Habari iliyosambazwa kwa vyombo vya habari ni kwamba rais Jakaya Kikwete amepewa tuzo nyingine ya The Icon of Democracy. Ajabu pamoja na wahusika kujisifu, ukichunguza sana unagundua kuwa nyuma ya tuzo hii kuna wanigeria. Kulikoni? Je kuna matapeli wanaomzunguka Kikwete na kusuka apewe upuuzi huu ili baadaye wahusika waje kumtoa upepo au kutafuta fursa na kuchukua kwa njia za uwekezaji uchwara kama ilivyokuwa kwenye tuzo nyingine ya kutia shaka ya The Most Impactful Leader of Africa iliyotolewa na Jarida lenye uhusiano na wanigeria? Maana tunaambiwa yupo Mwandishi wa habari ambaye pia ni pastor Elvis Ndubuisi Iruh kwenye tuzo ya sasa sawa na African Leadership Magazine ambalo makao yake makuu ni 13 Mambilla street,Off Aso Drive, Asokoro.P. O. Box 9824 Garki – Abuja, Nigeria.
↧