting used to what one is used to, we tend to judge things based on what is in our memory. Methinks, after the govt got away with many killings perpetrated by cops, came to the conclusion that it can get away with everything. It got away with EPA, Richmonduli, Meremeta, Mwananchi Gold, SUKITA and much more stinking stuff. So too, looking at mzee Pinder’s political resume and the way he came to being premier after Eddie Lowassa messed, we’re able to know why he uttered such so-called irresponsible things.
To jog your memory, as boozers, “we remember everything spoken during our kanywaji parliament.” This is how one boozer put it. He went on, “Pinder apart from messing when he’s Minister for Regional Administration and Local Governments, kept on showing how amnesic he is. He once rejected a shangingi so as to give it to another person to use. He pointlessly contradicted his snake oil of saving pauper’s dosh the same way he did recently in Dom when he threw such an expensive party for walaji.” Usanii mtupu!
A big laughter, and he goes on, “ He once told a lie before the Mjengo when he said that in January 5, 2011 Arusha police killings there was no foreign national while actually there was one Kenyan Paul Njuguna Kayele.” Such utterances caused a stir in the house thereby causing Arusha Town MP Godbless Lema to be kicked out after asserting that mzee Pinder told a lie something Anna Makidamakida did not like.
Another one chipped in, “So too, it’d be known that mzee Pinder had nothing to care about or lose to say what he said given that those killed and beaten were opposition guys. This is the type of rulers we now have.” He went on, “Do you remember how he assured the world he’d take on Dowans that ended up taking him in?”
Boozers were sickened to see the person they trusted immensely turning against the same people he swore to protect and serve. Up till now we can’t see the ethos, logos even pathos of mzee Pinder’s ‘wisdom’. What makes things worse for him so as to self-dressed down is the fact that the man is a lawyer who’s supposed to know and uphold the law to its spirit and letter.
When mzee Pinder ordered ndata to beat boozers shall they agitate for their rights, one boozer said that this was a sign of aging badly. The other said that mzee Pinder was suffering from malady known as kuvimbiwasis and kulewasis so as to become a wino. This is not our take though. Again, why did mzee Pinder decide to dress down? Who knows? Had the victims been his fans he’d have announce a national mourning week and those felled would be made martyrs.
Imagine. If what mzee Pinder said would come from the opposition telling their members to beat whoever attack them. Obviously, it’d have been branded terrorism and anarchism. Again, from mzee Pinder’s philosophy we learn that there are those who are above the law-those allowed to beat, torture and kill others without being brought to book as it happened in Kibanda’s, Ulimboka’s and Arusha’s cases. Sadly though, this way we’re letting our hunk go to the dogs. Mzee Pinder is lucky. His boss, mzee Jake Kiquette, seems to be at home with his militarism. Boozers were shocked to learn that when terrorists attacked innocent earthlings he swore to protect, he went on enjoying in the country of Brits. To add salt to the injury it came to light that they guy had a ‘very serious business’ of visiting Football Clubs posing for photo-ops while the so-called his people were perishing in the hand of his cops! Such sacrilege needs a great deal of negligence, ignorance or the courage of the mad. If this is the crop of the rulers we’ve, surely, we must brace ourselves for more troubles. If anything, this is vacuity and leadership vacuum that needs to be filled urgently.
Needless to say, mzee Pinder’s hit hard when he jabbered; boozers congratulate him on being able to unearth his true self that he hid for long. Some boozers said that we need to thank mzee Pinder instead of blaming him. First of all, there’s no any of his relatives among those who were felled in Arusha. Secondly, those who died were not the members of his party despite the fact that they were Tanzanians he cares less about. Thirdly, this is the way mzee Pinder shows his love of law and tranquility even if they are enhanced by breaking the law and through carnage and violence. Uhuni mtupu!
Mzee Pinder loves Boozers so dearly that he dispatched his cops to ‘massage’ them. One boozer left us in stitches when said that when Pinder’s regime promised better life for all they meant bitter life for all who are earthlings but not bigwigs. After all, brutality’s become another policy mzee Pinder‘s regime that’s turned boozer into experimental objects. Refer to many killings perpetrated by cops. Refer to oft harassment the opposing parties have been subjected to since the inception of pseudo multiparty democracy that has become 'demoncrazy' if not a crazy demon. Had it been democracy, do you think Jake’d have gone on enjoying in Brit land while walevi were dying? Think again.
Source: Thisday July1, 2013.
↧
↧
Is it endgame for Morsi?


The look of things in Egypt is that Egyptian President Mohamed Morsi is on his way out.The day he was to mark a year in office, he was shocked to see hundreds of thousands of disgruntled Egyptians thronging Tahrir Square urging Morsi relinquish power. Major reason for wanting Morsi to hit the road is that he has failed miserably. His mojo no longer works for him. Morsi did not want to go down easily. He threatened to take all measures to see to it he survives. As the time went by, the game of numbers started to take shape in that it needed bigger numbers for either Morsi to stay or leave. As fate has it, the game of numbers seems to favour the opposition thanks to commanding bigger numbers than Morsi. Morsi's Party headquarters were ransacked and nobody was there to defend them.
Mathematicians started seeing the oust of Morsi as imminent and unavoidable. The army delivered another big blow when it issued the ultimatum of 48 hours for Morsi to put his house in order. Worse enough military choppers flew over Tahrir Square where anti-Morsi demonstrators have camped but not over Nasr City where pro-Morsi have congregated. To break his neck, the army issued an ambiguous message that sent mixed signals to both Morsi and the opposition. Whether Morsi will stay or go, it is not easy to tell. Again, is this dramatic move the beginning of the end for Morsi? Surely time will tell accurately and punctually.
↧
Eti, "Obama anatafuta nini ‘bedroom’?"
Na Ansbert Ngurumo
RAIS Barack Obama, anaingia nchini Tanzania kesho mchana. Sihitaji kueleza nini kinaendelea hapa nchini kuhusu maandalizi ya mapokezi ya kiongozi huyo.
Yamesemwa mengi na kuandikwa mengi. Haya yanayoendelea mbele ya macho yetu na watawala wetu yanatosha kuitwa matusi dhidi ya utu wetu.
Iwe tulimwalika au alipanga mwenyewe kuja, kinachoendelea ni matusi zaidi ya yale yanayowahangaisha polisi wetu na kuwafanya wawakamate wanasiasa wa upinzani kuwa wanawatusi watawala.
Ndugu yangu mmoja ameniambia kuwa alipokuwa kijana wa shule moja ya sekondari mkoani Tabora, alipata fursa ya kuwa miongoni mwa vijana wachache waliochaguliwa kumpokea Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, alipotembelea Mkoa wa Tabora.
“Kama ilivyo kawaida, kulikuwa na maandalizi ya mapokezi ya Baba wa Taifa, wakati huo akiwa katika mwaka wake wa mwisho wa kuongoza taifa letu kama rais.
“Alifika eneo la mapokezi akitokea uwanja wa ndege, na burudani kadhaa zilifanyika; kisha akapewa nafasi kusalimu wananchi kabla ya kuingia ndani kwa ajili ya vikao vya ndani. Kama kawaida hakuchelewa kupiga vijembe palepale.
“Akawashukuru wananchi kwa kufika kumpokea. Kisha akasema; ‘Kwa niaba ya miti hii na mawe haya yaliyopigwa rangi, napenda kuwashukuru viongozi wa mji wa Tabora.’
“Akasema mawe yale na miti ile haijafanyiwa usafi muda mrefu lakini sasa kwa ujio wake vimepata fursa ya kupigwa rangi na kumwagiwa maji. Wananchi waliangua kicheko kikubwa.
“Kisha akarusha kijembe kingine kilichowauma viongozi wa mkoa. Akasema yeye hapendi harufu ya rangi inayopakwa kwenye kuta na mawe kama njia ya kupamba na kufanya usafi.
“Akasema anasikitika kuona viongozi wanang’ang’ania kupiga rangi kila mahali anapokwenda wakidhani wanamfurahisha, wakati kimsingi wanamkera sana. Hakuna aliyepiga makofi.”
Hadi hapa nani zaidi kati ya Obama na Nyerere? Wamarekani wameamua kututusi nasi tumekubali. Wamejenga hoja kuwa hapa si salama, kwa hiyo inabidi wao wenyewe wachukue jukumu la kumlinda rais wao na kutufukuza sote mjini.
Wao wamegeuka wenyeji, sisi tumegeuzwa wageni, tena wageni hatari kwa sababu wote kwa pamoja bila kujali nafasi zetu tunazotambiana nazo, tunaonekana ni magaidi mbele ya Wamarekani na rais wao.
Lakini ukweli usemwe, hivi wapi ni salama kati ya New York na Dar es Salaam? Askofu Desmond Tutu wa Afrika Kusini aliwahi kuwatibua Wamarekani katika mdahalo mmoja uliohusu usalama.
Aliwaambia Wamarekani kuwa alikuwa anajisikia salama akiwa Soweto kuliko akiwa New York. Alipoulizwa sababu alisema watu wengi wa Marekani wanatembea na silaha mifukoni mwao, kwa hiyo kuna silaha nyingi mitaani, kwenye treni, mabasi na hata kanisani.
Akasisitiza kuwa idadi ya silaha nyingi zilizo mitaani hata kama zina leseni, kwake ni tishio la usalama.
Rais Obama, iwe amekaribishwa kwetu au amejileta mwenyewe, wengi tulidhani ni mgeni wa kuishia sebuleni. Kinachoendelea sasa ni kama anatulazimisha tumkaribishe chumba cha kulala. Kwa ujio wake hakuna siri ya taifa itakayobaki bila kuwekwa wazi mbele yake.
Tumesikia waheshimiwa wetu waliozoea kupigiwa mizinga 21 na kutandaziwa zulia jekundu. Lakini safari hii ni makachero wa Obama watakaoamua nani aingie kumpa shikamoo Obama Kada na Mbunge wa CCM, Kapteni John Komba, aliwahi kuimba wimbo uitwao: ‘MGENI’. Katika wimbo huo anaeleza mgeni alivyoingia chumbani na kumwaga upupu. Matokeo ya upupu huo, baba na mama wanajikuna.
Obama anataka kuingia chumba cha kulala ili afanye nini huko? Mbona rais wa China amemtangulia? Mwanamwali wetu atakuwa salama kweli? Simaanishi Salma, namaanisha mwanamwali wetu wa taifa, yaani gesi, dhahabu, pembe za ndovu na tanzanite.
Kwa nini hataki kusubiri tumletee sokoni au angalau sebuleni? Anaingia chumbani kutafuta nini? na ‘kitanda’ hicho kitalaliwa wangapi?
Waafrika tunaruhusu mme mmoja, wake wengi; lakini si mke mmoja waume wengi! Hii mila yetu hivi sasa inapigwa vita lakini inavumilika.
Hii ya mwanamwali wetu wa taifa kugombaniwa na wanaume wengi itatuletea upupu, kwa sababu waume wengine wanaoingia huko ‘hata kupima hawajapima!’
Tena kwa Obama ni hatari zaidi kuingia chumba cha kulala, kwa sababu tumemsikia huko Senegal akipigia chapuo ushoga.
Asivyo na dogo, na kwa jeuri hii ya Wamarekani, Rais Obama anaweza kurudia kauli hiyo hapa Dar es Salaam, tena akasindikizwa na vicheko na tabasamu za watawala.
Kwa tabia yake hiyo ya kushabikia ushoga, kuna hatari akaingia chumbani na kumfukuza bibi harusi, ili abaki na baba yetu. Je, atakuwa salama?
Yawezekana lugha hii ya kishairi ikawauma baadhi ya wasomaji, hasa watawala na maswahiba wao. Lakini huu si utani.
Tumevuliwa nguo, tumedhalilishwa. Utu wetu umeondolewa kwa hiari ya watawala wetu. Kumbe haya ndiyo madhara ya kutembeza bakuli bila kikomo.
Tumekuwa tunashangilia kumwona rais wetu akishinda na kulala kwenye ndege, huku akidai anakwenda Ulaya, Asia na Marekani kuhemea.
Sasa ulaji umegeuka ‘uliwaji’. Kwa hakika tumeliwa na kugeuzwa kitoweo. Na sasa hawataki kulia kitoweo hiki sebuleni, bali chumba cha kulala. Tukubali kudhalilika kwa kiwango hicho? Na bado tunadai sisi ni raia wa nchi huru?
Chanzo: Tanzania Daima Jumapili Juni 30, 2013 ↧
Kumbe kaya haina ndata wala ndutu
JUZI nusu mgosi Machungi azipige na ndata bila kujali wangemlipua na mibomu yao ya kigaidi au la. Mgosi akiwa zake mitaa ya Buguruni kwa Mnyamani akipanga kwenda zake Kigogo Mwisho kudai njuluku zake toka kwa mzee Mipawa, si ndata wakamsimamisha na kusema eti ni ombaomba ambaye hapaswi kuonekana jijini kutokana na kuja kwa Rais Black Obamiza.
Kwa vile Mgosi anajua kuwa nilimfundisha huyu dogo wakati nikiwa profesa wa sheria pale Harvard University aliwaambia kuwa waache upumbavu wasidhani walevi wote ni fyatu na taahira wanaoweza kuabudia madaraka na misaada kama wale.
Hakuna kitu kiliwaacha hoi ndata kama Mgosi aliposema; “Nyinyi acheni ushamba. Msitifanye washamba. Huyo Baaka wenu kwa taaifa yenu amefundishwa na afiki yangu Mpayukaji. Isitoshe hapa kuna jeshi au umbea? Mbona mimeshindwa kumlinda Obamiza hadi waje waume toka kwake wakati nyinyi mkiangaia tu?”
Alitema bonge la mate baada ya kumaliza kuvuta msigara kali wake na kuendelea kuwapasha; “Kwa zina ja Zumbe kama nyinyi wanaume si mwende muwakamate ombaomba waiovaa masuti wakiruka na ndege wakiomba na kufichwa Uswazi. Acheni ushamba siku moja mtakujapigwa zongo shaui yenu.”
Kijiwe kilicheka na baadaye kutaka kulia baada ya kushuhudia unafiki wa ajabu. Bila kungoja, Msomi Mkata Tamaa aliamua kumwaga falsafa akisema; “Mmeona unafiki wa mwaka, ombaomba wenye masuti waliamua kuwatimua ombaomba wa manyang’unyang’u ili wasiaibike wakati ombaomba ni ombaomba hata awe na suti, msuli au rubega.”
Alibwia tangawizi yake na kuendelea; “Hakuna ombaomba anayeheshimika hata ajidanganye vipi. La msingi ni watu kutumia akili na kuinua maisha ya jamii zao badala ya kutumia makalio kufikiri kuwaibia na kuwageuza wenzao mabwege.”
Kabla ya kuendelea Mbwa Mwitu keshadandia; “Hivi kuja kwa Obamiza kunabadili ukweli kuwa kaya yetu ni bomubomu na inayoishi kwa kutegemea njuluku za kubomu na kusaidiwa?”
Leo ni bandika bandua. Mpemba naye anakatua mic; “Yakhe mwadhani msipobadilika kuja kwa Obamiza kutawabadili au mtaendelea kuumia. Angalia alivyofunga barabara zenu bila kujali kuwa hii inaathiri uchumi na maisha yetu.”
Mkata Tamaa anaamua kuchomekea; “Who cares kama hamna watu wenye akili kuwatetea? Wao wakienda kule kubomu wanapokewa kwa mlango wa uani na wala hawaonyeshwi hata kwenye vyombo vya umbea vya kule.”
Kapende kapata upenyo; “Hali ni kinyume kayani, wachovu wanashobokea kujipendekeza na kujidhalilisha ili njuluku ya kupeleka Uswazi iongezeke hata kwa gharama ya kuwatosa wachovu.”
Anakamua coffee yake na kuendelea; “Sijui kwanini watu wanapenda kufanya vitu kama vile hawana ‘common sense’, au wanatumia ‘uncommon sense’ kama common sense?” Kapende anavyokanyaga kimombo kila mtu anamwangalia mwenzake na kutabasamu kuona kijiwe kinavyogeuka chuo kikuu kama kile cha Manzese.
Anaendelea; “Kwanini hawataki kukubali kuwa alipokuja bwana mkubwa walijidhalilisha hadi kufanya kaya isikalike? Imefikia mahali walevi tukajiuliza: Obamiza anakuja kuchukua kaya nini?” Kijiwe hakina mbavu.
Mzee Kidevu naye hajivungi. Anakwanyua mic na kulonga; “Hivi hawa ndata na ndutu wetu wa kazi gani? Wanalipwa njuluku za nini tena wakila na kunywa dezo wakati hawaaminiki wala hawawezi kumlinda mtu mmoja na msafara wake?”
Msomi kapata nafasi tena ya kumwaga falsafa. Anaangalia hadhira yake huku na kule na kusema; “Nashangaa uwezo wa kufikiri wa akina Njaa Kaya. Je yeye si rahisi? Akienda kule haendi na zana zote za maangamizi na mibomu yote hii? Rais anakuja kutembea na ndege 56 za kimaangamizi, magari 14 na makachero mia kidogo. Au anakuja kuchukua kijiwe?”
Kabla ya kuendelea, Mbwa Mwitu anaingilia; “Thubutu. Akija hapa tunamtuliza na kahawa na anaondoka na kuacha kijiwe ngangari kama kawa. Nadhani akitaka anaweza kuchukua kijiwe cha ngunguri wanaobomubomu na kujikomba kwake.”
Msomi anachomekea; “Kitu cha kwanza, baada ya kusoma makandokando ya ziara ya Obamiza nilijiuliza kama itifaki inaruhusu. Hivi mnadhani ungekuwa wakati wa Mchonga, huyu jamaa angekuja na mibomu na miefubiai yake kutudhalilisha kama sasa?”
Kabla ya kuendelea, mzee Maneno anachomekea; “Msomi naomba nikupinge hapa. Hapa wa kulaumu si Jadwong bali wenyeji wake walioamua kumfunulia kila kitu.”
“We achia hapo utaua.” Mbwa Mwitu anachomekea na kuacha kijiwe hakina mbavu.
Msomi anaendelea kupeta; “Nadhani tatizo letu kubwa lililoleta huu utegemezi ni ile tabia ya kutokujiamini na kuamini katika uombaomba na kujikomba.”
Kabla ya kuendelea mgosi Machungi anakatua mic; “Mie mwenzenu niipoona tinavyopeekeshwa niliamua kumhamisha bi mkubwa. Maana huwezi kujua kama efubiai wanaweza weekeza huko.” Kila mtu hana mbavu jinsi Mgosi anavyohami ulaji wake.
Wakati tukivunjika mbavu, Mipawa anaamua kutuumiza zaidi; “Da hao jamaa wanaovaa miwani ya mbao nyeusi sipati picha waswahili wangapi watajifanya nao ni Wamarekani. Nahofia magaidi nao watakuwemo.”
Anabusu kashata na kuendelea; “Je, jamaa zangu wanaosingiziwa kujilipua watapona? Nadhani La-kaatare atakuwa na hali ngumu kuliko Mgosi anayehofia kuibiwa bi mkubwa. Jamani eh Michele aka Miwali Obamiza bomba. Umeona akina mafestiledi walivyojipendekeza?”
Mzee Maneno naye anavaa daruga na kudema; “Jamani eh, bi mkubwa Mchele na Obamiza si noma ila majamaa yake na wenyeji wao wanaofanya vitu kama machizi. Wanasahau kuwa ataondoka na maisha yataendelea!”
Mbwa Mwitu anachomekea; “Haya jamaa ni madhalilishaji eti yamemuwekea ngumu Obamiza kugusa hata chakula chetu! Sasa ugeni uko wapi? Kama walikuja na mipiza yao basi hawakuwa wageni wetu bali wavamizi.
“Mwenzenu natamani na rahisi angeenda kule akazira mipiza akaitisha pilau na ugali wetu ili wajue nasi jeuri. Angekuwa Mchonga nadhani kichuli kingepelekwa Marekani.” Kicheko kwa sana tu.
Mipawa anaingia ugani; “Beng’we ina maana hata kuoga, kunyx sorry kunonihino ni kwenye eafosiwani?”
Mchunguliaji ambaye muda wote alikuwa akicheka na kusoma gazeti anaamua kuingia ugani; “Kama kila kitu anataka kiwe u-Marekanini basi angeenda zake Florida na kuigiza kuwa yuko kwenye kijua cha Bongo. Ajabu jamaa zangu watajisifu kuwa uchumi umekua kwa vile amekuja Obamiza kutubamiza!”
“Wehu hao watakaosema uchumi umekua wakati wamefunga anga, barabara, mitaa hata huduma zetu za kichovu. Wakati mwingine tujilaumu kwa kuendelea na kile wakameruni huita colonial hangover yaani ulevi wa ukoloni. Watu wanafanya vitu kama hawana ubongo. Who know? Maybe Masaburi at work.” Msomi anaamua kukandia kwa kimombo na falsafa ya kisomi.
Zile njemba siyo efubiai? Acha niishie kabla sijayafanyia kitu mbaya.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 3, 2013.
Kwa vile Mgosi anajua kuwa nilimfundisha huyu dogo wakati nikiwa profesa wa sheria pale Harvard University aliwaambia kuwa waache upumbavu wasidhani walevi wote ni fyatu na taahira wanaoweza kuabudia madaraka na misaada kama wale.
Hakuna kitu kiliwaacha hoi ndata kama Mgosi aliposema; “Nyinyi acheni ushamba. Msitifanye washamba. Huyo Baaka wenu kwa taaifa yenu amefundishwa na afiki yangu Mpayukaji. Isitoshe hapa kuna jeshi au umbea? Mbona mimeshindwa kumlinda Obamiza hadi waje waume toka kwake wakati nyinyi mkiangaia tu?”
Alitema bonge la mate baada ya kumaliza kuvuta msigara kali wake na kuendelea kuwapasha; “Kwa zina ja Zumbe kama nyinyi wanaume si mwende muwakamate ombaomba waiovaa masuti wakiruka na ndege wakiomba na kufichwa Uswazi. Acheni ushamba siku moja mtakujapigwa zongo shaui yenu.”
Kijiwe kilicheka na baadaye kutaka kulia baada ya kushuhudia unafiki wa ajabu. Bila kungoja, Msomi Mkata Tamaa aliamua kumwaga falsafa akisema; “Mmeona unafiki wa mwaka, ombaomba wenye masuti waliamua kuwatimua ombaomba wa manyang’unyang’u ili wasiaibike wakati ombaomba ni ombaomba hata awe na suti, msuli au rubega.”
Alibwia tangawizi yake na kuendelea; “Hakuna ombaomba anayeheshimika hata ajidanganye vipi. La msingi ni watu kutumia akili na kuinua maisha ya jamii zao badala ya kutumia makalio kufikiri kuwaibia na kuwageuza wenzao mabwege.”
Kabla ya kuendelea Mbwa Mwitu keshadandia; “Hivi kuja kwa Obamiza kunabadili ukweli kuwa kaya yetu ni bomubomu na inayoishi kwa kutegemea njuluku za kubomu na kusaidiwa?”
Leo ni bandika bandua. Mpemba naye anakatua mic; “Yakhe mwadhani msipobadilika kuja kwa Obamiza kutawabadili au mtaendelea kuumia. Angalia alivyofunga barabara zenu bila kujali kuwa hii inaathiri uchumi na maisha yetu.”
Mkata Tamaa anaamua kuchomekea; “Who cares kama hamna watu wenye akili kuwatetea? Wao wakienda kule kubomu wanapokewa kwa mlango wa uani na wala hawaonyeshwi hata kwenye vyombo vya umbea vya kule.”
Kapende kapata upenyo; “Hali ni kinyume kayani, wachovu wanashobokea kujipendekeza na kujidhalilisha ili njuluku ya kupeleka Uswazi iongezeke hata kwa gharama ya kuwatosa wachovu.”
Anakamua coffee yake na kuendelea; “Sijui kwanini watu wanapenda kufanya vitu kama vile hawana ‘common sense’, au wanatumia ‘uncommon sense’ kama common sense?” Kapende anavyokanyaga kimombo kila mtu anamwangalia mwenzake na kutabasamu kuona kijiwe kinavyogeuka chuo kikuu kama kile cha Manzese.
Anaendelea; “Kwanini hawataki kukubali kuwa alipokuja bwana mkubwa walijidhalilisha hadi kufanya kaya isikalike? Imefikia mahali walevi tukajiuliza: Obamiza anakuja kuchukua kaya nini?” Kijiwe hakina mbavu.
Mzee Kidevu naye hajivungi. Anakwanyua mic na kulonga; “Hivi hawa ndata na ndutu wetu wa kazi gani? Wanalipwa njuluku za nini tena wakila na kunywa dezo wakati hawaaminiki wala hawawezi kumlinda mtu mmoja na msafara wake?”
Msomi kapata nafasi tena ya kumwaga falsafa. Anaangalia hadhira yake huku na kule na kusema; “Nashangaa uwezo wa kufikiri wa akina Njaa Kaya. Je yeye si rahisi? Akienda kule haendi na zana zote za maangamizi na mibomu yote hii? Rais anakuja kutembea na ndege 56 za kimaangamizi, magari 14 na makachero mia kidogo. Au anakuja kuchukua kijiwe?”
Kabla ya kuendelea, Mbwa Mwitu anaingilia; “Thubutu. Akija hapa tunamtuliza na kahawa na anaondoka na kuacha kijiwe ngangari kama kawa. Nadhani akitaka anaweza kuchukua kijiwe cha ngunguri wanaobomubomu na kujikomba kwake.”
Msomi anachomekea; “Kitu cha kwanza, baada ya kusoma makandokando ya ziara ya Obamiza nilijiuliza kama itifaki inaruhusu. Hivi mnadhani ungekuwa wakati wa Mchonga, huyu jamaa angekuja na mibomu na miefubiai yake kutudhalilisha kama sasa?”
Kabla ya kuendelea, mzee Maneno anachomekea; “Msomi naomba nikupinge hapa. Hapa wa kulaumu si Jadwong bali wenyeji wake walioamua kumfunulia kila kitu.”
“We achia hapo utaua.” Mbwa Mwitu anachomekea na kuacha kijiwe hakina mbavu.
Msomi anaendelea kupeta; “Nadhani tatizo letu kubwa lililoleta huu utegemezi ni ile tabia ya kutokujiamini na kuamini katika uombaomba na kujikomba.”
Kabla ya kuendelea mgosi Machungi anakatua mic; “Mie mwenzenu niipoona tinavyopeekeshwa niliamua kumhamisha bi mkubwa. Maana huwezi kujua kama efubiai wanaweza weekeza huko.” Kila mtu hana mbavu jinsi Mgosi anavyohami ulaji wake.
Wakati tukivunjika mbavu, Mipawa anaamua kutuumiza zaidi; “Da hao jamaa wanaovaa miwani ya mbao nyeusi sipati picha waswahili wangapi watajifanya nao ni Wamarekani. Nahofia magaidi nao watakuwemo.”
Anabusu kashata na kuendelea; “Je, jamaa zangu wanaosingiziwa kujilipua watapona? Nadhani La-kaatare atakuwa na hali ngumu kuliko Mgosi anayehofia kuibiwa bi mkubwa. Jamani eh Michele aka Miwali Obamiza bomba. Umeona akina mafestiledi walivyojipendekeza?”
Mzee Maneno naye anavaa daruga na kudema; “Jamani eh, bi mkubwa Mchele na Obamiza si noma ila majamaa yake na wenyeji wao wanaofanya vitu kama machizi. Wanasahau kuwa ataondoka na maisha yataendelea!”
Mbwa Mwitu anachomekea; “Haya jamaa ni madhalilishaji eti yamemuwekea ngumu Obamiza kugusa hata chakula chetu! Sasa ugeni uko wapi? Kama walikuja na mipiza yao basi hawakuwa wageni wetu bali wavamizi.
“Mwenzenu natamani na rahisi angeenda kule akazira mipiza akaitisha pilau na ugali wetu ili wajue nasi jeuri. Angekuwa Mchonga nadhani kichuli kingepelekwa Marekani.” Kicheko kwa sana tu.
Mipawa anaingia ugani; “Beng’we ina maana hata kuoga, kunyx sorry kunonihino ni kwenye eafosiwani?”
Mchunguliaji ambaye muda wote alikuwa akicheka na kusoma gazeti anaamua kuingia ugani; “Kama kila kitu anataka kiwe u-Marekanini basi angeenda zake Florida na kuigiza kuwa yuko kwenye kijua cha Bongo. Ajabu jamaa zangu watajisifu kuwa uchumi umekua kwa vile amekuja Obamiza kutubamiza!”
“Wehu hao watakaosema uchumi umekua wakati wamefunga anga, barabara, mitaa hata huduma zetu za kichovu. Wakati mwingine tujilaumu kwa kuendelea na kile wakameruni huita colonial hangover yaani ulevi wa ukoloni. Watu wanafanya vitu kama hawana ubongo. Who know? Maybe Masaburi at work.” Msomi anaamua kukandia kwa kimombo na falsafa ya kisomi.
Zile njemba siyo efubiai? Acha niishie kabla sijayafanyia kitu mbaya.
Chanzo: Tanzania Daima Julai 3, 2013.
↧
"Wanaopinga Tanganyika walaaniwe"
|
↧
↧
Obama Visit: Tanzania Should Not Brag

US President Barack Obama’s trips abroad are always iconic-cum-echoic despite the controversy they evoke. The amount of money spent on security details, economic expectations, issues addressed and whatnot. Looking at how a common mwananchi in Tanzania was negatively affected by Obama’s visit, Kenya must thank Lord that it did not go through such horribly harassing situation.
According to the Ministry Foreign Affairs’ directives, upcountry people who intended to travel to Dar shortly before or during Obama’s stay were advised against doing so. Many streets, roads and facilities were closed down to give room for Obama to visit some projects. America dispatched many aircraft, choppers, 14 armored vehicles and hundreds of Secret Service agents to Tanzania to enhance Obama’s security. Skeptic and disgruntled Tanzanians were interrogating the rationale of having their Tanzania People’s Defence Force (TPDF) and the violation of their airspace that’s temporarily shut down so as to force air travelers who were either coming to or departing from Dar es Salaam to relocate to other airports.
All of the sudden, Dar became a no-fly zone. Others interrogated the position of the country protocols. Others called this colonial mentality of worshiping rich countries to entice them to donate more money to this begging country with humongous resources. There were many discussions about the pros and cons of Obama’s visit to the country.
One columnist was quoted as saying, “Thank you for visiting, Mr. President, but can we have our country back?”
The country was held to ransom for three days simply because Obama was in the town! The lives of common wananchi was turned topsy turvy for the whole time Obama was in the country. One Swahili Daily, Tanzania Daima was quoted as saying that many concerned citizens voiced their concerned saying that closing roads and streets violates their basic right to movement. Again, President Jakaya Kikwete was laughing at the top of his lungs for enhancing such a ‘milestone’ which turned to be a nightmare for common mwananchi. To him the coming of Obama was more important than the lives of his earthlings. Again, many questioned Kikwete’s sanity and moral ground as far as media freedom is concerned.
The Committee to Protect Journalists wrote to Obama ahead of his visit to Tanzania to ask him touch on tribulations journalists in Tanzania have faced. Part of the letter read, “….several journalists have been attacked in connection with their work. In March, unknown assailants attacked Absalom Kibanda, chairman of Tanzanian Editor's Forum and managing editor of the New Habari media company, leaving the critical columnist with severe injuries. No one has been arrested. Local journalists also said they have often been threatened by officials and high-ranking businessmen via text messages, emails, or intermediaries. Reporters based outside the capital, Dar es Salaam, are often targeted, the sources said.”
When it comes to media freedom Tanzania might compete with Eritrea, Rwanda and Zimbabwe even though it has nary been in the news. Its media laws are archaic and draconian. For example, the 1976 Newspaper Act, allows the information minister to employ his discretionary powers to suspend even ban Newspapers or any publications he or she deems fit for the action. Apart from bad-media laws, Tanzania is among the most corrupt countries in Africa. It came to light a few months ago that Tanzania loses over one billion dollars in tax collection not to mention another big chunk of money that is lost to corruption annually. Government-owned Newspaper, the Daily News recently reported that the country loses Tsh 15 billion annually thanks to smuggling. It wrote, “The government suffers over 15bn/- loss annually in revenue due to smuggling and improperly taxed cement imports through Zanzibar, an industry source said in Dar es Salaam over the weekend.” Such a country can’t be an ideal one or excluded from failed state status if truth is visited. Furthermore, every year the office of the Controller and Auditor General (CAG) unearth and report mega corruption and nobody has ever been held accountable. Sadly though, every year witnesses the surge in corruption.
In other words many mistake Kikwete’s seemingly high standing in leadership. What is going on in Tanzania is no different from other African countries with regards to corruption and bad governance. Two days before Obama arrived in Tanzania; Kikwete was quoted saying that Tanzania is currently the most favoured country in investment. Unfortunately though, Tanzania despite attracting many investors has lagged behind economically due to the fact that investment is clouded by corruption. Again, the grave shines outwardly while it stinks inside. A recent incident involved a grenade attack on a political rally in Arusha where CHADEMA was wrapping its local government election campaigns. It was alleged without being refuted that police were behind the attack under the instructions of the ruling Chama Cha Mapinduzi (CCM). Instead of rebutting the allegations police embarked on white wash and witch hunt whereby CHADEMA leaders were harassed and temporary detained.
Looking at how Tanzanians suffered during Obama’s visit, Kenya needs to thank God for being skipped. I know many people will say that the coming of Obama means more cooperation with Tanzania. This does not hold water. Bill Clinton came to Tanzania and nothing changed. Essentially, Obama visited Tanzania not just because it is better than others. He came to erase or to minimize Chinese influence in the region. In March 2013 Chinese president Xi Jinping was a special guest in Dar and Pretoria all venues Obama visited.Those who know nuclear politics say that Obama visited Tanzania to make sure that the recently discovered uranium is not falling into wrong hands. So too, many types of minerals are being discovered in Tanzania something America needs to put a hand on before Chinese and other vultures does the same. So what attracted Obama to Tanzania is not democracy or good leadership but resources. If Kikwete were a shining example of good leadership as his spin doctors want us to believe, he’d not have attracted China the way he did so as force Obama to come to extinguish the fire China left behind.
Again, Kenya should thank Lord it was skipped by Obama otherwise after his arrival my Nairobian friends would have love to hate his coming.
Source:The African Executive Magazine July 3, 2013.
↧
Morsi saw it coming but didn't get it


This blog wrote yesterday that former Egyptian President Mohamed Morsi's regime was on its way out of power. We called what was going on an endgame. This is after the army threatened to take unspecified measures.Interestingly Morsi was under simulacrum or optical illusion so as not to see it coming. The army issued a 48 hour ultimatum that was flatly ignored by Morsi for his peril. Now that Morsi is history after the army toppled him, will Egyptians go home and rest leaving their hard-earned democracy in the hands of the junta? Will demonstrators feel at home by being part and parcel that has overthrown a democratically elected government? Will they be at home with the act of putting power in the hands of the military regime? Is this the end of struggles in Egypt or the beginning of yet another standoff? After deposing Morsi, the army appointed the Chief Justice of the Constitution Court, Adly Mansour to become an interim president who will preside over elections. A million-dollar question is: Is this the marriage of the Judiciary and the Army or gimmicks? The constitution was suspended and Morsi was said to be held in Luxor. Again, many still doubt the integrity of the army that has for long played the role of king maker. Others are blaming Muslim Brotherhood that backed Morsi for their role in bringing him down due to their hardheadedness. Also the fragmented opposition is not spared. Many see it as another puppet that enabled the army to regain power it lost after a stint soon after the first revolution. A bitter lesson for African potentates. Is the deposing of Morsi the beginning of the end of Sudanese strong man Omar Bashir and others in the Middle East and Africa South of Sahara? Morsi saw it coming but he did not accept it.
↧
Kipanya na watawala mapanya walivyonufaika na ziara ya Obama

↧
Barua ya wazi kwa Pinda toka kwa walevi

Baada ya Waziri Mkubwa, Mizengwe Pindapinda, kupinda na `kupayuka’ huku akifyatuka, kikao cha walevi kimemtuma mlevi kumpa salamu zake.
Kwanza, tunampenda na kumheshimu sana. Ila tunamshauri atubie kabla kiama hakijamshukia. Maana huwa tunasikia akisema `eti’ yeye ni mtu wa God utadhani wapo wa shetani ambaye hakuumba chochote.
Mbona huko nyuma hakuwa hivyo! Ameharibiwa na nini yarabi mwana wa farmer ambaye siku hizi amekuwa mwana milionea anayeweza kuvaa `misaa’ ya dhahabu ya bei mbaya.
Au `maulaji’ yamemlewesha kiasi cha kuanza kale ka ugonjwa kaitwako `Yusufuosis Makambiasis’ aliyesifika kwa kupayuka hovyo.
Sijui ameishia wapi baada ya kurithisha `ulaji’ kwa kitegemezi chake? Bongo kwa utawala wa kifalme sina mfano.
Yaani kila big anajitahidi kuhakikisha mikoba yake anampa kitegemezi chake! Je, wasio na madingi heavy wataishia kutawaliwa na kuliwa hadi lini? Anyway, hii siyo `inshu’ leo.
Kwa sisi wataalamu wa saikolojia, tunaweza kusema kuwa Pindapinda alipopayuka kuwa `ndata’ wawachape walevi hata wakiwanyotoa roho kama walivyofanya kule Arusha, yawezekana alikuwa akisumbuliwa na kile ambacho kitaalamu kinaitwa Cocktail Party Phenomenon (CPP), gonjwa ambalo huwasumbua wale wanaotumia sana hasa utumiaji wenyewe unapokuwa ni wa `dezo’ kama katika hali hii.
Mwenye kuugua ugonjwa huu mara nyingi anaweza kuongea bila mdomo wake na kichwa kuwasiliana. Kitaalamu tunasema kunakuwa na disconnection and confusion among neurons especially axoms in his amygdala. Hayo tuyaache maana ni ya wataalamu.
Kupayuka kwa Pindapinda kumenikumbusha wagonjwa wengine wanaougua ugonjwa wake yaani kihiyo Bill Lukuvy, Mwehujuu Nchembe, Nipe Mapepe Ninaye na Chris Mtikilila ambaye siku hizi hana tofauti na Lyatongolwa kwa kujikomba, ili pate `ulaji’ hata kama ni mchafu na haramu.
Hakuna mtu mwenye akili alitegemea mwanamume timamu kutoa kejeli na matusi ya nguoni wakati wa msiba wa mabomu iliyorushwa na washenzi wanaotumikia washenzi wenzao wanaoona ulaji ukiwaacha kutokana na ulafi na upogo wao.
Tumuulize bwana Pindapinda kwa niaba ya walevi waliotutuma. Kaka unataka wafe wangapi? Je, una habari kuwa kuna taasisi inaitwa ICC au International Criminal Court ambayo wale huiita International Komesha Korti ambayo siku hizi inawashughulikia walevi wa madaraka wanaoamini katika matumizi ya jinai kama uliyotetea?
Walevi wanasema umepinda sana na baadaye anaweza kupinduka kama siyo kufyatuka tena. Hivi kaka hujui kuwa ndata wameishadedisha walevi kibao?
Yaani pamoja na walevi wengi `kudedishwa’ hujaridhika! Kaka umekumbwa na nini au Sumba wameishasumbawanga?
Baada ya kusikia kauli zako za maangamizi yaani Words of Mass Destruction (WDM) kwa lugha ya Kibush kichaka, walevi tulikutana kwa mama muuza mitaa ambayo ni siri kubwa na kushauriana tukukabili ili kukunusuru.
Kwanza, tulikubaliana tukupe ushauri wa bure kuwa ufute kauli yako, kuomba msamaha na kutubia. Pili ujiuzulu japo kwa genge lenu kufanya hivyo ni ndoto.
Tatu, uje kwenye kikao chetu na kutupa `ofa ya ulabu’ ili tuwapoze jamaa wasije kustuka na kuamua kufanya kweli wewe na wenzio mkajikuta pabaya.
Tulihofia yasikukute makubwa kutokana na kujua kuwa umma wa walevi una nguvu kuliko hata bomu la nyuklia.
Ukiamua hao ndata hawawezi `kufua dafu’ zaidi ya kutoka mkuku kama ilivyotokea kule kwa Mwamali Kadhafi wa Kashafi `aliyededishwa’ kama kibaka.
Japo unaweza kuchukulia ushauri wetu kama mawazo ya kilevi na `tishatoto’, ufahamu mambo yamebadilika sana.
Nani alijua kuwa nguli kama Kadhafi angeuawa kama kibaka huku akilialia kama kichanga?
Kwa vile walevi wanakupenda na kukuzimia, wangependa usiaibike wala siku moja kuzomewa au kuja kujilaumu kwa kupayuka. Tunajua ulipitiwa kama ngurumbili.
Ukubali ulichemsha na kupayuka bila kufikiri vilivyo. Hivyo, usione aibu kutubu na kujirekebisha. Rasmi natoa pendekezo la nia nzuri toka kwa walevi.
Kwa vile walevi ni wajanja na great seers, tumeamua. Kama ushauri wetu wa bure utapuuzwa basi tuandamane hadi siku utakapofunga virago na kuachia `ulaji’ ili waje watu wengine wasio wagonjwa.
Tumepania kuhakikisha tunafanya kweli hata kama tutapaswa kuumizwa na hao ndata wako.
Tuko kwenye kampeni na ushauri kwa `bi wakubwa’ zetu kutusaidia kuandamana kwa kuvua nguo ili ulaaniwe na kigwena chako ambacho kimehalalisha ukandamizaji (Lwakatareing), utekaji (Kibanderings), vipigo (Ulimbokering) na mauaji (Mwangosirings) ya walevi.
Wana mpango wa kuonana na `bi mkubwa’ Tununu kwanza, ili wampe siri yao kama mother na madhara yatakayokukumba na familia yako.
Amini hivi si vitisho bali watafanya kweli ili likupate la kukupata. Jiulize wako wapi akina Ommy Ngunguri Mahitason?
Wako wapi akina Beno Mkaa Hapason aliyejifanya Mungu mtu asijue angeishia kuwa kituko na aibu kiasi cha kuhitaji kulindwa na Njaa Kaya ili asinyee debe?
Kaka, ninakushauri usidharau utume huu unaojikamilisha yaani self-fulfilling prophecy kwa kimakonde.
Kwani katika pita pita yangu mitaani nilishuhudia na kusikia hata ndege mbuzi na hata tumbili wakilaani kauli yako ambayo sisi tunasema ni bahati mbaya kiasi cha kukushauri utubie mara moja.
Kitu cha maana kufanya mbali na kuomba radhi na kutubu na kufunga ni kukubali kuwa `chata’ lako limeishiwa na hakuna anayelitaka tena kutokana na kutekwa na mafisi na `mafwisadi’ ukiachia mbali kutumia ndata kunyotoa roho za walevi.
Najua utasema tumetumwa na Chakudema kukupa fwacts hizi, huko Arusha utasingizia siasa na Ntwara nako je?
Ningekuwa wewe ningeanza kufanya mazoezi ya kuwa msemaji mkubwa wa upingaji baada ya kutupwa nje kama kiama na kuutema ukuu wa sirikali mjengoni ambako nako kumegeuka uwanja wa fujo ambapo mabondia uchwara kama Jay Nkamia wanatishia maisha ya wenzake.
Hata hivyo, ashukuru Mungu anawaonea akina mama. Angemgusa mtu kama kama Pita Msigwa si angeumizwa vibaya `jore’ huyu? Jay Nkamia `jore’?
Washikaji wangu wa kule Haubi Maziwa, Makomango, Babayu, Mombose, Chinyika, Chase, Gonga, Mbugutole, Farqwa, Itanda na Magu mpo?
Chanzo: Nipashe Jumamosi 6, 2013
↧
↧
How Obama unraveled Bongo-Peace Mystery
Our hunk’s always been surrounded by mysteries one of them being the whole boring manta of being referred to as an Island of Peace. Is it really an Island of Peace of an Island in pieces? How can it stop from being if we’re now baying for the blood of one another to have a third government and a third country of Danganyika? Is it an Island of Peace even for the victims of recent Arusha terror attack? Anyways, let us look at how US of A president Black Obama’s visit to the hunk solved this mystery by putting stinking liars and aggrandizers to shame.
Prior to the coming of Obama our hunk was wrongly considered to be independent, peaceable and secure. His coming revealed the secret of secrecy and self-cheating that everything’s spiffy. What a goof! Had it been, Obama’d have bothered to come with hundreds of Secret Service agents so as to burn over $100 Million. Again, how can an insecure hunk be peaceable if we face it? This means. All ballyhoos and brouhahas about peacability of the Island of Peace were but gimmicks and abracadabra. Our spin doctors are now in hot soup after losing their mojo and skulduggery Their highly guarded secret that enabled them to take us for a ride is now open. Usanii mtupu na rongorongo za kichovu!
As the days of his arrival drew near, everything started to unfold in the manner and speed nobody expected. The ridiculously true but hidden status of our rulers became clear though paradoxical.
Before the coming of Obama everything seemed to be intact and sound. Nobody knew that we’re manned by tin pot prefects that can be ordered by president of another hunk. We’re not making this up but the results of Obama’s stay in the hunk when they proved this beyond any doubt. Before the coming of Obama the presider of the country of cowboys and gun lovers I didn't know that our presiders we used to emulate were but prefects.
They can do everything to please their masters even sacrificing the boozers whose taxes fatten them. Our boozers are valuable when they pay taxes for enabling bigwigs to tanua. Thereafter, they’re but chaffs after seeds have been sifted.
So too, security organs are but white elephants scooping our dosh for doing nothing. Whoever disputes this should tell us why they’re unable to guard one Obama. Some boozers say that these guys are good at protecting drug barons, thugs and corrupt biggies. Likewise, our dog faces are good at lording it over Ntwara earthlings as it was recently reported without being refuted. They’re good at beating the civilians.
I didn't know that our hunk is a joint venture where by the US of A has many more shares than we have. The way Obama used our prefects for the whole while he’s in the hunk speaks volumes.
From this vantage one may say that our independence’s lost its gravitas thanks to the love of begging. Begging destroys the mind. To be proud of it is one of the characteristics of a sick mind. Again, what sort of hypocrisy was it for mighty beggars to expel dirty beggars? I was told that even the ‘matching guys’ who scratch the surface to get something to feed their duped families were expelled without bothering to think how their loved ones would survive.
When Alhaj Mwinyi likened our hunk with the head of a mad man which a boozer uses to learn how to trim, he knew what the future had to offer. Now I can see his rationale though he’s an architect of all this megalomania.
When Mchonga said that the hunk was going to the dogs he knew what’d happen. What self-fulfilling prophecy! Don’t tell me that Bwana Mkubwa brought many goodies especially business opportunity for the hunk. Phew! How did we benefit from the African Growth and Opportunity Act (Agoa) and Millennium Development Goals (MDGs)? Bwana Mkubwa might come with sound proposals. Again, looking at our venal potentates, nothing will come forth. Why are we going to keep on cascading into abject poverty despite hosting Bwana Mkubwa? Looking at the look of things, we’re renowned for offering tax holidays to every swindler who can dine and wine venal high and mighty. We’re entering in bogus and dubious agreement with scrupulous investors. We spend our hard-earned dosh unwisely. Corruption’s been legitimized in the hunk. Don’t get me wrong saying I’m telling lies. Tell me. When we’re told that some thugs stashed dosh in offshore banks, what measures did we take against them? We've become a society of rats that gnash everything. How many mega scam suspects are in our streets enjoying our dosh instead of being behind bars? How many looters are protected by the high and mighty? Can such a hunk be safe for Bwana Mkubwa? Maybe, he felt that due to our rust for dosh, some terrorists might buy our hyena-like officials and be able to attack him.
Today spin doctors are singing praises that soon power rationing will be history after Bwana Mkubwa promised to invest heavily in Energy Generating Projects under Power Africa Initiative (PAI). Nonsense! Is investing in Richmond-Dowans-Symbion outfit viable or corruption? If Mzee Nyerere created TANESCO that thieves felled and vended to nourish Pichmond-Dowans-Symbion axis of corruption, how’ll new projects survive? They’ll fell them the way the felled TANESCO. The darling buds of May.
One boozer, Zezete Mpendasifa left us in stitches. He said that Obama came to neutralize Chinese influence especially after he caught wind of uranium deposits that were recently discovered in our hunk.
Today’s nugget of wisdom is, “A promise is a comfort for a fool,” Gregory Isaacs, (1951-2010).
Source: Thisday July 8, 2013.
↧
Angalia Tanzania inavyobakwa
↧
Viongozi wa CCM "A" na CCM "B" wanapopata picha ya pamoja!
.jpg)
Waingereza husema a picture speaks a million words. Sijui hii picha hapo juu inakukumbusha au kumaanisha nini? Wapo waliovuma wakavumishwa na mwisho wakaishia kuwa wala makombo. Wapo waliopaa wakaishia kukatwa mbawa na kuishia kuwa mabingwa wa kujikomba ili waweze kuishi. Hakika katika picha hii imenoga hasa kutokana na kuongezeka wengine watatu yaani profesa Ibrahim Lipumba, maalim Seif Shariff Hamad na 'mchungaji' Christopher Mtikila. Hakika ngoma ya kisaliti inogile!
↧
Uhovyo wa Kikwete wazidi kufichuka


Rais Jakaya Mrisho Kikwete anaingia kwenye vitabu vya historia ya Tanzania kama rais wa hovyo sana anayeweza kudhalilishwa hata kutapeliwa kirahisi kwa sababu ya kutokuwa makini na kupenda sifa.
Tangu aingie madarakani, Kikwete amekumbwa na kashfa nyingi sana zikiwemo zile za wizi wa pesa ya umma toka kwenye Benki Kuu chini ya jinai ya EPA, kuteua watendaji wabovu, kuuza nchi kwa wawekezaji, kupokea rushwa ya suti, kusaini sheria feki, kutumia vibaya madaraka na pesa ya umma, Richmond, kuruhusu mkewe kuunda NGO ya mashaka, kuruhusu watoto wake kutumia madaraka yake kujitajirisha na kutumia vyombo vya habari kuwahujumu wapinzani wake.
Kashfa nyingine zinazomkabili Kikwete ni kutumia vibaya jeshi la polisi na wananchi kwa manufaa yake kisiasa, kupewa orodha ya wauza unga na majambazi asiwachukulie hatua, kuunda mitandao hatari kwa taifa, kutumia udini na ukanda kujinufaisha kisiasa, kutoa ahadi za uongo, kuzurura, kuunda serikali kubwa, kuunda mikoa na wilaya mpya kuwanufaisha marafiki zake, kushindwa kuulinda muungano na katiba, kuendekeza kujuana na kulipana fadhila ambavyo vimekuwa vigezo na msingi mkubwa wa uteuzi wake, kutotangaza mali zake, kuwakingia kifua wahalifu kama vile walioghushi shahada na sifa za kitaaluma, kumkingia kifua rais mstaafu Benjamin Mkapa,mkewe, wakweze na watoto na marafiki na washirika zake, kuwakingia kifua marafiki zake wanaotuhumiwa kwa ufisadi na kuwapigia kampeni, kushindwa kusimamia uchumi wa nchi, kuendelea kuingia mikataba ya kijambazi kwenye sekta za uwekezaji na nishati, kutojua anachopaswa kufanya kama rais, kulea udini, kutawala bila sera wala dira, kutumia watu wenye kutia shaka kama vile Salva Rweyemamu, 'profesa' Julius Nyang'oro aliyeandika kitabu cha maisha yake, kuamuru polisi kuua wananchi, kuhujumu demokrasia nchini, kutelekeza na kulihujumu taifa kwa ujumla na nyingine nyingi.
Hivi karibu kuliibuka kashfa ya kutumia kihiyo na profesa feki kuandika kitabu cha maisha yake. Bahati nzuri blogu hii mnamo tarehe 6 May 2012 ilichapisha kashfa ya Julius Nyang'oro mwandishi wa kitabu cha maisha ya Kikwete. Ni baada ya kupata dokezo toka kwa mdogo wa Nyang'oro kuwa angetoa kitabu cha maisha ya rais Kikwete. Mdogo huyu wa Nyang'oro alikuwa rafiki yetu ingawa baada ya kukandia kitabu husika urafiki huu ulikufa.
Kashfa hii ya hivi karibuni imelipotiwa na vyombo vya habari nje na ndani ya nchi. Kwa habari zaidi kuhusiana na kashfa ya profesa huyu tapeli na kihiyo BONYEZA HAPA.Pia BONYEZAHAPA.
↧
↧
Kikwete ateua fisadi mwingine kama ishara ya kulindana


Uteuzi wa Hilda Gondwe aliyekuwa Katibu Tawala mkoa wa Kilimanjaro ni ushahidi wa rais Jakaya Kikwete kulinda mafisadi. Mnamo tarehe 27 Mei 2010 blogu hii ilchapisha kashfa iliyomkabili Gondwe ambao alijitwalia gari la umma aina ya Toyota Land Cruiser VX iliyokuwa imenunuliwa miaka mitatu kabla kwa shilingi 155,000,000. Gondwe 'alinunua' gari hili kwa shilingi milioni moja na nusu tu huku akiusababishia umma hasara ya shilingi 149,000,000. Je rais na washauri wake hawakuliona au hawalikumbuki hili? Je inatoa picha gani kwa umma wa walipa kodi maskini wa nchi yetu? Ni ajabu kugundua kuwa mtu huyu ameteuliwa na rais kuwa mjumbe wa Kamati ya Maadili ya Viongozi wa umma nchini. Je anaingia mtu huyu asiye na maadili mle na maadili gani zaidi ya madili? Je huu si ushahidi mwingine wa Kikwete kulinda uoza na kutokuwa makini na kurudia makosa? Je hakuna watanzania safi wenye kuweza kufanya kazi hii hadi wateuliwa wahalifu wa kawaida kama Gondwe? Je Kikwete atajifunza na kubadilika lini? Je kuna haja ya umma kuendelea kumvumilia mtu kilaza kama huyu mgumu wa kujifunza na kubadilika? Hakika, maswali ni mengi kuliko majibu.
↧
Ukiwa na mindset kama hii jua hakuna nchi bali kusanyiko la panya au majuha

↧
Walevi wavunja radio ugeni wa Obama
.jpg)
Tulimshambulia Black Obama, jamaa aliyewapagawisha wapenda sifa hadi wakajidhalilisha. Tulimpa `kanywaji’ na kushushia na utumbo na mapafu hadi akachanganyikiwa na kusema, don’t kill me with kanywaji you boozers.
Alitusifia ukarimu wetu na jinsi tulivyobana matumizi tofauti na walevi wa sifa, waliokufuru kwa kufuja na kumtumia Obama kuiba fedha za wachovu. Kimsingi, kinachoitwa ukarimu si ukarimu chochote, bali kuwanyonya makapuku.
Hivi kaya kapuku inapata wapi jeuri ya kufunga shughuli za uzalishaji kama vile kufunga barabara na mitaa wakati kufanya hivyo kunaathiri uchumi wa mtu mmoja hata kaya?
Sisi tulimpa makaribisho kwenye baa tunakonywea. Hatakufanya marekebisho ya baa yetu kwa kuipaka rangi upya kama wao walivyafanya baa yao. Wala hatukwaambia wahusika wazibe mashimo kwenye barabara ya kuelekea kwenye baa yetu.
Walevi si watu wakujikomba na `kujigonga gonga’ kama vyangu. Sisi tunafanya kweli kwa kukata `kalaji’. Ukishapata `kalaji’ unafukia mashimo wala hayaonekani.
Hivyo, tulijua angeyaona mashimo wakati wa kuingia, lakini kutoka mkeka mtupu. Na ndivyo ilivyokuwa hadi tunamfikisha kwenye Air Fosi Wani alikuwa amechangamka usiambiwe.
Kimsingi, ni kwamba walevi tulinufaika na ujio wa Obama kuliko wale `waliojivua nguo’ bila sababu. Sisi hatubadili jina la baa yetu na kuiita Obama.
Badala yake tuliamua kumuingiza mjini na kuita baa yetu White House kuonyesha kuwa nasi ni vidume wa vidume. Pia tulimtaka tukienda Umarekanini abadili jina la White House na kuwa Uwanja wa Fisi.
Hivyo, siku moja mkisikia White House ikiitwa Uwanja wa Fisi msishangae. Na kweli ni uwanja wa fisi aitwaye Umarekanini.
Hata wake zetu walinufaika sana na ujio wa Michele ya Obama. Badala ya kujikanyaga na kiigereza uchwara kama cha bibi yule aliyesema I am the wife of Obama of my country like your Michele, walimkaribisha kwenye vibanda vyao vya `mamantilie’ na kumfundisha kusonga ugali.
Michele ameondoka mwenye furaha baada ya kupewa elimu ya kumuandalia mumewe chakula kilichokwenda chuo. Wake zetu waliletewa pizza. Walipoionja walisikia kichefu chefu kutokana na kujaa jibini au cheese kwa lugha ya kwao.
Hivyo, waliamua kumfunda Michele kwa kumfundisha mapishi ya kiafrika. Kati ya vyote walivyomfundisha na kumuandalia, Michele alipenda sana dagaa wa nazi na ugali na nguru wa kurumangia.
Pamoja na wake wa walevi kuwa `apeche alolo’, hawakujidhalilisha `kumpiga mizinga’ Michele, kwa vile wanajua hana fedha bali fedha ni za taifa.
Walifurahishwa na kauli ya Obama kuwaambia ombaomba wenye suti kuwa maendeleo yao, yataletwa na wao wenyewe na si kwa kuombaomba. Ajabu walengwa walionekana wakinua kutokana na kuwa hamnazo.
Kwa vile mlevi mkuu nilikuwa Sauzi, nilipokwenda kumjulia hali swahiba yangu tuliyesoma chuo Diba Madiba, niliandaa simpo ceremony kama Sauzi na Senegali.
Maana wao hawakufuja fedha za wachovu kumfurahisha tajiri wa kutupa ili awape misaada wakati wana watu na raslimali. Sikuona Jake Zuma akikenue meno kumuingiza mjini Obama ili akate pochi.
Jamaa yangu na rafiki yangu Macky Sall alimtolea kavu kavu kuwa ushoga Senegali haramuni. Alimwambia wazi wazi mbele yangu nikiwa naona na kusikia kuwa akome na akomae.
Na kweli Obama alituomba msamaha kukubali yaishe. Tulifunika kombe mwanaharamu akapita kwa salama salimini.
Baada ya kumkaribisha uwanja wa fisi na kumkuna, Obama alituibia siri kuwa hakufurahishwa na jinsi walevi wa sifa walivyompokea kwa israfu. Aliahidi kututumia whisky na kutukaribisha kwenye White House.
Alituahidi kuwa hatatupokea kama wezi wala kutupitisha mlango wa nyuma kama wale. Mwenzetu mmoja alitutibua aliposema eti ziara ya Obama imekwisha turejee kazini.
Nani afanye kazi wakati Obama ameleta neema? We ngoja utawasikia wakipeana sifa za kijinga utadhani maisha yao magumu yataondoka. Bila kuacha kutumia masaburi mkatumia akili na maarifa katika kusimamia `njuluku’ na raslimali za kaya hata aje Bill Gate mtaendelea kuwa makapuku.
Fedha mfiche Uswisi, mtegemee kuukata Uswazi. Shauri yenu utawakata. Badala ya kuishi Kanani mtaishi kama nyani juu miti. Obama ametuahidi misaada hadi tuchanganyikiwe.
Hivyo, hakuna haja ya kufanya kazi bali kufanya kazi moja tu ya kutumbua na kukuta `kalaji’ na kuzurura Ulaya. Walevi sasa wataanza kuishi kama Wamarekani kwa taarifa yenu.
Bling bling kwa sana na mabomu na mibunduki kwa fujo. Jamaa zangu wapingaji kaa mkao kuliwa na kulipuliwa. Hayo ndiyo maendeleo maana barabara zenu zinatengenezwa na `geshi’ lenu linapinduliwa na kubakia kanyabwoya.
Hakuna kitu kiliwaacha hoi walevi kama jinsi mzee mzima nilivyoangusha speech tena kwa kimakonde. Ilikuwa imejaa `mipwenti’ hiyo mpaka Obama akaniabia inatosha mzee.
Maana wewe si binadamu bali chuo. mimi sikufanya kama wale ambao walipoona Obamiza akijitingisha kidogo kama anacheza wao wakamwanga radhi kama hawana akili nzuri wasijue Obama alikuwa akiwasanifu.
Hakuna kitu tulichomkuna Obama kama kuwezesha kumuingiza bibi yake wa Kogelo kayani, tena bila kufuata kanuni za uhamiaji. Kwa vile kaya nzima ilikuwa imelewa uobama, tulimpitisha mipakani hata bila kuwa na pasi ya kusafiria.
Sisi walevi wajanja. Wala hatujamkaribisha Obamiza na mingoma tena yenyewe X. Hivi ukiona baba au mama zima linakata mauno wafikiri salama? Jamani huku ni kujidhalilisha na kuonyesha kuwa urithi wa mkoloni bado unatutafuna hata baada ya miaka 50.
Hata nilipotembelea kwenye chuo kikuu cha Harvard nilikuwa watu wanaamini kuwa urithi wa mwafrika ni mingoma jambo ambalo nililipinga sana.
Baada ya kuwatolea speech iliyokwenda chuo waliamini kuwa mimi ni mlevi na si mpuuzi wa mingoma ya kishetani. Hivi rais na ngoma wapi na wapi? Watu wanaangalia matatizo ya walevi nyinyi mnayakwepa na kujifanya mna raha za kukata mauno wakati ni njaa tupu.
Chanzo: Nipashe Jumamosi Juni 13, 2013.
↧